< Wahebrania 12 >

1 Sisi tunalo kundi hili kubwa la mashahidi mbele yetu. Kwa hiyo tuondoe kila kizuizi kinachotuzuia, na dhambi ile inayotung'ang'ania. Tupige mbio kwa uvumilivu katika mashindano yaliyowekwa mbele yetu.
Daawnok'o noon gúúrts gaw jamanotsi no detstsotse no'ats kur wotts keew jamwotsi no'ats deshts morro k'a'úbayr no shinatse beyiru nohewo k'amde kup'ar woc'one.
2 Tumwelekee Yesu ambaye ndiye aliyeianzisha imani yetu na ambaye ataikamilisha. Kwa ajili ya furaha iliyokuwa inamngojea, yeye alivumilia kifo msalabani, bila kujali juu ya aibu yake, na sasa anaketi upande wa kulia wa kiti cha enzi cha Mungu.
Nowos'etwere no imnetiyo ned'itsonat s'eentstso Iyesus ats no ááwo gerdeniye, bíwere b́ shinatse need'wtsts geneúwatse tuutson jitatse k'irr gac'ewo eegok'oor b́ taawrawo jitatse gondbek'on k'iro k'amb́dek'i, Ik' be jooroke k'ano maants be b́wtsi.
3 Fikirini juu ya mambo yaliyompata Yesu, jinsi alivyostahimili upinzani mkubwa kwa watu wenye dhambi. Basi, msife moyo, wala msikate tamaa.
Eshe taahr, maac'o it k'ut'rawok'o morretswots bín bo k'eefere k'amdek'tso Iyesusi s'ilde'ere.
4 Maana katika kupambana na dhambi, ninyi hamjapigana mpaka kiasi cha kumwaga damu yenu.
It morronton mak'orewoke s'ats kud'efetsosh b́borfetso k'eferafa'tee.
5 Je, mmesahau yale maneno ya kutia moyo ambayo Mungu anawataja ninyi kuwa wanawe? “Mwanangu, usidharau adhabu ya Bwana, wala usife moyo anapokukanya.
Ik'o b́ nana'ikok'o woshdek't itango kup'shosh hank'o bí ettso batk'rerte, «T naayo! doonzo sezo ketik'aye, b́ hadoshowere maac'o k'ut'k'aye,
6 Maana Bwana humwadhibu kila anayempenda, humpinga kila anayekubali kuwa mwanae.”
Doonzo b́ shuntsoniye b́ sezfoni, B́ nayik'owosh dekt b́s'iliruwono b́fayefoni.»
7 Vumilieni adhabu kwani ni mafundisho; Mungu huwatendea ninyi kama wanawe. Maana ni mwana gani asiyeadhibiwa na baba yake?
Ik'o b́ nanaúwotsk'o itn b́tawtsotse b́ sezo k'amoore, b́ niho bín b́ sezraw na'o kone?
8 Lakini msipoadhibiwa kama wana wengine, basi, ninyi si wanawe, bali ni wana haramu.
Nana'a wotts jamwots bo daatsiru sezo it were daatso it k'azal dik'al itna boko nana'a itnaliye.
9 Zaidi ya hayo sisi tunawaheshimu wazazi wetu waliotuzaa hata wanapotuadhibu. Basi, tunapaswa kumtii zaidi Baba yetu wa kiroho ili tupate kuishi.
Haniyere okoon, noúnetsi sezf meetsi nihwots detsfone b́teshi, bonowere mangiye nomangifoni, bere kashon beyosh kashi weeron nih wottsosh iki bogshde azazewo aawk'oneya noosh geyiwo b́k'azeti!
10 Wazazi wetu hapa duniani walituadhibu kwa muda, kama wao wenyewe walivyoona kuwa vema; lakini Mungu anatuadhibu kwa ajili ya faida yetu wenyewe, tupate kuushiriki utakatifu wake.
Bosh sheengo araat b́ be'etsok'on muk' gizewush noon sezrne, bímo b́ S'ayino kayitwotsi nowotish sheengosh noon sezfe.
11 Kuadhibiwa si jambo la kufurahisha bali la kuhuzunisha. Lakini wale waliofunzwa kuwa na nidhamu mwishowe watavuna tuzo la amani kutoka katika maisha adili!
Sez jamo manorish shiyanitka bako geneúshitk areratse, ilomo man dandek'ts ashuwotssh jeenon s'eentso kááw fini shwo boosh daatsituwe.
12 Basi, inueni mikono yenu inayolegea na kuimarisha magoti yenu yaliyo dhaifu.
Mansh it kish neftswotsnat itgubr maawtswotsi kup'ide'ere.
13 Endeleeni kutembea katika njia iliyonyoka, ili kile kilicholemaa kisiumizwe, bali kiponywe.
Doklirwo b́ kashitwok'owa bako b́ beyoke keer b́ tisherawok'o, it tufooshowere weerindi kááwo woshde'ere.
14 Jitahidini kuishi kwa amani na watu wote. Ishini maisha ya utakatifu, kwa sababu hakuna mtu atakayemwona Bwana bila ya maisha kama hayo.
S'ayn woteraniye konworu doonzo bek'osh b́ falawotse, ash jamonton jeenon bewore, S'ayinon beyoshowere kup'owere,
15 Jitahidini sana mtu yeyote asije akapoteza neema ya Mungu. Muwe waangalifu ili mti mchungu usizuke kati yenu na kuwaua wengi kwa sumu yake.
