< Yohana 2 >
1 Siku ya tatu kulikuwa na arusi mjini Kana, mkoani Galilaya. Mama yake Yesu alikuwapo,
第三天,在加利肋亞加納有婚宴,耶穌的母親在那裏;
2 naye Yesu alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.
耶穌和衪的門徒也疲請去赴婚宴。
3 Divai ilipokwisha, mama yake akamwambia, “Hawana divai!”
酒缺了,耶穌的母親向衪說:「他們沒有酒了。」
4 Yesu akamjibu, “Mama, usiniambie la kufanya. Saa yangu bado.”
耶穌回答說:「女人,這於我和妳有什麼關係?我的時刻尚未來到。」
5 Hapo mama yake akawaambia watumishi, “Lolote atakalowaambieni, fanyeni.”
衪的母親給僕役說:「他無論吩咐你們,你們就作什麼。」
6 Hapo palikuwa na mitungi sita ya mawe, ambayo kila mmoja uliweza kuchukua kiasi cha madebe mawili au matatu. Ilikuwa imewekwa hapo kufuatana na desturi ya Kiyahudi ya kutawadha.
在那裏放著六口石缸,是為猶太人取潔用的;每口可容納兩三桶水。
7 Yesu akawaambia, “Ijazeni mitungi hiyo maji.” Nao wakaijaza mpaka juu.
耶穌向僕役說:「你們把缸灌滿水吧! 」他們就灌滿了,直到缸口。
8 Kisha akawaambia, “Sasa choteni mkampelekee mkuu wa karamu.”
然後,耶穌給他說:「現在你們舀出來,送給司席。」他們便送去了。
9 Mkuu wa karamu alipoonja hayo maji, kumbe yalikuwa yamegeuka kuwa divai. Yeye hakujua ilikotoka, (lakini wale watumishi waliochota maji walijua). Mkuu wa karamu akamwita bwana arusi,
司席一嘗已變成酒的水─並不知是從那裏來的,舀水的僕役卻知道─司席便叫了新郎來,
10 akamwambia, “Kila mtu huandaa divai nzuri kwanza hata wakisha tosheka huandaa ile hafifu. Lakini wewe umeiweka divai nzuri mpaka sasa!”
向他說:「人人都先擺上好酒,當客人都喝夠了,才擺上次第的;你卻把好酒保留到現在。」
11 Yesu alifanya ishara hii ya kwanza huko Kana, Galilaya, akaonyesha utukufu wake; nao wanafunzi wake wakamwamini.
這是耶穌所行的第一個神跡,是在加利肋亞納匝肋行的;衪顯示了自己的光榮,衪的門徒們就信從了衪。
12 Baada ya hayo, Yesu alishuka pamoja na mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake, wakaenda Kafarnaumu ambako walikaa kwa siku chache.
此後,衪和衪的母親、弟兄和門徒下到葛法翁,在那裏住了不多幾天。
13 Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa imekaribia; hivyo Yesu akaenda Yerusalemu.
猶太人的逾越節近了,耶穌便上了耶路撒冷。
14 Hekaluni aliwakuta watu wakiuza ng'ombe, kondoo na njiwa, na wavunja fedha walikuwa wamekaa kwenye meza zao.
在殿院裏,衪發現了賣牛、羊、鴿子的,和坐在錢莊上兌換銀錢的人,
15 Akatengeneza mjeledi wa kamba, akawafukuza wote nje ya Hekalu pamoja na kondoo na ng'ombe wao, akazimwaga sarafu za wenye kuvunja fedha na kupindua meza zao.
就用繩索做了一條鞭子,把眾人連羊帶牛,從殿院都趕出去,傾倒了換錢者的銀錢,推翻了他們的桌子;
16 Akawaambia wale waliokuwa wanauza njiwa, “Ondoeni vitu hivi hapa. Msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa soko!”
給賣鴿的人說:「把這東西從這裏拿出去,不要使我父的殿宇成為商場。」
17 Wanafunzi wake wakakumbuka kwamba Maandiko yasema: “Upendo wangu kwa nyumba yako waniua.”
衪的門徒們就想起了經上記載的:『我對你的殿宇所懷的熱忱,把我耗敬盡。』的話。
18 Baadhi ya Wayahudi wakamwuliza Yesu, “Utafanya muujiza gani kuonyesha kwamba unayo haki kufanya mambo haya?”
猶太人便追問衪說:「你給我們顯什麼神跡,證明你有權柄作這些事?」
19 Yesu akawaambia, “Vunjeni Hekalu hili, nami nitalijenga kwa siku tatu.”
耶穌回答他們說:「你們拆毀這座聖殿,三天之內,我要把它重建起來。」
20 Hapo Wayahudi wakasema, “Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arobaini na sita. Je, wewe utalijenga kwa siku tatu?”
猶太人就說:「這座聖殿建築了四十六年,你在三天之內就會重建起它來嗎?」
21 Lakini Yesu alikuwa anaongea juu ya Hekalu ambalo ni mwili wake.
但耶穌所提的聖所,是指衪自己的身體。
22 Basi, alipofufuliwa kutoka wafu, wanafunzi wake walikumbuka kwamba alikuwa amesema hayo, wakaamini Maandiko Matakatifu na yale maneno aliyokuwa akisema Yesu.
所以,當衪所死者中復活以後,衪的門徒就想起了衪曾說過這話,便相信了聖經和耶穌說過的話。
23 Yesu alipokuwa Yerusalemu kwa sikukuu ya Pasaka, watu wengi walimwamini walipoona ishara alizozifanya.
當耶穌在耶路撒冷過逾越節時,有許多人看見衪所行的神跡,便信從了衪;
24 Lakini Yesu hakuwa na imani nao kwa sababu aliwajua wote.
耶穌卻不信任他們,因為衪認識眾人;
25 Hakuhitaji kuambiwa chochote juu ya watu, maana aliyajua barabara mambo yote yaliyomo mioyoni mwao.
衪並不需要誰告訴衪,人是怎麼的,因為衪認識人心裏有什麼。