< Yakobo 1 >

1 Mimi Yakobo, mtumishi wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo, nawaandikia ninyi, makabila kumi na mawili, yaliyotawanyika ulimwenguni! Salaam!
James, a servant of God and of the Lord Jesus Christ, To the twelve tribes of the Dispersion: Greetings.
2 Ndugu zangu, muwe na furaha mnapopatwa na majaribu mbalimbali,
Consider it pure joy, my brothers, when you encounter trials of many kinds,
3 kwani mwajua kwamba imani yenu ikisha stahimili, itawapatieni uvumilivu.
because you know that the testing of your faith develops perseverance.
4 Muwe na hakika kwamba uvumilivu wenu utawategemeza mpaka mwisho, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu, bila kupungukiwa chochote.
Allow perseverance to finish its work, so that you may be mature and complete, not lacking anything.
5 Lakini kama mmoja wenu ametindikiwa hekima, basi, anapaswa kumwomba Mungu ambaye atampatia; kwani Mungu huwapa wote kwa wingi na kwa ukarimu.
Now if any of you lacks wisdom, he should ask God, who gives generously to all without finding fault, and it will be given to him.
6 Lakini anapaswa kuomba kwa imani bila mashaka yoyote. Mtu aliye na mashaka ni kama mawimbi ya bahari ambayo husukumwa na kutupwatupwa na upepo.
But he must ask in faith, without doubting, because he who doubts is like a wave of the sea, blown and tossed by the wind.
7 Mtu wa namna hiyo, mwenye nia mbili na asiye na msimamo katika mwenendo wake wote,
That man should not expect to receive anything from the Lord.
8 asidhani ya kwamba atapata chochote kile kutoka kwa Bwana.
He is a double-minded man, unstable in all his ways.
9 Ndugu aliye maskini anapaswa kufurahi wakati Mungu anapomkweza,
The brother in humble circumstances should exult in his high position.
10 naye tajiri anapaswa kufurahi anaposhushwa na Mungu. Maana tajiri atatoweka kama ua la porini.
But the one who is rich should exult in his low position, because he will pass away like a flower of the field.
11 Jua huchomoza na kwa joto lake kali hukausha mimea, nayo maua yake huanguka, na uzuri wake wote huharibika. Vivyo hivyo, tajiri ataangamizwa katika shughuli zake.
For the sun rises with scorching heat and withers the plant; its flower falls and its beauty is lost. So too, the rich man will fade away in the midst of his pursuits.
12 Heri mtu anayebaki mwaminifu katika majaribu, kwani akisha stahimili atapewa tuzo la uzima ambalo Mungu aliwaahidia wale wanaompenda.
Blessed is the man who perseveres under trial, because when he has stood the test, he will receive the crown of life that God has promised to those who love Him.
13 Kama mtu akijaribiwa, asiseme: “Ninajaribiwa na Mungu.” Maana Mungu hawezi kujaribiwa na uovu, wala yeye hamjaribu mtu yeyote.
When tempted, no one should say, “God is tempting me.” For God cannot be tempted by evil, nor does He tempt anyone.
14 Lakini mtu hujaribiwa anapovutwa na kunaswa na tamaa zake mbaya.
But each one is tempted when by his own evil desires he is lured away and enticed.
15 Tamaa ikiiva huzaa dhambi; nayo dhambi ikikomaa huzaa kifo.
Then after desire has conceived, it gives birth to sin; and sin, when it is full-grown, gives birth to death.
16 Ndugu zangu wapenzi, msidanganyike!
Do not be deceived, my beloved brothers.
17 Kila kipaji chema na kila zawadi kamilifu hutoka mbinguni; hutoka kwa Baba, Muumba wa mianga, ambaye habadiliki wala hana alama yoyote ya ugeugeu.
Every good and perfect gift is from above, coming down from the Father of the heavenly lights, with whom there is no change or shifting shadow.
18 Kwa kupenda kwake mwenyewe alituzaa kwa neno lake la ukweli, ili tuwe namna ya matunda ya kwanza miongoni mwa viumbe vyake.
He chose to give us birth through the word of truth, that we would be a kind of firstfruits of His creation.
19 Ndugu zangu wapenzi, kumbukeni jambo hili! Kila mtu na awe mwepesi wa kusikia lakini asiwe mwepesi wa kusema wala mwepesi wa kukasirika.
My beloved brothers, understand this: Everyone should be quick to listen, slow to speak, and slow to anger,
20 Mwenye hasira hawezi kutimiza matakwa ya Mungu yaliyo ya haki.
for man’s anger does not bring about the righteousness that God desires.
21 Kwa hiyo, tupilieni mbali mwenendo mchafu na tabia zote mbovu; jiwekeni chini ya Mungu na kupokea ule ujumbe uliopandwa mioyoni mwenu, ambao waweza kuziokoa nafsi zenu.
Therefore, get rid of all moral filth and every expression of evil, and humbly accept the word planted in you, which can save your souls.
22 Msijidanganye wenyewe kwa kusikiliza tu neno lake, bali litekelezeni kwa vitendo.
Be doers of the word, and not hearers only. Otherwise, you are deceiving yourselves.
23 Yeyote anayesikiliza hilo neno lakini halitekelezi, huyo ni kama mtu anayejiangalia sura yake mwenyewe katika kioo.
For anyone who hears the word but does not carry it out is like a man who looks at his face in a mirror,
24 Hujiangalia mwenyewe, kisha huenda zake, na mara husahau jinsi alivyo.
and after observing himself goes away and immediately forgets what he looks like.
25 Lakini mtu anayeangalia kwa makini sheria kamilifu ambayo huwapa watu uhuru, mtu anayeendelea kuizingatia, na si kuisikia tu na kuisahau baadaye, bali anaitekeleza, mtu huyo atabarikiwa katika kila kitu anachofanya.
But the one who looks intently into the perfect law of freedom, and continues to do so—not being a forgetful hearer, but an effective doer—he will be blessed in what he does.
26 Kama mtu akijiona kuwa ni mtu mwenye dini, lakini hawezi kuutawala ulimi wake, dini yake haifai kitu, na anajidanganya mwenyewe.
If anyone considers himself religious and yet does not bridle his tongue, he deceives his heart and his religion is worthless.
27 Dini iliyo safi na isiyo na hitilafu mbele ya Mungu Baba ni hii: Kuwasaidia yatima na wajane katika shida zao, na kujilinda mwenyewe usichafuliwe na ulimwengu huu.
Pure and undefiled religion before our God and Father is this: to care for orphans and widows in their distress, and to keep oneself from being polluted by the world.

< Yakobo 1 >