< Wahebrania 9 >

1 Agano la kwanza lilikuwa na taratibu zake za ibada na pia mahali patakatifu pa ibada palipojengwa na watu.
سَ پْرَتھَمو نِیَمَ آرادھَنایا وِوِدھَرِیتِبھِرَیہِکَپَوِتْرَسْتھانینَ چَ وِشِشْٹَ آسِیتْ۔
2 Palitengenezwa hema ambayo sehemu yake ya nje iliitwa Mahali Patakatifu. Humo mlikuwa na kinara cha taa, meza na mikate iliyotolewa kwa Mungu.
یَتو دُوشْیَمیکَں نِرَمِییَتَ تَسْیَ پْرَتھَمَکوشْٹھَسْیَ نامَ پَوِتْرَسْتھانَمِتْیاسِیتْ تَتْرَ دِیپَورِکْشو بھوجَناسَنَں دَرْشَنِییَپُوپاناں شْرینِی چاسِیتْ۔
3 Nyuma ya pazia la pili, kulikuwa na hema iliyoitwa Mahali Patakatifu Kupita Pote.
تَتْپَشْچادْ دْوِتِییایاسْتِرَشْکَرِنْیا اَبھْیَنْتَرے تِپَوِتْرَسْتھانَمِتِنامَکَں کوشْٹھَماسِیتْ،
4 Humo mlikuwa na madhabahu ya dhahabu kwa ajili ya kufukizia ubani, na Sanduku la Agano, ambalo lilikuwa limepakwa dhahabu pande zote, na ndani yake mlikuwa na chungu cha dhahabu kilichokuwa na mana; fimbo ya Aroni iliyokuwa imechanua majani, na vile vibao viwili vilivyoandikwa agano.
تَتْرَ چَ سُوَرْنَمَیو دھُوپادھارَح پَرِتَح سُوَرْنَمَنْڈِتا نِیَمَمَنْجُوشا چاسِیتْ تَنْمَدھْیے مانّایاح سُوَرْنَگھَٹو ہارونَسْیَ مَنْجَرِتَدَنْڈَسْتَکْشِتَو نِیَمَپْرَسْتَرَو،
5 Juu ya hilo Sanduku kulikuwa na viumbe vilivyodhihirisha kuweko kwa Mungu, na mabawa yao yalitanda juu ya mahali ambapo dhambi huondolewa. Lakini sasa, hatuwezi kusema kinaganaga juu ya mambo hayo.
تَدُپَرِ چَ کَرُناسَنے چھایاکارِنَو تیجومَیَو کِرُوباواسْتامْ، ایتیشاں وِشیشَورِتّانْتَکَتھَنایَ نایَں سَمَیَح۔
6 Mipango hiyo ilitekelezwa kisha ikawa desturi kwa makuhani kuingia kila siku katika hema ya nje kutoa huduma zao.
ایتیشْوِیدرِکْ نِرْمِّتیشُ یاجَکا اِیشْوَرَسیوامْ اَنُتِشْٹھَنَتو دُوشْیَسْیَ پْرَتھَمَکوشْٹھَں نِتْیَں پْرَوِشَنْتِ۔
7 Lakini kuhani Mkuu peke yake ndiye anayeingia katika lile hema la pili; naye hufanya hivyo mara moja tu kwa mwaka. Anapoingia ndani huwa amechukua damu ambayo anamtolea Mungu kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya dhambi ambazo watu wamezitenda bila wao wenyewe kujua.
کِنْتُ دْوِتِییَں کوشْٹھَں پْرَتِوَرْشَمْ ایکَکرِتْوَ ایکاکِنا مَہایاجَکینَ پْرَوِشْیَتے کِنْتْواتْمَنِمِتَّں لوکانامْ اَجْنانَکرِتَپاپانانْچَ نِمِتَّمْ اُتْسَرْجَّنِییَں رُدھِرَمْ اَنادایَ تینَ نَ پْرَوِشْیَتے۔
8 Kutokana na taratibu hizo Roho Mtakatifu anafundisha wazi kwamba wakati ile hema ya nje ingali ipo imesimama, njia ya kuingia Mahali Patakatifu haijafunguliwa.
