< Yohana 11 >

1 Mtu mmoja aitwaye Lazaro, mwenyeji wa Bethania, alikuwa mgonjwa. (Kijiji cha Bethania kilikuwa mahali walipokaa Maria na Martha, dada yake.
Now a certain [man] was sick, [named] Lazarus, of Bethany, the town of Mary and her sister Martha.
2 Maria ndiye yule aliyempaka Bwana marashi na kumpangusa kwa nywele zake. Lazaro, kaka yake, ndiye aliyekuwa mgonjwa.)
(It was [that] Mary who anointed the Lord with ointment, and wiped his feet with her hair, whose brother Lazarus was sick.)
3 Basi, hao dada wakatuma ujumbe huu kwa Yesu: “Bwana, rafiki yako ni mgonjwa!”
Therefore his sisters sent to him, saying, Lord, behold, he whom thou lovest is sick.
4 Yesu aliposikia hivyo akasema, “Ugonjwa huo hautaleta kifo, ila ni kwa ajili ya kumtukuza Mungu; ameugua ili kwa njia hiyo Mwana wa Mungu atukuzwe.”
When Jesus heard [that], he said, This sickness is not to death, but for the glory of God, that the Son of God may be glorified by it.
5 Yesu aliwapenda Martha, dada yake na Lazaro.
Now Jesus loved Martha, and her sister, and Lazarus.
6 Alipopata habari kwamba Lazaro ni mgonjwa, Yesu aliendelea kukaa mahali hapo alipokuwa kwa siku mbili zaidi.
When therefore he had heard that he was sick, he abode two days still in the same place where he was.
7 Kisha akawaambia wanafunzi wake, “Twendeni tena Yudea!”
Then after that he saith to [his] disciples, Let us ho into Judea again.
8 Wanafunzi wakamwambia, “Mwalimu! Muda mfupi tu umepita tangu Wayahudi walipotaka kukuua kwa mawe, nawe unataka kwenda huko tena?”
[His] disciples say to him, Master, the Jews of late sought to stone thee; and goest thou thither again?
9 Yesu akajibu, “Je, saa za mchana si kumi na mbili? Basi, mtu akitembea mchana hawezi kujikwaa kwa kuwa anauona mwanga wa ulimwengu huu.
Jesus answered, Are there not twelve hours in the day? If any man walketh in the day, he stumbleth not, because he seeth the light of this world.
10 Lakini mtu akitembea usiku atajikwaa kwa maana mwanga haumo ndani yake.”
But if a man walketh in the night, he stumbleth, because there is no light in him.
11 Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini mimi nitakwenda kumwamsha.”
These things he said: and after that he saith to them, Our friend Lazarus sleepeth; but I go that I may awake him out of sleep.
12 Wanafunzi wake wakamwambia, “Bwana, ikiwa amelala, basi atapona.”
Then said his disciples, Lord, if he sleepeth he will do well.
13 Wao walidhani kwamba alikuwa amesema juu ya kulala usingizi, kumbe alikuwa amesema juu ya kifo cha Lazaro.
Now Jesus spoke of his death: but they thought that he had spoken of taking rest in sleep.
14 Basi, Yesu akawaambia waziwazi, “Lazaro amekufa;
Then said Jesus to them plainly, Lazarus is dead.
15 Lakini nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini. Haya, twendeni kwake.”
And I am glad for your sakes that I was not there, to the intent ye may believe; nevertheless, let us go to him.
16 Thoma (aitwaye Pacha) akawaambia wanafunzi wenzake, “Twendeni nasi tukafe pamoja naye!”
Then said Thomas, who is called Didymus, to his fellow-disciples, Let us also go, that we may die with him.
17 Yesu alipofika huko alikuta Lazaro amekwisha kaa kaburini kwa siku nne.
Then when Jesus came, he found that he had lain in the grave four days already.
18 Kijiji cha Bethania kilikuwa karibu na Yerusalemu umbali upatao kilomita tatu.
(Now Bethany was nigh to Jerusalem, about fifteen furlongs distant.)
19 Wayahudi wengi walikuwa wamefika kwa Martha na Maria kuwafariji kwa kifo cha kaka yao.
And many of the Jews came to Martha and Mary, to comfort them concerning their brother.
