< Waefeso 4 >
1 Basi, mimi niliye mfungwa kwa kuwa namtumikia Bwana, nawasihi muishi maisha yanayostahili wito mlioitiwa.
所以我在這主內為囚犯的懇求你們,行動務要與你們所受的寵召相稱,
2 Muwe daima wanyenyekevu, wapole na wenye saburi; vumilianeni ninyi kwa ninyi kwa mapendo.
凡事要謙遜、溫和、忍耐,在愛德中彼此擔待,
3 Fanyeni bidii ya kuhifadhi umoja uletwao na Roho kwa kuzingatia amani iliyo kati yenu.
盡力以和平的聯繫,保持心神的合一,
4 Kuna mwili mmoja na Roho mmoja, kama vile tumaini mliloitiwa na Mungu ni moja.
因為只有一個身體和一個聖神,正如你們蒙召,同有一個希望一樣。
5 Kuna Bwana mmoja, imani moja na ubatizo mmoja;
只有一個主,一個信德,一個洗禮;
6 kuna Mungu mmoja na Baba wa wote, ambaye yuko juu ya wote, afanya kazi katika yote na yuko katika yote.
只有一個天主和眾人之父,祂超越眾人,貫通眾人,且在眾人之內。
7 Kila mmoja wetu amepewa neema kadiri ya kipimo alichojaliwa na Kristo.
但我們各人所領受的恩寵,卻是按照基督賜恩的尺度。
8 Kama yasemavyo Maandiko: “Alipopaa mbinguni juu kabisa, alichukua mateka; aliwapa watu zawadi.”
為此經上說:『祂帶領俘虜,升上高天,且把恩惠賜與人。』
9 Basi, inaposemwa: “alipaa juu,” ina maana gani? Maana yake ni kwamba, kwanza alishuka mpaka chini kabisa duniani.
說祂上升了,豈不是說祂曾下降到地下嗎﹖
10 Basi, huyo aliyeshuka hapa duniani, ndiye aliyepaa juu ya mbingu zote apate kuujaza ulimwengu.
那下降的,正是上升超乎諸之上,以充滿萬有的那一位,
11 Ndiye aliyewapa watu zawadi: wengine aliwajalia wawe mitume, wengine manabii, wengine wawe waeneza Habari Njema, wengine wachungaji na walimu.
就是祂賜與這些人作宗徒,那些人作先知,有的作傳福音者,有的作司牧和教師,
12 Alifanya hivyo apate kuwatayarisha watu wote wa Mungu kwa ajili ya kazi ya huduma ya Kikristo ili kuujenga mwili wa Kristo,
為成全聖徒,使之各盡其職;為建樹基督的身體,
13 na hivyo sote tuufikie umoja wa imani na kumjua Mwana wa Mungu; tuwe watu waliokomaa na kuufikia utimilifu wake Kristo mwenyewe.
直到我們眾人都達到對於天主子,有有一致的信仰和認識,成為成年人,達到基督圓滿年齡的程度;
14 Basi, hatutakuwa tena kama watoto, tukitupwa na kupeperushwa huko na huko kwa kila upepo wa mafundisho wanayozua watu wadanganyifu, ili wawapotoshe wengine kwa hila.
使我們不再作小孩子,為各種教義之風所飄盪,所捲去,而中了人的陰謀,陷於入荒謬的詭計;
15 Ila, sisi tukisema ukweli kwa moyo wa mapendo tutakua zidi katika kila jambo kulingana na Kristo ambaye ndiye kichwa;
反而在愛德中持守真理,在各方面長進,而歸於那為元首的基督,
16 chini ya uongozi wake, viungo vyote vya mwili hushikamana pamoja, na mwili wote hutegemezwa kwa msaada wa viungo vyake. Basi, kila kiungo kikitekeleza kazi yake ipasavyo, mwili wote hukua na kujijenga katika upendo.
