< Yakobo 4 >
1 Mapigano na magombano yote kati yenu yanatoka wapi? Hutoka katika tamaa zenu mbaya ambazo hupigana daima ndani yenu.
Whence wars and fightings among you? Do they not come hence, even from your lusts, which war in your members?
2 Mnatamani vitu na kwa vile hamvipati mko tayari kuua; mwatamani sana kupata vitu, lakini hamvipati, hivyo mnagombana na kupigana. Hampati kile mnachotaka kwa sababu hamkiombi kwa Mungu.
You strongly desire, and have not; you kill, and are zealous, and can not obtain. You fight and war, but have not, because you ask not.
3 Tena, mnapoomba hampati kwa sababu mnaomba kwa nia mbaya; mnaomba ili mpate kutosheleza tamaa zenu.
You ask, and do not receive, because you ask wickedly, that you may spend upon your lusts.
4 Ninyi ni watu msio na uaminifu kama wazinzi. Je, hamjui kwamba kuwa rafiki wa ulimwengu ni kuwa adui wa Mungu? Yeyote anayetaka kuwa rafiki wa ulimwengu anajifanya adui wa Mungu.
Adulterers, and adulteresses, do you not know that the friendship of the world is enmity against God? Whosoever, therefore, will be a friend of the world, is counted an enemy of God.
5 Msifikiri kwamba Maandiko Matakatifu yamesema maneno ya bure, yanaposema: “Roho ambaye Mungu amemweka ndani yetu ana wivu mkubwa.”
Do you think that the scripture speaks in vain? And does the spirit, who dwells in us, strongly incline to envy?
6 Lakini, neema tunayopewa na Mungu ina nguvu zaidi; kama yasemavyo Maandiko: “Mungu huwapinga wenye majivuno lakini huwapa neema wanyenyekevu.”
But he gives greater favor. For it says, "God resists the proud, but gives favor to the humble."
7 Basi, jiwekeni chini ya Mungu; mpingeni Ibilisi naye atawakimbieni.
Therefore, be subject to God. Resist the devil, and he will flee from you.
8 Mkaribieni Mungu, naye atakuja karibu nanyi. Osheni mikono yenu enyi wakosefu! Safisheni mioyo yenu enyi wanafiki!
Draw nigh to God, and he will draw nigh to you. Cleanse your hands, you sinners; and purify your hearts, you men of two minds.
9 Oneni huzuni, lieni na kuomboleza; kicheko chenu na kiwe kilio; na furaha yenu iwe huzuni kubwa.
Be exceedingly afflicted, and mourn, and weep; and let your laughter be turned into mourning, and your joy into sadness.
10 Nyenyekeeni mbele ya Bwana, naye atawainueni.
Be humble in the presence of the Lord, and he will lift you up.
11 Ndugu, msilaumiane ninyi kwa ninyi. Anayemlaumu ndugu yake na kumhukumu, huyo huilaumu na kuihukumu Sheria. Kama ukiihukumu Sheria, basi, wewe huitii Sheria, bali waihukumu.
He who speaks against his brother, and condemns his brother, speaks against the law, and condemns the law. But if you condemn the law, you are not a doer of the law, but a judge.
12 Mungu peke yake ndiye mwenye kuweka Sheria na kuhukumu. Ni yeye peke yake anayeweza kuokoa na kuangamiza. Basi, wewe ni nani hata umhukumu binadamu mwenzako?
There is one lawgiver, who is able to save, and to destroy. Who are you, that condemn another?
13 Basi, sasa sikilizeni ninyi mnaosema: “Leo au kesho tutakwenda katika mji fulani na kukaa huko mwaka mzima tukifanya biashara na kupata faida.”
Come, now, you who say, To-day, or to-morrow, we will go to such a city, and will abide there one year, and traffic in merchandise, and get gain;
14 Ninyi hamjui hata maisha yenu yatakavyokuwa kesho! Ninyi ni kama ukungu unaotokea kwa muda mfupi tu na kutoweka tena.
who do not know what shall be to-morrow. For what is your life? It is, indeed, a smoke, which appears for a little while, and then vanishes away.
15 Mngalipaswa kusema: “Bwana akitujalia tutaishi na tutafanya hiki au kile.”
Instead of which, you ought to say, If the Lord will, we shall live, and do this, or that.
16 Lakini sasa mwajivuna na kujigamba; majivuno ya namna hiyo ni mabaya.
But now you boast in your proud speeches: all such boasting is evil.
17 Basi, mtu ambaye hafanyi lile jambo jema analojua kwamba anapaswa kulifanya, anatenda dhambi.
Wherefore, to him who know how to do good, and does it not, to him it is sin.