< Waefeso 6 +
1 Enyi watoto, watiini wazazi wenu Kikristo maana hili ni jambo jema.
you who [are] Children, do obey the parents of you in [the] Lord; this for is right.
2 “Waheshimu Baba na mama yako,” hii ndiyo amri ya kwanza ambayo imeongezewa ahadi, yaani,
do honor the Father of you and mother, which is [the] commandment first with a promise,
3 “Upate fanaka na miaka mingi duniani.”
that well with you it may be and you will be long-lived upon the earth.
4 Nanyi akina baba, msiwachukize watoto wenu ila waleeni katika nidhamu na mafundisho ya Kikristo.
And you who [are] fathers, not do provoke the children of you, but do bring up them in [the] discipline and admonition of [the] Lord.
5 Enyi watumwa, watiini mabwana zenu hapa duniani kwa hofu na tetemeko; fanyeni hivyo kwa unyofu wa moyo kana kwamba mnamtumikia Kristo.
you who [are] slaves, do obey the according to flesh masters with fear and trembling in sincerity of the heart of you as to Christ.
6 Fanyeni hivyo si tu wakati wanapowatazama ili mjipendekeze kwao, bali tumikieni kwa moyo kama atakavyo Mungu kwa sababu ninyi ni watumishi wa Kristo.
not with eye-service as men-pleasers but as servants of (*k*) Christ doing the will of God from [the] heart
7 Muwe radhi kutumikia kwa ajili ya Bwana na si kwa ajili ya watu.
with good will rendering service as to the Lord and not to men,
8 Kumbukeni kwamba kila mtu mwenye kutenda mema, awe mtumwa au mtu huru, atapokea tuzo lake kutoka kwa Bwana.
knowing that each one (what *ko*) (maybe *NK(o)*) whatever he shall do good this he will receive [back] from (the *k*) Lord whether slave or free.
9 Nanyi mnaotumikiwa, watendeeni vivyo hivyo watumwa wenu, na acheni kutumia vitisho. Kumbukeni kwamba ninyi pia kama vile wao, mnaye Bwana yuleyule mbinguni, kwake cheo cha mtu si kitu.
And you who [are] masters, the [same things] them do perform toward them giving up the threatening, knowing that (also *no*) of them and of you the master is in [the] heavens and partiality not there is with Him.
10 Hatimaye, nawatakeni muwe imara katika kuungana na Bwana na kwa msaada wa nguvu yake kuu.
(Henceforth *N(k)O*) (brothers of mine *K*) do be empowered in [the] Lord and in the strength of the might of Him.
11 Vaeni silaha anazowapeni Mungu mpate kuzipinga mbinu mbaya za Ibilisi.
do put on the complete armor of God for to be able you to stand against the schemes of the devil;
12 Maana vita vyenu si vita kati yetu na binadamu, bali ni vita dhidi ya jeshi ovu la ulimwengu wa roho; tunapigana na watawala, wakuu na wenye nguvu wanaomiliki ulimwengu huu wa giza. (aiōn )
because not is to us the wrestling against blood and flesh but against the rulers, against the authorities, against the cosmic powers of the darkness (*k*) (age *K*) this, against the spiritual [forces] of evil in the heavenly realms. (aiōn )
13 Kwa sababu hiyo, vaeni silaha za Mungu ili siku ile itakapofika muweze kuyapinga mashambulio ya adui; na mkisha pigana mpaka mwisho, muwe bado thabiti.
Because of this do take up the complete armor of God, so that you may be able to withstand in the day evil and all things having done to stand.
14 Basi, simameni imara! Ukweli uwe kama ukanda kiunoni mwenu, uadilifu uwe kama vazi la kujikinga kifuani,
do stand therefore having girded the loins of you with truth and having put on the breastplate of righteousness
15 na hamu ya kutangaza Habari Njema ya amani iwe kama viatu miguuni mwenu.
and having shod the feet with [the] readiness of the gospel of peace;
16 Zaidi ya hayo yote, imani iwe daima kama ngao mikononi mwenu, iwawezeshe kuizima mishale ya moto ya yule Mwovu.
(besides *N(k)O*) all having taken up the shield of faith with which you will be able all the arrows of the evil one which enflamed to quench;
17 Upokeeni wokovu kama kofia yenu ya chuma, na neno la Mungu kama upanga mnaopewa na Roho Mtakatifu.
And the helmet of salvation (do take *NK(O)*) and the sword of the Spirit which is declaration of God;
18 Salini daima, mkiomba msaada wa Mungu. Salini kila wakati kwa nguvu ya Roho. Kesheni bila kuchoka mkisali kwa ajili ya watu wote wa Mungu.
through all [times] prayer and supplication praying in every season in [the] Spirit and unto (this *k*) watching with all perseverance and with supplication for all saints
19 Niombeeni nami pia ili niongeapo Mungu anijalie cha kusema, niweze kuwajulisha watu fumbo la Habari Njema kwa uthabiti.
and also for me, that to me (may be given *N(k)O*) divine utterance in [the] opening of the mouth of mine with boldness to make known the mystery of the gospel,
20 Mimi ni balozi kwa ajili ya Habari Njema hiyo ingawa sasa niko kifungoni. Ombeni, basi, ili niweze kuwa hodari katika kuitangaza kama inipasavyo.
for which I am an ambassador in a chain, that in it I may be bold as it behooves me to speak.
21 Tukiko, ndugu yetu mpenzi na mtumishi mwaminifu wa Bwana, atawapeni habari zangu zote mpate kujua ninachofanya.
That now may know also you yourselves the [things] concerning me myself, what I am doing, all things will make known to you Tychicus the beloved brother and faithful servant in [the] Lord,
22 Namtuma kwenu awapeni habari zetu mpate kuwa na moyo.
whom I have sent to you for this very purpose that you may know the [things] concerning us, and he may encourage the hearts of you.
23 Ninawatakieni ninyi ndugu amani, upendo na imani kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
Peace to the brothers and love with faith from God [the] Father and [the] Lord Jesus Christ.
24 Nawatakia neema ya Mungu wote wanaompenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa mapendo yasiyo na mwisho.
Grace [be] with all those loving the Lord of us Jesus Christ in incorruptibility (Amen. to Ephesian it was written from Rome through Tychicus. *K*)