< Waefeso 2 >
1 Ninyi mlikuwa mmekufa kwa sababu ya makosa na dhambi zenu.
You were made alive when you were dead in your transgressions and sins,
2 Wakati ule mliishi kufuatana na mtindo mbaya wa ulimwengu huu, mkawa mnamtii mtawala wa pepo wenye nguvu wa anga, pepo ambao huwatawala sasa watu wasiomtii Mungu. (aiōn )
in which you once walked according to the course of this world, according to the prince of the power of the air, the spirit who now works in the children of disobedience; (aiōn )
3 Na hata sisi sote tulikuwa kama wao; tuliishi kufuatana na tamaa zetu za kidunia na kufanya tu mambo yale yaliyoipendeza miili na akili zetu. Kidunia, sisi kama vile pia wao, tulistahili ghadhabu ya Mungu.
among whom we also all once lived in the lust of our flesh, doing the desires of the flesh and of the mind, and were by nature children of wrath, even as the rest.
4 Lakini Mungu ni mwenye huruma nyingi. Alitupenda kwa mapendo yasiyopimika,
But God, being rich in mercy, for his great love with which he loved us,
5 hata, ingawa tulikuwa tumekufa kwa sababu ya dhambi, alitufanya hai pamoja na Kristo. Kwa neema ya Mungu ninyi mmeokolewa.
even when we were dead through our trespasses, made us alive together with Christ (by grace you have been saved),
6 Kwa kuungana na Kristo Yesu, Mungu alitufufua pamoja naye, tukatawale pamoja naye mbinguni.
and raised us up with him, and made us to sit with him in the heavenly places in Christ Jesus,
7 Ndivyo alivyopenda kuonyesha kwa watu wa nyakati za baadaye, ukuu wa neema yake aliyotujalia kwa ukarimu katika kuungana kwetu na Kristo Yesu. (aiōn )
that in the ages to come he might show the exceeding riches of his grace in kindness toward us in Christ Jesus; (aiōn )
8 Maana, kwa neema ya Mungu mmekombolewa kwa njia ya imani. Jambo hili si matokeo ya juhudi zenu, bali ni zawadi ya Mungu.
for by grace you have been saved through faith, and that not of yourselves; it is the gift of God,
9 Wala halitokani na matendo yenu wenyewe, asije mtu akajivunia kitu.
not of works, that no one would boast.
10 Sisi ni viumbe vyake Mungu, na kwa kuungana na Kristo Yesu, alituumba kwa ajili ya kuishi maisha ya matendo mema aliyotutayarishia tuyatende.
For we are his workmanship, created in Christ Jesus for good works, which God prepared before that we would walk in them.
11 Ninyi mlio kwa asili watu wa mataifa mengine—mnaoitwa, “wasiotahiriwa” na Wayahudi ambao hujiita, “Waliotahiriwa,” (kwa sababu ya kile wanachoifanyia miili yao) —kumbukeni mlivyokuwa zamani.
Therefore remember that once you, the non-Jews in the flesh, who are called "uncircumcision" by that which is called "circumcision," (in the flesh, made by hands);
12 Wakati ule ninyi mlikuwa bila Kristo; mlikuwa nje ya jamii ya Israeli; mlikuwa wageni na hamkuwa na sehemu yoyote katika lile agano la zile ahadi. Mlikuwa bila matumaini Mungu hapa duniani.
that you were at that time separate from Christ, alienated from the commonwealth of Israel, and foreigners to the covenants of the promise, having no hope and without God in the world.
13 Lakini sasa, kwa kuungana na Kristo Yesu, ninyi ambao hapo awali mlikuwa mbali, mmekaribishwa kwa njia ya damu yake Kristo.
But now in Christ Jesus you who once were far away have been brought near by the blood of Christ.
14 Maana Kristo mwenyewe ametuletea amani kwa kuwafanya Wayahudi na watu wa mataifa mengine kuwa jamii moja. Kwa mwili wake yeye mwenyewe aliubomoa ule ukuta uliowatenganisha na kuwafanya maadui.
For he is our peace, who made both one, and broke down the middle wall of partition,
15 Aliiondoa ile Sheria ya Wayahudi pamoja na amri zake na kanuni zake, ili kutokana na jamii hizo mbili aumbe jamii moja mpya katika umoja naye na hivyo kuleta amani.
having abolished in the flesh the hostility, the law of commandments contained in ordinances, that he might create in himself one new man of the two, making peace;
16 Kwa mwili wake, Kristo aliuangamiza uadui wao; kwa msalaba wake aliziunganisha jamii hizo kuwa moja na kuzipatanisha na Mungu.
and might reconcile them both in one body to God through the cross, by which he put to death their enmity.
17 Basi, Kristo alikuja akahubiri Habari Njema ya amani kwenu ninyi watu wa mataifa mengine mliokuwa mbali na Mungu, na pia kwa Wayahudi ambao walikuwa karibu na Mungu.
He came and preached peace to you who were far off and peace to those who were near.
18 Hivyo, kwa njia yake, sisi sote, Wayahudi na watu wa mataifa mengine, tunaweza kumwendea Baba katika Roho mmoja.
For through him we both have our access in one Spirit to the Father.
19 Basi, ninyi si wageni tena, wala si watu wa nje; ninyi ni raia pamoja na watu wa Mungu, na ni watu wa jamaa ya Mungu.
So then you are no longer foreigners and noncitizens, but you are fellow citizens with the saints, and of the household of God,
20 Mmejengwa juu ya msingi uliowekwa na mitume na manabii, naye Kristo mwenyewe ndiye jiwe kuu la msingi.
being built on the foundation of the apostles and prophets, Christ Jesus himself being the chief cornerstone;
21 Yeye ndiye mwenye kulitengeneza jengo lote na kulikuza hata liwe hekalu takatifu kwa ajili ya B wana.
in whom the whole building, fitted together, grows into a holy temple in the Lord;
22 Katika kuungana naye, ninyi pia mnajengwa pamoja na wote wengine, muwe makao ya Mungu kwa njia ya Roho wake.
in whom you also are built together for a habitation of God in the Spirit.