< Waefeso 5 >

1 Kwa hiyo, mwigeni Mungu, maana ninyi ni watoto wake wapenzi.
Bądźcież tedy naśladowcami Bożymi, jako dzieci miłe;
2 Upendo uongoze maisha yenu, kama vile Kristo alivyotupenda, na kwa ajili yetu akajitoa mwenyewe kama dhabihu yenye harufu nzuri na tambiko impendezayo Mungu.
A chodźcie w miłości, jako i Chrystus umiłował nas i wydał samego siebie na ofiarę i na zabicie Bogu ku wdzięcznej wonności.
3 Kwa vile ninyi ni watu wa Mungu, basi uasherati, uchafu wowote ule au choyo visitajwe kamwe miongoni mwenu.
A wszeteczeństwo i wszelka nieczystość albo łakomstwo niechaj nie będzie ani mianowane między wami, jako przystoi na świętych.
4 Tena maneno ya aibu, ya upuuzi au ubishi, yote hayo hayafai kwenu; maneno ya kumshukuru Mungu ndiyo yanayofaa.
Także sprośność i błazeńskie mowy, i żarty, które nie przystoją, ale raczej dziękowanie.
5 Jueni wazi kwamba mwasherati yeyote au mchafu au mfisadi, (ufisadi ni sawa na kuabudu sanamu), au mtu yeyote wa aina hiyo hataambulia chochote katika Utawala wa Kristo na wa Mungu.
Bo to wiecie, iż żaden wszetecznik, albo nieczysty, albo łakomca, (który jest bałwochwalcą), nie ma dziedzictwa w królestwie Chrystusowem i Bożem.
6 Msikubali kudanganywa na mtu kwa maneno matupu; maana, kwa sababu ya mambo kama hayo ghadhabu ya Mungu huwajia wote wasiomtii.
Niechaj was nikt nie zwodzi próżnemi mowami; albowiem dla tych rzeczy przychodzi gniew Boży na synów upornych;
7 Basi, msishirikiane nao.
Nie bądźcież tedy uczestnikami ich.
8 Zamani ninyi mlikuwa gizani, lakini sasa ninyi mko katika mwanga kwa kuungana na Bwana. Ishini kama watoto wa mwanga:
Albowiemeście byli niekiedy ciemnością; aleście teraz światłością w Panu; chodźcież jako dziatki światłości,
9 maana matokeo ya mwanga ni wema kamili, uadilifu na ukweli.
(Bo owoc Ducha zależy we wszelakiej dobrotliwości i w sprawiedliwości i w prawdzie.)
10 Jaribuni kujua yale yanayompendeza Bwana.
Obierając to, co by się podobało Panu;
11 Msishiriki katika matendo yasiyofaa, ya giza bali yafichueni.
A nie spółkujcie z uczynkami niepożytecznemi ciemności, ale je raczej strofujcie.
12 Mambo yanayotendwa kwa siri ni aibu hata kuyataja.
Albowiem co się potajemnie od nich dzieje, sromota i mówić.
13 Lakini mambo yale yanayotendwa katika mwanga, ukweli wake hudhihirishwa;
Lecz to wszystko, gdy bywa od światłości strofowane, bywa objawione; albowiem to wszystko, co bywa objawione, jest światłością;
14 na kila kilichodhihirishwa huwa mwanga. Ndiyo maana Maandiko yasema: “Amka wewe uliyelala, fufuka kutoka wafu, naye Kristo atakuangaza.”
Dlatego mówi Pismo: Ocuć się, który śpisz i powstań od umarłych, a oświeci cię Chrystus.
15 Basi, muwe waangalifu jinsi mnavyoishi: Msiishi kama wapumbavu, bali kama wenye hekima.
Patrzajcie tedy, jakobyście ostrożnie chodzili, nie jako niemądrzy, ale jako mądrzy.
16 Tumieni vizuri muda mlio nao maana siku hizi ni mbaya.
Czas odkupując; bo dni złe są.
