< Yohana 11 >
1 Mtu mmoja aitwaye Lazaro, mwenyeji wa Bethania, alikuwa mgonjwa. (Kijiji cha Bethania kilikuwa mahali walipokaa Maria na Martha, dada yake.
Now a man named Lazarus was sick. He was from Bethany, the village of Mary and her sister Martha.
2 Maria ndiye yule aliyempaka Bwana marashi na kumpangusa kwa nywele zake. Lazaro, kaka yake, ndiye aliyekuwa mgonjwa.)
(Mary was the one who anointed the Lord with ointment and wiped his feet with her hair; it was her brother Lazarus who was sick.)
3 Basi, hao dada wakatuma ujumbe huu kwa Yesu: “Bwana, rafiki yako ni mgonjwa!”
So the sisters sent word to Jesus, “Lord, behold, the one yoʋ love is sick.”
4 Yesu aliposikia hivyo akasema, “Ugonjwa huo hautaleta kifo, ila ni kwa ajili ya kumtukuza Mungu; ameugua ili kwa njia hiyo Mwana wa Mungu atukuzwe.”
But when Jesus heard this, he said, “This sickness will not end in death but is for the glory of God, so that the Son of God may be glorified through it.”
5 Yesu aliwapenda Martha, dada yake na Lazaro.
Now Jesus loved Martha, her sister Mary, and Lazarus.
6 Alipopata habari kwamba Lazaro ni mgonjwa, Yesu aliendelea kukaa mahali hapo alipokuwa kwa siku mbili zaidi.
But when he heard that Lazarus was sick, he stayed where he was for two more days.
7 Kisha akawaambia wanafunzi wake, “Twendeni tena Yudea!”
After that he said to the disciples, “Let us go to Judea again.”
8 Wanafunzi wakamwambia, “Mwalimu! Muda mfupi tu umepita tangu Wayahudi walipotaka kukuua kwa mawe, nawe unataka kwenda huko tena?”
The disciples said to him, “Rabbi, the Jews were just recently seeking to stone yoʋ, and yet you are going there again?”
9 Yesu akajibu, “Je, saa za mchana si kumi na mbili? Basi, mtu akitembea mchana hawezi kujikwaa kwa kuwa anauona mwanga wa ulimwengu huu.
Jesus answered, “Are there not twelve hours in the day? If anyone walks in the day, he does not stumble, because he sees the light of this world.
10 Lakini mtu akitembea usiku atajikwaa kwa maana mwanga haumo ndani yake.”
But if anyone walks in the night, he stumbles, because the light is not in him.”
11 Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini mimi nitakwenda kumwamsha.”
After saying this, he said to them, “Our friend Lazarus has fallen asleep, but I am going there to wake him up.”
12 Wanafunzi wake wakamwambia, “Bwana, ikiwa amelala, basi atapona.”
His disciples said, “Lord, if he has fallen asleep, he will recover.”
13 Wao walidhani kwamba alikuwa amesema juu ya kulala usingizi, kumbe alikuwa amesema juu ya kifo cha Lazaro.
(They thought Jesus was speaking about natural sleep, but he was actually speaking about Lazarus' death.)
14 Basi, Yesu akawaambia waziwazi, “Lazaro amekufa;
Then Jesus told them plainly, “Lazarus has died,
15 Lakini nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini. Haya, twendeni kwake.”
and I rejoice for your sake that I was not there, so that you may believe. But let us go to him.”
16 Thoma (aitwaye Pacha) akawaambia wanafunzi wenzake, “Twendeni nasi tukafe pamoja naye!”
Then Thomas (called Didymus) said to his fellow disciples, “Let us go too, so that we may die with him.”
17 Yesu alipofika huko alikuta Lazaro amekwisha kaa kaburini kwa siku nne.
When Jesus arrived, he found that Lazarus had been in the tomb for four days already.
18 Kijiji cha Bethania kilikuwa karibu na Yerusalemu umbali upatao kilomita tatu.
Now Bethany was less than two miles from Jerusalem,
19 Wayahudi wengi walikuwa wamefika kwa Martha na Maria kuwafariji kwa kifo cha kaka yao.
and many of the Jews had joined the women who were with Martha and Mary, to console them about their brother.
