< Wagalatia 1 >

1 Mimi Paulo mtume,
Paul, an apostle, not from men, nor through man, but through Jesus Christ, and God the Father, who raised him from the dead, —
2 na ndugu wote walio pamoja nami, tunayaandikia makanisa yaliyoko Galatia. Mimi nimepata kuwa mtume si kutokana na mamlaka ya binadamu, wala si kwa nguvu ya mtu, bali kwa uwezo wa Yesu Kristo na wa Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka wafu.
and all the brethren that are with me, to the churches of Galatia:
3 Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
Grace be to you and peace from God the Father, and from our Lord Jesus Christ,
4 Kristo alijitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na mapenzi ya Mungu wetu na Baba, ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu mbaya wa sasa. (aiōn g165)
who gave himself for our sins, that he might deliver us from the present evil world, according to the will of God our Father; (aiōn g165)
5 Kwake yeye uwe utukufu milele! Amina. (aiōn g165)
to whom be the glory for ever and ever! Amen. (aiōn g165)
6 Nashangaa kwamba muda mfupi tu umepita, nanyi mnamwasi yule aliyewaita kwa neema ya Kristo, mkafuata Habari Njema ya namna nyingine.
I marvel that ye are so soon turning from him that called you in the grace of Christ, to a different gospel;
7 Lakini hakuna “Habari Njema” nyingine. Ukweli ni kwamba wako watu wanaowavurugeni, watu wanaotaka kuipotosha Habari Njema ya Kristo.
which is not another; only there are certain persons who are troubling you, and seeking to change entirely the gospel of Christ.
8 Lakini, hata kama mmoja wetu au malaika kutoka mbinguni, atawahubirieni Habari Njema tofauti na ile tuliyowahubirieni sisi, basi huyo na alaaniwe!
But even if we or an angel from heaven should preach a gospel to you contrary to that which we preached to you, let him be accursed!
9 Tulikwisha sema, na sasa nasema tena: kama mtu yeyote anawahubirieni Habari Njema ya aina nyingine, tofauti na ile mliyokwisha pokea, huyo na alaaniwe!
As we have said before, so I now say again, If any one preach a gospel to you contrary to that which ye received, let him be accursed!
10 Sasa nataka kibali cha nani: cha binadamu, ama cha Mungu? Au je, nataka kuwapendeza watu? Kama ningefanya hivyo, mimi singekuwa kamwe mtumishi wa Kristo.
For do I now seek the favor of men, or of God? Or am I endeavoring to please men? If I were still pleasing men, I should not be the servant of Christ.
11 Ndugu, napenda mfahamu kwamba ile Habari Njema niliyoihubiri si ujumbe wa kibinadamu.
But I assure you, brethren, that the gospel which was preached by me is not after man;
12 Wala mimi sikuipokea kutoka kwa binadamu, wala sikufundishwa na mtu. Yesu Kristo mwenyewe ndiye aliyenifunulia.
for I did not receive it from man nor was I taught it by any man, but it was revealed to me by Jesus Christ.
13 Bila shaka mlikwisha sikia jinsi nilivyokuwa ninaishi zamani kwa kuzingatia dini ya Kiyahudi, na jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kupita kiasi na kutaka kuliharibu kabisa.
For ye have heard of my conduct formerly in Judaism; that beyond measure I persecuted the church of God, and was destroying it,
14 Naam, mimi niliwashinda wengi wa wananchi wenzangu wa rika langu katika kuizingatia dini ya Kiyahudi, nikajitahidi sana kuyashika mapokeo ya wazee wetu.
and made progress in Judaism beyond many of the same age with me in my nation, being more exceedingly zealous for the traditions of my fathers.
15 Lakini Mungu, kwa neema yake, alikuwa ameniteua hata kabla sijazaliwa, akaniita nimtumikie.
But when it pleased him who set me apart from my very birth, and called me through his grace,
16 Mara tu alipoamua kunifunulia Mwanae kusudi niihubiri Habari Njema yake kwa watu wa mataifa mengine, bila kutafuta maoni ya binadamu,
to reveal his Son within me, that I might publish the glad tidings of him among the gentiles, immediately I conferred not with flesh and blood,
17 na bila kwenda kwanza Yerusalemu kwa wale waliopata kuwa mitume kabla yangu, nilikwenda kwanza Arabia, kisha nikarudi tena Damasko.
neither did I go up to Jerusalem to those who were apostles before me, but I went away into Arabia, and returned again to Damascus.
18 Ilikuwa tu baada ya miaka mitatu, ndipo nilipokwenda Yerusalemu kuonana na Kefa; nilikaa kwake siku kumi na tano.
Then, after three years, I went up to Jerusalem to become acquainted with Cephas, and stayed with him fifteen days;
19 Lakini sikuwaona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
but no other of the apostles did I see, save James the brother of the Lord.
20 Haya ninayowaandikieni, Mungu anajua; sisemi uongo.
Now as to what I am writing to you, behold, before God, I do not lie.
21 Baadaye nilikwenda katika tarafa za Siria na Kilikia.
Afterwards I came into the regions of Syria and Cilicia;
22 Wakati huo, mimi binafsi sikujulikana kwa jumuiya za Wakristo kule Yudea.
and I was unknown by face to the churches of Judaea which were in Christ;
23 Walichokuwa wanajua ni kile tu walichosikia: “Mtu yule aliyekuwa akitutesa hapo awali, sasa anaihubiri imani ileile aliyokuwa anajaribu kuiangamiza.”
but they were only hearing that “He who was once our persecutor is now preaching the faith which he was once destroying”;
24 Basi, wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.
and they glorified God in me.

< Wagalatia 1 >