< Yohana 11 >

1 Mtu mmoja aitwaye Lazaro, mwenyeji wa Bethania, alikuwa mgonjwa. (Kijiji cha Bethania kilikuwa mahali walipokaa Maria na Martha, dada yake.
Now a certain man was sick, Lazarus from Bethany, the village of Mary and her sister Martha.
2 Maria ndiye yule aliyempaka Bwana marashi na kumpangusa kwa nywele zake. Lazaro, kaka yake, ndiye aliyekuwa mgonjwa.)
It was the Mary who anointed the Lord with ointment, and wiped His feet with her hair, whose brother Lazarus was sick.
3 Basi, hao dada wakatuma ujumbe huu kwa Yesu: “Bwana, rafiki yako ni mgonjwa!”
These sisters therefore sent to Him, saying, “Lord, one You love is sick!”
4 Yesu aliposikia hivyo akasema, “Ugonjwa huo hautaleta kifo, ila ni kwa ajili ya kumtukuza Mungu; ameugua ili kwa njia hiyo Mwana wa Mungu atukuzwe.”
When Jesus heard this, He said, “This sickness won’t end in death, but for God’s glory, so that God’s Son may be glorified by it.”
5 Yesu aliwapenda Martha, dada yake na Lazaro.
Now Jesus sincerely loved Martha, and her sister, and Lazarus.
6 Alipopata habari kwamba Lazaro ni mgonjwa, Yesu aliendelea kukaa mahali hapo alipokuwa kwa siku mbili zaidi.
Yet, when He heard that Lazarus was sick, Jesus stayed where He was for two more days.
7 Kisha akawaambia wanafunzi wake, “Twendeni tena Yudea!”
After this, He said to the disciples, “Let’s go back to Judea.”
8 Wanafunzi wakamwambia, “Mwalimu! Muda mfupi tu umepita tangu Wayahudi walipotaka kukuua kwa mawe, nawe unataka kwenda huko tena?”
The disciples said to Him, “Rabbi, the Jews were just recently trying to stone You! Are You really going back there?”
9 Yesu akajibu, “Je, saa za mchana si kumi na mbili? Basi, mtu akitembea mchana hawezi kujikwaa kwa kuwa anauona mwanga wa ulimwengu huu.
Jesus answered, “Aren’t there twelve hours of daylight? Anyone who walks by day doesn’t stumble, because he sees the light of this world.
10 Lakini mtu akitembea usiku atajikwaa kwa maana mwanga haumo ndani yake.”
But anyone who walks by night stumbles, because the light isn’t in him.”
11 Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini mimi nitakwenda kumwamsha.”
After He had said this, He told them, “Our friend Lazarus has fallen asleep, but I am going there to wake him up.”
12 Wanafunzi wake wakamwambia, “Bwana, ikiwa amelala, basi atapona.”
The disciples therefore said to Him, “Lord, if he is sleeping, he will recover.”
13 Wao walidhani kwamba alikuwa amesema juu ya kulala usingizi, kumbe alikuwa amesema juu ya kifo cha Lazaro.
Now Jesus had spoken of his death, but they thought that He was talking about literal sleep.
14 Basi, Yesu akawaambia waziwazi, “Lazaro amekufa;
So Jesus told them plainly, “Lazarus is dead,
15 Lakini nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini. Haya, twendeni kwake.”
and I am glad for your sakes that I wasn’t there, so that you may believe — but let’s go to him.”
16 Thoma (aitwaye Pacha) akawaambia wanafunzi wenzake, “Twendeni nasi tukafe pamoja naye!”
Therefore Thomas, who is called the Twin, said to his fellow disciples, “Let’s go, too, that we may die with Him.”
17 Yesu alipofika huko alikuta Lazaro amekwisha kaa kaburini kwa siku nne.
When Jesus arrived, he found that Lazarus had already been in the tomb four days.
18 Kijiji cha Bethania kilikuwa karibu na Yerusalemu umbali upatao kilomita tatu.
Bethany was near Jerusalem, about fifteen stadia away,
19 Wayahudi wengi walikuwa wamefika kwa Martha na Maria kuwafariji kwa kifo cha kaka yao.
and many of the Jews had come to Martha and Mary, to comfort them concerning their brother.
