< Wakolosai 3 >

1 Basi, ikiwa mmefufuka pamoja na Kristo, panieni mambo ya juu, kule Kristo aliko, ameketi upande wa kulia wa Mungu.
לכן אם קמתם עם המשיח בקשו את אשר למעלה אשר המשיח ישב שם לימין האלהים׃
2 Muwe na hamu ya mambo ya huko juu, na siyo mambo ya hapa duniani.
את אשר למעלה יהגה לבבכם לא את אשר בארץ׃
3 Maana ninyi mmekufa na uzima wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
כי מתם וחייכם צפונים עם המשיח באלהים׃
4 Uzima wenu halisi ni Kristo, na wakati atakapotokea ndipo nanyi pia mtakapotokea pamoja naye katika utukufu.
בעת הגלות המשיח אשר הוא חייכם גם אתם תגלו עמו בכבוד׃
5 Basi, komesheni kabisa kila kitu kilicho ndani yenu ambacho chahusika na mambo ya kidunia: uasherati, uchafu, shauku, tamaa mbaya na uchu (ambao ni sawa na kuabudu sanamu).
על כן תמותתו את אבריכם בארץ את הזנות והטמאה והזמה והתאות הרעות ונטות אחרי הבצע אשר היא עבודת אלילים׃
6 Kwa sababu ya mambo hayo hasira ya Mungu huwajia wote wanaomwasi.
כי בגלל אלה בא חרון אלהים על בני חמרי׃
7 Wakati mmoja ninyi pia mliishi kufuatana na mambo hayo, mlipotawaliwa nayo.
אשר גם אתם הלכתם בהם מלפנים בחיותכם בתוכם׃
8 Lakini sasa mnapaswa kuachana na mambo haya yote: hasira, tamaa, uovu; kufuru au maneno yasiyofaa yasitoke kamwe vinywani mwenu.
אך עתה הסירו מכם כל אלה את הרגז את הכעס את הרשע את הגדוף ואת דברי נבלה מפיכם׃
9 Msiambiane uongo, kwani ninyi mmekwisha vua ule utu wa kale pamoja na matendo yake yote,
ואל תשקרו איש בעמיתו כי פשטתם את האדם הישן עם פעלותיו׃
10 mkavaa utu mpya. Huu unaendelea kurekebishwa na Mungu, Muumba wake, kadiri ya mfano wake, ili mpate kumjua Mungu kwa ukamilifu.
ולבשתם את האדם החדש המתחדש בדעת כצלם בראו׃
11 Katika hali hii, hakuna tena tofauti kati ya Mgiriki na Myahudi, aliyetahiriwa na asiyetahiriwa, msomi na asiye msomi, mtumwa na mtu aliye huru. Kristo ni kila kitu, na yumo katika yote.
אשר אין שם יוני ויהודי אין מילה וערלה אין לעז וסקותי אין עבד ובן חורין כי המשיח הוא הכל ובכל׃
12 Ninyi ni watu wake Mungu; yeye aliwapenda na kuwateua. Kwa hiyo basi, vaeni moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
לכן אתם כבחירי האלהים הקדשים והחביבים לבשו המון רחמים ונדיבות ונמיכות רוח וענוה וארך אפים׃
13 Vumilianeni na kusameheana iwapo mmoja wenu analo jambo lolote dhidi ya mwenzake. Mnapaswa kusameheana kama Bwana alivyowasamehe ninyi.
ותשאו איש את רעהו ותסלחו בהיות לכם ריב איש עם אחיו כאשר המשיח סלח לכם כן תסלחו גם אתם׃
14 Zaidi ya hayo yote, zingatieni upendo kwani upendo huunganisha kila kitu katika umoja ulio kamili.
ועל כל אלה לבשו האהבה היא אגדת השלמות׃
15 Nayo amani ya Kristo itawale mioyoni mwenu; maana kwa ajili hiyo ninyi mmeitwa katika mwili huo mmoja. Tena muwe na shukrani!
וישלט בלבבכם שלום האלהים אשר נקראתם לו בגוף אחד וזבחו תודה׃
16 Ujumbe wa Kristo ukae ndani yenu pamoja na utajiri wake wote. Fundishaneni na kushauriana kwa hekima yote. Imbeni zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Mungu mioyoni mwenu kwa shukrani.
דבר האדון ישכן בקרבכם בשפע רב בכל חכמה ותלמדו ותעוררו את נפשכם בתהלות ותשבחות ושירות רוחניות ושירו ליהוה בנעימה בלבבכם׃
17 Na, kila mfanyacho kwa neno au tendo, fanyeni vyote kwa jina la Bwana Yesu na kumshukuru Mungu Baba kwa njia yake.
וכל אשר תעשו הן במלין הן בפעל עשו בשם האדון ישוע והודו לאלהים אבינו על ידי׃
18 Enyi akina mama, watiini waume zenu, kwani ndivyo apendavyo Bwana.
אתן הנשים הכנענה לבעליכן כראוי באדנינו׃
19 Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali kwao.
אתם האנשים אהבו את נשיכם ואל תתמרמרו אליהן׃
20 Enyi watoto, watiini wazazi wenu daima maana hiyo humpendeza Bwana.
הבנים שמעו אל ילדיכם בכל דבר כי הוא לרצון לאדנינו׃
21 Nanyi wazazi, msiwachukize watoto wenu, la sivyo watakata tamaa.
האבות אל תרגיזו את בניכם פן יחתו׃
22 Enyi watumwa, watiini wakuu wenu wa kidunia katika mambo yote, na si tu wakati wanapowatazama kwa kuwa mnataka kujipendekeza kwao; ila fanyeni hivyo kwa moyo wote, kwa sababu ya kumcha Bwana.
העבדים שמעו בכל דבר אל אדניכם לפי הבשר לא בעבודה למראה העין כמבקשי חן בני אדם כי אם בתם לבב כיראי האלהים׃
23 Kila mfanyalo, fanyeni kwa moyo wote, kwa sababu ya Bwana na si kwa ajili ya mtu.
כל אשר תעשו עשו בכל נפשכם כמו ליהוה ולא לבני אדם׃
24 Kumbukeni kwamba atawapeni tuzo lile alilowawekea watu wake. Mtumikieni Kristo Bwana!
וידעתם כי תקבלו מאת יהוה גמול הירשה כי את אדנינו המשיח עבדים אתם׃
25 Atendaye mabaya atalipwa kufuatana na ubaya wake; Mungu hana ubaguzi.
וכל עשה עול הוא ישא העול אשר עשה ואין שם משא פנים׃

< Wakolosai 3 >