< Yohana 13 >
1 Ilikuwa kabla ya sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua kwamba saa yake ya kuondoka ulimwenguni na kwenda kwa Baba ilikuwa imefika. Alikuwa amewapenda daima watu wake walioko duniani; naam, aliwapenda mpaka mwisho!
Now before the feast of the Passover, Yeshua, knowing that his time had come that he would depart from this world to the Father, having loved his own who were in the world, he loved them to the end.
2 Basi, Yesu na wanafunzi wake walikuwa mezani kwa chakula cha jioni. Ibilisi alikwisha mtia Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti, nia ya kumsaliti Yesu.
And during the meal, the devil had already put into the heart of Judah the Iskriot, Shim'on's son, to betray him.
3 Yesu alijua kwamba Baba alikuwa amemkabidhi kila kitu, na kwamba alikuwa ametoka kwa Mungu na anarudi kwa Mungu.
Because he knew that the Father had given all things into his hands, and that he came forth from God, and was going to God,
4 Basi, Yesu aliondoka mezani, akaweka kando vazi lake, akachukua kitambaa na kujifunga kiunoni.
arose from the meal, and removed his outer garments. He took a towel, and wrapped a towel around his waist.
5 Kisha akatia maji katika bakuli, akaanza kuwaosha wanafunzi wake miguu na kuipangusa kwa kile kitambaa alichojifungia.
Then he poured water into the basin, and began to wash the talmidim' feet, and to wipe them with the towel that was wrapped around him.
6 Basi, akamfikia Simoni Petro; naye Petro akasema, “Bwana, wewe utaniosha miguu mimi?”
Then he came to Shim'on Peter. He said to him, "Lord, do you wash my feet?"
7 Yesu akamjibu, “Huelewi sasa ninachofanya lakini utaelewa baadaye.”
Yeshua answered him, "You do not know what I am doing now, but you will understand later."
8 Petro akamwambia, “Wewe hutaniosha miguu kamwe!” Yesu akamjibu, “Nisipokuosha hutakuwa na uhusiano nami tena.” (aiōn )
Peter said to him, "You will never wash my feet." Yeshua answered him, "If I do not wash you, you have no part with me." (aiōn )
9 Simoni Petro akamwambia, “Bwana, nioshe, si miguu tu, bali na mikono yangu na kichwa pia.”
Shim'on Peter said to him, "Lord, not my feet only, but also my hands and my head."
10 Yesu akamwambia, “Aliyekwisha oga hana lazima ya kunawa isipokuwa miguu, maana amekwisha takata mwili wote. Ninyi mmetakata, lakini si nyote.”
Yeshua said to him, "Someone who has bathed only needs to have his feet washed, but is completely clean. You are clean, but not all of you."
11 (Yesu alimjua yule ambaye atamsaliti, ndiyo maana alisema: “Ninyi mmetakata, lakini si nyote.”)
For he knew him who would betray him, therefore he said, "You are not all clean."
12 Alipokwisha waosha miguu na kuvaa tena vazi lake, aliketi mezani, akawaambia, “Je, mmeelewa hayo niliyowatendeeni?
So when he had washed their feet, put his outer garment back on, and sat down again, he said to them, "Do you know what I have done to you?
13 Ninyi mwaniita Mwalimu na Bwana, nanyi mwasema vyema, kwa kuwa ndimi.
You call me, 'Teacher' and 'Lord.' You say so correctly, for so I am.
14 Basi, ikiwa mimi niliye Bwana na Mwalimu, nimewaosha ninyi miguu, nanyi pia mnapaswa kuoshana miguu.
If I then, the Lord and the Teacher, have washed your feet, you also ought to wash one another's feet.
15 Nimewapeni mfano, ili nanyi pia mfanye kama nilivyowafanyieni.
For I have given you an example, that you also should do as I have done to you.
16 Kweli nawaambieni, mtumishi si mkuu zaidi kuliko bwana wake, wala mtume si mkuu zaidi kuliko yule aliyemtuma.
Truly, truly, I tell you, a servant is not greater than his master, neither one who is sent greater than he who sent him.
17 Basi, ikiwa mwayajua hayo, mtakuwa na heri mkiyatekeleza.
If you know these things, blessed are you if you do them.
18 “Haya nisemayo hayawahusu ninyi nyote. Mimi nawajua wale niliowachagua. Lakini lazima yatimie Maandiko Matakatifu yasemayo: Yule aliyeshiriki chakula changu amegeuka kunishambulia.
I do not speak concerning all of you. I know whom I have chosen. But that the Scripture may be fulfilled, 'He who ate my bread has lifted up his heel against me.'
19 Mimi nimewaambieni mambo haya sasa kabla hayajatokea, ili yatakapotokea mpate kuamini kuwa mimi ndimi.
I am telling you this now before it happens, so that when it does happen you may believe that I am he.
