< Wahebrania 1 >

1 Hapo zamani, Mungu alisema na babu zetu mara nyingi kwa namna nyingi kwa njia ya manabii,
purā ya īśvaro bhaviṣyadvādibhiḥ pitṛlokebhyo nānāsamaye nānāprakāraṁ kathitavān
2 lakini siku hizi za mwisho, amesema nasi kwa njia ya Mwanae. Yeye ndiye ambaye kwa njia yake Mungu aliumba ulimwengu na akamteua avimiliki vitu vyote. (aiōn g165)
sa etasmin śeṣakāle nijaputreṇāsmabhyaṁ kathitavān| sa taṁ putraṁ sarvvādhikāriṇaṁ kṛtavān tenaiva ca sarvvajaganti sṛṣṭavān| (aiōn g165)
3 Yeye ni mng'ao wa utukufu wa Mungu, na mfano kamili wa hali ya Mungu mwenyewe, akiutegemeza ulimwengu kwa neno lake lenye nguvu. Baada ya kuwapatia binadamu msamaha wa dhambi zao, aliketi huko juu mbinguni, upande wa kulia wa Mungu Mkuu.
sa putrastasya prabhāvasya pratibimbastasya tattvasya mūrttiścāsti svīyaśaktivākyena sarvvaṁ dhatte ca svaprāṇairasmākaṁ pāpamārjjanaṁ kṛtvā ūrddhvasthāne mahāmahimno dakṣiṇapārśve samupaviṣṭavān|
4 Mwana ni mkuu zaidi kuliko malaika, kama vile jina alilopewa na Mungu ni kuu zaidi kuliko jina lao.
divyadūtagaṇād yathā sa viśiṣṭanāmno 'dhikārī jātastathā tebhyo'pi śreṣṭho jātaḥ|
5 Maana Mungu hakumwambia kamwe hata mmoja wa malaika wake: “Wewe ni Mwanangu; Mimi leo nimekuwa Baba yako.” Wala hakusema juu ya malaika yeyote: “Mimi nitakuwa Baba yake, naye atakuwa Mwanangu.”
yato dūtānāṁ madhye kadācidīśvareṇedaṁ ka uktaḥ? yathā, "madīyatanayo 'si tvam adyaiva janito mayā|" punaśca "ahaṁ tasya pitā bhaviṣyāmi sa ca mama putro bhaviṣyati|"
6 Lakini Mungu alipokuwa anamtuma Mwanae mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, alisema: “Malaika wote wa Mungu wanapaswa kumwabudu.”
aparaṁ jagati svakīyādvitīyaputrasya punarānayanakāle tenoktaṁ, yathā, "īśvarasya sakalai rdūtaireṣa eva praṇamyatāṁ|"
7 Lakini kuhusu malaika, Mungu alisema: “Mungu awafanya malaika wake kuwa pepo, na watumishi wake kuwa ndimi za moto.”
dūtān adhi tenedam uktaṁ, yathā, "sa karoti nijān dūtān gandhavāhasvarūpakān| vahniśikhāsvarūpāṁśca karoti nijasevakān||"
8 Lakini kumhusu Mwana, Mungu alisema: “Utawala wako ee Mungu, wadumu milele na milele! Wewe wawatawala watu wako kwa haki. (aiōn g165)
kintu putramuddiśya tenoktaṁ, yathā, "he īśvara sadā sthāyi tava siṁhāsanaṁ bhavet| yāthārthyasya bhaveddaṇḍo rājadaṇḍastvadīyakaḥ| (aiōn g165)
9 Wewe wapenda uadilifu na kuchukia uovu. Ndiyo maana Mungu, Mungu wako amekuweka wakfu na kukumiminia furaha kubwa zaidi kuliko wenzako.”
puṇye prema karoṣi tvaṁ kiñcādharmmam ṛtīyase| tasmād ya īśa īśaste sa te mitragaṇādapi| adhikāhlādatailena secanaṁ kṛtavān tava||"
10 Pia alisema: “Bwana, wewe uliumba dunia hapo mwanzo, mbingu ni kazi ya mikono yako.
punaśca, yathā, "he prabho pṛthivīmūlam ādau saṁsthāpitaṁ tvayā| tathā tvadīyahastena kṛtaṁ gaganamaṇḍalaṁ|
11 Hizo zitatoweka, lakini wewe wabaki daima, zote zitachakaa kama vazi.
ime vinaṁkṣyatastvantu nityamevāvatiṣṭhase| idantu sakalaṁ viśvaṁ saṁjariṣyati vastravat|
12 Utazikunjakunja kama koti, nazo zitabadilishwa kama vazi. Lakini wewe ni yuleyule daima, na maisha yako hayatakoma.”
saṅkocitaṁ tvayā tattu vastravat parivartsyate| tvantu nityaṁ sa evāsī rnirantāstava vatsarāḥ||"
13 Mungu hakumwambia kamwe hata mmoja wa malaika wake: “Keti upande wangu wa kulia, mpaka niwaweke adui zako chini ya miguu yako.”
aparaṁ dūtānāṁ madhye kaḥ kadācidīśvareṇedamuktaḥ? yathā, "tavārīn pādapīṭhaṁ te yāvannahi karomyahaṁ| mama dakṣiṇadigbhāge tāvat tvaṁ samupāviśa||"
14 Malaika ni roho tu wanaomtumikia Mungu, na Mungu huwatuma wawasaidie wale watakaopokea wokovu.
ye paritrāṇasyādhikāriṇo bhaviṣyanti teṣāṁ paricaryyārthaṁ preṣyamāṇāḥ sevanakāriṇa ātmānaḥ kiṁ te sarvve dūtā nahi?

< Wahebrania 1 >