< Wagalatia 2 >

1 Baada ya miaka kumi na minne, nilikwenda tena Yerusalemu pamoja na Barnaba; nilimchukua pia Tito pamoja nami.
Потом же по четыренадесяти летех паки взыдох во Иерусалим с Варнавою, поем с собою и Тита.
2 Kwenda kwangu kulitokana na ufunuo alionipa Mungu. Katika kikao cha faragha niliwaeleza hao viongozi ujumbe wa Habari Njema niliohubiri kwa watu wa mataifa. Nilifanya hivyo kusudi kazi yangu niliyokuwa nimefanya, na ile ninayofanya sasa isije ikawa bure.
Взыдох же по откровению, и предложих им благовествование, еже проповедую во языцех, наедине же мнимым, да не како вотще теку, или текох.
3 Lakini, hata mwenzangu Tito, ambaye ni Mgiriki, hakulazimika kutahiriwa,
Но ни Тит, иже со мною, Еллин сый, нужден бысть обрезатися.
4 ingawa kulikuwa na ndugu wengine wa uongo waliotaka atahiriwe. Watu hawa walijiingiza kwa ujanja na kupeleleza uhuru wetu tulio nao katika kuungana na Kristo Yesu, ili wapate kutufanya watumwa.
И за пришедшую лжебратию, иже привнидоша соглядати свободы нашея, юже имамы о Христе Иисусе, да нас поработят:
5 Hatukukubaliana nao hata kidogo ili ukweli wa Habari Njema ubaki nanyi daima.
имже ни к часу повинухомся в покорение, да истина благовестия пребудет в вас.
6 Lakini watu hawa wanaosemekana kuwa ni viongozi—kama kweli walikuwa hivyo au sivyo, kwangu si kitu, maana Mungu hahukumu kwa kuangalia mambo ya nje—watu hawa hawakuwa na kitu cha kuongeza katika Habari hii Njema kama niihubirivyo.
От мнящихся же быти что, якови некогда беша, ничтоже ми разнствует: лица Бог человеча не приемлет. Мне бо мнимии ничтоже привозложиша:
7 Badala yake, walitambua kwamba Mungu alikuwa amenituma kuhubiri Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine kama vile Petro alivyokuwa ametumwa kuihubiri kwa Wayahudi.
но сопротивное, уразумевше, яко уверено ми бысть благовестие необрезания, якоже Петру обрезания:
8 Maana, yule aliyemwezesha Petro kuwa mtume kwa Wayahudi, ndiye aliyeniwezesha nami pia kuwa mtume kwa watu wa mataifa mengine.
ибо Споспешествовавый Петру в послание обрезания, споспешествова и мне во языки:
9 Basi, Yakobo, Kefa na Yohane, ambao waonekana kuwa viongozi wakuu, walitambua kwamba Mungu alinijalia neema hiyo, wakatushika sisi mkono, yaani Barnaba na mimi, iwe ishara ya ushirikiano. Sisi ilitupasa tukafanye kazi kati ya watu wa mataifa mengine, na wao kati ya Wayahudi.
и познавше благодать данную ми, Иаков и Кифа и Иоанн, мнимии столпи быти, десницы даша мне и Варнаве общения, да мы во языки, они же во обрезание,
10 Wakatuomba lakini kitu kimoja: tuwakumbuke maskini; jambo ambalo nimekuwa nikijitahidi kutekeleza.
точию нищих да помнима: еже и потщахся сие истое сотворити.
11 Lakini Kefa alipofika Antiokia nilimpinga waziwazi maana alikuwa amekosea.
Егда же прииде Петр во Антиохию, в лице ему противустах, яко зазорен бе.
12 Awali, kabla ya watu kadhaa waliokuwa wametumwa na Yakobo kuwasili hapo, Petro alikuwa akila pamoja na watu wa mataifa mengine. Lakini, baada ya hao watu kufika, aliacha kabisa kula pamoja na watu wa mataifa mengine, kwa kuogopa kikundi cha waliosisitiza tohara.
Прежде бо даже не приити неким от Иакова, с языки ядяше: егда же приидоша, опряташеся и отлучашеся, бояся сущих от обрезания.
13 Hata ndugu wengine Wayahudi walimuunga mkono Petro katika kitendo hiki cha unafiki, naye Barnaba akakumbwa na huo unafiki wao.
И лицемеришася с ним и прочии Иудеи, яко и Варнаве пристати лицемерству их.
14 Basi, nilipoona kuwa msimamo wao kuhusu ukweli wa Habari Njema haukuwa umenyooka, nikamwambia Kefa mbele ya watu wote: “Ingawa wewe ni Myahudi, unaishi kama watu wa mataifa mengine na si kama Myahudi! Unawezaje, basi kujaribu kuwalazimisha watu wa mataifa mengine kuishi kama Wayahudi?”
Но егда видех, яко не право ходят ко истине Благовествования, рекох Петру пред всеми: аще ты, Иудей сый, язычески, а не иудейски живеши, почто языки нудиши иудейски жительствовати?
15 Kweli, sisi kwa asili ni Wayahudi, na si watu wa mataifa mengine hao wenye dhambi!
Мы естеством Иудее, а не от язык грешницы:
16 Lakini, tunajua kwa hakika kwamba mtu hawezi kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa kuitii Sheria, bali tu kwa kumwamini Yesu Kristo. Na sisi pia tumemwamini Yesu Kristo ili tupate kukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya imani yetu kwa Kristo, na si kwa kuitii Sheria.
уведевше же, яко не оправдится человек от дел закона, но токмо верою Иисус Христовою, и мы во Христа Иисуса веровахом, да оправдимся от веры Христовы, а не от дел закона: зане не оправдится от дел закона всяка плоть.
17 Sasa, ikiwa katika kutafuta kukubaliwa kuwa waadilifu kwa kuungana na Kristo sisi tunaonekana kuwa wenye dhambi, je, jambo hili lina maana kwamba Kristo anasaidia utendaji wa dhambi? Hata kidogo!
Аще ли, ищуще оправдитися о Христе, обретохомся и сами грешницы, Христос убо греху ли служитель? Да не будет.
18 Lakini ikiwa ninajenga tena kile nilichokwisha bomoa, basi nahakikisha kwamba mimi ni mhalifu.
Аще бо, яже разорих, сия паки созидаю, преступника себе представляю.
19 Maana, kuhusu Sheria hiyo, mimi nimekufa; Sheria yenyewe iliniua, nipate kuishi kwa ajili ya Mungu. Mimi nimeuawa pamoja na Kristo msalabani,
Аз бо законом закону умрох, да Богови жив буду. Христови сраспяхся:
20 na sasa naishi, lakini si mimi tena, bali Kristo anaishi ndani yangu. Maisha haya ninayoishi sasa naishi kwa imani, imani katika Mwana wa Mungu aliyenipenda hata akayatoa maisha yake kwa ajili yangu.
живу же не ктому аз, но живет во мне Христос. А еже ныне живу во плоти, верою живу Сына Божия, возлюбившаго мене и предавшаго Себе по мне.
21 Sipendi kuikataa neema ya Mungu. Kama mtu huweza kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa njia ya Sheria, basi, Kristo alikufa bure!
Не отметаю благодати Божия. Аще бо законом правда, убо Христос туне умре.

< Wagalatia 2 >