Ititsere konshoru Ik' s'aato b́ shaprawok'o it atso korde'ere, mank'owere s'aam shuu iko shuwit s'ap'o ititse boc'r iti b́ kic'irawok'o, aywotsno b́ kimshrawok'o korde'ere.
16 Jihadharini ili miongoni mwenu pasiwe na mtu mwasherati au mtu asiyemcha Mungu kama Esau, aliyeuza haki yake ya mzaliwa wa kwanza kwa mlo mmoja.
Gusiyetso wee iknoti móósha ett b́ took k'aabo kemtso Esawkok'o shayri ash woterawo ititsere b́ daatserawok'o it atso korde'ere.
17 Ninyi mnafahamu kwamba hata alipotaka kuipata tena ile baraka iliyokuwa yake, alikataliwa, maana hakupata tena nafasi ya kutubu, ingawa aliitafuta kwa machozi.
Esaw il s'aato aaniy dek'osh b́ geyor s'aatman bísh baziyetsok'o danfte, b́k'altso woniyosh kup'dek't eepfetst b́geyiyalor weero daatso falratse.
18 Ninyi hamkuwasili mlimani Sinai, ambao unaweza kushikika kama walivyofanya watu wa Israeli, hamkufika kwenye moto uwakao, penye giza, tufani,
Kishon shuu'etwok wee mis'etuo Sin gurok borafa'ate, bamplomants, shatits t'alwots, eegurahi jongokowere,
19 mvumo wa tarumbeta na sauti ya maneno. Wale waliosikia sauti hiyo waliomba wasisikie tena neno jingine,
Ezbedi k'arokowere wee keeweyiru aap'o b́ shishetwoko borafa'ate, aap'ets keewman shishts ashuwots «Eshe bodre haniyak k'osho noosh aap'ek'aye» et bok'onfetso bodrnee.
20 kwani hawakuweza kustahimili amri iliyotolewa: “Atakayegusa mlima huu, hata kama ni mnyama, atapigwa mawe.”
«Gizo dab gurman b́ t'awiyal Shútson togeyar k'irwee» Etiru tzaziyo boats b́mangtsosh bín kuro falratsne.
21 Hayo yote yalionekana ya kutisha mno, hata Mose akasema, “Naogopa na kutetemeka.”
Manoke bek'ets keewman eenonat shatiik b́teshtsotse dab́ Muse woor «Taa shataat, k'ewere» bí et.
22 Lakini ninyi mmefika katika mlima wa Sioni, kwenye mji wa Mungu aliye hai. Mmefika Yerusalemu, mji wa mbinguni, ambapo wamekusanyika malaika elfu nyingi wasiohesabika.
Itiyelee S'iyon guromants t'inwtsertee, bihe kashetso Ik'o kito wotts daritstsu Iyerusalemiye, genee'úwon kakwedek'tswotsok, ay kumon taawet mlakiwotsok t'inrte,
23 Mmefika kwenye kusanyiko kubwa la wazaliwa wa kwanza wa Mungu, ambao majina yao yameandikwa mbinguni. Mnasimama mbele ya Mungu aliye hakimu wa wote, na mbele ya roho za watu waadilifu waliofanywa kuwa wakamilifu.
Bo shúútso darots guut'etswotsok, k'aab nana'a wotts amantsuwots ko'eetsok, kááw angshitu Izar izewerokonat s'ayin wotat daatsts shayirwotsok t'inrte.
24 Mmefika kwa Yesu ambaye ameratibisha agano jipya, na ambaye damu yake iliyomwagika inasema mambo mema zaidi kuliko ile ya Abeli.
Handr taareyosh dag taalotse manik wottso Iyesusnat Abeel s'atsoniyere k'antso keewiru fakets s'atsookowere t'inrte.
25 Basi, jihadharini msije mkakataa kumsikiliza yeye ambaye anasema nanyi. Kama wale walikataa kumsikiliza yule aliyewaonya hapa duniani hawakuokoka, sisi tutawezaje kuokoka kama tukikataa kumsikiliza yule anayetuonya kutoka mbinguni?
Keewirman de'atsone it erawok'o itatso korde'ere, Ekeewots Ik'o ashon datsatse boosh b́ keewre k'ewatsone ettswots b́shirotse kesho bomaawiyakon, bére noo darotse noosh keewirwo dek'onok'azal awuk'o kalrniya b́ kishotse kesho nofaliti!
26 Wakati ule sauti ilitetemesha nchi, lakini sasa ameahidi: “Nitatetemesha nchi tena, lakini si nchi tu bali pia mbingu.”
Manoor bí aap'o datso shek'ere, «andmó datsu mec'ro b́woterawo aani dabr darono dabde'er shek'ituwe» eton keewure.
27 Neno hili: “tena” linatuonyesha kwamba vitu vyote vilivyoumbwa vitatetemeshwa na kutoweka ili vibaki vile visivyotetemeshwa.
Han «Iknoto dabr, » etiru keewoniye b́ kitsiriyee shek'eraw keewwots kup'arr bobetuwok'o shek'eyirwots wee azeets keewwots bobeyoke botuwitok'oniye.
28 Sisi basi, na tushukuru kwani tunapokea utawala usiotikisika. Tuwe na shukrani na kumwabudu Mungu kwa namna itakayompendeza, kwa ibada na hofu;
Eshe noo shek'eraw mengstu nonaatetwotse Ik'o udoonee, b́ gene'úwitwok'oon mangiyonat shatoon bísh finone.
29 maana Mungu wetu kweli ni moto mkali unaoteketeza.
No Ik'o Izar Izewer mitsit tawok'oyiye.

< Wahebrania 12 >