< Yohana 11 >

1 Mtu mmoja aitwaye Lazaro, mwenyeji wa Bethania, alikuwa mgonjwa. (Kijiji cha Bethania kilikuwa mahali walipokaa Maria na Martha, dada yake.
Now a certain man was sick, Lazarus from Bethany, of the village of Mary and her sister, Martha.
2 Maria ndiye yule aliyempaka Bwana marashi na kumpangusa kwa nywele zake. Lazaro, kaka yake, ndiye aliyekuwa mgonjwa.)
It was that Mary who had anointed the Lord with ointment and wiped his feet with her hair, whose brother Lazarus was sick.
3 Basi, hao dada wakatuma ujumbe huu kwa Yesu: “Bwana, rafiki yako ni mgonjwa!”
The sisters therefore sent to him, saying, “Lord, behold, he for whom you have great affection is sick.”
4 Yesu aliposikia hivyo akasema, “Ugonjwa huo hautaleta kifo, ila ni kwa ajili ya kumtukuza Mungu; ameugua ili kwa njia hiyo Mwana wa Mungu atukuzwe.”
But when Jesus heard it, he said, “This sickness is not to death, but for the glory of God, that God’s Son may be glorified by it.”
5 Yesu aliwapenda Martha, dada yake na Lazaro.
Now Jesus loved Martha, and her sister, and Lazarus.
6 Alipopata habari kwamba Lazaro ni mgonjwa, Yesu aliendelea kukaa mahali hapo alipokuwa kwa siku mbili zaidi.
When therefore he heard that he was sick, he stayed two days in the place where he was.
7 Kisha akawaambia wanafunzi wake, “Twendeni tena Yudea!”
Then after this he said to the disciples, “Let’s go into Judea again.”
8 Wanafunzi wakamwambia, “Mwalimu! Muda mfupi tu umepita tangu Wayahudi walipotaka kukuua kwa mawe, nawe unataka kwenda huko tena?”
The disciples asked him, “Rabbi, the Jews were just trying to stone you. Are you going there again?”
9 Yesu akajibu, “Je, saa za mchana si kumi na mbili? Basi, mtu akitembea mchana hawezi kujikwaa kwa kuwa anauona mwanga wa ulimwengu huu.
Jesus answered, “Aren’t there twelve hours of daylight? If a man walks in the day, he doesn’t stumble, because he sees the light of this world.
10 Lakini mtu akitembea usiku atajikwaa kwa maana mwanga haumo ndani yake.”
But if a man walks in the night, he stumbles, because the light isn’t in him.”
11 Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini mimi nitakwenda kumwamsha.”
He said these things, and after that, he said to them, “Our friend Lazarus has fallen asleep, but I am going so that I may awake him out of sleep.”
12 Wanafunzi wake wakamwambia, “Bwana, ikiwa amelala, basi atapona.”
The disciples therefore said, “Lord, if he has fallen asleep, he will recover.”
13 Wao walidhani kwamba alikuwa amesema juu ya kulala usingizi, kumbe alikuwa amesema juu ya kifo cha Lazaro.
Now Jesus had spoken of his death, but they thought that he spoke of taking rest in sleep.
14 Basi, Yesu akawaambia waziwazi, “Lazaro amekufa;
So Jesus said to them plainly then, “Lazarus is dead.
15 Lakini nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini. Haya, twendeni kwake.”
I am glad for your sakes that I was not there, so that you may believe. Nevertheless, let’s go to him.”
16 Thoma (aitwaye Pacha) akawaambia wanafunzi wenzake, “Twendeni nasi tukafe pamoja naye!”
Thomas therefore, who is called Didymus, said to his fellow disciples, “Let’s also go, that we may die with him.”
17 Yesu alipofika huko alikuta Lazaro amekwisha kaa kaburini kwa siku nne.
So when Jesus came, he found that he had been in the tomb four days already.
18 Kijiji cha Bethania kilikuwa karibu na Yerusalemu umbali upatao kilomita tatu.
Now Bethany was near Jerusalem, about fifteen stadia away.
19 Wayahudi wengi walikuwa wamefika kwa Martha na Maria kuwafariji kwa kifo cha kaka yao.
Many of the Jews had joined the women around Martha and Mary, to console them concerning their brother.