20 Basi, Martha aliposikia kwamba Yesu alikuwa anakuja, akaenda kumlaki; lakini Maria alibaki nyumbani.
When Martha heard that Jesus was coming, she went out to meet him, but Mary stayed home.
21 Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!
Then Martha said to Jesus, “Lord, if You had been here, my brother wouldn’t have died.
22 Lakini najua kwamba hata sasa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”
Even now I know that God will give you whatever You ask of Him.”
23 Yesu akamwambia, “Kaka yako atafufuka.”
Jesus told her, “Your brother will rise again.”
24 Martha akamjibu, “Najua kwamba atafufuka wakati wa ufufuo, siku ya mwisho.”
Martha replied, “I know that he will rise again in the resurrection on the last day.”
25 Yesu akamwambia, “Mimi ndimi ufufuo na uzima. Anayeniamini mimi hata kama anakufa, ataishi:
Jesus told her, “I am the resurrection and the life. Whoever believes in me will live even if they die,
26 na kila anayeishi na kuniamini, hatakufa kamwe. Je, waamini hayo?” (aiōn g165)
and everyone who lives and believes in me will never die. Do you believe this?” (aiōn g165)
27 Martha akamwambia, “Ndiyo Bwana! Naamini kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni.”
“Yes, Lord,” she answered, “I have believed that You are the Christ, God’s Son, who was to come into the world.”
28 Baada ya kusema hayo, Martha alikwenda kumwita Maria, dada yake, akamwabia faraghani, “Mwalimu yuko hapa, anakuita.”
When she had said this, she went back and called Mary, her sister, saying secretly, “The Teacher is here, and is asking for you.”
29 Naye aliposikia hivyo, akainuka mara, akamwendea Yesu.
When she heard this, she arose quickly, and went to Him.
30 Yesu alikuwa hajaingia kijijini, ila alikuwa bado mahali palepale Martha alipomlaki.
Jesus had not yet entered the village, but was still at the place where Martha met Him.
31 Basi, Wayahudi waliokuwa nyumbani pamoja na Maria wakimfariji walipomwona ameinuka na kutoka nje ghafla, walimfuata. Walidhani alikuwa anakwenda kaburini kuomboleza.
The Jews who were with her in the house, consoling her, saw Mary get up quickly and go out. They followed her, saying, “She is going to the tomb to weep there.”
32 Basi, Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa na kumwona, alipiga magoti, akamwabia, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!”
When Mary came to where Jesus was, she saw Him, and fell at His feet, saying to Him, “Lord, if You had been here, my brother wouldn’t have died.”
33 Yesu alipomwona analia, na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye wanalia pia, alijawa na huzuni na kufadhaika moyoni.
When Jesus saw her weeping, and the Jews who came with her weeping, He groaned in the spirit and was troubled.
34 Kisha akawauliza, “Mlimweka wapi?” Wakamwambia, “Bwana, njoo uone.”
He asked, “Where have you laid him?” They replied, “Lord, come and see.”
35 Yesu akalia machozi.
Jesus wept.
36 Basi, Wayahudi wakasema, “Tazameni jinsi alivyompenda!”
So the Jews were saying, “See how He loved him!”
37 Lakini baadhi yao wakasema, “Je, huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya Lazaro asife?”
But some of them said, “Couldn’t this man, who opened the eyes of the blind man, have kept this man from dying?”
38 Basi, Yesu akiwa amehuzunika tena moyoni, akafika kaburini. Kaburi lenyewe lilikuwa pango, na lilikuwa limefunikwa kwa jiwe.
Then Jesus, again groaning in Himself, came to the tomb. It was a cave, and a boulder was placed against the entrance.
39 Yesu akasema, “Ondoeni hilo jiwe!” Martha, dada yake huyo aliyekufa, akamwambia, “Bwana, amekwishaanza kunuka; amekaa kaburini siku nne!”
Jesus said, “Take away the boulder.” Martha, the dead man’s sister, said to Him, “Lord, by this time there is a stench, because he has been dead four days.”
40 Yesu akamwambia, “Je, sikukwambia kwamba ukiamini utaona utukufu wa Mungu?”
Jesus told her, “Didn’t I tell you that if you would believe you would see God’s glory?”
