< Yohana 12 >
1 Siku sita kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu alifika Bethania alikoishi Lazaro ambaye Yesu alikuwa amemfufua kutoka wafu.
Then, six days before the Passover, Jesus came to Bethany, where Lazarus was (the deceased whom He raised from the dead).
2 Huko walimwandalia chakula cha jioni, naye Martha akawa anawatumikia. Lazaro alikuwa mmoja wa wale waliokuwa mezani pamoja na Yesu.
So they gave a dinner for Him there—Martha was serving, while Lazarus was one of those reclining at the table with Him.
3 Basi, Maria alichukua chupa ya marashi ya nardo safi ya thamani kubwa, akampaka Yesu miguu na kuipangusa kwa nywele zake. Nyumba yote ikajaa harufu ya marashi.
Then Mary, bringing a pound of pure oil of nard, very costly, anointed Jesus' feet, and wiped His feet with her hair! And the house was filled with the fragrance of the oil.
4 Basi, Yuda Iskarioti, mmoja wa wale kumi na wawili ambaye ndiye atakayemsaliti Yesu, akasema,
Then one of His disciples, Judas Iscariot, Simon's son (who was about to betray Him), said,
5 “Kwa nini marashi hayo hayakuuzwa kwa fedha dinari mia tatu, wakapewa maskini?”
“Why wasn't this oil sold for 300 denarii and given to the poor?”
6 Alisema hivyo, si kwa kuwa alijali chochote juu ya maskini, bali kwa sababu alikuwa mweka hazina, na kwa kuwa alikuwa mwizi, mara kwa mara aliiba kutoka katika hiyo hazina.
(Now he did not say this because the poor mattered to him, but because he was a thief and had the money box; and used to pilfer what was put in it.)
7 Lakini Yesu akasema, “Msimsumbue huyu mama! Mwacheni ayaweke kwa ajili ya siku ya mazishi yangu.
So Jesus said: “Let her be; she has performed this with a view to my burial.
8 Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini hamtakuwa nami siku zote.”
For you always have the poor with you, but you do not always have me.”
9 Wayahudi wengi walisikia kwamba Yesu alikuwa Bethania. Basi, wakafika huko si tu kwa ajili ya kumwona Yesu, ila pia wapate kumwona Lazaro ambaye Yesu alimfufua kutoka wafu.
Then a large crowd of the Jews learned that He was there; and they came, not only because of Jesus but also to see Lazarus, whom He had raised from the dead.
10 Makuhani wakuu waliamua pia kumwua Lazaro,
So the chief priests decided to kill Lazarus as well,
11 Maana kwa sababu ya Lazaro Wayahudi wengi waliwaasi viongozi wao, wakamwamini Yesu.
in that because of him many of the Jews were defecting and believing into Jesus.
12 Kesho yake, kundi kubwa la watu waliokuja kwenye sikukuu walisikia kuwa Yesu alikuwa njiani kuja Yerusalemu.
The next day a large crowd that had come to the feast, when they heard that Jesus was coming into Jerusalem,
13 Basi, wakachukua matawi ya mitende, wakatoka kwenda kumlaki; wakapaaza sauti wakisema: “Hosana! Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana. Abarikiwe mfalme wa Israeli.”
took branches from palm trees and went out to meet Him. And they started shouting: “Hosanna!” “Blessed is He who comes in the name of the Lord!” “King of Israel!”
14 Yesu akampata mwana punda mmoja akapanda juu yake kama yasemavyo Maandiko:
And finding a young donkey Jesus sat on it; just as it is written:
15 “Usiogope mji wa Sioni! Tazama, Mfalme wako anakuja, Amepanda mwana punda.”
“Fear no more, daughter of Zion. Look, your King is coming, sitting on a donkey's colt!”
16 Wakati huo wanafunzi wake hawakuelewa mambo hayo, lakini Yesu alipokwisha tukuzwa, ndipo walipokumbuka kwamba hayo yalikuwa yameandikwa juu yake, na kwamba watu walikuwa wamemtendea hivyo.
(Now His disciples did not understand these things at first; but when Jesus was glorified, then they remembered that these things were written about Him, and they had done them to Him.)
17 Kundi la watu wale waliokuwa pamoja naye wakati alipomwita Lazaro kutoka kaburini, akamfufua kutoka wafu, walisema yaliyotukia.