اِتْیَنینَ پَوِتْرَ آتْما یَتْ جْناپَیَتِ تَدِدَں تَتْ پْرَتھَمَں دُوشْیَں یاوَتْ تِشْٹھَتِ تاوَتْ مَہاپَوِتْرَسْتھانَگامِی پَنْتھا اَپْرَکاشِتَسْتِشْٹھَتِ۔
9 Jambo hili ni mfano wa nyakati za sasa. Linaonyesha kwamba zawadi na dhabihu zinazotolewa kwa Mungu haziwezi kuifanya mioyo ya wale wanaoabudu kuwa mikamilifu,
تَچَّ دُوشْیَں وَرْتَّمانَسَمَیَسْیَ درِشْٹانْتَح، یَتو ہیتوح سامْپْرَتَں سَںشودھَنَکالَں یاوَدْ یَنِّرُوپِتَں تَدَنُساراتْ سیواکارِنو مانَسِکَسِدّھِکَرَنےسَمَرْتھابھِح
10 kwani haya yote yanahusika na vyakula, vinywaji na taratibu mbalimbali za kutawadha. Yote hayo ni maagizo ya njenje tu; na nguvu yake hukoma wakati Mungu atakaporekebisha vitu vyote.
کیوَلَں کھادْیَپیییشُ وِوِدھَمَجَّنیشُ چَ شارِیرِکَرِیتِبھِ رْیُکْتانِ نَیویدْیانِ بَلِدانانِ چَ بھَوَنْتِ۔
11 Lakini Kristo amekwisha fika, akiwa Kuhani Mkuu wa mambo yaliyo mema, ambayo sasa yamekwisha fika. Yeye anatoa huduma zake katika hema iliyo bora na kamilifu zaidi, isiyofanywa kwa mikono ya watu, yaani isiyo ya ulimwengu huu ulioumbwa.
اَپَرَں بھاوِمَنْگَلاناں مَہایاجَکَح کھْرِیشْٹَ اُپَسْتھایاہَسْتَنِرْمِّتینارْتھَتَ ایتَتْسرِشْٹے رْبَہِرْبھُوتینَ شْریشْٹھینَ سِدّھینَ چَ دُوشْیینَ گَتْوا
12 Yeye aliingia Mahali Patakatifu mara moja tu, tena hakuwa amechukua damu ya mbuzi wala ng'ombe, bali aliingia kwa damu yake yeye mwenyewe, akatupatia ukombozi wa milele. (aiōnios g166)
چھاگاناں گووَتْساناں وا رُدھِرَمْ اَنادایَ سْوِییَرُدھِرَمْ آدایَیکَکرِتْوَ ایوَ مَہاپَوِتْرَسْتھانَں پْرَوِشْیانَنْتَکالِکاں مُکْتِں پْراپْتَوانْ۔ (aiōnios g166)
13 Watu waliokuwa najisi kidini waliweza kutakasika na kuwa safi waliponyunyiziwa damu ya mbuzi na ya ng'ombe pamoja na majivu ya ndama.
