< Wagalatia 6 >

1 Ndugu, kama mkimwona mtu fulani amekosea, basi, ninyi mnaoongozwa na Roho mwonyeni mtu huyo ajirekebishe; lakini fanyeni hivyo kwa upole, mkiwa na tahadhari msije nanyi wenyewe mkajaribiwa.
Even if any one should be overtaken in a fault, brothers, you that are spiritual ought, in a gentle spirit, to restore such a one, each one of you looking to himself, lest you too be tempted.
2 Saidianeni kubeba mizigo yenu na hivyo mtatimiza sheria ya Kristo.
Ever be bearing one another’s burdens, and so be fulfilling the law of Christ.
3 Mtu akijiona kuwa ni kitu, na kumbe si kitu, huyo anajidanganya mwenyewe.
If a man fancies himself to be somebody when he is really nobody he is deceiving himself.
4 Lakini kila mmoja na aupime vizuri mwenendo wake mwenyewe. Ukiwa mwema, basi, anaweza kuona fahari juu ya alichofanya bila kuwa na sababu ya kujilinganisha na mtu mwingine.
Let each one test his own work, and he will then have something to be proud of by comparing himself with himself, and not with any one else;
5 Maana kila mmoja anao mzigo wake mwenyewe wa kubeba.
for every one must carry his own pack load.
6 Mwenye kufundishwa neno la Mungu na amshirikishe mwalimu wake riziki zake.
He, however, who is being taught in the message, should always share with his instructor in all the good things which he possesses.
7 Msidanganyike; Mungu hafanyiwi dhihaka. Alichopanda mtu ndicho atakachovuna.
Be not deceived. God is not mocked. Whatever a man sows, that will he also reap.
8 Apandaye katika tamaa za kidunia, atavuna humo uharibifu; lakini akipanda katika Roho, atavuna kutoka kwa Roho uzima wa milele. (aiōnios g166)
The man who is sowing to his flesh will of the flesh reap corruption; but he who is sowing to the Spirit will of the Spirit reap life eternal. (aiōnios g166)
9 Basi, tusichoke kutenda mema; maana tusipolegea tutavuna mavuno kwa wakati wake.
And let us not be weary in well-doing, for in due season we shall reap if we faint not.
10 Kwa hiyo, tukiwa bado na wakati, tuwatendee watu wote mema, na hasa ndugu wa imani yetu.
So then, as we have opportunity, let is do good to all men, but especially to those who are of the household of faith.
11 Tazameni jinsi nilivyoandika kwa herufi kubwa, kwa mkono wangu mwenyewe.
See with what large letters I have written to you in my own handwriting!
12 Wale wanaotaka kuonekana wazuri kwa mambo ya mwili ndio wanaotaka kuwalazimisha ninyi mtahiriwe. Wanafanya hivyo kwa sababu moja tu: kusudi wao wenyewe wasije wakadhulumiwa kwa sababu ya msalaba wa Kristo.
Those who are trying to compel you to be circumcised are such as wish to make a fair show in the flesh, only that they may not suffer persecution for the cross of Christ.
13 Maana, hao wenyewe waliotahiriwa hawaishiki Sheria; huwataka ninyi mtahiriwe wapate kujivunia alama hiyo mwilini mwenu.
Even those who are being circumcised, are not themselves keeping the Law, but they want you to be circumcised so that they may glory in your flesh.
14 Lakini mimi sitajivunia kamwe chochote isipokuwa msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo; maana kwa njia ya msalaba huo ulimwengu umesulubiwa kwangu, nami nimesulubiwa kwa ulimwengu.
God forbid that I should glory in anything except in the cross of our Lord Jesus Christ, upon which the world has been crucified to me and I have been crucified to the world.
15 Kutahiriwa au kutotahiriwa si kitu; cha maana ni kuwa kiumbe kipya.
For in Jesus Christ neither is circumcision anything, nor uncircumcision, but a new creation.
16 Wanaoufuata mwongozo huo nawatakia amani na huruma; amani na huruma kwa Israeli—Wateule wa Mungu.
On all who will govern their lives by this rule and on the Israel of God may peace and mercy rest.
17 Basi, sasa mtu yeyote asinisumbue tena, maana alama nilizo nazo mwilini mwangu ni zile za Yesu.
From this time forth let no one trouble me, for I bear branded in my body the marks of Jesus, my Master.
18 Ndugu, nawatakieni ninyi nyote neema ya Bwana wetu Kristo. Amina.
May the grace of our Lord Jesus Christ be with your spirit, brothers. Amen.

< Wagalatia 6 >