So the crowd that had been with Him when He called Lazarus out of the tomb and raised him from the dead continued to testify.
18 Kwa hiyo umati huo wa watu ulimlaki, maana wote walisikia kwamba Yesu alikuwa amefanya ishara hiyo.
That is also why the crowd met Him, because they heard that He had performed this sign.
19 Basi, Mafarisayo wakaambiana, “Mnaona? Hatuwezi kufanya chochote! Tazameni, ulimwengu wote unamfuata.”
So the Pharisees said among themselves: “You can see that you are not making any difference! Just look, the world has gone off after Him!”
20 Kulikuwa na Wagiriki kadhaa miongoni mwa watu waliokuwa wamefika Yerusalemu kuabudu wakati wa sikukuu hiyo.
Now there were some Greeks among those who went up to worship at the feast.
21 Hao walimwendea Filipo, mwenyeji wa Bethsaida katika Galilaya, wakasema, “Mheshimiwa, tunataka kumwona Yesu.”
So these men approached Philip, who was from Bethsaida in Galilee, and requested of him saying, “Sir, we want to see Jesus.”
22 Filipo akaenda akamwambia Andrea, nao wawili wakaenda kumwambia Yesu.
Philip goes and tells Andrew, and in turn Andrew and Philip tell Jesus.
23 Yesu akawaambia, “Saa ya kutukuzwa kwa Mwana wa Mtu imefika!
But Jesus answered them saying: “The hour has come for the Son of the Man to be glorified.
24 Kweli nawaambieni, punje ya ngano hubaki punje tu isipokuwa ikianguka katika udongo na kufa. Kama ikifa, basi huzaa matunda mengi.
Most assuredly I say to you, if a grain of wheat, having fallen into the ground, does not die, it remains alone; but if it dies it bears a lot of fruit.
25 Anayependa maisha yake, atayapoteza; anayeyachukia maisha yake katika ulimwengu huu, atayaweka kwa ajili ya uzima wa milele. (aiōnios )
The one ‘loving’ his life will waste it, and the one ‘hating’ his life, in this world, will preserve it into eternal life. (aiōnios )
26 Anayetaka kunitumikia ni lazima anifuate, hivyo kwamba popote pale nilipo mimi ndipo na mtumishi wangu atakapokuwa. Mtu yeyote anayenitumikia Baba yangu atampa heshima.
If anyone would serve me, let him follow me; and where I am, my servant will be too. Further, if anyone serves me, the Father will honor him.
27 “Sasa roho yangu imefadhaika, na niseme nini? Je, niseme: Baba, usiruhusu saa hii inifikie? Lakini ndiyo maana nimekuja—ili nipite katika saa hii.
“Now my soul is distressed, and what should I say—‘Father, rescue me from this hour’? But this is why I came to this hour—
28 Baba, ulitukuze jina lako.” Hapo sauti ikasema kutoka mbinguni, “Nimelitukuza, na nitalitukuza tena.”
‘Father, glorify your name!’” Then a Voice came out of Heaven, “I have both glorified it and will glorify it again!”
29 Umati wa watu waliokuwa wamesimama hapo walisikia sauti hiyo, na baadhi yao walisema, “Malaika ameongea naye!”
So the crowd that was standing by and listening said that it had thundered. Others said, “An angel has spoken to Him.”
30 Lakini Yesu akawaambia, “Sauti hiyo haikutokea kwa ajili yangu mimi, ila kwa ajili yenu.
Jesus answered and said: “It was not for my sake that this Voice came, but for your sakes.
31 Sasa ndio wakati wa ulimwengu huu kuhukumiwa; sasa mtawala wa ulimwengu huu atapinduliwa.
Now is the judgment of this world; now the ruler of this world will be thrown out.
32 Nami nitakapoinuliwa juu ya nchi nitamvuta kila mmoja kwangu.”
While I, if I be lifted up from the earth, I will draw all people to myself.”
33 (Kwa kusema hivyo alionyesha atakufa kifo gani).
(Now He said this to indicate by what kind of death He was about to die.)
