+ Wakolosai 1 >

1 Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Timotheo,
Paweł, Apostoł Jezusa Chrystusa przez wolę Bożą, i Tymoteusz brat,
2 tunawaandikia ninyi watu wa Mungu huko Kolosai, ndugu zetu waaminifu katika kuungana na Kristo. Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu.
Tym, którzy są w Kolosiech, świętym i wiernym braciom w Chrystusie Jezusie. Łaska wam i pokój niech będzie od Boga, Ojca naszego, i od Pana Jezusa Chrystusa.
3 Daima tunamshukuru Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, wakati tunapowaombea.
Dziękujemy Bogu i Ojcu Pana naszego Jezusa Chrystusa, zawsze modląc się za was,
4 Maana tumesikia juu ya imani yenu katika Kristo Yesu na juu ya upendo wenu kwa watu wote wa Mungu.
Usłyszawszy o wierze waszej w Chrystusie Jezusie i miłości przeciwko wszystkim świętym,
5 Wakati ujumbe ule wa kweli, yaani Habari Njema, ilipowafikieni kwa mara ya kwanza, mlipata kusikia juu ya lile tumaini linalopatikana kwake. Kwa sababu hiyo imani na upendo wenu vinategemea jambo lile mnalotumainia ambalo mmewekewa salama mbinguni.
Dla nadziei onej wam odłożonej w niebiesiech, o którejście przedtem słyszeli przez słowo prawdy, to jest Ewangielii,
6 Habari Njema inazidi kuzaa matunda na kuenea ulimwenguni kote kama vile ilivyofanya kwenu ninyi tangu siku ile mliposikia juu ya neema ya Mungu na kuitambua ilivyo kweli.
Która przyszła do was jako i na wszystek świat, i przynosi owoc, jako i u was, od onego dnia, któregoście usłyszeli i poznali łaskę Bożą w prawdzie.
7 Mlijifunza juu ya neema ya Mungu kutoka kwa Epafra, mtumishi mwenzetu, ambaye ni mfanyakazi mwaminifu wa Kristo kwa niaba yetu.
Jakoście się też nauczyli od Epafry, miłego spółsługi naszego, który jest wiernym sługą Chrystusowym dla was;
8 Yeye alitupa habari za upendo wenu mliojaliwa na Roho.
Który też oznajmił nam miłość waszę w duchu.
9 Kwa sababu hiyo tumekuwa tukiwaombeeni daima tangu tulipopata habari zenu. Tunamwomba Mungu awajazeni ujuzi kamili wa mapenzi yake, awajazeni hekima yote na elimu iletwayo na Roho wake.
Dlatego i my od onego dnia, któregośmy to usłyszeli, nie przestajemy się za was modlić i prosić, abyście byli napełnieni znajomością woli jego we wszelkiej mądrości i w wyrozumieniu duchownem.
10 Hapo mtaweza kuishi kama anavyotaka Bwana na kutenda daima yanayompendeza. Maisha yenu yatakuwa yenye matunda ya kila namna ya matendo mema na mtazidi kukua katika kumjua Mungu.
Abyście chodzili przystojnie przed Panem ku wszelkiemu jego upodobaniu, w każdym uczynku dobrym owoc przynosząc i rosnąc w znajomości Bożej,
11 Mungu awajalieni nguvu kwa uwezo wake mtukufu ili mweze kustahimili kila kitu kwa uvumilivu.
Wszelką mocą umocnieni będąc według chwalebnej mocy jego, ku wszelkiej cierpliwości i nieskwapliwości z radością,
12 Na kwa furaha, mshukuruni Baba aliyewawezesha ninyi kuwa na sehemu yenu katika mambo yale Mungu aliyowawekea watu wake katika utawala wa mwanga.
Dziękując Ojcu, który nas godnymi uczynił, abyśmy byli uczestnikami dziedzictwa świętych w światłości;
13 Yeye alituokoa katika nguvu ya giza, akatuleta salama katika ufalme wa Mwanae mpenzi,
Który nas wyrwał z mocy ciemności i przeniósł do królestwa Syna swego miłego,
14 ambaye kwa njia yake tunakombolewa, yaani dhambi zetu zinaondolewa.
W którym mamy odkupienie przez krew jego, to jest odpuszczenie grzechów;
15 Kristo ni mfano wa Mungu asiyeonekana; ni mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
Który jest obrazem Boga niewidzialnego i pierworodny wszystkich rzeczy stworzonych.
16 Maana kwa njia yake vitu vyote viliumbwa duniani na mbinguni, vitu vinavyoonekana na visivyoonekana: wenye enzi, watawala, wakuu na wenye mamlaka. Vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake.
Albowiem przezeń stworzone są wszystkie rzeczy, które są na niebie i na ziemi, widzialne i niewidzialne, bądź trony, bądź państwa, bądź księstwa, bądź zwierzchności, wszystko przezeń i dla niego stworzone jest.
