< Waefeso 5 >
1 Kwa hiyo, mwigeni Mungu, maana ninyi ni watoto wake wapenzi.
Soyez donc les imitateurs de Dieu, comme des enfants bien-aimés;
2 Upendo uongoze maisha yenu, kama vile Kristo alivyotupenda, na kwa ajili yetu akajitoa mwenyewe kama dhabihu yenye harufu nzuri na tambiko impendezayo Mungu.
Et marchez dans la charité, comme le Christ qui nous a aimés, et s'est offert lui-même à Dieu pour nous en oblation et en victime d'agréable odeur.
3 Kwa vile ninyi ni watu wa Mungu, basi uasherati, uchafu wowote ule au choyo visitajwe kamwe miongoni mwenu.
Que ni la fornication, ni aucune impureté, ni l'avarice, ne soient même nommées parmi vous, comme il convient à des saints;
4 Tena maneno ya aibu, ya upuuzi au ubishi, yote hayo hayafai kwenu; maneno ya kumshukuru Mungu ndiyo yanayofaa.
Ni aucune parole déshonnête, ni bouffonnerie, ni plaisanterie, qui sont des choses malséantes; mais qu'on y entende plutôt des actions de grâces.
5 Jueni wazi kwamba mwasherati yeyote au mchafu au mfisadi, (ufisadi ni sawa na kuabudu sanamu), au mtu yeyote wa aina hiyo hataambulia chochote katika Utawala wa Kristo na wa Mungu.
Car vous savez ceci, qu'aucun fornicateur, ou impudique, ou avare, qui est un idolâtre, n'a part à l'héritage du royaume de Christ et de Dieu.
6 Msikubali kudanganywa na mtu kwa maneno matupu; maana, kwa sababu ya mambo kama hayo ghadhabu ya Mungu huwajia wote wasiomtii.
Que personne ne vous séduise par de vains discours; car c'est à cause de ces choses que la colère de Dieu vient sur les enfants rebelles.
7 Basi, msishirikiane nao.
N'ayez donc point de part avec eux.
8 Zamani ninyi mlikuwa gizani, lakini sasa ninyi mko katika mwanga kwa kuungana na Bwana. Ishini kama watoto wa mwanga:
Car vous étiez autrefois ténèbres, mais à présent vous êtes lumière dans le Seigneur; marchez comme des enfants de lumière;
9 maana matokeo ya mwanga ni wema kamili, uadilifu na ukweli.
Car le fruit de l'Esprit consiste en toute sorte de bonté, de justice et de vérité.
10 Jaribuni kujua yale yanayompendeza Bwana.
Examinez ce qui est agréable au Seigneur.
11 Msishiriki katika matendo yasiyofaa, ya giza bali yafichueni.
Et ne prenez aucune part aux œuvres infructueuses des ténèbres, mais bien plutôt condamnez-les.
12 Mambo yanayotendwa kwa siri ni aibu hata kuyataja.
Car il est même honteux de dire ce que ces gens font en secret.
13 Lakini mambo yale yanayotendwa katika mwanga, ukweli wake hudhihirishwa;
Mais tout ce qui est condamné est manifesté par la lumière; car tout ce qui est manifesté devient lumière.
14 na kila kilichodhihirishwa huwa mwanga. Ndiyo maana Maandiko yasema: “Amka wewe uliyelala, fufuka kutoka wafu, naye Kristo atakuangaza.”
C'est pour cela qu'il est dit: Réveille-toi, toi qui dors, et te relève d'entre les morts, et Christ t'éclairera.
15 Basi, muwe waangalifu jinsi mnavyoishi: Msiishi kama wapumbavu, bali kama wenye hekima.
Prenez donc garde à vous conduire avec circonspection, non comme des insensés, mais comme des personnes sages;
16 Tumieni vizuri muda mlio nao maana siku hizi ni mbaya.
Rachetez le temps; car les jours sont mauvais.