本著祂,全身都結構緊湊,藉著各關節的互相補助,按照各肢體的功用,各盡其職,使身體不斷增長,在愛德中將它建立起來。
17 Basi, kwa jina la Bwana, nawaonyeni: msiishi tena kama watu wasiomjua Mungu, ambao fikira zao zimekuwa upuuzi mtupu,
為此我說,且在主內苦勸你們,生活不要再像外邦人,順隨自己的虛妄思念而生活;
18 na akili zao zimo gizani. Wako mbali na uzima wa Mungu, kwa sababu ya upumbavu ulio ndani yao na ukaidi wao.
他們的理智受了蒙蔽,因著他們的無知和固執,與天主的生命隔絕了。
19 Wamepotoka na hawana aibu, wamejitosa katika ufisadi; hufanya kwa pupa kila aina ya mambo ya aibu.
這樣的人既已麻木,便縱情恣慾,貪行各種不潔。
20 Lakini ninyi hamkujifunza hivyo juu ya Kristo.
但你們卻不是這樣學了基督。
21 Ni dhahiri kwamba mlisikia barabara habari zake, na mkiwa wafuasi wake mkafundishwa ukweli ulivyo katika Yesu.
如果你們真聽過祂,按照在耶穌內的真理,在祂內受過教,
22 Basi, acheni mwenendo wenu wa awali, yaani ule utu wenu wa kale uliokuwa unaangamizwa kwa tamaa zake danganyifu.
就該脫去你們照從前生活的舊人,就是因順從享樂的慾念而敗壞的舊人,
23 Jirekebisheni upya rohoni na katika fikira zenu.
應在心思念慮上大改換一新,
24 Vaeni hali mpya ya utu ambayo imeumbwa kwa mfano wa Mungu na ambayo hujionyesha katika maisha ya kweli ya uadilifu na utakatifu.
穿上新人,就是按天主的肖像所造,具有真實的正義和聖善的新人。
25 Kwa hiyo, acheni uongo. Kila mmoja anapaswa kumwambia mwenzake ukweli, maana kila mmoja wetu ni kiungo cha mwili wa Kristo.
為此,你們應該戒絕謊言,彼此應該說實話,因為我們彼此都是一身的肢體。
26 Kama mkikasirika, msikubali hasira yenu iwafanye mtende dhambi, na wala msikae na hasira kutwa nzima.
『你們縱然動怒,但是不可犯罪;』不可讓太陽在你們含怒時西落,
27 Msimpe Ibilisi nafasi.
也不可給魔鬼留有餘地。
28 Aliyekuwa akiiba, asiibe tena, bali na aanze kufanya kazi njema kwa mikono yake, apate kuwa na kitu cha kumsaidia mtu aliye maskini.
那以前偷竊的,不要再偷竊,卻更要勞苦,親手賺取正當的利潤,好能賙濟貧乏的人。
29 Maneno mabaya hata yasisikike kamwe miongoni mwenu; kila mara maneno yenu yawe ya kufaa na ambayo hujenga na kuwasaidia wengine, ili yawaneemeshe wasikilizaji wenu.
一切壞話都不可出於你們的口;但看事情的需要,說造就人的話,叫聽眾獲得益處。
30 Msimhuzunishe Roho Mtakatifu wa Mungu maana Roho huyo ni alama ya Mungu kwenu kwamba ninyi ni watu wake, na thibitisho kwamba siku itakuja ambapo Mungu atawakomboeni.
你們不要叫天主的聖神憂鬱,因為你們是在祂內受了印證,以待得救的日子。
31 Basi, achaneni na uhasama, chuki, hasira, kelele, matusi! Achaneni na kila uovu!
一切毒辣、怨恨、忿怒、爭吵、毀謗以及弓切邪惡,都要從你們中除掉;
32 Muwe na moyo mwema na wenye kuhurumiana; kila mmoja na amsamehe mwenzake kama naye Mungu alivyowasamehe ninyi kwa njia ya Kristo.
彼此相待,要良善,要仁慈,互相寬恕,如同天主在基督內寬恕了你們一樣。