41 Basi, wakaliondoa lile jiwe. Yesu akatazama juu mbinguni, akasema, “Nakushukuru Baba kwa kuwa wewe wanisikiliza.
Then they took the boulder away from the place where the dead man was lying. Jesus lifted up His eyes and said, “Father, I thank You that You have heard me.
42 Najua kwamba unanisikiliza daima. Lakini nimesema hayo kwa ajili ya watu hawa waliopo hapa ili wapate kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.”
I know that You always hear me, but because of the people who are standing here I said this, that they may believe that You sent me.”
43 Alipokwisha sema hayo, akaita kwa sauti kubwa: “Lazaro! Toka nje!”
Now when He had said these things, He called loudly, “Lazarus, come out!”
44 Huyo aliyekuwa amekufa akatoka nje, huku amefungwa sanda miguu na mikono, na uso wake umefunikwa. Yesu akawaambia, “Mfungueni, mkamwache aende zake.”
He who had died came out, bound hand and foot with wrappings, and his face was wrapped around with a cloth. Jesus told them, “Unbind him, and let him go.”
45 Basi, Wayahudi wengi waliokuwa wamefika kwa Maria walipoona kitendo hicho alichokifanya Yesu wakamwamini.
Then many of the Jews who had come to Mary, and had seen the things Jesus did, believed in Him.
46 Lakini baadhi yao walikwenda kwa Mafarisayo wakatoa taarifa ya jambo hilo alilofanya Yesu.
But some of them went away to the Pharisees and told them what Jesus did.
47 kwa hiyo makuhani wakuu na Mafarisayo wakafanya kikao cha Baraza kuu, wakasema, “Tufanye nini? Mtu huyu anafanya ishara nyingi mno.
Then the chief priests and the Pharisees gathered a council and said, “What are we doing? For this Man performs many signs.
48 Tukimwacha tu watu wote watamwamini, nao Waroma watakuja kuliharibu Hekalu letu na taifa letu!”
If we let Him go on like this, everyone will believe in Him, and the Romans will come and take away both our place and our nation.”
49 Hapo, mmoja wao aitwaye Kayafa, ambaye alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, akawaambia, “Ninyi hamjui kitu!
Then a certain one of them, Caiaphas, who was high priest that year, told them, “You don’t know anything,
50 Je, hamwoni kwamba ni afadhali kwenu mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa zima liangamizwe?”
nor do you take into account that it’s better for you that one man should die for the people, than for the whole nation to perish.”
51 Yeye hakusema hivyo kwa hiari yake mwenyewe, bali kwa vile alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, alibashiri kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa lao;
He didn’t say this on his own initiative; but being high priest that year, he prophesied that Jesus was going to die for the nation,
52 na wala si kwa ajili yao tu, bali pia apate kuwaleta pamoja watoto wa Mungu waliotawanyika.
and not for the nation only, but that Jesus might also gather together into one God’s children who are scattered abroad.
53 Basi, tangu siku hiyo viongozi wa Wayahudi walifanya mipango ya kumwua Yesu.
So from that day on, they planned together to kill Jesus.
54 Kwa hiyo, Yesu hakutembea tena hadharani kati ya Wayahudi, bali alitoka hapo, akaenda mahali karibu na jangwa, katika mji uitwao Efraimu. Akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.
Therefore Jesus stopped walking publicly among the Jews, but went away from there to the region near the wilderness, into a city called Ephraim, and there He stayed with the disciples.
55 Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa karibu, na watu wengi walikwenda Yerusalemu ili wajitakase kabla ya sikukuu hiyo.
Now the Passover of the Jews was near, and many went from the country up to Jerusalem before the Passover, to purify themselves.
56 Basi, wakawa wanamtafuta Yesu; nao walipokusanyika pamoja Hekaluni wakaulizana, “Mwaonaje? Yaonekana kwamba haji kabisa kwenye sikukuu, au sivyo?”
Then they were looking for Jesus, and spoke among themselves as they stood in the temple, “What do you think? Isn’t He coming to the feast at all?”
57 Makuhani wakuu na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba mtu akijua mahali aliko Yesu awaarifu kusudi wamtie nguvuni.
Now the chief priests and the Pharisees had given a command, that anyone who knew where Jesus was should report it, that they might arrest Him.

< Yohana 11 >