< Waefeso 5 >

1 Kwa hiyo, mwigeni Mungu, maana ninyi ni watoto wake wapenzi.
estote ergo imitatores Dei sicut filii carissimi
2 Upendo uongoze maisha yenu, kama vile Kristo alivyotupenda, na kwa ajili yetu akajitoa mwenyewe kama dhabihu yenye harufu nzuri na tambiko impendezayo Mungu.
et ambulate in dilectione sicut et Christus dilexit nos et tradidit se ipsum pro nobis oblationem et hostiam Deo in odorem suavitatis
3 Kwa vile ninyi ni watu wa Mungu, basi uasherati, uchafu wowote ule au choyo visitajwe kamwe miongoni mwenu.
fornicatio autem et omnis inmunditia aut avaritia nec nominetur in vobis sicut decet sanctos
4 Tena maneno ya aibu, ya upuuzi au ubishi, yote hayo hayafai kwenu; maneno ya kumshukuru Mungu ndiyo yanayofaa.
aut turpitudo aut stultiloquium aut scurrilitas quae ad rem non pertinent sed magis gratiarum actio
5 Jueni wazi kwamba mwasherati yeyote au mchafu au mfisadi, (ufisadi ni sawa na kuabudu sanamu), au mtu yeyote wa aina hiyo hataambulia chochote katika Utawala wa Kristo na wa Mungu.
hoc enim scitote intellegentes quod omnis fornicator aut inmundus aut avarus quod est idolorum servitus non habet hereditatem in regno Christi et Dei
6 Msikubali kudanganywa na mtu kwa maneno matupu; maana, kwa sababu ya mambo kama hayo ghadhabu ya Mungu huwajia wote wasiomtii.
nemo vos seducat inanibus verbis propter haec enim venit ira Dei in filios diffidentiae
7 Basi, msishirikiane nao.
nolite ergo effici participes eorum
8 Zamani ninyi mlikuwa gizani, lakini sasa ninyi mko katika mwanga kwa kuungana na Bwana. Ishini kama watoto wa mwanga:
eratis enim aliquando tenebrae nunc autem lux in Domino ut filii lucis ambulate
9 maana matokeo ya mwanga ni wema kamili, uadilifu na ukweli.
fructus enim lucis est in omni bonitate et iustitia et veritate
10 Jaribuni kujua yale yanayompendeza Bwana.
probantes quid sit beneplacitum Deo
11 Msishiriki katika matendo yasiyofaa, ya giza bali yafichueni.
et nolite communicare operibus infructuosis tenebrarum magis autem et redarguite
12 Mambo yanayotendwa kwa siri ni aibu hata kuyataja.
quae enim in occulto fiunt ab ipsis turpe est et dicere
13 Lakini mambo yale yanayotendwa katika mwanga, ukweli wake hudhihirishwa;
omnia autem quae arguuntur a lumine manifestantur omne enim quod manifestatur lumen est
14 na kila kilichodhihirishwa huwa mwanga. Ndiyo maana Maandiko yasema: “Amka wewe uliyelala, fufuka kutoka wafu, naye Kristo atakuangaza.”
propter quod dicit surge qui dormis et exsurge a mortuis et inluminabit tibi Christus
15 Basi, muwe waangalifu jinsi mnavyoishi: Msiishi kama wapumbavu, bali kama wenye hekima.
videte itaque fratres quomodo caute ambuletis non quasi insipientes sed ut sapientes
16 Tumieni vizuri muda mlio nao maana siku hizi ni mbaya.
redimentes tempus quoniam dies mali sunt
17 Kwa hiyo, msiwe wapumbavu, bali jaribuni kujua matakwa ya Bwana.
propterea nolite fieri inprudentes sed intellegentes quae sit voluntas Domini
18 Acheni kulewa divai maana hiyo itawaangamiza, bali mjazwe Roho Mtakatifu.
et nolite inebriari vino in quo est luxuria sed implemini Spiritu
19 Zungumzeni kwa maneno ya Zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Bwana nyimbo na zaburi kwa shukrani mioyoni mwenu.
loquentes vobismet ipsis in psalmis et hymnis et canticis spiritalibus cantantes et psallentes in cordibus vestris Domino
20 Mshukuruni Mungu Baba daima kwa ajili ya yote, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
gratias agentes semper pro omnibus in nomine Domini nostri Iesu Christi Deo et Patri
21 Kila mmoja amstahi mwenzake kwa sababu ya kumcha Kristo.
subiecti invicem in timore Christi
22 Wake wawatii waume zao kama kumtii Bwana.
mulieres viris suis subditae sint sicut Domino
23 Maana mume anayo mamlaka juu ya mkewe, kama vile Kristo alivyo na mamlaka juu ya kanisa; naye Kristo mwenyewe hulikomboa kanisa, mwili wake.
quoniam vir caput est mulieris sicut Christus caput est ecclesiae ipse salvator corporis
24 Kama vile kanisa linavyomtii Kristo, vivyo hivyo, wake wawatii waume zao katika mambo yote.
sed ut ecclesia subiecta est Christo ita et mulieres viris suis in omnibus
25 Nanyi waume, wapendeni wake zenu kama Kristo alivyolipenda kanisa, akajitoa mwenyewe sadaka kwa ajili yake.
viri diligite uxores sicut et Christus dilexit ecclesiam et se ipsum tradidit pro ea
26 Alifanya hivyo, ili kwa neno lake, aliweke wakfu kwa Mungu, baada ya kulifanya safi kwa kuliosha katika maji,
ut illam sanctificaret mundans lavacro aquae in verbo
27 kusudi ajipatie kanisa lililo takatifu na safu kabisa, kanisa lisilo na doa, kasoro au chochote cha namna hiyo.
ut exhiberet ipse sibi gloriosam ecclesiam non habentem maculam aut rugam aut aliquid eiusmodi sed ut sit sancta et inmaculata
28 Basi, waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe.
ita et viri debent diligere uxores suas ut corpora sua qui suam uxorem diligit se ipsum diligit
29 (Hakuna mtu yeyote auchukiaye mwili wake; badala ya kuuchukia, huulisha na kuuvika. Ndivyo naye Kristo anavyolitunza kanisa,
nemo enim umquam carnem suam odio habuit sed nutrit et fovet eam sicut et Christus ecclesiam
30 maana sisi ni viungo vya mwili wake.)
quia membra sumus corporis eius de carne eius et de ossibus eius
31 Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Kwa hiyo, mwanamume atawaacha baba na mama yake, ataungana na mkewe, nao wawili watakuwa mwili mmoja.”
propter hoc relinquet homo patrem et matrem suam et adherebit uxori suae et erunt duo in carne una
32 Kuna ukweli uliofichika katika maneno haya, nami naona kwamba yamhusu Kristo na kanisa lake.
sacramentum hoc magnum est ego autem dico in Christo et in ecclesia
33 Lakini yanawahusu ninyi pia: kila mume lazima ampende mkewe kama nafsi yake mwenyewe, naye mke anapaswa kumstahi mumewe.
verumtamen et vos singuli unusquisque suam uxorem sicut se ipsum diligat uxor autem ut timeat virum

< Waefeso 5 >