17 Kwa hiyo, msiwe wapumbavu, bali jaribuni kujua matakwa ya Bwana.
C'est pourquoi ne soyez pas sans prudence, mais comprenez quelle est la volonté du Seigneur.
18 Acheni kulewa divai maana hiyo itawaangamiza, bali mjazwe Roho Mtakatifu.
Ne vous enivrez point de vin, qui mène au dérèglement; mais soyez remplis de l'Esprit;
19 Zungumzeni kwa maneno ya Zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Bwana nyimbo na zaburi kwa shukrani mioyoni mwenu.
Entretenez-vous ensemble par des psaumes, des hymnes et des cantiques spirituels, chantant et psalmodiant de votre cœur au Seigneur;
20 Mshukuruni Mungu Baba daima kwa ajili ya yote, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
Rendez grâces toujours pour toutes choses à Dieu le Père, au nom de notre Seigneur Jésus-Christ.
21 Kila mmoja amstahi mwenzake kwa sababu ya kumcha Kristo.
Soumettez-vous les uns aux autres dans la crainte de Dieu.
22 Wake wawatii waume zao kama kumtii Bwana.
Femmes, soyez soumises à vos propres maris, comme au Seigneur,
23 Maana mume anayo mamlaka juu ya mkewe, kama vile Kristo alivyo na mamlaka juu ya kanisa; naye Kristo mwenyewe hulikomboa kanisa, mwili wake.
Parce que le mari est le chef de la femme, comme aussi le Christ est le chef de l'Église, qui est son corps, dont il est le Sauveur.
24 Kama vile kanisa linavyomtii Kristo, vivyo hivyo, wake wawatii waume zao katika mambo yote.
Or, de même que l'Église est soumise à Christ, que les femmes le soient aussi à leurs propres maris en toutes choses.
25 Nanyi waume, wapendeni wake zenu kama Kristo alivyolipenda kanisa, akajitoa mwenyewe sadaka kwa ajili yake.
Maris, aimez vos femmes, comme aussi Christ a aimé l'Église, et s'est livré lui-même pour elle;
26 Alifanya hivyo, ili kwa neno lake, aliweke wakfu kwa Mungu, baada ya kulifanya safi kwa kuliosha katika maji,
Afin de la sanctifier, en la purifiant et en la lavant par l'eau de la parole;
27 kusudi ajipatie kanisa lililo takatifu na safu kabisa, kanisa lisilo na doa, kasoro au chochote cha namna hiyo.
Pour la faire paraître devant lui une Église glorieuse, sans tache, ni ride, ni rien de semblable, mais sainte et irrépréhensible.
28 Basi, waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe.
C'est ainsi que les maris doivent aimer leurs femmes comme leurs propres corps. Celui qui aime sa femme, s'aime lui-même.
29 (Hakuna mtu yeyote auchukiaye mwili wake; badala ya kuuchukia, huulisha na kuuvika. Ndivyo naye Kristo anavyolitunza kanisa,
Car personne n'a jamais haï sa propre chair, mais il la nourrit et l'entretient, comme le Seigneur le fait à l'égard de l'Église;
30 maana sisi ni viungo vya mwili wake.)
Parce que nous sommes les membres de son corps, étant de sa chair et de ses os.
31 Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Kwa hiyo, mwanamume atawaacha baba na mama yake, ataungana na mkewe, nao wawili watakuwa mwili mmoja.”
C'est pourquoi l'homme quittera son père et sa mère, et s'attachera à sa femme; et les deux ne seront qu'une seule chair.
32 Kuna ukweli uliofichika katika maneno haya, nami naona kwamba yamhusu Kristo na kanisa lake.
Ce mystère est grand; je le dis par rapport à Christ et à l'Église.
33 Lakini yanawahusu ninyi pia: kila mume lazima ampende mkewe kama nafsi yake mwenyewe, naye mke anapaswa kumstahi mumewe.
Ainsi, que chacun de vous aime sa femme comme lui-même, et que la femme respecte son mari.