ورِشَچھاگاناں رُدھِرینَ گَوِیبھَسْمَنَح پْرَکْشیپینَ چَ یَدْیَشُچِلوکاح شارِیرِشُچِتْوایَ پُویَنْتے،
14 Lakini, kwa damu ya Kristo, mambo makuu zaidi hufanyika! Kwa nguvu za Roho wa milele, Kristo alijitolea mwenyewe dhabihu kamilifu kwa Mungu. Damu yake itatutakasa dhamiri zetu kutokana na matendo yaletayo kifo, ili tupate kumtumikia Mungu aliye hai. (aiōnios g166)
تَرْہِ کِں مَنْیَدھْوے یَح سَداتَنیناتْمَنا نِشْکَلَنْکَبَلِمِوَ سْوَمیویشْوَرایَ دَتَّوانْ، تَسْیَ کھْرِیشْٹَسْیَ رُدھِرینَ یُشْماکَں مَناںسْیَمَریشْوَرَسْیَ سیوایَے کِں مرِتْیُجَنَکیبھْیَح کَرْمَّبھْیو نَ پَوِتْرِیکارِشْیَنْتے؟ (aiōnios g166)
15 Kwa hiyo, Kristo ndiye aliyeratibisha agano jipya ili wale walioitwa na Mungu wazipokee baraka za milele walizoahidiwa. Watazipata, kwani kifo kimetokea ambacho huwakomboa watu kutoka yale makosa waliyofanya wakati wa lile agano la kale. (aiōnios g166)
سَ نُوتَنَنِیَمَسْیَ مَدھْیَسْتھوبھَوَتْ تَسْیابھِپْرایویَں یَتْ پْرَتھَمَنِیَمَلَنْگھَنَرُوپَپاپیبھْیو مرِتْیُنا مُکْتَو جاتایامْ آہُوتَلوکا اَنَنْتَکالِییَسَمْپَدَح پْرَتِجْناپھَلَں لَبھیرَنْ۔ (aiōnios g166)
16 Kwa kawaida wosia hutambuliwa tu kama kifo cha yule aliyeufanya huo wosia kimethibitishwa.
یَتْرَ نِیَمو بھَوَتِ تَتْرَ نِیَمَسادھَکَسْیَ بَلے رْمرِتْیُنا بھَوِتَوْیَں۔
17 Wosia hauwezi kutekelezwa mpaka kumetokea kifo, kwani wosia hauna maana ikiwa mwenye kuufanya bado anaishi.
یَتو ہَتینَ بَلِنا نِیَمَح سْتھِرِیبھَوَتِ کِنْتُ نِیَمَسادھَکو بَلِ رْیاوَتْ جِیوَتِ تاوَتْ نِیَمو نِرَرْتھَکَسْتِشْٹھَتِ۔
18 Ndiyo maana hata lile agano la kwanza halikuwekwa bila damu kumwagwa.
تَسْماتْ سَ پُورْوَّنِیَموپِ رُدھِرَپاتَں وِنا نَ سادھِتَح۔
19 Kwanza Mose aliwatangazia watu wote amri zote kama ilivyokuwa katika Sheria; kisha akachukua damu ya ndama pamoja na maji, na kwa kutumia majani ya mti uitwao husopo na pamba nyekundu, akakinyunyizia kile kitabu cha Sheria na hao watu wote.
پھَلَتَح سَرْوَّلوکانْ پْرَتِ وْیَوَسْتھانُسارینَ سَرْوّا آجْناح کَتھَیِتْوا مُوسا جَلینَ سِنْدُورَوَرْنَلومْنا ایشووَترِنینَ چَ سارْدّھَں گووَتْساناں چھاگانانْچَ رُدھِرَں گرِہِیتْوا گْرَنْتھے سَرْوَّلوکیشُ چَ پْرَکْشِپْیَ بَبھاشے،
20 Mose alisema: “Hii ni damu inayothibitisha agano mliloamriwa na Mungu mlitii.”
یُشْمانْ اَدھِیشْوَرو یَں نِیَمَں نِرُوپِتَوانْ تَسْیَ رُدھِرَمیتَتْ۔
21 Vilevile Mose aliinyunyizia damu ile hema na vyombo vya ibada.
تَدْوَتْ سَ دُوشْیےپِ سیوارْتھَکیشُ سَرْوَّپاتْریشُ چَ رُدھِرَں پْرَکْشِپْتَوانْ۔
22 Naam, kadiri ya Sheria karibu kila kitu chaweza kutakaswa kwa damu, na dhambi nazo zaondolewa tu ikiwa damu imemwagwa.