20 Basi, Martha aliposikia kwamba Yesu alikuwa anakuja, akaenda kumlaki; lakini Maria alibaki nyumbani.
When Martha heard that Jesus was coming, she went to meet him, but Mary remained seated in the house.
21 Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!
Then Martha said to Jesus, “Lord, if yoʋ had been here, my brother would not have died.
22 Lakini najua kwamba hata sasa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”
But even now I know that God will give yoʋ whatever yoʋ ask of him.”
23 Yesu akamwambia, “Kaka yako atafufuka.”
Jesus said to her, “Yoʋr brother will rise again.”
24 Martha akamjibu, “Najua kwamba atafufuka wakati wa ufufuo, siku ya mwisho.”
Martha said to him, “I know that he will rise again in the resurrection on the last day.”
25 Yesu akamwambia, “Mimi ndimi ufufuo na uzima. Anayeniamini mimi hata kama anakufa, ataishi:
Jesus said to her, “I am the resurrection and the life. He who believes in me, though he may die, yet shall he live.
26 na kila anayeishi na kuniamini, hatakufa kamwe. Je, waamini hayo?” (aiōn )
No one who lives and believes in me will ever die. Do yoʋ believe this?” (aiōn )
27 Martha akamwambia, “Ndiyo Bwana! Naamini kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni.”
She said to him, “Yes, Lord, I have come to believe that yoʋ are the Christ, the Son of God, who is to come into the world.”
28 Baada ya kusema hayo, Martha alikwenda kumwita Maria, dada yake, akamwabia faraghani, “Mwalimu yuko hapa, anakuita.”
After saying this, she went and called her sister Mary, saying in private, “The Teacher is here and is calling for yoʋ.”
29 Naye aliposikia hivyo, akainuka mara, akamwendea Yesu.
When Mary heard this, she rose quickly and went to him.
30 Yesu alikuwa hajaingia kijijini, ila alikuwa bado mahali palepale Martha alipomlaki.
(Now Jesus had not yet come into the village, but was in the place where Martha had met him.)
31 Basi, Wayahudi waliokuwa nyumbani pamoja na Maria wakimfariji walipomwona ameinuka na kutoka nje ghafla, walimfuata. Walidhani alikuwa anakwenda kaburini kuomboleza.
When the Jews who were in the house with Mary, consoling her, saw her rise quickly and go out, they followed her, saying, “She is going to the tomb to weep there.”
32 Basi, Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa na kumwona, alipiga magoti, akamwabia, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!”
When Mary came to where Jesus was and saw him, she fell at his feet and said to him, “Lord, if yoʋ had been here, my brother would not have died.”
33 Yesu alipomwona analia, na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye wanalia pia, alijawa na huzuni na kufadhaika moyoni.
When Jesus saw her weeping, and the Jews who had come with her also weeping, he was deeply moved in his spirit and troubled.
34 Kisha akawauliza, “Mlimweka wapi?” Wakamwambia, “Bwana, njoo uone.”
He said, “Where have you laid him?” They said to him, “Lord, come and see.”
36 Basi, Wayahudi wakasema, “Tazameni jinsi alivyompenda!”
So the Jews said, “See how he loved him!”
37 Lakini baadhi yao wakasema, “Je, huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya Lazaro asife?”
But some of them said, “Could not he who opened the eyes of the blind man have also kept this man from dying?”
38 Basi, Yesu akiwa amehuzunika tena moyoni, akafika kaburini. Kaburi lenyewe lilikuwa pango, na lilikuwa limefunikwa kwa jiwe.
Deeply moved once more, Jesus came to the tomb. (It was a cave, and a stone was lying against it.)
39 Yesu akasema, “Ondoeni hilo jiwe!” Martha, dada yake huyo aliyekufa, akamwambia, “Bwana, amekwishaanza kunuka; amekaa kaburini siku nne!”
Jesus said, “Take away the stone.” Martha, the sister of the man who had died, said to him, “Lord, there is already a stench, for it is the fourth day.”
40 Yesu akamwambia, “Je, sikukwambia kwamba ukiamini utaona utukufu wa Mungu?”
Jesus said to her, “Did I not tell yoʋ that if yoʋ believed yoʋ would see the glory of God?”