20 Kweli nawaambieni anayempokea yule ninayemtuma anaponipokea mimi; na anayenipokea mimi, anampokea yule aliyenituma.”
Truly, truly, I tell you, he who receives whomever I send, receives me; and he who receives me, receives him who sent me."
21 Alipokwisha sema hayo, Yesu alifadhaika sana rohoni, akasema wazi, “Kweli nawaambieni, mmoja wenu atanisaliti!”
When Yeshua had said this, he was troubled in spirit, and testified, "Truly, truly, I tell you that one of you will betray me."
22 Wanafunzi wakatazama wasiweze kabisa kujua anasema nani.
The talmidim looked at one another, perplexed about whom he spoke.
23 Mmoja wa wanafunzi, ambaye Yesu alikuwa anampenda sana, alikuwa ameketi karibu na Yesu.
One of his talmidim, whom Yeshua loved, was reclining against Yeshua's chest.
24 Basi, Simoni Petro akamwashiria na kusema: “Mwulize anasema juu ya nani.”
Shim'on Peter therefore motioned to him to inquire who it was he was talking about.
25 Mwanafunzi huyo akasogea karibu zaidi na Yesu, akamwuliza, “Bwana, ni nani?”
He, leaning back, as he was, on Yeshua's chest, asked him, "Lord, who is it?"
26 Yesu akajibu, “Yule nitakayempa kipande cha mkate nilichochovya katika sahani, ndiye.” Basi, akatwaa kipande cha mkate, akakichovya katika sahani, akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti.
Yeshua therefore answered, "It is he to whom I will give this piece of matzah when I have dipped it." So when he had dipped the piece of matzah, he gave it to Judah, the son of Shim'on the Iskriot.
27 Yuda alipokwisha pokea kipande hicho, Shetani akamwingia. Basi Yesu akamwambia, “Unachotaka kufanya, kifanye haraka!”
After the piece of matzah, then Satan entered into him. Then Yeshua said to him, "What you do, do quickly."
28 Lakini hakuna hata mmoja wa wale waliokaa pale mezani aliyefahamu kwa nini alikuwa amemwambia hivyo.
Now none of those reclining knew why he said this to him.
29 Kwa kuwa Yuda alikuwa na wajibu wa kuutunza mfuko wa fedha, baadhi yao walidhani kwamba Yesu alikuwa amemwambia anunue vilivyohitajiwa kwa sikukuu, au kwamba alikuwa amemwambia akatoe chochote kwa maskini.
For some thought, because Judah had the money box, that Yeshua said to him, "Buy what things we need for the feast," or that he should give something to the poor.
30 Basi, Yuda alipokwisha twaa kile kipande cha mkate, akatoka nje mara. Na ilikuwa usiku.
Therefore, having received the piece of matzah, he went out immediately; and it was night.
31 Baada ya Yuda kuondoka, Yesu akasema, “Sasa Mwana wa Mtu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake.
When he had gone out, Yeshua said, "Now the Son of Man has been glorified, and God has been glorified in him.
32 Na kama utukufu wa Mungu umefunuliwa ndani ya Mwana, basi, naye Mungu ataudhihirisha utukufu wa Mwana ndani yake mwenyewe, na atafanya hivyo mara.
If God has been glorified in him, God will also glorify him in himself, and he will glorify him at once.
33 “Watoto wangu, bado niko nanyi kwa muda mfupi tu. Mtanitafuta, lakini sasa nawaambieni yale niliyowaambia viongozi wa Wayahudi: Niendako ninyi hamwezi kwenda!
Little children, I will be with you a little while longer. You will seek me, and as I said to the Jewish leaders, 'Where I am going, you cannot come,' so now I tell you.
34 Nawapeni amri mpya: pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda ninyi.
A new commandment I give to you, that you love one another. Just as I have loved you, you also must love one another.
35 Mkipendana, watu wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu.”
By this everyone will know that you are my talmidim, if you have love for one another."
36 Simoni Petro akamwuliza, “Bwana, unakwenda wapi?” Yesu akajibu, “Niendako huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye.”
Shim'on Peter said to him, "Lord, where are you going?" Yeshua answered, "Where I am going, you cannot follow now, but you will follow afterwards."
37 Petro akamwambia “Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Niko tayari kufa kwa ajili yako!”
Peter said to him, "Lord, why can I not follow you now? I will lay down my life for you."
38 Yesu akajibu, “Je, uko tayari kweli kufa kwa ajili yangu? Kweli nakwambia, kabla jogoo hajawika utanikana mara tatu!”
Yeshua answered him, "Will you lay down your life for me? Truly, truly, I tell you, the rooster won't crow until you have denied me three times.