< Wagalatia 6 >

1 Ndugu, kama mkimwona mtu fulani amekosea, basi, ninyi mnaoongozwa na Roho mwonyeni mtu huyo ajirekebishe; lakini fanyeni hivyo kwa upole, mkiwa na tahadhari msije nanyi wenyewe mkajaribiwa.
My friends, if someone is led astray by sin, you who are spiritual should bring them back with a gentle spirit. Watch out that you don't get tempted too.
2 Saidianeni kubeba mizigo yenu na hivyo mtatimiza sheria ya Kristo.
Carry each other's burdens, for in this way you fulfill the law of Christ.
3 Mtu akijiona kuwa ni kitu, na kumbe si kitu, huyo anajidanganya mwenyewe.
Those who think they're really something—when they're actually nothing—only fool themselves.
4 Lakini kila mmoja na aupime vizuri mwenendo wake mwenyewe. Ukiwa mwema, basi, anaweza kuona fahari juu ya alichofanya bila kuwa na sababu ya kujilinganisha na mtu mwingine.
Carefully examine your actions. Then you can be satisfied with yourself, without comparing yourself to anyone else.
5 Maana kila mmoja anao mzigo wake mwenyewe wa kubeba.
We have to take responsibility for ourselves.
6 Mwenye kufundishwa neno la Mungu na amshirikishe mwalimu wake riziki zake.
Those that are taught the Word should treat their teachers well, sharing with them all good things.
7 Msidanganyike; Mungu hafanyiwi dhihaka. Alichopanda mtu ndicho atakachovuna.
Don't be fooled, God can't be treated with contempt: whatever you sow, that's what you reap.
8 Apandaye katika tamaa za kidunia, atavuna humo uharibifu; lakini akipanda katika Roho, atavuna kutoka kwa Roho uzima wa milele. (aiōnios g166)
If you sow according to your sinful human nature, from that nature you'll reap self-destruction. But if you sow according to the Spirit, from the Spirit you'll reap eternal life. (aiōnios g166)
9 Basi, tusichoke kutenda mema; maana tusipolegea tutavuna mavuno kwa wakati wake.
Let's never tire of doing good, for we'll reap a harvest at the proper time, if we don't give up.
10 Kwa hiyo, tukiwa bado na wakati, tuwatendee watu wote mema, na hasa ndugu wa imani yetu.
So while we have time, let's do good to everyone—especially to those who belong to the family of faith.
11 Tazameni jinsi nilivyoandika kwa herufi kubwa, kwa mkono wangu mwenyewe.
Notice how big the letters are, now that I'm writing with my own hand!
12 Wale wanaotaka kuonekana wazuri kwa mambo ya mwili ndio wanaotaka kuwalazimisha ninyi mtahiriwe. Wanafanya hivyo kwa sababu moja tu: kusudi wao wenyewe wasije wakadhulumiwa kwa sababu ya msalaba wa Kristo.
Those people who only want to make a good impression are forcing you to be circumcised just so they won't be persecuted for the cross of Christ.
13 Maana, hao wenyewe waliotahiriwa hawaishiki Sheria; huwataka ninyi mtahiriwe wapate kujivunia alama hiyo mwilini mwenu.
Even those who are circumcised don't keep the law, but they want to have you circumcised so that they can boast about you and claim you as their followers.
14 Lakini mimi sitajivunia kamwe chochote isipokuwa msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo; maana kwa njia ya msalaba huo ulimwengu umesulubiwa kwangu, nami nimesulubiwa kwa ulimwengu.
May I never boast except in the cross of our Lord Jesus Christ. Through this cross, the world has been crucified to me, and I've been crucified as far as the world is concerned.
15 Kutahiriwa au kutotahiriwa si kitu; cha maana ni kuwa kiumbe kipya.
Circumcision or uncircumcision doesn't matter—what matters is that we're created brand new!
16 Wanaoufuata mwongozo huo nawatakia amani na huruma; amani na huruma kwa Israeli—Wateule wa Mungu.
Peace and mercy to all who follow this principle, and to the Israel of God!
17 Basi, sasa mtu yeyote asinisumbue tena, maana alama nilizo nazo mwilini mwangu ni zile za Yesu.
Please, don't anyone trouble me anymore, because I carry on my body the scars of Jesus.
18 Ndugu, nawatakieni ninyi nyote neema ya Bwana wetu Kristo. Amina.
My brothers and sisters, may the grace of our Lord Jesus Christ be with your spirit. Amen.

< Wagalatia 6 >