< Wahebrania 3 >

1 Ndugu zangu watu wa Mungu ambao mmeitwa na Mungu, fikirini juu ya Yesu ambaye Mungu alimtuma awe Kuhani Mkuu wa imani tunayoiungama.
Wherefore, holy brethren, partakers of the heavenly calling, consider the apostle and high priest of our confession, Christ Jesus,
2 Yeye alikuwa mwaminifu kwa Mungu aliyemteua kufanya kazi yake kama vile Mose alivyokuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu.
who is faithful to him that appointed him, as Moses also was faithful in all his house.
3 Mjenzi wa nyumba hupata heshima zaidi kuliko hiyo nyumba yenyewe. Hali kadhalika naye Yesu anastahili heshima kubwa zaidi kuliko Mose.
For this man is counted worthy of more glory than Moses, inasmuch as he who has builded the house, has more honor than the house.
4 Kila nyumba hujengwa na mjenzi fulani—na Mungu ndiye mjenzi wa vitu vyote.
For every house is builded by some one; but he that built all things is God.
5 Mose alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Bwana kama mtumishi, na alinena juu ya mambo ambayo Mungu atayasema hapo baadaye.
And Moses indeed was faithful in all his house as a servant, to bear testimony to those things which were to be spoken afterward;
6 Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana mwenye mamlaka juu ya nyumba ya Mungu. Sisi ni nyumba yake kama tukizingatia uhodari wetu na uthabiti wetu katika kile tunachotumainia.
but Christ, as a Son over his own house; whose house we are, if we hold the confidence and the joy of our hope firm to the end.
7 Kwa hiyo, basi, kama asemavyo Roho Mtakatifu: “Kama mkisikia sauti ya Mungu leo,
Wherefore, as the Holy Spirit says: To-day, if you will hear his voice,
8 msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama wazee wenu walivyokuwa wakati walipomwasi Mungu; kama walivyokuwa siku ile kule jangwani,
harden not your hearts, as in the bitter provocation, in the day of trial in the wilderness,
9 Huko wazee wenu walinijaribu na kunichunguza, asema Bwana, ingawa walikuwa wameyaona matendo yangu kwa miaka arobaini.
where your fathers tried me, proved me, and saw my works forty years.
10 Kwa sababu hiyo niliwakasirikia watu hao nikasema, Fikira za watu hawa zimepotoka, hawajapata kamwe kuzijua njia zangu.
Where fore, I was angry with that generation, and said, They do always err in their heart, and they have not known my ways:
11 Basi, nilikasirika, nikaapa: Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko.”
so that I swore in my anger, They shall not enter into my rest.
12 Basi ndugu, jihadharini asije akawako yeyote miongoni mwenu aliye na moyo mbaya hivyo na asiyeamini hata kujitenga na Mungu aliye hai.
Take heed, brethren, lest there be in any of you an evil heart of unbelief in apostatizing from the living God.
13 Maadamu hiyo “Leo” inayosemwa katika Maandiko bado inatuhusu sisi, mnapaswa kusaidiana daima, ili mtu yeyote miongoni mwenu asidanganywe na dhambi na kuwa mkaidi.
But exhort one another daily, while it is called To-day, lest any of you be hardened by the deceitfulness of sin.
14 Maana sisi tunashirikiana na Kristo ikiwa tutazingatia kwa uthabiti tumaini tulilokuwa nalo mwanzoni.
For we are partakers of the Christ, if we hold our begun confidence firm to the end;
15 Maandiko yasema hivi: “Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama wazee wenu walivyokuwa wakati walipomwasi Mungu.”
while it is said, To-day, if you will hear his voice, harden not your hearts, as in the bitter provocation.
16 Ni akina nani basi, waliosikia sauti ya Mungu wakamwasi? Ni wale wote walioongozwa na Mose kutoka Misri.
For some, when they had heard, did bitterly provoke; yet, not all that came out of Egypt by Moses.
17 Mungu aliwakasirikia akina nani kwa miaka arobaini? Aliwakasirikia wale waliotenda dhambi, maiti zao zikatapakaa kule jangwani.
But with whom was he angry forty years? Was it not with those who sinned, whose carcasses fell in the wilderness?
18 Mungu alipoapa: “Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko,” alikuwa anawasema akina nani? Alikuwa anasema juu ya hao walioasi.
But to whom did he swear that they should not enter into his rest, but to those who believed not?
19 Basi, twaona kwamba hawakuingia huko kwa sababu hawakuamini.
And so we see that they could not enter in because of unbelief.

< Wahebrania 3 >