20 Basi, Martha aliposikia kwamba Yesu alikuwa anakuja, akaenda kumlaki; lakini Maria alibaki nyumbani.
Then Martha, as soon as she heard that Jesus was coming, went and met him: but Mary sat in the house.
21 Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!
Then said Martha to Jesus, Lord, if thou hadst been here, my brother had not died.
22 Lakini najua kwamba hata sasa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”
But I know that even now, whatever thou wilt ask of God, God will give [it] thee.
23 Yesu akamwambia, “Kaka yako atafufuka.”
Jesus saith to her, Thy brother shall rise again.
24 Martha akamjibu, “Najua kwamba atafufuka wakati wa ufufuo, siku ya mwisho.”
Martha saith to him, I know that he will rise again in the resurrection at the last day.
25 Yesu akamwambia, “Mimi ndimi ufufuo na uzima. Anayeniamini mimi hata kama anakufa, ataishi:
Jesus said to her, I am the resurrection, and the life: he that believeth in me, though he were dead, yet shall he live:
26 na kila anayeishi na kuniamini, hatakufa kamwe. Je, waamini hayo?” (aiōn g165)
And whoever liveth, and believeth in me, shall never die. Believest thou this? (aiōn g165)
27 Martha akamwambia, “Ndiyo Bwana! Naamini kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni.”
She saith to him, Yes, Lord, I believe that thou art the Christ, the Son of God, who was to come into the world.
28 Baada ya kusema hayo, Martha alikwenda kumwita Maria, dada yake, akamwabia faraghani, “Mwalimu yuko hapa, anakuita.”
And when she had so said, she went and called Mary her sister secretly, saying, The Master is come, and calleth for thee.
29 Naye aliposikia hivyo, akainuka mara, akamwendea Yesu.
As soon as she heard [that], she arose quickly, and came to him.
30 Yesu alikuwa hajaingia kijijini, ila alikuwa bado mahali palepale Martha alipomlaki.
Now Jesus had not yet come into the town, but was in that place where Martha met him.
31 Basi, Wayahudi waliokuwa nyumbani pamoja na Maria wakimfariji walipomwona ameinuka na kutoka nje ghafla, walimfuata. Walidhani alikuwa anakwenda kaburini kuomboleza.
The Jews then who were with her in the house, and comforted her, when they saw Mary that she rose hastily, and went out, followed her, saying, She goeth to the grave to weep there.
32 Basi, Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa na kumwona, alipiga magoti, akamwabia, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!”
Then when Mary had come where Jesus was, and saw him, she fell down at his feet, saying to him, Lord, if thou hadst been here, my brother had not died.
33 Yesu alipomwona analia, na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye wanalia pia, alijawa na huzuni na kufadhaika moyoni.
When Jesus therefore saw her weeping, and the Jews also weeping who came with her, he groaned in the spirit, and was troubled;
34 Kisha akawauliza, “Mlimweka wapi?” Wakamwambia, “Bwana, njoo uone.”
And said, Where have ye laid him? They say to him, Lord, come and see.
35 Yesu akalia machozi.
Jesus wept.
36 Basi, Wayahudi wakasema, “Tazameni jinsi alivyompenda!”
Then said the Jews, Behold how he loved him!
37 Lakini baadhi yao wakasema, “Je, huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya Lazaro asife?”
And some of them said, Could not this man, who opened the eyes of the blind, have caused that even this man should not have died?
38 Basi, Yesu akiwa amehuzunika tena moyoni, akafika kaburini. Kaburi lenyewe lilikuwa pango, na lilikuwa limefunikwa kwa jiwe.
Jesus therefore again groaning in himself, cometh to the grave. It was a cave, and a stone lay upon it.
39 Yesu akasema, “Ondoeni hilo jiwe!” Martha, dada yake huyo aliyekufa, akamwambia, “Bwana, amekwishaanza kunuka; amekaa kaburini siku nne!”
Jesus said, Take ye away the stone. Martha, the sister of him that was dead, saith to him, Lord, by this time his body is offensive: for he hath been [dead] four days.
40 Yesu akamwambia, “Je, sikukwambia kwamba ukiamini utaona utukufu wa Mungu?”
Jesus saith to her, Said I not to thee, that if thou wouldest believe, thou shouldest see the glory of God?
