< Wagalatia 2 >
1 Baada ya miaka kumi na minne, nilikwenda tena Yerusalemu pamoja na Barnaba; nilimchukua pia Tito pamoja nami.
Sa ti weti kirau nan ti nazita aki maha urshalima nan barnabas, maziki titos nan mi.
2 Kwenda kwangu kulitokana na ufunuo alionipa Mungu. Katika kikao cha faragha niliwaeleza hao viongozi ujumbe wa Habari Njema niliohubiri kwa watu wa mataifa. Nilifanya hivyo kusudi kazi yangu niliyokuwa nimefanya, na ile ninayofanya sasa isije ikawa bure.
Ma nyene barki upaakahutizeta Asere sama buki a nu zatu rusa Asere. Ma buki anu sa gongon a nikira, barki indaa suma nani ma sumi uhura ba.
3 Lakini, hata mwenzangu Tito, ambaye ni Mgiriki, hakulazimika kutahiriwa,
Me titus me cangi sa ma zi nan mi sa maa zi una girik, a gwaari me in ni kara.
4 ingawa kulikuwa na ndugu wengine wa uongo waliotaka atahiriwe. Watu hawa walijiingiza kwa ujanja na kupeleleza uhuru wetu tulio nao katika kuungana na Kristo Yesu, ili wapate kutufanya watumwa.
Anu hem a zenzen wa eh innu hunze wa gun kuno ukem usa upebu uri anyimo Yeso vana. Wa nyari ti cukuno we arere.
5 Hatukukubaliana nao hata kidogo ili ukweli wa Habari Njema ubaki nanyi daima.
Ta gaa duru u nya nice a tiye me, barki kadandere ka tize tiso ti cukuno nan shi.
6 Lakini watu hawa wanaosemekana kuwa ni viongozi—kama kweli walikuwa hivyo au sivyo, kwangu si kitu, maana Mungu hahukumu kwa kuangalia mambo ya nje—watu hawa hawakuwa na kitu cha kuongeza katika Habari hii Njema kama niihubirivyo.
Senki anu sa hira wa teki aye anu, ma buka gusa wateki vat wa kinkin imum ba.
7 Badala yake, walitambua kwamba Mungu alikuwa amenituma kuhubiri Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine kama vile Petro alivyokuwa ametumwa kuihubiri kwa Wayahudi.
Ure uwetu, wa iri a nyam tize tiso ta nusa a gwara we ba, gūsa a nya bitrus tize tiso u hana anu dira ugwara.
8 Maana, yule aliyemwezesha Petro kuwa mtume kwa Wayahudi, ndiye aliyeniwezesha nami pia kuwa mtume kwa watu wa mataifa mengine.
Asere, sa ma gamirka Bitrus ma cukuno unu tarsa u Yeso barki anu rusa Asere, cangi ma wuzi katuma anyimo am.
9 Basi, Yakobo, Kefa na Yohane, ambao waonekana kuwa viongozi wakuu, walitambua kwamba Mungu alinijalia neema hiyo, wakatushika sisi mkono, yaani Barnaba na mimi, iwe ishara ya ushirikiano. Sisi ilitupasa tukafanye kazi kati ya watu wa mataifa mengine, na wao kati ya Wayahudi.
Sa yakubu kefas nan yohana, sa urusi agi we wani wa barka udenge wa Asere me, wa gāna nikara sa Asere a nyam, wa ziki Barnabas nan miwa wuzi anime barki tiha ahira anu sa wa taa Asere ba.
10 Wakatuomba lakini kitu kimoja: tuwakumbuke maskini; jambo ambalo nimekuwa nikijitahidi kutekeleza.
Wa nyari ticas ti ringi anu dira, imum igesa ma inki iriban.
11 Lakini Kefa alipofika Antiokia nilimpinga waziwazi maana alikuwa amekosea.
Uganiya sa kefas ma eh u antakiya ma gwarka a mu henu meme s ma chami.
