< Wagalatia 1 >

1 Mimi Paulo mtume,
Paul, an apostle, (not from men, nor by man, but by Jesus Christ, and God the Father, who raised him from the dead, )
2 na ndugu wote walio pamoja nami, tunayaandikia makanisa yaliyoko Galatia. Mimi nimepata kuwa mtume si kutokana na mamlaka ya binadamu, wala si kwa nguvu ya mtu, bali kwa uwezo wa Yesu Kristo na wa Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka wafu.
and all the brethren that are with me, to the churches of Galatia:
3 Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
grace be to you, and peace from God the Father, and from our Lord Jesus Christ,
4 Kristo alijitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na mapenzi ya Mungu wetu na Baba, ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu mbaya wa sasa. (aiōn g165)
who gave himself for our sins, that he might deliver us from this present evil age, according to the will of our God and Father, (aiōn g165)
5 Kwake yeye uwe utukufu milele! Amina. (aiōn g165)
to whom be glory from age to age. Amen. (aiōn g165)
6 Nashangaa kwamba muda mfupi tu umepita, nanyi mnamwasi yule aliyewaita kwa neema ya Kristo, mkafuata Habari Njema ya namna nyingine.
I am astonished that you are so soon turning away from him that called you into the grace of Christ, to another gospel:
7 Lakini hakuna “Habari Njema” nyingine. Ukweli ni kwamba wako watu wanaowavurugeni, watu wanaotaka kuipotosha Habari Njema ya Kristo.
which is nothing else than that there are some who trouble you, and are determined to pervert the gospel of the Christ.
8 Lakini, hata kama mmoja wetu au malaika kutoka mbinguni, atawahubirieni Habari Njema tofauti na ile tuliyowahubirieni sisi, basi huyo na alaaniwe!
But though we, or an angel from heaven, preach to you any other gospel than that which we have preached, let him be accursed.
9 Tulikwisha sema, na sasa nasema tena: kama mtu yeyote anawahubirieni Habari Njema ya aina nyingine, tofauti na ile mliyokwisha pokea, huyo na alaaniwe!
As we said before, so even now I say again, if any one preaches to you any other gospel than that which you have received, let him be accursed.
10 Sasa nataka kibali cha nani: cha binadamu, ama cha Mungu? Au je, nataka kuwapendeza watu? Kama ningefanya hivyo, mimi singekuwa kamwe mtumishi wa Kristo.
For, do I now seek the favor of men, or of God? or do I strive to please men? If, indeed, I would still please men, I should not be the servant of Christ.
11 Ndugu, napenda mfahamu kwamba ile Habari Njema niliyoihubiri si ujumbe wa kibinadamu.
But I make known to you, brethren, that the gospel which is preached by me, is not according to man:
12 Wala mimi sikuipokea kutoka kwa binadamu, wala sikufundishwa na mtu. Yesu Kristo mwenyewe ndiye aliyenifunulia.
for neither did I receive it from man, nor was it taught me, but by the revelation of Jesus Christ.
13 Bila shaka mlikwisha sikia jinsi nilivyokuwa ninaishi zamani kwa kuzingatia dini ya Kiyahudi, na jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kupita kiasi na kutaka kuliharibu kabisa.
For you have heard of my former mode of life in Judaism, that I greatly persecuted the church of God, and laid it waste;
14 Naam, mimi niliwashinda wengi wa wananchi wenzangu wa rika langu katika kuizingatia dini ya Kiyahudi, nikajitahidi sana kuyashika mapokeo ya wazee wetu.
and I surpassed in Judaism many of my own age and nation, being more exceedingly zealous for the tradition of my fathers.
15 Lakini Mungu, kwa neema yake, alikuwa ameniteua hata kabla sijazaliwa, akaniita nimtumikie.
But when God, who chose me from my mother’s womb, and called me by his grace, was pleased
16 Mara tu alipoamua kunifunulia Mwanae kusudi niihubiri Habari Njema yake kwa watu wa mataifa mengine, bila kutafuta maoni ya binadamu,
to reveal his Sou in me, that I might preach him among the Gentiles, I at once declined all conference with flesh and blood:
17 na bila kwenda kwanza Yerusalemu kwa wale waliopata kuwa mitume kabla yangu, nilikwenda kwanza Arabia, kisha nikarudi tena Damasko.
nor did I go up to Jerusalem, to those who were apostles before me; but I went away into Arabia, and then returned to Damascus.
18 Ilikuwa tu baada ya miaka mitatu, ndipo nilipokwenda Yerusalemu kuonana na Kefa; nilikaa kwake siku kumi na tano.
Then, after three years, I went up to Jerusalem, in order to become personally acquainted with Peter; and I remained with him fifteen days:
19 Lakini sikuwaona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
but of the apostles I saw no other, but James the brother of the Lord.
20 Haya ninayowaandikieni, Mungu anajua; sisemi uongo.
With respect to the things which I now write to you, behold, before God I lie not.
21 Baadaye nilikwenda katika tarafa za Siria na Kilikia.
Then, I went into the regions of Syria and Cilicia:
22 Wakati huo, mimi binafsi sikujulikana kwa jumuiya za Wakristo kule Yudea.
but I was not known, in person, to the churches of Judea which are in Christ.
23 Walichokuwa wanajua ni kile tu walichosikia: “Mtu yule aliyekuwa akitutesa hapo awali, sasa anaihubiri imani ileile aliyokuwa anajaribu kuiangamiza.”
They had heard only that he who formerly persecuted us was now preaching the faith which he once destroyed.
24 Basi, wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.
And they glorified God in me.

< Wagalatia 1 >