20 Basi, Martha aliposikia kwamba Yesu alikuwa anakuja, akaenda kumlaki; lakini Maria alibaki nyumbani.
Then when Martha heard that Jesus was coming, she went and met him, but Mary stayed in the house.
21 Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!
Therefore Martha said to Jesus, “Lord, if you would have been here, my brother wouldn’t have died.
22 Lakini najua kwamba hata sasa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”
Even now I know that whatever you ask of God, God will give you.”
23 Yesu akamwambia, “Kaka yako atafufuka.”
Jesus said to her, “Your brother will rise again.”
24 Martha akamjibu, “Najua kwamba atafufuka wakati wa ufufuo, siku ya mwisho.”
Martha said to him, “I know that he will rise again in the resurrection at the last day.”
25 Yesu akamwambia, “Mimi ndimi ufufuo na uzima. Anayeniamini mimi hata kama anakufa, ataishi:
Jesus said to her, “I am the resurrection and the life. He who believes in me will still live, even if he dies.
26 na kila anayeishi na kuniamini, hatakufa kamwe. Je, waamini hayo?” (aiōn g165)
Whoever lives and believes in me will never die. Do you believe this?” (aiōn g165)
27 Martha akamwambia, “Ndiyo Bwana! Naamini kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni.”
She said to him, “Yes, Lord. I have come to believe that you are the Christ, God’s Son, he who comes into the world.”
28 Baada ya kusema hayo, Martha alikwenda kumwita Maria, dada yake, akamwabia faraghani, “Mwalimu yuko hapa, anakuita.”
When she had said this, she went away and called Mary, her sister, secretly, saying, “The Teacher is here and is calling you.”
29 Naye aliposikia hivyo, akainuka mara, akamwendea Yesu.
When she heard this, she arose quickly and went to him.
30 Yesu alikuwa hajaingia kijijini, ila alikuwa bado mahali palepale Martha alipomlaki.
Now Jesus had not yet come into the village, but was in the place where Martha met him.
31 Basi, Wayahudi waliokuwa nyumbani pamoja na Maria wakimfariji walipomwona ameinuka na kutoka nje ghafla, walimfuata. Walidhani alikuwa anakwenda kaburini kuomboleza.
Then the Jews who were with her in the house and were consoling her, when they saw Mary, that she rose up quickly and went out, followed her, saying, “She is going to the tomb to weep there.”
32 Basi, Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa na kumwona, alipiga magoti, akamwabia, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!”
Therefore when Mary came to where Jesus was and saw him, she fell down at his feet, saying to him, “Lord, if you would have been here, my brother wouldn’t have died.”
33 Yesu alipomwona analia, na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye wanalia pia, alijawa na huzuni na kufadhaika moyoni.
When Jesus therefore saw her weeping, and the Jews weeping who came with her, he groaned in the spirit and was troubled,
34 Kisha akawauliza, “Mlimweka wapi?” Wakamwambia, “Bwana, njoo uone.”
and said, “Where have you laid him?” They told him, “Lord, come and see.”
35 Yesu akalia machozi.
Jesus wept.
36 Basi, Wayahudi wakasema, “Tazameni jinsi alivyompenda!”
The Jews therefore said, “See how much affection he had for him!”
37 Lakini baadhi yao wakasema, “Je, huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya Lazaro asife?”
Some of them said, “Couldn’t this man, who opened the eyes of him who was blind, have also kept this man from dying?”
38 Basi, Yesu akiwa amehuzunika tena moyoni, akafika kaburini. Kaburi lenyewe lilikuwa pango, na lilikuwa limefunikwa kwa jiwe.
Jesus therefore, again groaning in himself, came to the tomb. Now it was a cave, and a stone lay against it.
39 Yesu akasema, “Ondoeni hilo jiwe!” Martha, dada yake huyo aliyekufa, akamwambia, “Bwana, amekwishaanza kunuka; amekaa kaburini siku nne!”
Jesus said, “Take away the stone.” Martha, the sister of him who was dead, said to him, “Lord, by this time there is a stench, for he has been dead four days.”
40 Yesu akamwambia, “Je, sikukwambia kwamba ukiamini utaona utukufu wa Mungu?”
Jesus said to her, “Didn’t I tell you that if you believed, you would see God’s glory?”
