< Matendo 8 >
1 Saulo naye alikiona kitendo hicho cha kumwua Stefano kuwa sawa. Siku hiyo kanisa la Yerusalemu lilianza kuteswa vibaya. Waumini wote, isipokuwa tu wale mitume, walilazimika kutawanyika katika sehemu za mashambani za Yudea na Samaria.
A Saul zezwolił na zabicie jego. I wszczęło się onegoż czasu wielkie prześladowanie przeciwko zborowi, który był w Jeruzalemie, i rozproszyli się wszyscy po krainach ziemi Judzkiej i Samaryi, oprócz Apostołów.
2 Watu wamchao Mungu, walimzika Stefano na kumfanyia maombolezo makubwa.
I pogrzebli Szczepana mężowie bogobojni i uczynili nad nim płacz wielki.
3 Wakati huohuo, Saulo alijaribu kuliangamiza kanisa. Alikwenda katika kila nyumba, akawatoa nje waumini, wanaume kwa wanawake, akawatia gerezani.
A Saul niszczył zbór, wchodząc w domy, a wywłóczając męże i niewiasty, podawał je do więzienia.
4 Wale waumini waliotawanyika, walikwenda kila mahali wakihubiri ule ujumbe.
A ci, którzy byli rozproszeni, chodzili opowiadając słowo Boże.
5 Naye Filipo aliingia katika mji wa Samaria na kumhubiri Kristo kwa wenyeji wa hapo.
Lecz Filip zaszedłszy do miasta Samaryjskiego, opowiadał im Chrystusa.
6 Watu walijiunga kusikiliza kwa makini ule ujumbe wa Filipo na kuona ile miujiza aliyoifanya.
A lud miał wzgląd jednomyślnie na to, co Filip mówił, słuchając i widząc cuda, które czynił.
7 Maana pepo wachafu waliokuwa wamewapagaa watu wengi waliwatoka wakipiga kelele kubwa; na pia watu wengi waliokuwa wamepooza viungo na waliolemaa waliponywa.
Albowiem duchy nieczyste od wielu tych, którzy je mieli, wołając głosem wielkim wychodziły, a wiele powietrzem ruszonych i chromych uzdrowieni są.
8 Kukawa na furaha kubwa katika mji ule.
I stała się radość wielka w onem mieście.
9 Basi, kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Simoni ambaye alikuwa amekwisha fanya uchawi wake katika mji huo kwa muda na kuwashangaza watu wa Samaria, akijiona kuwa yeye ni mtu maarufu.
A niektóry mąż, imieniem Szymon, był przedtem w onem mieście bawiący się nauką czarnoksięską i lud Samaryjski mamił, powiadając się być czymś wielkim.
10 Watu wote, wadogo na wakubwa, walimsikiliza kwa makini wakisema, “Simoni ndiye ile nguvu ya kimungu inayoitwa Nguvu Kubwa.”
Na którego się oglądali wszyscy od najmniejszego aż do największego, mówiąc: Tenci jest ona moc Boża wielka.
11 Walivutiwa sana naye kwa vile alikuwa amewashangaza kwa uchawi wake kwa muda mrefu.
A oglądali się nań przeto, iż je od niemałego czasu mamił czarnoksięstwy swemi.
12 Lakini walipouamini ujumbe wa Filipo juu ya Habari Njema ya Ufalme wa Mungu na jina la Yesu Kristo, walibatizwa, wanawake na wanaume.
A gdy uwierzyli Filipowi, opowiadającemu królestwo Boże i imię Jezusa Chrystusa, chrzcili się mężowie i niewiasty.
13 Hata Simoni aliamini; baada ya kubatizwa ilikuwa akiandamana na Filipo, akastaajabia maajabu na miujiza iliyokuwa inafanyika.
Tedy i sam Szymon uwierzył, a ochrzciwszy się, trzymał się Filipa, a widząc cuda i mocy wielkie, które się działy, zdumiewał się.
14 Wale mitume waliokuwa kule Yerusalemu walipopata habari kwamba wenyeji wa Samaria nao wamelipokea neno la Mungu, waliwatuma kwao Petro na Yohane.
A usłyszawszy Apostołowie, którzy byli w Jeruzalemie, iż Samaryja przyjęła słowo Boże, posłali do nich Piotra i Jana.