41 Basi, wakaliondoa lile jiwe. Yesu akatazama juu mbinguni, akasema, “Nakushukuru Baba kwa kuwa wewe wanisikiliza.
Then they took away the stone [from the place] where the dead was laid. And Jesus lifted up [his] eyes, and said, Father, I thank thee that thou hast heard me:
42 Najua kwamba unanisikiliza daima. Lakini nimesema hayo kwa ajili ya watu hawa waliopo hapa ili wapate kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.”
And I knew that thou hearest me always: but because of the people who stand by, I said [it], that they may believe that thou hast sent me.
43 Alipokwisha sema hayo, akaita kwa sauti kubwa: “Lazaro! Toka nje!”
And when he had thus spoken, he cried with a loud voice, Lazarus, come forth.
44 Huyo aliyekuwa amekufa akatoka nje, huku amefungwa sanda miguu na mikono, na uso wake umefunikwa. Yesu akawaambia, “Mfungueni, mkamwache aende zake.”
And he that was dead came forth, bound hand and foot with grave-clothes: and his face was bound about with a napkin. Jesus saith to them, Loose him, and let him go.
45 Basi, Wayahudi wengi waliokuwa wamefika kwa Maria walipoona kitendo hicho alichokifanya Yesu wakamwamini.
Then many of the Jews who came to Mary, and had seen the things which Jesus did, believed on him.
46 Lakini baadhi yao walikwenda kwa Mafarisayo wakatoa taarifa ya jambo hilo alilofanya Yesu.
But some of them went to the Pharisees, and told them what things Jesus had done.
47 kwa hiyo makuhani wakuu na Mafarisayo wakafanya kikao cha Baraza kuu, wakasema, “Tufanye nini? Mtu huyu anafanya ishara nyingi mno.
Then the chief priests and the Pharisees convened a council, and said, What do we? for this man performeth many miracles.
48 Tukimwacha tu watu wote watamwamini, nao Waroma watakuja kuliharibu Hekalu letu na taifa letu!”
If we let him thus alone, all [men] will believe on him: and the Romans will come, and take away both our place and nation.
49 Hapo, mmoja wao aitwaye Kayafa, ambaye alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, akawaambia, “Ninyi hamjui kitu!
And one of them, [named] Caiaphas, being the high priest that same year, said to them, Ye know nothing at all,
50 Je, hamwoni kwamba ni afadhali kwenu mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa zima liangamizwe?”
Nor consider that it is expedient for us, that one man should die for the people, and that the whole nation perish not.
51 Yeye hakusema hivyo kwa hiari yake mwenyewe, bali kwa vile alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, alibashiri kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa lao;
And this he spoke not of himself: but being high priest that year, he prophesied that Jesus should die for that nation;
52 na wala si kwa ajili yao tu, bali pia apate kuwaleta pamoja watoto wa Mungu waliotawanyika.
And not for that nation only, but that also he should assemble in one the children of God that were scattered abroad.
53 Basi, tangu siku hiyo viongozi wa Wayahudi walifanya mipango ya kumwua Yesu.
Then from that day forth they took counsel together to put him to death.
54 Kwa hiyo, Yesu hakutembea tena hadharani kati ya Wayahudi, bali alitoka hapo, akaenda mahali karibu na jangwa, katika mji uitwao Efraimu. Akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.
Jesus therefore walked no more openly among the Jews; but went thence to a country near to the wilderness, into a city called Ephraim, and there continued with his disciples.
55 Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa karibu, na watu wengi walikwenda Yerusalemu ili wajitakase kabla ya sikukuu hiyo.
And the Jews' passover was nigh at hand: and many went out of the country to Jerusalem before the passover, to purify themselves.
56 Basi, wakawa wanamtafuta Yesu; nao walipokusanyika pamoja Hekaluni wakaulizana, “Mwaonaje? Yaonekana kwamba haji kabisa kwenye sikukuu, au sivyo?”
Then they sought for Jesus, and spoke among themselves, as they stood in the temple, What think ye, that he will not come to the feast?
57 Makuhani wakuu na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba mtu akijua mahali aliko Yesu awaarifu kusudi wamtie nguvuni.
Now both the chief priests and the Pharisees had given a commandment, that, if any man knew where he was, he should show [it], that they might take him.

< Yohana 11 >