< Yohana 13 >

1 Ilikuwa kabla ya sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua kwamba saa yake ya kuondoka ulimwenguni na kwenda kwa Baba ilikuwa imefika. Alikuwa amewapenda daima watu wake walioko duniani; naam, aliwapenda mpaka mwisho!
And before the feast of the passover, Jesus knowing that the hour has come when He must depart out of this world to His Father, having loved His own who were in the world, with divine love, He loved them perfectly.
2 Basi, Yesu na wanafunzi wake walikuwa mezani kwa chakula cha jioni. Ibilisi alikwisha mtia Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti, nia ya kumsaliti Yesu.
And the supper being on hand, the devil already having entered into the heart, that Judas Iscariot, the son of Simon, should betray Him,
3 Yesu alijua kwamba Baba alikuwa amemkabidhi kila kitu, na kwamba alikuwa ametoka kwa Mungu na anarudi kwa Mungu.
knowing that the Father has given all things into His hands, and He came out from God, and is going away to God,
4 Basi, Yesu aliondoka mezani, akaweka kando vazi lake, akachukua kitambaa na kujifunga kiunoni.
He rises from the supper, and lays aside His garments, and taking a towel, girded Himself;
5 Kisha akatia maji katika bakuli, akaanza kuwaosha wanafunzi wake miguu na kuipangusa kwa kile kitambaa alichojifungia.
then He pours water into a bowl, and began to wash the feet of the disciples, and to wipe them with the towel with which He was girded.
6 Basi, akamfikia Simoni Petro; naye Petro akasema, “Bwana, wewe utaniosha miguu mimi?”
Then He comes to Simon Peter; he says to Him; Lord, do you wash my feet?
7 Yesu akamjibu, “Huelewi sasa ninachofanya lakini utaelewa baadaye.”
Jesus responded and said to him, What I do you know not now; but shall understand hereafter.
8 Petro akamwambia, “Wewe hutaniosha miguu kamwe!” Yesu akamjibu, “Nisipokuosha hutakuwa na uhusiano nami tena.” (aiōn g165)
Peter says to Him, You may never wash my feet. Jesus responded to him, If I wash thee not, thou hast not part with me. (aiōn g165)
9 Simoni Petro akamwambia, “Bwana, nioshe, si miguu tu, bali na mikono yangu na kichwa pia.”
And Simon Peter says to Him, Lord, not only my feet, but my hands and my head.
10 Yesu akamwambia, “Aliyekwisha oga hana lazima ya kunawa isipokuwa miguu, maana amekwisha takata mwili wote. Ninyi mmetakata, lakini si nyote.”
Jesus says to Him, He that is bathed hath no need to wash his hands, but is altogether clean: and you are clean, but not all.
11 (Yesu alimjua yule ambaye atamsaliti, ndiyo maana alisema: “Ninyi mmetakata, lakini si nyote.”)
For He knew the one betraying Him. On this account He said, You are not all clean.
12 Alipokwisha waosha miguu na kuvaa tena vazi lake, aliketi mezani, akawaambia, “Je, mmeelewa hayo niliyowatendeeni?
Then when He washed their feet, and took His garments, and sat down again, He said to them, Do you understand what I have done to you?
13 Ninyi mwaniita Mwalimu na Bwana, nanyi mwasema vyema, kwa kuwa ndimi.
You call me Master and Lord, and you speak beautifully; for I am.
14 Basi, ikiwa mimi niliye Bwana na Mwalimu, nimewaosha ninyi miguu, nanyi pia mnapaswa kuoshana miguu.
If then I, your Lord and Master, washed your feet, you ought also to wash the feet of one another.
15 Nimewapeni mfano, ili nanyi pia mfanye kama nilivyowafanyieni.
For I have given unto you an example, that you may also do as I have done to you.
16 Kweli nawaambieni, mtumishi si mkuu zaidi kuliko bwana wake, wala mtume si mkuu zaidi kuliko yule aliyemtuma.
Truly, truly, I say unto you, The servant is not greater than his lord; nor the apostle greater than him that sent him.
17 Basi, ikiwa mwayajua hayo, mtakuwa na heri mkiyatekeleza.
If you know these things, happy are ye if you may do them.
18 “Haya nisemayo hayawahusu ninyi nyote. Mimi nawajua wale niliowachagua. Lakini lazima yatimie Maandiko Matakatifu yasemayo: Yule aliyeshiriki chakula changu amegeuka kunishambulia.
I do not speak concerning you all: I know whom I have chosen: but that the Scripture may be fulfilled, He that eateth bread with me has lifted up his heel against me.
19 Mimi nimewaambieni mambo haya sasa kabla hayajatokea, ili yatakapotokea mpate kuamini kuwa mimi ndimi.
Now I tell you before it takes place, in order that you may believe, when it may be done, that I am He.
