< Wahebrania 12 >

1 Sisi tunalo kundi hili kubwa la mashahidi mbele yetu. Kwa hiyo tuondoe kila kizuizi kinachotuzuia, na dhambi ile inayotung'ang'ania. Tupige mbio kwa uvumilivu katika mashindano yaliyowekwa mbele yetu.
Therefore let us also, who have all these witnesses surrounding us like clouds, cast from us all encumbrances, and sin, which is always prepared for us; and let us run with patience the race that is appointed for us.
2 Tumwelekee Yesu ambaye ndiye aliyeianzisha imani yetu na ambaye ataikamilisha. Kwa ajili ya furaha iliyokuwa inamngojea, yeye alivumilia kifo msalabani, bila kujali juu ya aibu yake, na sasa anaketi upande wa kulia wa kiti cha enzi cha Mungu.
And let us look on Jesus, who hath become the commencement and the completion of our faith; who, on account of the joy there was for him, endured the cross, and surrendered himself to opprobrium; and is seated on the right hand of the throne of God.
3 Fikirini juu ya mambo yaliyompata Yesu, jinsi alivyostahimili upinzani mkubwa kwa watu wenye dhambi. Basi, msife moyo, wala msikate tamaa.
Behold, therefore, how much he suffered from sinners, from them who are adversaries of their own soul, that ye may not be discouraged, nor your soul become remiss.
4 Maana katika kupambana na dhambi, ninyi hamjapigana mpaka kiasi cha kumwaga damu yenu.
Ye have not yet come unto blood, in the contest against sin.
5 Je, mmesahau yale maneno ya kutia moyo ambayo Mungu anawataja ninyi kuwa wanawe? “Mwanangu, usidharau adhabu ya Bwana, wala usife moyo anapokukanya.
And ye have forgotten the monition, which saith to you, as to children, My son, disregard not the chastening of the Lord; nor let thy soul faint, when thou art rebuked by him.
6 Maana Bwana humwadhibu kila anayempenda, humpinga kila anayekubali kuwa mwanae.”
For, whom the Lord loveth, he chasteneth; and he scourgeth those sons, for whom he hath kind regards.
7 Vumilieni adhabu kwani ni mafundisho; Mungu huwatendea ninyi kama wanawe. Maana ni mwana gani asiyeadhibiwa na baba yake?
Therefore endure ye the chastisement; because God is dealing with you as with sons. For what son is there, whom his father chasteneth not?
8 Lakini msipoadhibiwa kama wana wengine, basi, ninyi si wanawe, bali ni wana haramu.
But if ye are without that chastisement, with which every one is chastened, ye are become strangers and not sons.
9 Zaidi ya hayo sisi tunawaheshimu wazazi wetu waliotuzaa hata wanapotuadhibu. Basi, tunapaswa kumtii zaidi Baba yetu wa kiroho ili tupate kuishi.
And if our fathers of the flesh chastened us, and we revered them, how much more ought we to be submissive to our spiritual fathers, and live?
10 Wazazi wetu hapa duniani walituadhibu kwa muda, kama wao wenyewe walivyoona kuwa vema; lakini Mungu anatuadhibu kwa ajili ya faida yetu wenyewe, tupate kuushiriki utakatifu wake.
For they chastened us for a short time, according to their pleasure; but God, for our advantage, that we may become partakers of his holiness.
11 Kuadhibiwa si jambo la kufurahisha bali la kuhuzunisha. Lakini wale waliofunzwa kuwa na nidhamu mwishowe watavuna tuzo la amani kutoka katika maisha adili!
Now all chastisement, in the time of it, is not accounted a matter of joy, but of grief: yet, afterwards, it yieldeth the fruits of peace and righteousness to them who are exercised by it.
12 Basi, inueni mikono yenu inayolegea na kuimarisha magoti yenu yaliyo dhaifu.
Wherefore, strengthen ye your relaxed hands, and your tottering knees:
13 Endeleeni kutembea katika njia iliyonyoka, ili kile kilicholemaa kisiumizwe, bali kiponywe.
and make straight paths for your feet, that the limb which is lame may not be wrenched, but may be healed.
14 Jitahidini kuishi kwa amani na watu wote. Ishini maisha ya utakatifu, kwa sababu hakuna mtu atakayemwona Bwana bila ya maisha kama hayo.
Follow after peace with every man; and after holiness, without which a man will not see our Lord.
15 Jitahidini sana mtu yeyote asije akapoteza neema ya Mungu. Muwe waangalifu ili mti mchungu usizuke kati yenu na kuwaua wengi kwa sumu yake.