17 Kristo alikuwako kabla ya vitu vyote; kwa kuungana naye, vyote vyadumu mahali pake.
A on jest przed wszystkimi i wszystko w nim stoi.
18 Yeye ni kichwa cha mwili wake, yaani kanisa; yeye ni chanzo cha uhai wa huo mwili. Yeye ndiye mwanzo, mzaliwa wa kwanza aliyefufuliwa kutoka wafu, ili awe na nafasi ya kwanza katika vitu vyote.
On też jest głową ciała, to jest kościoła, który jest początkiem i pierworodnym z umarłych, aby on między wszystkimi przodkował;
19 Maana Mungu alipenda utimilifu wote uwe ndani yake.
Ponieważ się upodobało Ojcu, aby w nim wszystka zupełność mieszkała.
20 Kwa njia yake Mungu alivipatanisha naye vitu vyote naam, viumbe vyote mbinguni na duniania; alileta amani kwa damu ya Kristo msalabani.
I żeby przezeń z sobą pojednał wszystko, uczyniwszy pokój przez krew krzyża jego; przezeń, mówię, tak to, co jest na ziemi, jako i to, co jest na niebiesiech.
21 Hapo kwanza ninyi pia mlikuwa mbali na Mungu na mlikuwa adui zake kwa sababu ya fikira zenu na matendo yenu maovu.
I was, którzyście niekiedy byli oddaleni i nieprzyjaciele umysłem w złośliwych uczynkach, teraz też pojednał.
22 Lakini sasa, kwa kifo cha Mwanae aliyeishi hapa duniani, Mungu amewapatanisha naye, kusudi awalete mbele yake mkiwa watakatifu, safi na bila lawama.
Ciałem własnem swojem przez śmierć, aby was wystawił świętemi i niepokalanemi, i bez nagany przed obliczem swojem;
23 Mnapaswa, lakini kuendelea kuwa imara na thabiti katika imani hiyo, na msikubali kusukumwa mbali na tumaini lile mlilopata wakati mlipoisikia Habari Njema. Mimi Paulo nimekuwa mtumishi wa hiyo Habari Njema ambayo imekwisha hubiriwa kila kiumbe duniani.
Jeźli tylko trwacie w wierze ugruntowani i utwierdzeni, a nie poruszeni od nadziei Ewangielii, którąście słyszeli, która jest kazana wszelkiemu stworzeniu, które jest pod niebem, której ja Paweł stałem się sługą;
24 Na sasa nafurahi kuteseka kwa ajili yenu, maana kwa mateso yangu hapa duniani, nasaidia kukamilisha kile kilichopungua bado katika mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, yaani kanisa.
Który się teraz raduję w doległościach moich dla was i dopełniam ostatków ucisków Chrystusowych na ciele mojem za ciało jego, które jest kościół.
25 Nami nimefanywa kuwa mtumishi wa kanisa kufuatana na mpango wake Mungu ambao alinikabidhi kwa faida yenu. Mpango wenyewe ni kuutangaza kwa ukamilifu ujumbe wake,
Któregom się ja stał sługą według daru Bożego, który mi jest dany dla was, abym wypełnił słowo Boże,
26 ambao ni siri aliyowaficha binadamu wote tangu milele, lakini sasa amewajulisha watu wake. (aiōn g165)
To jest, tajemnicę onę, która była zakryta od wieków i od rodzajów, ale teraz objawiona jest świętym jego. (aiōn g165)
27 Mpango wa Mungu ni kuwajulisha watu wake siri hii kuu na tukufu ambayo ni kwa ajili ya watu wote. Na, siri yenyewe ndiyo hii: Kristo yuko ndani yenu, na jambo hilo lamaanisha kwamba ninyi mtaushiriki utukufu wa Mungu.
Którym chciał Bóg oznajmić, jakie jest bogactwo tej tajemnicy chwalebnej między poganami, która jest Chrystus między wami, nadzieja ona chwały;
28 Kwa sababu hiyo tunamhubiri Kristo kwa watu wote; tunawaonya na kuwafundisha wote kwa hekima yote, ili tuweze kumleta kila mmoja mbele ya Mungu akiwa amekomaa katika kuungana na Kristo.
Którego my opowiadamy, napominając każdego człowieka i ucząc każdego człowieka we wszelkiej mądrości, abyśmy wystawili każdego człowieka doskonałym w Chrystusie Jezusie;
29 Kwa madhumuni hayo mimi nafanya kazi na kujitahidi nikiitumia nguvu kuu ya Kristo ifanyayo kazi ndani yangu.
W czem też pracuję, bojując według skutecznej mocy jego, która we mnie dzieło swoje potężnie sprawuje.

+ Wakolosai 1 >