41 Basi, wakaliondoa lile jiwe. Yesu akatazama juu mbinguni, akasema, “Nakushukuru Baba kwa kuwa wewe wanisikiliza.
So they took away the stone from where the dead man was lying. Then Jesus lifted up his eyes and said, “Father, I thank yoʋ that yoʋ have heard me.
42 Najua kwamba unanisikiliza daima. Lakini nimesema hayo kwa ajili ya watu hawa waliopo hapa ili wapate kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.”
I know that yoʋ always hear me, but I say this for the benefit of the crowd that is standing here, so that they may believe that yoʋ sent me.”
43 Alipokwisha sema hayo, akaita kwa sauti kubwa: “Lazaro! Toka nje!”
After saying this, he cried out with a loud voice, “Lazarus, come out!”
44 Huyo aliyekuwa amekufa akatoka nje, huku amefungwa sanda miguu na mikono, na uso wake umefunikwa. Yesu akawaambia, “Mfungueni, mkamwache aende zake.”
Then the man who had died came out, his feet and his hands bound with strips of cloth, and his face wrapped in a cloth. Jesus said to them, “Unbind him, and let him go.”
45 Basi, Wayahudi wengi waliokuwa wamefika kwa Maria walipoona kitendo hicho alichokifanya Yesu wakamwamini.
Therefore many of the Jews who had come to Mary, and had seen what Jesus did, believed in him.
46 Lakini baadhi yao walikwenda kwa Mafarisayo wakatoa taarifa ya jambo hilo alilofanya Yesu.
But some of them went to the Pharisees and told them what Jesus had done.
47 kwa hiyo makuhani wakuu na Mafarisayo wakafanya kikao cha Baraza kuu, wakasema, “Tufanye nini? Mtu huyu anafanya ishara nyingi mno.
So the chief priests and the Pharisees convened a meeting of the Sanhedrin and said, “What are we going to do? For this man is doing many signs.
48 Tukimwacha tu watu wote watamwamini, nao Waroma watakuja kuliharibu Hekalu letu na taifa letu!”
If we allow him to continue like this, everyone will believe in him, and the Romans will come and take away our holy place and our nation.”
49 Hapo, mmoja wao aitwaye Kayafa, ambaye alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, akawaambia, “Ninyi hamjui kitu!
But one of them, Caiaphas, who was high priest that year, said to them, “You do not know anything,
50 Je, hamwoni kwamba ni afadhali kwenu mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa zima liangamizwe?”
nor do you consider that it is better for us to have one man die for the people than to have the whole nation perish.”
51 Yeye hakusema hivyo kwa hiari yake mwenyewe, bali kwa vile alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, alibashiri kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa lao;
(He said this not of his own accord, but as high priest that year he prophesied that Jesus was going to die for the nation,
52 na wala si kwa ajili yao tu, bali pia apate kuwaleta pamoja watoto wa Mungu waliotawanyika.
and not only for the nation, but also to gather together and unite the children of God scattered abroad.)
53 Basi, tangu siku hiyo viongozi wa Wayahudi walifanya mipango ya kumwua Yesu.
So from that day they plotted together to kill him.
54 Kwa hiyo, Yesu hakutembea tena hadharani kati ya Wayahudi, bali alitoka hapo, akaenda mahali karibu na jangwa, katika mji uitwao Efraimu. Akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.
Therefore Jesus no longer went around openly among the Jews. Instead, he departed from there to the region near the wilderness, to a town called Ephraim, where he spent time with his disciples.
55 Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa karibu, na watu wengi walikwenda Yerusalemu ili wajitakase kabla ya sikukuu hiyo.
Now the Passover of the Jews was near, and many people went up to Jerusalem from the countryside to purify themselves before the Passover.
56 Basi, wakawa wanamtafuta Yesu; nao walipokusanyika pamoja Hekaluni wakaulizana, “Mwaonaje? Yaonekana kwamba haji kabisa kwenye sikukuu, au sivyo?”
They were looking for Jesus and saying to one another as they stood in the temple courts, “What do you think? That he will not come to the feast at all?”
57 Makuhani wakuu na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba mtu akijua mahali aliko Yesu awaarifu kusudi wamtie nguvuni.
(Now the chief priests and the Pharisees had given an order that if anyone knew where Jesus was, he should report it, so that they could arrest him.)