< Yohana 16 >

1 “Nimewaambieni hayo kusudi msiiache imani yenu.
Je vous ai dit ces choses, afin que vous ne vous scandalisiez point.
2 Watu watawatenga ninyi na masunagogi yao. Tena, wakati unakuja ambapo kila atakayewaua ninyi atadhani anamhudumia Mungu.
Ils vous chasseront des synagogues; l'heure même vient où quiconque vous fera mourir croira rendre un culte à Dieu.
3 Watawatendeeni mambo hayo kwa sababu hawamjui Baba, wala hawanijui mimi.
Et ils vous feront cela, parce qu'ils n'ont connu ni mon Père, ni moi.
4 Basi, nimewaambieni mambo haya ili saa yake itakapofika mkumbuke kwamba niliwaambieni. “Sikuwaambieni mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
Mais je vous ai dit ces choses, afin que lorsque l'heure sera venue, vous vous souveniez que je vous les ai dites. Je ne vous les ai pas dites dès le commencement, parce que j'étais avec vous.
5 Lakini sasa namwendea yule aliyenituma; na hakuna hata mmoja wenu anayeniuliza: Unakwenda wapi?
Mais maintenant je m'en vais à celui qui m'a envoyé, et aucun de vous ne me demande: Où vas-tu?
6 Kwa kuwa nimewaambieni mambo hayo mmejaa huzuni mioyoni mwenu.
Mais, parce que je vous ai dit ces choses, la tristesse a rempli votre cœur.
7 Lakini, nawaambieni ukweli: afadhali kwenu mimi niende zangu, maana nisipokwenda Msaidizi hatakuja kwenu. Lakini nikienda, basi, nitamtuma kwenu.
Toutefois, je vous dis la vérité, il vous est avantageux que je m'en aille; car si je ne m'en vais, le Consolateur ne viendra point à vous; et si je m'en vais, je vous l'enverrai.
8 Naye atakapokuja atawathibitishia walimwengu kwamba wamekosea kuhusu dhambi, uadilifu na hukumu ya Mungu.
Et quand il sera venu, il convaincra le monde de péché, de justice et de jugement:
9 Wamekosea kuhusu dhambi kwa sababu hawaniamini;
De péché, parce qu'ils ne croient point en moi;
10 kuhusu uadilifu, kwa sababu naenda zangu kwa Baba, nanyi hamtaniona tena;
De justice, parce que je m'en vais à mon Père, et que vous ne me verrez plus;
11 kuhusu hukumu kwa sababu mkuu wa ulimwengu huu amekwisha hukumiwa.
De jugement, parce que le prince de ce monde est déjà jugé.
12 “Ninayo bado mengi ya kuwaambieni, ila kwa sasa hamwezi kuyastahimili.
J'ai encore plusieurs choses à vous dire; mais elles sont encore au-dessus de votre portée.
13 Lakini atakapokuja huyo Roho wa kweli atawaongoza kwenye ukweli wote; maana hatasema kwa mamlaka yake mwenyewe, bali atawaambieni yote atakayosikia, na atasema mambo yatakayokuwa yanakuja.
Mais quand celui-là, l'Esprit de vérité, sera venu, il vous conduira dans toute la vérité, car il ne parlera point par lui-même, mais il dira tout ce qu'il aura entendu, et vous annoncera les choses à venir.
14 Yeye atanitukuza mimi kwa kuwa atawaambieni yale atakayopata kutoka kwangu.
C'est lui qui me glorifiera, parce qu'il prendra de ce qui est à moi, et qu'il vous l'annoncera.
15 Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu; ndiyo maana nimesema kwamba huyo Roho Mtakatifu atawaambieni yale atakayopata kutoka kwangu.
Tout ce que le Père a, est à moi; c'est pourquoi j'ai dit qu'il prendra de ce qui est à moi, et qu'il vous l'annoncera.
16 “Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona!”
Encore un peu de temps et vous ne me verrez plus; et de nouveau, un peu après, vous me verrez, parce que je m'en vais au Père.
17 Hapo baadhi ya wanafunzi wake wakaulizana, “Ana maana gani anapotwambia: Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona? Tena anasema: Kwa kuwa ninakwenda kwa Baba!”
Et quelques-uns de ses disciples se dirent les uns aux autres: Qu'est-ce qu'il nous dit: Dans peu de temps vous ne me verrez plus, et: De nouveau, un peu après, vous me verrez; et: Parce que je m'en vais au Père?
18 Basi, wakawa wanaulizana, “Ana maana gani anaposema: Bado kitambo kidogo? Hatuelewi anaongelea nini.”
Ils disaient donc: Qu'est-ce qu'il dit: Dans peu de temps? Nous ne savons ce qu'il dit.