And be careful, lest any be found among you destitute of the grace of God; or lest some root of bitterness shoot forth germs, and trouble you; and thereby many be defiled:
16 Jihadharini ili miongoni mwenu pasiwe na mtu mwasherati au mtu asiyemcha Mungu kama Esau, aliyeuza haki yake ya mzaliwa wa kwanza kwa mlo mmoja.
or lest any one be found among you a fornicator; or a heedless one like Esau, who for one mess of food, sold his primogeniture.
17 Ninyi mnafahamu kwamba hata alipotaka kuipata tena ile baraka iliyokuwa yake, alikataliwa, maana hakupata tena nafasi ya kutubu, ingawa aliitafuta kwa machozi.
For ye know that, afterwards when he wished to inherit the blessing, he was rejected; for he found not a place for repentance, although he sought it with tears.
18 Ninyi hamkuwasili mlimani Sinai, ambao unaweza kushikika kama walivyofanya watu wa Israeli, hamkufika kwenye moto uwakao, penye giza, tufani,
For ye have not come to the fire that burned, and the tangible mount; nor to the darkness and obscurity and tempest;
19 mvumo wa tarumbeta na sauti ya maneno. Wale waliosikia sauti hiyo waliomba wasisikie tena neno jingine,
nor to the sound of the trumpet, and the voice of words, which they who heard, entreated that it might no more be spoken to them;
20 kwani hawakuweza kustahimili amri iliyotolewa: “Atakayegusa mlima huu, hata kama ni mnyama, atapigwa mawe.”
for they could not endure what was commanded. And even a beast, if it approached the mountain, was to be stoned.
21 Hayo yote yalionekana ya kutisha mno, hata Mose akasema, “Naogopa na kutetemeka.”
And so terrible was the sight, that Moses said, I fear and tremble.
22 Lakini ninyi mmefika katika mlima wa Sioni, kwenye mji wa Mungu aliye hai. Mmefika Yerusalemu, mji wa mbinguni, ambapo wamekusanyika malaika elfu nyingi wasiohesabika.
But ye have come to Mount Zion, and to the city of the living God, the Jerusalem that is in heaven; and to the assemblies of myriads of angels;
23 Mmefika kwenye kusanyiko kubwa la wazaliwa wa kwanza wa Mungu, ambao majina yao yameandikwa mbinguni. Mnasimama mbele ya Mungu aliye hakimu wa wote, na mbele ya roho za watu waadilifu waliofanywa kuwa wakamilifu.
and to the church of the first-born, who are enrolled in heaven and to God the judge of all; and to the spirits of the just, who are perfected;
24 Mmefika kwa Yesu ambaye ameratibisha agano jipya, na ambaye damu yake iliyomwagika inasema mambo mema zaidi kuliko ile ya Abeli.
and to Jesus, the Mediator of the new covenant; and to the sprinkling, of his blood, which speaketh better than that of Abel.
25 Basi, jihadharini msije mkakataa kumsikiliza yeye ambaye anasema nanyi. Kama wale walikataa kumsikiliza yule aliyewaonya hapa duniani hawakuokoka, sisi tutawezaje kuokoka kama tukikataa kumsikiliza yule anayetuonya kutoka mbinguni?
Beware, therefore, lest ye refuse to hear him who speaketh with you. For if they escaped not, who refused to hear him who spake with them on the earth, how much more shall we not, if we refuse to hear him who speaketh with us from heaven?
26 Wakati ule sauti ilitetemesha nchi, lakini sasa ameahidi: “Nitatetemesha nchi tena, lakini si nchi tu bali pia mbingu.”
Whose voice then shook the earth; but now he hath promised, and said, yet again once more, I will shake not the earth only, but also heaven.
27 Neno hili: “tena” linatuonyesha kwamba vitu vyote vilivyoumbwa vitatetemeshwa na kutoweka ili vibaki vile visivyotetemeshwa.
And this his expression, Once more, indicateth the mutation of the things that are shaken, because they are fabricated; that the things which will not be shaken, may remain.
28 Sisi basi, na tushukuru kwani tunapokea utawala usiotikisika. Tuwe na shukrani na kumwabudu Mungu kwa namna itakayompendeza, kwa ibada na hofu;
Since, therefore, we have received a kingdom that is unshaken, let us grasp the grace whereby we may serve and please God, with reverence and fear.
29 maana Mungu wetu kweli ni moto mkali unaoteketeza.
For our God is a consuming fire.

< Wahebrania 12 >