15 Walipofika waliwaombea hao waumini ili wampokee Roho Mtakatifu;
Którzy tam przyszedłszy, modlili się za nimi, aby przyjęli Ducha Świętego.
16 maana wakati huo Roho Mtakatifu hakuwa ameshukia yeyote kati yao; walikuwa wamebatizwa tu kwa jina la Bwana Yesu.
(Albowiem jeszcze był na żadnego z nich nie zstąpił; ale tylko pochrzczeni byli w imię Pana Jezusowe.)
17 Basi, Petro na Yohane wakawawekea mikono hao waumini, nao wakampokea Roho Mtakatifu.
Tedy na nie wkładali ręce, a oni przyjmowali Ducha Świętego.
18 Hapo Simoni aling'amua kwamba kwa kuwekewa mikono ya mitume waumini walipewa Roho Mtakatifu. Hivyo aliwapa Petro na Yohane fedha akisema,
A ujrzawszy Szymon, że przez wkładanie rąk apostolskich był dawany Duch Święty, przyniósł im pieniądze.
19 “Nipeni na mimi uwezo huo ili yeyote nitakayemwekea mikono, apokee Roho Mtakatifu.”
Mówiąc: Dajcie i mnie tę moc, aby ten, na któregokolwiek bym ręce włożył, wziął Ducha Świętego.
20 Lakini Petro akamjibu, “Potelea mbali na fedha zako kwa vile unafikiri kwamba unaweza kununua karama ya Mungu kwa fedha!
I rzekł mu Piotr: Pieniądze twoje niech z tobą będą na zginienie, żeś mniemał, żeby dar Boży miał być za pieniądze nabywany.
21 Huna sehemu yoyote wala haki katika kazi hiyo kwa maana moyo wako hauko sawa mbele ya macho ya Mungu.
Nie masz w tej rzeczy cząstki, ani losu, gdy serce twoje nie jest proste przed obliczem Bożem.
22 Kwa hiyo, tubu ubaya wako huu na umwombe Bwana naye anaweza kukusamehe fikira kama hizo.
Przetoż pokutuj z tej twojej złości, a proś Boga; ować snać będzie odpuszczony ten zamysł serca twego.
23 Ni dhahiri kwangu kwamba umejaa wivu mkali na mfungwa wa dhambi!”
Albowiem cię widzę być w gorzkości żółci i w związce nieprawości.
24 Simoni akajibu, “Tafadhali, niombeeni kwa Bwana lisije likanipata lolote kati ya hayo mliyosema.”
Odpowiedziawszy tedy Szymon, rzekł: Módlcie się wy za mną Panu, aby na mię nic nie przyszło z tych rzeczy, któreście powiedzieli.
25 Baada ya Petro na Yohane kutoa ushuhuda wao na kuutangaza ujumbe wa Bwana, walirudi Yerusalemu. Walipokuwa wanarudi walihubiri Habari Njema katika vijiji vingi vya Samaria.
A tak oni oświadczywszy i opowiedziawszy słowo Pańskie, wrócili się do Jeruzalemu i w wielu miasteczkach Samarytańskich Ewangieliję opowiadali.
26 Malaika wa Bwana alimwambia Filipo, “Jitayarishe uende kusini kupitia njia inayotoka Yerusalemu kwenda Gaza.” (Njia hiyo hupita jangwani.)
Lecz Anioł Pański rzekł do Filipa, mówiąc: Wstań, a idź ku południowi na drogę, która od Jeruzalemu idzie ku Gazie, która jest pusta.
27 Basi, Filipo akajiweka tayari, akaanza safari. Wakati huohuo kulikuwa na Mwethiopia mmoja, towashi, ambaye alikuwa anasafiri kuelekea nyumbani. Huyo mtu alikuwa ofisa maarufu wa hazina ya Kandake, malkia wa Ethiopia. Alikuwa amekwenda huko Yerusalemu kuabudu na wakati huo alikuwa anarudi akiwa amepanda gari la kukokotwa.
