< Wahebrania 3 >

1 Ndugu zangu watu wa Mungu ambao mmeitwa na Mungu, fikirini juu ya Yesu ambaye Mungu alimtuma awe Kuhani Mkuu wa imani tunayoiungama.
Derföre, I helige bröder, som delaktige ären uti den himmelska kallelsen, akter på Apostelen, och öfversta Presten, den vi bekännom, Christum Jesum;
2 Yeye alikuwa mwaminifu kwa Mungu aliyemteua kufanya kazi yake kama vile Mose alivyokuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu.
Hvilken trogen är honom, som honom gjort hafver, såsom ock Moses, i allt hans hus;
3 Mjenzi wa nyumba hupata heshima zaidi kuliko hiyo nyumba yenyewe. Hali kadhalika naye Yesu anastahili heshima kubwa zaidi kuliko Mose.
Så mycket större äro värd än Moses, som han hafver större äro, som huset byggde, än sjelfva huset.
4 Kila nyumba hujengwa na mjenzi fulani—na Mungu ndiye mjenzi wa vitu vyote.
Ty hvart och ett hus bygges af någon; men Gud är den, som all ting gjort hafver.
5 Mose alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Bwana kama mtumishi, na alinena juu ya mambo ambayo Mungu atayasema hapo baadaye.
Och Moses var trogen i allt hans hus, såsom en tjenare, de ting till vittnesbörd, som framdeles yppas skulle;
6 Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana mwenye mamlaka juu ya nyumba ya Mungu. Sisi ni nyumba yake kama tukizingatia uhodari wetu na uthabiti wetu katika kile tunachotumainia.
Men Christus, såsom en Son, i sitt hus; hvilket hus vi ärom, om vi annars förtröstningen, och hoppsens berömmelse, intill ändan fast behålle.
7 Kwa hiyo, basi, kama asemavyo Roho Mtakatifu: “Kama mkisikia sauti ya Mungu leo,
Derföre, såsom den Helge Ande säger: I dag, om I fån höra hans röst,
8 msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama wazee wenu walivyokuwa wakati walipomwasi Mungu; kama walivyokuwa siku ile kule jangwani,
Så förhärder icke edor hjerta; såsom skedde i vredene på frestelsedagen, i öknene;
9 Huko wazee wenu walinijaribu na kunichunguza, asema Bwana, ingawa walikuwa wameyaona matendo yangu kwa miaka arobaini.
Då edre fäder frestade mig; de bepröfvade, och sågo min verk, i fyratio år.
10 Kwa sababu hiyo niliwakasirikia watu hao nikasema, Fikira za watu hawa zimepotoka, hawajapata kamwe kuzijua njia zangu.
Derföre vardt jag vred på detta slägtet, och sade: Alltid fara de ville med hjertat; men de visste icke mina vägar;
11 Basi, nilikasirika, nikaapa: Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko.”
Så att jag ock svor i mine vrede: De skola icke komma uti mina rolighet.
12 Basi ndugu, jihadharini asije akawako yeyote miongoni mwenu aliye na moyo mbaya hivyo na asiyeamini hata kujitenga na Mungu aliye hai.
Ser till, käre bröder, att tilläfventyrs uti någon edra icke är ett argt och otroget hjerta, som träder ifrå lefvandes Gud.
13 Maadamu hiyo “Leo” inayosemwa katika Maandiko bado inatuhusu sisi, mnapaswa kusaidiana daima, ili mtu yeyote miongoni mwenu asidanganywe na dhambi na kuwa mkaidi.
Utan förmaner eder sjelfva alla dagar, så länge det nämnes: I dag; att ingen ibland eder blifver förhärd, genom syndenes bedragelse.
14 Maana sisi tunashirikiana na Kristo ikiwa tutazingatia kwa uthabiti tumaini tulilokuwa nalo mwanzoni.
Ty vi äre delaktige vordne af Christo; om vi annars trona, som vi begynt hafve, fast behålle intill ändan.
15 Maandiko yasema hivi: “Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama wazee wenu walivyokuwa wakati walipomwasi Mungu.”
Emedan det sägs: I dag, om I fån höra hans röst, så förhärder icke edor hjerta, såsom skedde i vredene.
16 Ni akina nani basi, waliosikia sauti ya Mungu wakamwasi? Ni wale wote walioongozwa na Mose kutoka Misri.
Ty somlige, som henne hörde, förtörnade honom; men icke alle, som farne voro utaf Egypten, genom Mosen.
17 Mungu aliwakasirikia akina nani kwa miaka arobaini? Aliwakasirikia wale waliotenda dhambi, maiti zao zikatapakaa kule jangwani.
Men hvilkom var han vred i fyratio år? Var han icke dem som syndat hade, hvilkas kroppar förföllo i öknene?
18 Mungu alipoapa: “Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko,” alikuwa anawasema akina nani? Alikuwa anasema juu ya hao walioasi.
Men hvilkom svor han då, att de icke skulle komma in i hans rolighet, utan dem otrognom?
19 Basi, twaona kwamba hawakuingia huko kwa sababu hawakuamini.
Och vi sem, att de icke kunde ingå, för otrones skull.

< Wahebrania 3 >