41 Basi, wakaliondoa lile jiwe. Yesu akatazama juu mbinguni, akasema, “Nakushukuru Baba kwa kuwa wewe wanisikiliza.
So they took away the stone from the place where the dead man was lying. Jesus lifted up his eyes and said, “Father, I thank you that you listened to me.
42 Najua kwamba unanisikiliza daima. Lakini nimesema hayo kwa ajili ya watu hawa waliopo hapa ili wapate kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.”
I know that you always listen to me, but because of the multitude standing around I said this, that they may believe that you sent me.”
43 Alipokwisha sema hayo, akaita kwa sauti kubwa: “Lazaro! Toka nje!”
When he had said this, he cried with a loud voice, “Lazarus, come out!”
44 Huyo aliyekuwa amekufa akatoka nje, huku amefungwa sanda miguu na mikono, na uso wake umefunikwa. Yesu akawaambia, “Mfungueni, mkamwache aende zake.”
He who was dead came out, bound hand and foot with wrappings, and his face was wrapped around with a cloth. Jesus said to them, “Free him, and let him go.”
45 Basi, Wayahudi wengi waliokuwa wamefika kwa Maria walipoona kitendo hicho alichokifanya Yesu wakamwamini.
Therefore many of the Jews who came to Mary and saw what Jesus did believed in him.
46 Lakini baadhi yao walikwenda kwa Mafarisayo wakatoa taarifa ya jambo hilo alilofanya Yesu.
But some of them went away to the Pharisees and told them the things which Jesus had done.
47 kwa hiyo makuhani wakuu na Mafarisayo wakafanya kikao cha Baraza kuu, wakasema, “Tufanye nini? Mtu huyu anafanya ishara nyingi mno.
The chief priests therefore and the Pharisees gathered a council, and said, “What are we doing? For this man does many signs.
48 Tukimwacha tu watu wote watamwamini, nao Waroma watakuja kuliharibu Hekalu letu na taifa letu!”
If we leave him alone like this, everyone will believe in him, and the Romans will come and take away both our place and our nation.”
49 Hapo, mmoja wao aitwaye Kayafa, ambaye alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, akawaambia, “Ninyi hamjui kitu!
But a certain one of them, Caiaphas, being high priest that year, said to them, “You know nothing at all,
50 Je, hamwoni kwamba ni afadhali kwenu mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa zima liangamizwe?”
nor do you consider that it is advantageous for us that one man should die for the people, and that the whole nation not perish.”
51 Yeye hakusema hivyo kwa hiari yake mwenyewe, bali kwa vile alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, alibashiri kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa lao;
Now he didn’t say this of himself, but being high priest that year, he prophesied that Jesus would die for the nation,
52 na wala si kwa ajili yao tu, bali pia apate kuwaleta pamoja watoto wa Mungu waliotawanyika.
and not for the nation only, but that he might also gather together into one the children of God who are scattered abroad.
53 Basi, tangu siku hiyo viongozi wa Wayahudi walifanya mipango ya kumwua Yesu.
So from that day forward they took counsel that they might put him to death.
54 Kwa hiyo, Yesu hakutembea tena hadharani kati ya Wayahudi, bali alitoka hapo, akaenda mahali karibu na jangwa, katika mji uitwao Efraimu. Akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.
Jesus therefore walked no more openly amongst the Jews, but departed from there into the country near the wilderness, to a city called Ephraim. He stayed there with his disciples.
55 Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa karibu, na watu wengi walikwenda Yerusalemu ili wajitakase kabla ya sikukuu hiyo.
Now the Passover of the Jews was at hand. Many went up from the country to Jerusalem before the Passover, to purify themselves.
56 Basi, wakawa wanamtafuta Yesu; nao walipokusanyika pamoja Hekaluni wakaulizana, “Mwaonaje? Yaonekana kwamba haji kabisa kwenye sikukuu, au sivyo?”
Then they sought for Jesus and spoke with one another as they stood in the temple, “What do you think—that he isn’t coming to the feast at all?”
57 Makuhani wakuu na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba mtu akijua mahali aliko Yesu awaarifu kusudi wamtie nguvuni.
Now the chief priests and the Pharisees had commanded that if anyone knew where he was, he should report it, that they might seize him.

< Yohana 11 >