A on wstawszy, szedł. A oto mąż Murzyn rzezaniec, komornik królowej murzyńskiej Kandaces, który był nad wszystkiemi skarbami jej, a przyjechał był do Jeruzalemu, aby się modlił;
28 Alipokuwa anasafiri, alikuwa akijisomea kitabu cha nabii Isaya.
I wracał się, siedząc na wozie swoim, a czytał Izajasza proroka.
29 Basi, Roho Mtakatifu akamwambia Filipo, “Nenda karibu na gari hilo ukafuatane nalo.”
I rzekł Duch Filipowi: Przystąp, a przyłącz się do tego wozu.
30 Filipo akakimbilia karibu na gari, akamsikia huyo mtu akisoma katika kitabu cha nabii Isaya. Hapo Filipo akamwuliza, “Je, unaelewa hayo unayosoma?”
A przybieżawszy Filip, usłyszał go czytającego Izajasza proroka i rzekł: Rozumieszże, co czytasz?
31 Huyo mtu akamjibu, “Ninawezaje kuelewa bila mtu kunielewesha?” Hapo akamwalika Filipo apande juu, aketi pamoja naye.
A on rzekł: Jakoż mogę rozumieć, jeźliby mi kto nie wyłożył? I prosił Filipa, a wstąpił i siedział z nim.
32 Basi, sehemu ya Maandiko Matakatifu aliyokuwa anasoma ilikuwa hii: “Alikuwa kama kondoo anayepelekwa kuchinjwa; kimya kama vile mwana kondoo anaponyolewa manyoya, yeye naye hakutoa sauti hata kidogo.
A miejsce onego Pisma, które czytał, to było: Jako owca ku zabiciu wiedziony jest, a jako baranek niemy przed tym, który go strzyże, tak nie otworzył ust swoich;
33 Alifedheheshwa na kunyimwa haki. Hakuna atakayeweza kuongea juu ya kizazi chake, kwa maana maisha yake yameondolewa duniani.”
W uniżeniu jego sąd jego zniesiony jest, a rodzaj jego któż wypowie? albowiem zniesiony był z ziemi żywot jego.
34 Huyo Mwethiopia akamwambia Filipo, “Niambie, huyu nabii anasema juu ya nani? Anasema mambo haya juu yake yeye mwenyewe au juu ya mtu mwingine?”
A odpowiadając rzezaniec Filipowi, rzekł: Proszę cię, o kim to prorok mówi? Sam o sobie, czyli o kim innym?
35 Basi, Filipo akianzia na sehemu hiyo ya Maandiko Matakatifu, akamweleza Habari Njema juu ya Yesu.
Tedy otworzywszy Filip usta swe, a począwszy od tego Pisma, opowiadał mu Jezusa.
36 Walipokuwa bado wanaendelea na safari walifika mahali penye maji na huyo ofisa akasema, “Mahali hapa pana maji; je, kuna chochote cha kunizuia nisibatizwe?”
A gdy jechali drogą, przyjechali nad jednę wodę. Tedy rzekł rzezaniec: Otóż woda! Cóż na przeszkodzie, abym nie miał być ochrzczony?
37 Filipo akasema, “Kama unaamini kwa moyo wako wote unaweza kubatizwa.” Naye akajibu, “Naam, ninaamini kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu.”
I rzekł Filip: Jeźliż wierzysz z całego serca, wolnoć. A on odpowiedziawszy, rzekł: Wierzę, iż Jezus Chrystus jest Syn Boży.
38 Basi, huyo ofisa akaamuru lile gari lisimame; na wote wawili, Filipo na huyo ofisa wakashuka majini, naye Filipo akambatiza.
I kazał stanąć wozowi; i zstąpili obadwaj w wodę, Filip i rzezaniec, i ochrzcił go.
39 Walipotoka majini Roho wa Bwana akamfanya Filipo atoweke. Na huyo Mwethiopia hakumwona tena; lakini akaendelea na safari yake akiwa amejaa furaha.
A gdy wystąpili z wody, porwał Filipa Duch Pański i nie widział go więcej rzezaniec, ale jechał drogą swoją, radując się.
40 Filipo akajikuta yuko Azoto, akapita katika miji yote akihubiri Habari Njema mpaka alipofika Kaisarea.
A Filip aż w Azocie jest znaleziony, a chodząc kazał Ewangieliję po wszystkich miastach, aż przyszedł do Cezaryi.