17 Kwa hiyo, msiwe wapumbavu, bali jaribuni kujua matakwa ya Bwana.
Przetoż nie bądźcie nierozumnymi, ale zrozumiewającymi, która jest wola Pańska.
18 Acheni kulewa divai maana hiyo itawaangamiza, bali mjazwe Roho Mtakatifu.
A nie upijajcie się winem, w którem jest rozpusta; ale bądźcie napełnieni duchem,
19 Zungumzeni kwa maneno ya Zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Bwana nyimbo na zaburi kwa shukrani mioyoni mwenu.
Rozmawiając z sobą przez psalmy i hymny, i pieśni duchowne, śpiewając i grając w sercu swojem Panu,
20 Mshukuruni Mungu Baba daima kwa ajili ya yote, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
Dzięki czyniąc zawsze za wszystko, w imieniu Pana naszego, Jezusa Chrystusa, Bogu i Ojcu.
21 Kila mmoja amstahi mwenzake kwa sababu ya kumcha Kristo.
Będąc poddani jedni drugim w bojaźni Bożej.
22 Wake wawatii waume zao kama kumtii Bwana.
Żony! bądźcie poddane mężom swoim, jako Panu;
23 Maana mume anayo mamlaka juu ya mkewe, kama vile Kristo alivyo na mamlaka juu ya kanisa; naye Kristo mwenyewe hulikomboa kanisa, mwili wake.
Albowiem mąż jest głową żony, jako i Chrystus głową kościoła; a on jest zbawicielem ciała.
24 Kama vile kanisa linavyomtii Kristo, vivyo hivyo, wake wawatii waume zao katika mambo yote.
Jako tedy kościół poddany jest Chrystusowi, tak też żony mężom swoim we wszystkiem.
25 Nanyi waume, wapendeni wake zenu kama Kristo alivyolipenda kanisa, akajitoa mwenyewe sadaka kwa ajili yake.
Mężowie! miłujcie żony wasze, jako i Chrystus umiłował kościół i wydał samego siebie za niego,
26 Alifanya hivyo, ili kwa neno lake, aliweke wakfu kwa Mungu, baada ya kulifanya safi kwa kuliosha katika maji,
Aby go poświęcił, oczyściwszy omyciem wody przez słowo;
27 kusudi ajipatie kanisa lililo takatifu na safu kabisa, kanisa lisilo na doa, kasoro au chochote cha namna hiyo.
Aby go sobie wystawił chwalebnym kościołem, nie mającym zmazy albo zmarszczku, albo czego takiego, ale iżby był święty i bez nagany.
28 Basi, waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe.
Tak powinni mężowie miłować żony swoje, jako swoje własne ciała; kto miłuje żonę swoję, samego siebie miłuje.
29 (Hakuna mtu yeyote auchukiaye mwili wake; badala ya kuuchukia, huulisha na kuuvika. Ndivyo naye Kristo anavyolitunza kanisa,
Albowiem żaden nigdy ciała swego nie miał w nienawiści, ale je żywi i ogrzewa, jako i Pan kościół.
30 maana sisi ni viungo vya mwili wake.)
Gdyżeśmy członkami ciała jego, z ciała jego i z kości jego.
31 Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Kwa hiyo, mwanamume atawaacha baba na mama yake, ataungana na mkewe, nao wawili watakuwa mwili mmoja.”
Dlatego opuści człowiek ojca swego i matkę, i przyłączy się do żony swojej, i będą dwoje jednem ciałem.
32 Kuna ukweli uliofichika katika maneno haya, nami naona kwamba yamhusu Kristo na kanisa lake.
Tajemnica to wielka jest; lecz ja mówię o Chrystusie i o kościele.
33 Lakini yanawahusu ninyi pia: kila mume lazima ampende mkewe kama nafsi yake mwenyewe, naye mke anapaswa kumstahi mumewe.
A wszakże i każdy z was z osobna niechaj miłuje żonę swoję jako siebie samego, a żona niech się boi męża swego.

< Waefeso 5 >