< Wahebrania 4 >
1 Mungu alituahidia kwamba tutaweza kupata pumziko hilo alilosema. Basi, na tuogope ili yeyote kati yenu asije akashindwa kupata pumziko hilo.
Antao arè hañeveñe, hera ho zoeñ’ ama’ iaia ama’areo, t’ie nilesa amy fampitamañe mbe añey: ty fizilihañe amy fitofà’ey ao.
2 Maana Habari Njema imehubiriwa kwetu kama vile ilivyohubiriwa kwa hao watu wa kale. Lakini ujumbe huo haukuwafaa chochote, maana waliusikia lakini hawakuupokea kwa imani.
Toe nitaroñeñe aman-tika manahake te tam’ iereo i talili-soay; fe tsy nahasoa iareo i tsara nitaroñeñey, amy t’ie tsy natrao’ o nijanjiñeo fatokisañe.
3 Basi, sisi tunaoamini tunapata pumziko hilo aliloahidi Mungu. Kama alivyosema: “Nilikasirika, nikaapa: Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko.” Mungu alisema hayo ingawa kazi yake ilikuwa imekwisha malizika tangu alipoumba ulimwengu.
Itika miantokeo ro mizilik’ amy fitofàñey, (ty amy tsinara’e ty hoe, Ie nifantàko an-kabosehañe t’ie tsy himoak’ amy fitofakoy ao.) ndra te nifanehafeñe boak’ am-pifotora’ ty voatse toy o fitoloñañeo.
4 Maana Maandiko yasema mahali fulani kuhusu siku ya saba: “Mungu alipumzika siku ya saba, akaacha kazi zake zote.”
Fa eo ty tsaraeñe ty amy faha-fitoy ty hoe: Nitroatse amo hene fitoloña’eo, ami’ty andro faha-fito t’i Andrianañahare.
5 Tena jambo hili lasemwa pia: “Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko.”
Le tinovo’e ty hoe: Tsy himoak’ amy fitofàkoy iereo.
6 Wale waliotangulia kuhubiriwa Habari Njema hawakupata pumziko hilo kwa sababu hawakuamini. Wapo, basi, wengine ambao wangejaliwa kulipata.
Aa kanao mbe hizilike ao ty ila’e, naho nilesa ka tsy nizilik’ ao ty amy fanjeharañey o nitaroñeñe valoha’eo,
7 Jambo hili ni wazi, kwani Mungu aliweka siku nyingine ambayo inaitwa “Leo”. Miaka mingi baadaye Mungu alisema juu ya hiyo siku kwa maneno ya Daudi katika Maandiko yaliyokwisha tajwa: “Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu.”
le nañoriza’e andro indraike atao Anito amy nampisaontsie’e i Davide haehae atoiy amy tsara’ey ty hoe: Anito, naho janji’areo ty fiarañanaña’e ko mampientetse arofo.
8 Kama Yoshua angaliwapa watu hao hilo pumziko, Mungu hangalisema baadaye juu ya siku nyingine.
Aa naho nitolora’ i Josoa fitofàñe, tsy ho nitalilie’e andro ila’e afara.
9 Kwa hiyo, basi, bado lipo pumziko kwa watu wa Mungu kama kule kupumzika kwake Mungu siku ya saba.
Inao, toe mbe eo ho a ondatin’ Añahareo ty fañambenañe Sabotse;
10 Maana, kila anayepata pumziko aliloahidi Mungu atapumzika baada ya kazi yake kama vile pia Mungu alivyopumzika baada ya yake.
amy te mitofa amo fitoloña’eo ty mizilik’ amy Sabotse’ey, hambañe aman’ Añahare amy azey.
11 Basi, tujitahidi kupata pumziko hilo, ili asiwepo yeyote miongoni mwenu atakayeshindwa, kama walivyofanya wao kwa sababu ya ukosefu wao wa imani.
Antao arè himane fizilik’ amy fitofàñey, tsy mone hikapotrake am-pitsikombeañe i fanjeharañey.
12 Neno la Mungu ni hai na lina nguvu; ni kali zaidi kuliko upanga wenye makali kuwili. Hukata kabisa mpaka mahali ambapo moyo na roho hukutana, mpaka pale vikutanapo viungo vya mwili na mafuta. Neno hilo huchambua nia na fikira za mioyo ya watu.
Toe veloñe naho mahatafetetse o tsaran’ Añahareo, masioñe te amy ze fibara sambelela’e, mitrofake pak’ ami’ty fifamitraña’ ty fañova ami’ty arofo, naho o fangeo amo betro’eo; naho mahatsikarake o fivetsevetse naho safirin’ arofoo,
13 Hakuna kiumbe chochote kilichofichika mbele ya Mungu; kila kitu kimefunuliwa wazi mbele ya macho yake. Kwake, sisi sote tutapaswa kutoa hoja ya matendo yetu.
vaho tsy eo ty namboareñe ze mietake ama’e; fa kila miborake naho mivendratse am-pihaino’ i hamolily an-tikañey.
14 Basi, tunapaswa kuzingatia kwa uthabiti imani tunayoiungama. Maana tunaye Kuhani Mkuu aliyeingia mpaka kwa Mungu mwenyewe—Yesu, Mwana wa Mungu.
Aa kanao amam-Pisorom-bey nahafiranga o likerañeo tika, toe Iesoà Anan’ Añahare, le antao hifahatse ami’ty iantofan-tikañe.
15 Huyu Kuhani Mkuu wetu si mmoja ambaye hawezi kutuunga mkono katika unyonge wetu, ila ni Kuhani Mkuu ambaye alijaribiwa kama sisi kwa kila namna lakini hakutenda dhambi.
Amy t’ie tsy amam-Pisorombey tsy mahay milèñ’ arofo amo halemèn-tikañeo, ie nizizieñe amy ze he’e manahak’ itika, fe tsy aman-tahiñe.
16 Basi, na tukikaribie bila hofu kiti cha enzi cha Mungu, palipo na neema, ili tukajipatie huruma na neema ya kutusaidia wakati wa lazima.
Antao arè hahasibeke hitotoke mb’amy fiambesan-kasoay, hiferenaiñañe, naho hitretrezañe an-tsan-kasotriañe.