12 Awali, kabla ya watu kadhaa waliokuwa wametumwa na Yakobo kuwasili hapo, Petro alikuwa akila pamoja na watu wa mataifa mengine. Lakini, baada ya hao watu kufika, aliacha kabisa kula pamoja na watu wa mataifa mengine, kwa kuogopa kikundi cha waliosisitiza tohara.
Uganiya sa wanu aye ba sa ahira yakubu, kefas mazi innare nan nanu zatu u urusa Asere. Barki anu me wa eh, mā ceki a zatu rusa Asere ma kunna biyau banu sa nyara a gwari aye me.
13 Hata ndugu wengine Wayahudi walimuunga mkono Petro katika kitendo hiki cha unafiki, naye Barnaba akakumbwa na huo unafiki wao.
Ukasu anu me cangi wa muti nice nan na nu bihunze me.
14 Basi, nilipoona kuwa msimamo wao kuhusu ukweli wa Habari Njema haukuwa umenyooka, nikamwambia Kefa mbele ya watu wote: “Ingawa wewe ni Myahudi, unaishi kama watu wa mataifa mengine na si kama Myahudi! Unawezaje, basi kujaribu kuwalazimisha watu wa mataifa mengine kuishi kama Wayahudi?”
Sama iri tanu tiwe me ti daa tize tiso me ba, ma gu in kefas aje awē me vat, ''inka hū yahudawa mani u ciki anyimo anu zatu rusa Asere sarki gu uyahudawa ba aneni udi wu wa wuzi ticukuno gū ahahudawa?''
15 Kweli, sisi kwa asili ni Wayahudi, na si watu wa mataifa mengine hao wenye dhambi!
Haru me ayahudawa wani u yoo dā anu zatu rusa Asere a madini.
16 Lakini, tunajua kwa hakika kwamba mtu hawezi kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa kuitii Sheria, bali tu kwa kumwamini Yesu Kristo. Na sisi pia tumemwamini Yesu Kristo ili tupate kukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya imani yetu kwa Kristo, na si kwa kuitii Sheria.
Vat anime ti rusa senki u inko iriba anyimo Yeso van Asere. Haru me cangi ta ribe anyimo a Yeso barki ti wu lauanyimo vana Asere daki katuma ku inko utize ba. Barki u inko utize da uye mada lau ba.
17 Sasa, ikiwa katika kutafuta kukubaliwa kuwa waadilifu kwa kuungana na Kristo sisi tunaonekana kuwa wenye dhambi, je, jambo hili lina maana kwamba Kristo anasaidia utendaji wa dhambi? Hata kidogo!
Barki inka, tizin nu nyara ti wu lau anyimo vana Asere haru me cangi anu a madini wani Yeso ma kinkize imum ibur? Babu koka inde.
18 Lakini ikiwa ninajenga tena kile nilichokwisha bomoa, basi nahakikisha kwamba mimi ni mhalifu.
Inka ma kuri ma barki imum sa ma charin, ma bezi mi unu zatu tarsa inko tize tini.
19 Maana, kuhusu Sheria hiyo, mimi nimekufa; Sheria yenyewe iliniua, nipate kuishi kwa ajili ya Mungu. Mimi nimeuawa pamoja na Kristo msalabani,
Gu anyimo u inko utize me ma, wii a hira inko tize me, barki in wuzi Asere katuma.
20 na sasa naishi, lakini si mimi tena, bali Kristo anaishi ndani yangu. Maisha haya ninayoishi sasa naishi kwa imani, imani katika Mwana wa Mungu aliyenipenda hata akayatoa maisha yake kwa ajili yangu.
A gamirkam na Yeso da mi mani in haka ba vana Asere mani ma raa' anyimo am. Tanu tige inzin anipum, in haka anyimo u inko iriba a vana Asere sa ma zi innu su um ma nya nice ni meme barki mi.
21 Sipendi kuikataa neema ya Mungu. Kama mtu huweza kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa njia ya Sheria, basi, Kristo alikufa bure!
Da ma vate u benki wa Asere, inka tanu ti lau ake a kem tini anyimo u inko utize, vana Asere ma wi hem.