< Wagalatia 6 >

1 Ndugu, kama mkimwona mtu fulani amekosea, basi, ninyi mnaoongozwa na Roho mwonyeni mtu huyo ajirekebishe; lakini fanyeni hivyo kwa upole, mkiwa na tahadhari msije nanyi wenyewe mkajaribiwa.
Brothers, even if someone is caught in some wrongdoing, you who are spiritual must restore such a one in a spirit of gentleness; looking to yourself so that you also are not tempted.
2 Saidianeni kubeba mizigo yenu na hivyo mtatimiza sheria ya Kristo.
Bear one another's burdens, and so you will fulfill the law of Christ.
3 Mtu akijiona kuwa ni kitu, na kumbe si kitu, huyo anajidanganya mwenyewe.
For if anyone thinks himself to be something when he is nothing, he deceives himself.
4 Lakini kila mmoja na aupime vizuri mwenendo wake mwenyewe. Ukiwa mwema, basi, anaweza kuona fahari juu ya alichofanya bila kuwa na sababu ya kujilinganisha na mtu mwingine.
But let each one test his own work, and then he will take pride in himself and not in his neighbor.
5 Maana kila mmoja anao mzigo wake mwenyewe wa kubeba.
For every person will bear his own load.
6 Mwenye kufundishwa neno la Mungu na amshirikishe mwalimu wake riziki zake.
But let him who is taught in the word share all good things with him who teaches.
7 Msidanganyike; Mungu hafanyiwi dhihaka. Alichopanda mtu ndicho atakachovuna.
Do not be deceived. God is not mocked, for whatever a person sows, that he will also reap.
8 Apandaye katika tamaa za kidunia, atavuna humo uharibifu; lakini akipanda katika Roho, atavuna kutoka kwa Roho uzima wa milele. (aiōnios g166)
For he who sows to his own flesh will from the flesh reap corruption. But he who sows to the Spirit will from the Spirit reap everlasting life. (aiōnios g166)
9 Basi, tusichoke kutenda mema; maana tusipolegea tutavuna mavuno kwa wakati wake.
Let us not be weary in doing good, for we will reap in due season, if we do not give up.
10 Kwa hiyo, tukiwa bado na wakati, tuwatendee watu wote mema, na hasa ndugu wa imani yetu.
So then, as we have opportunity, let us do what is good toward all people, and especially toward those who are of the household of the faith.
11 Tazameni jinsi nilivyoandika kwa herufi kubwa, kwa mkono wangu mwenyewe.
See with what large letters I write to you with my own hand.
12 Wale wanaotaka kuonekana wazuri kwa mambo ya mwili ndio wanaotaka kuwalazimisha ninyi mtahiriwe. Wanafanya hivyo kwa sababu moja tu: kusudi wao wenyewe wasije wakadhulumiwa kwa sababu ya msalaba wa Kristo.
As many as desire to make a good showing in the flesh, they compel you to be circumcised; only that they may not be persecuted for the cross of Christ.
13 Maana, hao wenyewe waliotahiriwa hawaishiki Sheria; huwataka ninyi mtahiriwe wapate kujivunia alama hiyo mwilini mwenu.
For even they who receive circumcision do not keep the law themselves, but they desire to have you circumcised, that they may boast in your flesh.
14 Lakini mimi sitajivunia kamwe chochote isipokuwa msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo; maana kwa njia ya msalaba huo ulimwengu umesulubiwa kwangu, nami nimesulubiwa kwa ulimwengu.
But far be it from me to boast, except in the cross of our Lord Jesus Christ, through which the world has been crucified to me, and I to the world.
15 Kutahiriwa au kutotahiriwa si kitu; cha maana ni kuwa kiumbe kipya.
For neither is circumcision anything, nor uncircumcision, but a new creation.
16 Wanaoufuata mwongozo huo nawatakia amani na huruma; amani na huruma kwa Israeli—Wateule wa Mungu.
As many as walk by this rule, peace and mercy be on them, and on God's Israel.
17 Basi, sasa mtu yeyote asinisumbue tena, maana alama nilizo nazo mwilini mwangu ni zile za Yesu.
From now on, let no one cause me any trouble, for I bear the marks of Jesus branded on my body.
18 Ndugu, nawatakieni ninyi nyote neema ya Bwana wetu Kristo. Amina.
The grace of our Lord Jesus Christ be with your spirit, brothers. Amen.

< Wagalatia 6 >