اَپَرَں وْیَوَسْتھانُسارینَ پْرایَشَح سَرْوّانِ رُدھِرینَ پَرِشْکْرِیَنْتے رُدھِرَپاتَں وِنا پاپَموچَنَں نَ بھَوَتِ چَ۔
23 Vitu hivi ambavyo ni mfano tu wa mambo halisi ya mbinguni, vililazimika kutakaswa kwa namna hiyo. Lakini vitu vya mbinguni huhitaji dhabihu iliyo bora zaidi.
اَپَرَں یانِ سْوَرْگِییَوَسْتُوناں درِشْٹانْتاسْتیشامْ ایتَیح پاوَنَمْ آوَشْیَکَمْ آسِیتْ کِنْتُ ساکْشاتْ سْوَرْگِییَوَسْتُونامْ ایتیبھْیَح شْریشْٹھے رْبَلِدانَیح پاوَنَماوَشْیَکَں۔
24 Maana Kristo hakuingia Mahali Patakatifu palipojengwa kwa mikono ya watu, ambapo ni mfano tu wa kile kilicho halisi. yeye aliingia mbinguni kwenyewe ambako sasa anasimama mbele ya Mungu kwa ajili yetu.
یَتَح کھْرِیشْٹَح سَتْیَپَوِتْرَسْتھانَسْیَ درِشْٹانْتَرُوپَں ہَسْتَکرِتَں پَوِتْرَسْتھانَں نَ پْرَوِشْٹَوانْ کِنْتْوَسْمَنِّمِتَّمْ اِدانِیمْ اِیشْوَرَسْیَ ساکْشادْ اُپَسْتھاتُں سْوَرْگَمیوَ پْرَوِشْٹَح۔
25 Kuhani Mkuu wa Wayahudi huingia Mahali Patakatifu kila mwaka akiwa amechukua damu ya mnyama; lakini Kristo hakuingia humo ili ajitoe mwenyewe mara nyingi,
یَتھا چَ مَہایاجَکَح پْرَتِوَرْشَں پَرَشونِتَمادایَ مَہاپَوِتْرَسْتھانَں پْرَوِشَتِ تَتھا کھْرِیشْٹینَ پُنَح پُنَراتْموتْسَرْگو نَ کَرْتَّوْیَح،
26 maana ingalikuwa hivyo, Kristo angalipaswa kuteswa mara nyingi tangu kuumbwa ulimwengu. Lakini sasa nyakati hizi zinapokaribia mwisho wake, yeye ametokea mara moja tu, kuondoa dhambi kwa kujitoa yeye mwenyewe dhabihu. (aiōn g165)
کَرْتَّوْیے سَتِ جَگَتَح سرِشْٹِکالَمارَبھْیَ بَہُوارَں تَسْیَ مرِتْیُبھوگَ آوَشْیَکوبھَوَتْ؛ کِنْتْوِدانِیں سَ آتْموتْسَرْگینَ پاپَناشارْتھَمْ ایکَکرِتْوو جَگَتَح شیشَکالے پْرَچَکاشے۔ (aiōn g165)
27 Basi, kama vile kila mtu hufa mara moja tu, kisha husimama mbele ya hukumu ya Mungu,
اَپَرَں یَتھا مانُشَسْیَیکَکرِتْوو مَرَنَں تَتْ پَشْچادْ وِچارو نِرُوپِتوسْتِ،
28 vivyo hivyo Kristo naye alijitoa dhabihu mara moja tu kwa ajili ya kuziondoa dhambi za wengi. Atakapotokea mara ya pili si kwa ajili ya kupambana na dhambi, bali ni kwa ajili ya kuwaokoa wale wanaomngojea.
تَدْوَتْ کھْرِیشْٹوپِ بَہُوناں پاپَوَہَنارْتھَں بَلِرُوپینَیکَکرِتْوَ اُتْسَسرِجے، اَپَرَں دْوِتِییَوارَں پاپادْ بھِنَّح سَنْ یے تَں پْرَتِیکْشَنْتے تیشاں پَرِتْرانارْتھَں دَرْشَنَں داسْیَتِ۔

< Wahebrania 9 >