+ Wakolosai 1 >

1 Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Timotheo,
PAUL, a legate of Jesus the Messiah by the pleasure of God, and Timothy a brother,
2 tunawaandikia ninyi watu wa Mungu huko Kolosai, ndugu zetu waaminifu katika kuungana na Kristo. Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu.
to them who are at Colosse, the brethren, holy and believing in Jesus the Messiah: peace be with you, and grace from God our Father.
3 Daima tunamshukuru Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, wakati tunapowaombea.
We give thanks to God, the Father of our Lord Jesus the Messiah, at all times, and pray for you;
4 Maana tumesikia juu ya imani yenu katika Kristo Yesu na juu ya upendo wenu kwa watu wote wa Mungu.
lo, ever since we heard of your faith in Jesus the Messiah, and of your love to all the saints;
5 Wakati ujumbe ule wa kweli, yaani Habari Njema, ilipowafikieni kwa mara ya kwanza, mlipata kusikia juu ya lile tumaini linalopatikana kwake. Kwa sababu hiyo imani na upendo wenu vinategemea jambo lile mnalotumainia ambalo mmewekewa salama mbinguni.
because of the hope that is laid up for you in heaven, of which ye heard before in the word of truth of the gospel;
6 Habari Njema inazidi kuzaa matunda na kuenea ulimwenguni kote kama vile ilivyofanya kwenu ninyi tangu siku ile mliposikia juu ya neema ya Mungu na kuitambua ilivyo kweli.
which is announced to you, as also to all the world; and which groweth and yieldeth fruits, as it doth also among you from the day ye heard and knew the grace of God in reality:
7 Mlijifunza juu ya neema ya Mungu kutoka kwa Epafra, mtumishi mwenzetu, ambaye ni mfanyakazi mwaminifu wa Kristo kwa niaba yetu.
as ye learned from Epaphras, our beloved fellow-servant, who is for you a faithful minister of the Messiah;
8 Yeye alitupa habari za upendo wenu mliojaliwa na Roho.
and who hath made known to us your love in the Spirit.
9 Kwa sababu hiyo tumekuwa tukiwaombeeni daima tangu tulipopata habari zenu. Tunamwomba Mungu awajazeni ujuzi kamili wa mapenzi yake, awajazeni hekima yote na elimu iletwayo na Roho wake.
Therefore we also, from the day we heard of it, have not ceased to pray for you; and to ask that ye may be filled with a knowledge of the good pleasure of God, in all wisdom, and in all spiritual understanding;
10 Hapo mtaweza kuishi kama anavyotaka Bwana na kutenda daima yanayompendeza. Maisha yenu yatakuwa yenye matunda ya kila namna ya matendo mema na mtazidi kukua katika kumjua Mungu.
that ye may walk as is right, and may please God with all good works, and may yield fruits, and grow in the knowledge of God;
11 Mungu awajalieni nguvu kwa uwezo wake mtukufu ili mweze kustahimili kila kitu kwa uvumilivu.
and may be strengthened with all strength, according to the greatness of his glory, in all patience and long suffering;
12 Na kwa furaha, mshukuruni Baba aliyewawezesha ninyi kuwa na sehemu yenu katika mambo yale Mungu aliyowawekea watu wake katika utawala wa mwanga.
and may, with joy, give thanks to God the Father, who hath fitted us for a portion of the inheritance of the saints in light;
13 Yeye alituokoa katika nguvu ya giza, akatuleta salama katika ufalme wa Mwanae mpenzi,
and hath rescued us from the dominion of darkness, and transferred us to the kingdom of his beloved Son;
14 ambaye kwa njia yake tunakombolewa, yaani dhambi zetu zinaondolewa.
by whom we have redemption and remission of sins:
15 Kristo ni mfano wa Mungu asiyeonekana; ni mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
who is the likeness of the invisible God, and the first-born of all creatures:
16 Maana kwa njia yake vitu vyote viliumbwa duniani na mbinguni, vitu vinavyoonekana na visivyoonekana: wenye enzi, watawala, wakuu na wenye mamlaka. Vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake.
and by him was created every thing that is in heaven and on earth, all that is seen and all that is unseen, whether thrones, or dominions, or principalities, or sovereignties; every thing was through him, and was created by him:
17 Kristo alikuwako kabla ya vitu vyote; kwa kuungana naye, vyote vyadumu mahali pake.
and he was prior to all, and by him every thing exists.
