< Wahebrania 1 >
1 Hapo zamani, Mungu alisema na babu zetu mara nyingi kwa namna nyingi kwa njia ya manabii,
God, who at sundry times, and various ways, spake of old unto the fathers by the prophets, hath in these last days spoken to us by his Son,
2 lakini siku hizi za mwisho, amesema nasi kwa njia ya Mwanae. Yeye ndiye ambaye kwa njia yake Mungu aliumba ulimwengu na akamteua avimiliki vitu vyote. (aiōn )
whom He hath appointed heir of all things, by whom also He made the worlds. (aiōn )
3 Yeye ni mng'ao wa utukufu wa Mungu, na mfano kamili wa hali ya Mungu mwenyewe, akiutegemeza ulimwengu kwa neno lake lenye nguvu. Baada ya kuwapatia binadamu msamaha wa dhambi zao, aliketi huko juu mbinguni, upande wa kulia wa Mungu Mkuu.
Who being the refulgence of his glory and the imprest image of his person, and sustaining all things by his powerful word, having by Himself performed the purging away of our sins, sat down at the right hand of the majesty on high.
4 Mwana ni mkuu zaidi kuliko malaika, kama vile jina alilopewa na Mungu ni kuu zaidi kuliko jina lao.
Being as much superior to the angels, as He inheriteth a name more excellent than they.
5 Maana Mungu hakumwambia kamwe hata mmoja wa malaika wake: “Wewe ni Mwanangu; Mimi leo nimekuwa Baba yako.” Wala hakusema juu ya malaika yeyote: “Mimi nitakuwa Baba yake, naye atakuwa Mwanangu.”
For to which of the angels did He ever say, "Thou art my Son, this day have I begotten thee?" and again, "I will be to Him a Father, and He shall be to me a Son?"
6 Lakini Mungu alipokuwa anamtuma Mwanae mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, alisema: “Malaika wote wa Mungu wanapaswa kumwabudu.”
and when He again introduceth the First-born into the world, he saith, "And let all the angels of God worship Him."
7 Lakini kuhusu malaika, Mungu alisema: “Mungu awafanya malaika wake kuwa pepo, na watumishi wake kuwa ndimi za moto.”
And as to the angels He saith, "Who maketh his angels spirits and his ministers a flame of fire:"
8 Lakini kumhusu Mwana, Mungu alisema: “Utawala wako ee Mungu, wadumu milele na milele! Wewe wawatawala watu wako kwa haki. (aiōn )
but to the Son, "Thy throne, O God, is for ever and ever; the sceptre of thy kingdom is a sceptre of righteousness: (aiōn )
9 Wewe wapenda uadilifu na kuchukia uovu. Ndiyo maana Mungu, Mungu wako amekuweka wakfu na kukumiminia furaha kubwa zaidi kuliko wenzako.”
thou lovest righteousness and hatest iniquity; therefore God, even thy God, hath anointed thee with the oil of gladness above thine associates."
10 Pia alisema: “Bwana, wewe uliumba dunia hapo mwanzo, mbingu ni kazi ya mikono yako.
And in another place, "Thou, Lord, in the beginning hast founded the earth, and the heavens are the works of thy hands:
11 Hizo zitatoweka, lakini wewe wabaki daima, zote zitachakaa kama vazi.
they shall perish, but thou remainest; and they shall all grow old as a garment,
12 Utazikunjakunja kama koti, nazo zitabadilishwa kama vazi. Lakini wewe ni yuleyule daima, na maisha yako hayatakoma.”
and as a mantle wilt thou fold them up, and they shall be changed; but thou art the same, and thy years shall not fail."
13 Mungu hakumwambia kamwe hata mmoja wa malaika wake: “Keti upande wangu wa kulia, mpaka niwaweke adui zako chini ya miguu yako.”
But to which of the angels hath He ever said, "Sit thou at my right hand, till I make thine enemies thy footstool?"
14 Malaika ni roho tu wanaomtumikia Mungu, na Mungu huwatuma wawasaidie wale watakaopokea wokovu.
Are they not all ministring spirits, sent forth to attend on those who shall be heirs of salvation?