19 Yesu alijua kwamba walitaka kumwuliza, basi akawaambia, “Je, mnaulizana juu ya yale niliyosema: Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona?
Jésus donc, connaissant qu'ils voulaient l'interroger, leur dit: Vous vous interrogez les uns les autres sur ce que j'ai dit: Dans peu de temps vous ne me verrez plus; et de nouveau, un peu après, vous me verrez.
20 Nawaambieni kweli, ninyi mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utafurahi: mtaona huzuni lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.
En vérité, en vérité je vous dis, que vous pleurerez, et vous vous lamenterez, et le monde se réjouira; vous serez dans la tristesse; mais votre tristesse sera changée en joie.
21 Wakati mama anapojifungua huona huzuni kwa sababu saa ya maumivu imefika; lakini akisha jifungua hayakumbuki tena maumivu hayo kwa sababu ya furaha kwamba mtu amezaliwa duniani.
Quand une femme accouche, elle a des douleurs, parce que son terme est venu; mais dès qu'elle est accouchée d'un enfant, elle ne se souvient plus de son travail, à cause de sa joie de ce qu'un homme est né dans le monde.
22 Ninyi pia mna huzuni sasa; lakini nitawajieni tena, nanyi mtajaa furaha mioyoni mwenu, na furaha hiyo hakuna mtu atakayeiondoa kwenu.
De même, vous êtes maintenant dans la tristesse; mais je vous verrai de nouveau, et votre cœur se réjouira, et personne ne vous ravira votre joie.
23 Siku hiyo hamtaniomba chochote. Kweli nawaambieni, chochote mtakachomwomba Baba kwa jina langu, atawapeni.
Et en ce jour-là vous ne m'interrogerez plus sur rien. En vérité, en vérité je vous dis, que tout ce que vous demanderez au Père en mon nom, il vous le donnera.
24 Mpaka sasa hamjaomba chochote kwa jina langu. Ombeni nanyi mtapata ili furaha yenu ikamilike.
Jusqu'à présent vous n'avez rien demandé en mon nom; demandez, et vous recevrez, afin que votre joie soit accomplie.
25 “Nimewaambieni mambo hayo kwa mafumbo. Lakini wakati utakuja ambapo sitasema tena nanyi kwa mafumbo, bali nitawaambieni waziwazi juu ya Baba.
Je vous ai dit ces choses en similitudes; mais le temps vient que je ne vous parlerai plus en similitudes, mais je vous parlerai ouvertement du Père.
26 Siku hiyo mtaomba kwa jina langu, na siwaambii kwamba nitamwomba Baba kwa niaba yenu;
En ce jour vous demanderez en mon nom, et je ne vous dis point que je prierai le Père pour vous,
27 maana yeye mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu ninyi mmenipenda mimi na mmeamini kwamba nimetoka kwa Mungu.
Car le Père lui-même vous aime, parce que vous m'avez aimé, et que vous avez cru que je suis issu de Dieu.
28 Mimi nilitoka kwa Baba, nikaja ulimwenguni; na sasa nauacha ulimwengu na kurudi kwa Baba.”
Je suis issu du Père, et je suis venu dans le monde; je laisse de nouveau le monde, et je vais au Père.
29 Basi, wanafunzi wake wakamwambia, “Ahaa! Sasa unasema waziwazi kabisa bila kutumia mafumbo.
Ses disciples lui dirent: Voici, maintenant tu parles ouvertement, et tu ne dis point de similitude.
30 Sasa tunajua kwamba wewe unajua kila kitu, na huna haja ya kuulizwa maswali na mtu yeyote; kwa hiyo tunaamini kwamba umetoka kwa Mungu.”
Maintenant nous savons que tu sais toutes choses, et que tu n'as pas besoin que personne t'interroge; c'est pour cela que nous croyons que tu es issu de Dieu.
31 Yesu akawajibu, “Je, mnaamini sasa?
Jésus leur répondit: Vous croyez maintenant?
32 Wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo ninyi nyote mtatawanyika kila mtu kwake, nami nitaachwa peke yangu. Kumbe, lakini mimi siko peke yangu, maana Baba yu pamoja nami.
Voici, l'heure vient, et elle est déjà venue, que vous serez dispersés chacun de son côté, et que vous me laisserez seul; mais je ne suis pas seul, parce que mon Père est avec moi.
33 Nimewaambieni mambo haya ili mpate kuwa na amani katika kuungana nami. Ulimwenguni mtapata masumbuko; lakini jipeni moyo! Mimi nimeushinda ulimwengu!”
Je vous ai dit ces choses, afin que vous ayez la paix en moi; vous aurez des afflictions dans le monde; mais prenez courage, j'ai vaincu le monde.

< Yohana 16 >