20 Kweli nawaambieni anayempokea yule ninayemtuma anaponipokea mimi; na anayenipokea mimi, anampokea yule aliyenituma.”
Truly, truly, I say unto you, The one receiving the one whom I may send, receiveth me; and the one receiving me, receives Him that sent me.
21 Alipokwisha sema hayo, Yesu alifadhaika sana rohoni, akasema wazi, “Kweli nawaambieni, mmoja wenu atanisaliti!”
Jesus saying these things, was troubled in spirit, and testified, and said; Truly, truly, I say unto you, that one of you shall betray me.
22 Wanafunzi wakatazama wasiweze kabisa kujua anasema nani.
Then the disciples began to look to one another, being at a loss concerning which one He speaks.
23 Mmoja wa wanafunzi, ambaye Yesu alikuwa anampenda sana, alikuwa ameketi karibu na Yesu.
And one of His disciples, whom Jesus loved, was leaning on the bosom of Jesus.
24 Basi, Simoni Petro akamwashiria na kusema: “Mwulize anasema juu ya nani.”
Then Simon Peter beckons to him, to ask who he might be concerning whom He speaks.
25 Mwanafunzi huyo akasogea karibu zaidi na Yesu, akamwuliza, “Bwana, ni nani?”
And that one, falling toward the bosom of Jesus says to Him, Lord, who is he?
26 Yesu akajibu, “Yule nitakayempa kipande cha mkate nilichochovya katika sahani, ndiye.” Basi, akatwaa kipande cha mkate, akakichovya katika sahani, akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti.
And Jesus responds, He is that one to whom, having dipped the morsel, I will give it. And having dipped the morsel, He takes it, and gives it to Judas Iscariot, the son of Simon.
27 Yuda alipokwisha pokea kipande hicho, Shetani akamwingia. Basi Yesu akamwambia, “Unachotaka kufanya, kifanye haraka!”
And after the morsel, Satan entered into him. Then Jesus says to him; What thou art doing, do more quickly.
28 Lakini hakuna hata mmoja wa wale waliokaa pale mezani aliyefahamu kwa nini alikuwa amemwambia hivyo.
And no one of those sitting with Him knew what He said to him:
29 Kwa kuwa Yuda alikuwa na wajibu wa kuutunza mfuko wa fedha, baadhi yao walidhani kwamba Yesu alikuwa amemwambia anunue vilivyohitajiwa kwa sikukuu, au kwamba alikuwa amemwambia akatoe chochote kwa maskini.
for some thought, as Judas had the purse, that Jesus says to him, Purchase some of those things of which we have need at the supper; or something that he might give to the poor.
30 Basi, Yuda alipokwisha twaa kile kipande cha mkate, akatoka nje mara. Na ilikuwa usiku.
Then he having taken the morsel, went out immediately: and it was night.
31 Baada ya Yuda kuondoka, Yesu akasema, “Sasa Mwana wa Mtu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake.
Then when he went out, Jesus says, Now is the Son of man glorified, and God is glorified in Him.
32 Na kama utukufu wa Mungu umefunuliwa ndani ya Mwana, basi, naye Mungu ataudhihirisha utukufu wa Mwana ndani yake mwenyewe, na atafanya hivyo mara.
And if God is glorified in Him, God will indeed glorify Him in Himself, and will glorify Him immediately.
33 “Watoto wangu, bado niko nanyi kwa muda mfupi tu. Mtanitafuta, lakini sasa nawaambieni yale niliyowaambia viongozi wa Wayahudi: Niendako ninyi hamwezi kwenda!
Children, I am still with you. You shall seek me, and as I said to the Jews, Whither I go, you are not able to come; and now I say to you.
34 Nawapeni amri mpya: pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda ninyi.
I give unto a new commandment, That you must love one another with divine love; as I have loved you with divine love, that you must also love one another with divine love:
35 Mkipendana, watu wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu.”
in this shall all know that you are my disciples, if you may have divine love one with another.
36 Simoni Petro akamwuliza, “Bwana, unakwenda wapi?” Yesu akajibu, “Niendako huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye.”
Simon Peter says to Him; Lord, whither do you go? Jesus responded, Whither I go you are not able to follow me now; but shall follow me hereafter.
37 Petro akamwambia “Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Niko tayari kufa kwa ajili yako!”
Peter says to Him; Lord, why am I not able to follow thee now? I will lay down my soul for thee.
38 Yesu akajibu, “Je, uko tayari kweli kufa kwa ajili yangu? Kweli nakwambia, kabla jogoo hajawika utanikana mara tatu!”
Jesus responds to him, Wilt thou lay down thy soul for me? Truly, truly, I say unto thee, that the cock shall not crow, until thou shalt thrice deny me.

< Yohana 13 >