18 Yeye ni kichwa cha mwili wake, yaani kanisa; yeye ni chanzo cha uhai wa huo mwili. Yeye ndiye mwanzo, mzaliwa wa kwanza aliyefufuliwa kutoka wafu, ili awe na nafasi ya kwanza katika vitu vyote.
And he is the head of the body the church; as he is the head and first-born from among the dead, that he might be the first in all things.
19 Maana Mungu alipenda utimilifu wote uwe ndani yake.
For it pleased the Father, that in him all fullness should dwell;
20 Kwa njia yake Mungu alivipatanisha naye vitu vyote naam, viumbe vyote mbinguni na duniania; alileta amani kwa damu ya Kristo msalabani.
and by him, to reconcile all things to himself; and through him, he hath pacified, with the blood of his cross, both those on earth and those in heaven.
21 Hapo kwanza ninyi pia mlikuwa mbali na Mungu na mlikuwa adui zake kwa sababu ya fikira zenu na matendo yenu maovu.
And also to you, who were before alienated and enemies in your minds, because of your evil deeds,
22 Lakini sasa, kwa kifo cha Mwanae aliyeishi hapa duniani, Mungu amewapatanisha naye, kusudi awalete mbele yake mkiwa watakatifu, safi na bila lawama.
to you, he hath now given peace, by the body of his flesh, and by his death; that he might establish you in his presence, holy, without blemish, and without offence;
23 Mnapaswa, lakini kuendelea kuwa imara na thabiti katika imani hiyo, na msikubali kusukumwa mbali na tumaini lile mlilopata wakati mlipoisikia Habari Njema. Mimi Paulo nimekuwa mtumishi wa hiyo Habari Njema ambayo imekwisha hubiriwa kila kiumbe duniani.
provided ye continue in your faith, your foundation being firm, and ye be not removed from the hope of the gospel; of which ye have heard, that it is proclaimed in all the creation beneath heaven; of which gospel I Paul am a minister.
24 Na sasa nafurahi kuteseka kwa ajili yenu, maana kwa mateso yangu hapa duniani, nasaidia kukamilisha kile kilichopungua bado katika mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, yaani kanisa.
And I rejoice in the sufferings which are for your sakes; and, in my flesh, I fill up the deficiency in the afflictions of the Messiah, in behalf of his body, which is the church;
25 Nami nimefanywa kuwa mtumishi wa kanisa kufuatana na mpango wake Mungu ambao alinikabidhi kwa faida yenu. Mpango wenyewe ni kuutangaza kwa ukamilifu ujumbe wake,
of which I am a minister, according to the dispensation of God which is given to me among you, that I should fulfill the word of God,
26 ambao ni siri aliyowaficha binadamu wote tangu milele, lakini sasa amewajulisha watu wake. (aiōn g165)
namely, that mystery, which was hidden for ages and generations, but is now revealed to his saints; (aiōn g165)
27 Mpango wa Mungu ni kuwajulisha watu wake siri hii kuu na tukufu ambayo ni kwa ajili ya watu wote. Na, siri yenyewe ndiyo hii: Kristo yuko ndani yenu, na jambo hilo lamaanisha kwamba ninyi mtaushiriki utukufu wa Mungu.
to whom God would make known what is the riches of the glory of this mystery among the Gentiles; which mystery is the Messiah; who in you is the hope of our glory;
28 Kwa sababu hiyo tunamhubiri Kristo kwa watu wote; tunawaonya na kuwafundisha wote kwa hekima yote, ili tuweze kumleta kila mmoja mbele ya Mungu akiwa amekomaa katika kuungana na Kristo.
whom we proclaim, and teach and make known to every man, in all wisdom; that we may present every man perfect in Jesus the Messiah.
29 Kwa madhumuni hayo mimi nafanya kazi na kujitahidi nikiitumia nguvu kuu ya Kristo ifanyayo kazi ndani yangu.
And for this also, I toil and strive, with the aid of the strength that is imparted to me.

+ Wakolosai 1 >