34 Basi, umati huo ukamjibu, “Sisi tunaambiwa na Sheria yetu kwamba Kristo atadumu milele. Wawezaje basi, kusema ati Mwana wa Mtu anapaswa kuinuliwa? Huyo Mwana wa Mtu ni nani?” (aiōn )
The people answered Him: “We have heard from the Law that the Messiah remains forever; and so how can you say, ‘The Son of the Man must be lifted up’? Who is this ‘the Son of the Man’?” (aiōn )
35 Yesu akawaambia, “Mwanga bado uko nanyi kwa muda mfupi. Tembeeni mngali mnao huo mwanga ili giza lisiwapate; maana atembeaye gizani hajui aendako.
Then Jesus said to them: “The Light will be with you just a little longer. Walk while you have the light, so that darkness does not overtake you; the one who walks in the darkness does not know where he is going.
36 Basi, wakati mnao huo mwanga uaminini ili mpate kuwa watu wa mwanga.” Baada ya kusema maneno hayo, Yesu alikwenda zake na kujificha mbali nao.
While you have the Light, believe into the Light, so that you may become sons of light.” Jesus said these things, and going away He was hidden from them.
37 Ingawa Yesu alifanya miujiza hii yote mbele yao, wao hawakumwamini.
Although He had performed so many signs in their presence, they were not believing into Him;
38 Hivyo maneno aliyosema nabii Isaya yakatimia: “Bwana, nani aliyeuamini ujumbe wetu? Na uwezo wa Bwana umedhihirishwa kwa nani?”
so that the word spoken by Isaiah the prophet should be fulfilled: “Lord, who has believed what we heard? And to whom has the arm of the Lord really been revealed?”
39 Hivyo hawakuweza kuamini, kwani Isaya tena alisema:
Therefore they were unable to believe, in that Isaiah said again:
40 “Mungu ameyapofusha macho yao, amezipumbaza akili zao; wasione kwa macho yao, wasielewe kwa akili zao; wala wasinigeukie, asema Bwana, ili nipate kuwaponya.”
“He has blinded their eyes and hardened their hearts, lest they should see with their eyes and understand with their hearts and should turn around, and I would heal them.”
41 Isaya alisema maneno haya kwa sababu aliuona utukufu wa Yesu, akasema habari zake.
Isaiah said these things when he saw His glory and spoke concerning Him.
42 Hata hivyo, wengi wa viongozi wa Wayahudi walimwamini Yesu. Lakini kwa sababu ya Mafarisayo, hawakumkiri hadharani kwa kuogopa kwamba watatengwa na sunagogi.
Nevertheless, even among the rulers many believed into Him, but because of the Pharisees they did not confess Him, so they would not be expelled from the synagogue;
43 Walipendelea kusifiwa na watu kuliko kusifiwa na Mungu
for they loved the praise of men more than the praise of God.
44 Kisha Yesu akasema kwa sauti kubwa, “Mtu aliyeniamini, haniamini mimi tu, ila anamwamini pia yule aliyenituma.
Jesus called out and said: “The one believing into me believes not into me but into Him who sent me.
45 Anayeniona mimi anamwona pia yule aliyenituma.
And the one seeing me sees Him who sent me.
46 Mimi ni mwanga, nami nimekuja ulimwenguni ili wote wanaoniamini wasibaki gizani.
I, Light, have come into the world so that everyone who believes into me will not remain in the darkness.
47 Anayeyasikia maneno yangu lakini hayashiki mimi sitamhukumu; maana sikuja kuhukumu ulimwengu bali kuuokoa.
Also, if someone hears my words and does not believe, I do not judge him; because I did not come to judge the world but to save the world.
48 Asiyeyashika maneno yangu anaye wa kumhukumu: neno lile nililosema ni hakimu wake siku ya mwisho.
The one who rejects me and does not receive my sayings has that which judges him—the word that I have spoken, that is what will judge him on the last day;
49 Mimi sikunena kwa mamlaka yangu mwenyewe, ila Baba aliyenituma ndiye aliyeniamuru niseme nini na niongee nini.
because I have not spoken on my own, but the Father who sent me, He gave me a command, what I should say and what I should speak.
50 Nami najua kuwa amri yake huleta uzima wa milele. Basi, mimi nasema tu yale Baba aliyoniagiza niyaseme.” (aiōnios )
And I know that His command is eternal life. So whatever I say, I say it just like the Father told me.” (aiōnios )