< Matendo 8 >

1 Saulo naye alikiona kitendo hicho cha kumwua Stefano kuwa sawa. Siku hiyo kanisa la Yerusalemu lilianza kuteswa vibaya. Waumini wote, isipokuwa tu wale mitume, walilazimika kutawanyika katika sehemu za mashambani za Yudea na Samaria.
Men Saulus fandt Behag i hans Mord. Og paa den Dag udbrød der en stor Forfølgelse imod Menigheden i Jerusalem, og de adspredtes alle over Judæas og Samarias Egne, undtagen Apostlene.
2 Watu wamchao Mungu, walimzika Stefano na kumfanyia maombolezo makubwa.
Men gudfrygtige Mænd begravede Stefanus og holdt en stor Veklage over ham.
3 Wakati huohuo, Saulo alijaribu kuliangamiza kanisa. Alikwenda katika kila nyumba, akawatoa nje waumini, wanaume kwa wanawake, akawatia gerezani.
Men Saulus plagede Menigheden og gik ind i Husene og trak baade Mænd og Kvinder frem og lod dem sætte i Fængsel.
4 Wale waumini waliotawanyika, walikwenda kila mahali wakihubiri ule ujumbe.
Imidlertid gik de, som bleve adspredte, omkring og forkyndte Evangeliets Ord.
5 Naye Filipo aliingia katika mji wa Samaria na kumhubiri Kristo kwa wenyeji wa hapo.
Da kom Filip til Byen Samaria og prædikede Kristus for dem.
6 Watu walijiunga kusikiliza kwa makini ule ujumbe wa Filipo na kuona ile miujiza aliyoifanya.
Og Skarerne gave endrægtigt Agt paa det, som blev sagt af Filip, idet de hørte og saa de Tegn, som han gjorde.
7 Maana pepo wachafu waliokuwa wamewapagaa watu wengi waliwatoka wakipiga kelele kubwa; na pia watu wengi waliokuwa wamepooza viungo na waliolemaa waliponywa.
Thi der var mange, som havde urene Aander, og af hvem disse fore ud, raabende med høj Røst; og mange værkbrudne og lamme bleve helbredede.
8 Kukawa na furaha kubwa katika mji ule.
Og der blev en stor Glæde i denne By.
9 Basi, kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Simoni ambaye alikuwa amekwisha fanya uchawi wake katika mji huo kwa muda na kuwashangaza watu wa Samaria, akijiona kuwa yeye ni mtu maarufu.
Men en Mand, ved Navn Simon, var i Forvejen i Byen og drev Trolddom og satte Samarias Folk i Forbavselse, idet han udgav sig selv for at være noget stort.
10 Watu wote, wadogo na wakubwa, walimsikiliza kwa makini wakisema, “Simoni ndiye ile nguvu ya kimungu inayoitwa Nguvu Kubwa.”
Paa ham gave alle Agt, smaa og store, og sagde: „Det er ham, som man kalder Guds store Kraft.”
11 Walivutiwa sana naye kwa vile alikuwa amewashangaza kwa uchawi wake kwa muda mrefu.
Men de gave Agt paa ham, fordi han i lang Tid havde sat dem i Forbavselse ved sine Trolddomskunster.
12 Lakini walipouamini ujumbe wa Filipo juu ya Habari Njema ya Ufalme wa Mungu na jina la Yesu Kristo, walibatizwa, wanawake na wanaume.
Men da de troede Filip, som forkyndte Evangeliet om Guds Rige og Jesu Kristi Navn, lode de sig døbe, baade Mænd og Kvinder.
13 Hata Simoni aliamini; baada ya kubatizwa ilikuwa akiandamana na Filipo, akastaajabia maajabu na miujiza iliyokuwa inafanyika.
Men Simon troede ogsaa selv, og efter at være døbt holdt han sig nær til Filip; og da han saa Tegn og store kraftige Gerninger ske, forbavsedes han højligt.
14 Wale mitume waliokuwa kule Yerusalemu walipopata habari kwamba wenyeji wa Samaria nao wamelipokea neno la Mungu, waliwatuma kwao Petro na Yohane.
Men da Apostlene i Jerusalem hørte, at Samaria havde taget imod Guds Ord, sendte de Peter og Johannes til dem,
15 Walipofika waliwaombea hao waumini ili wampokee Roho Mtakatifu;
og da disse vare komne derned, bade de for dem om, at de maatte faa den Helligaand;
16 maana wakati huo Roho Mtakatifu hakuwa ameshukia yeyote kati yao; walikuwa wamebatizwa tu kwa jina la Bwana Yesu.
thi den var endnu ikke falden paa nogen af dem, men de vare blot døbte til den Herres Jesu Navn.
17 Basi, Petro na Yohane wakawawekea mikono hao waumini, nao wakampokea Roho Mtakatifu.
Da lagde de Hænderne paa dem, og de fik den Helligaand.
18 Hapo Simoni aling'amua kwamba kwa kuwekewa mikono ya mitume waumini walipewa Roho Mtakatifu. Hivyo aliwapa Petro na Yohane fedha akisema,
Men da Simon saa, at den Helligaand blev given ved Apostlenes Haandspaalæggelse, bragte han dem Penge og sagde:
19 “Nipeni na mimi uwezo huo ili yeyote nitakayemwekea mikono, apokee Roho Mtakatifu.”
„Giver ogsaa mig denne Magt, at, hvem jeg lægger Hænderne paa, han maa faa den Helligaand.”
20 Lakini Petro akamjibu, “Potelea mbali na fedha zako kwa vile unafikiri kwamba unaweza kununua karama ya Mungu kwa fedha!
Men Peter sagde til ham: „Gid dit Sølv maa gaa til Grunde tillige med dig, fordi du mente at kunne erhverve Guds Gave for Penge.
21 Huna sehemu yoyote wala haki katika kazi hiyo kwa maana moyo wako hauko sawa mbele ya macho ya Mungu.
Du har ikke Del eller Lod i dette Ord; thi dit Hjerte er ikke ret for Gud.
22 Kwa hiyo, tubu ubaya wako huu na umwombe Bwana naye anaweza kukusamehe fikira kama hizo.
Omvend dig derfor fra denne din Ondskab og bed Herren, om dog dit Hjertes Paafund maatte forlades dig.
23 Ni dhahiri kwangu kwamba umejaa wivu mkali na mfungwa wa dhambi!”
Thi jeg ser, at du er stedt i Bitterheds Galde og Uretfærdigheds Lænke.”
24 Simoni akajibu, “Tafadhali, niombeeni kwa Bwana lisije likanipata lolote kati ya hayo mliyosema.”
Men Simon svarede og sagde: „Beder I for mig til Herren, for at intet af det, som I have sagt, skal komme over mig.”
25 Baada ya Petro na Yohane kutoa ushuhuda wao na kuutangaza ujumbe wa Bwana, walirudi Yerusalemu. Walipokuwa wanarudi walihubiri Habari Njema katika vijiji vingi vya Samaria.
Men da de havde vidnet og talt Herrens Ord, vendte de tilbage til Jerusalem, og de forkyndte Evangeliet i mange af Samaritanernes Landsbyer.
26 Malaika wa Bwana alimwambia Filipo, “Jitayarishe uende kusini kupitia njia inayotoka Yerusalemu kwenda Gaza.” (Njia hiyo hupita jangwani.)
Men en Herrens Engel talte til Filip og sagde: „Staa op og gaa mod Syd paa den Vej, som gaar ned fra Jerusalem til Gaza; den er øde.”
27 Basi, Filipo akajiweka tayari, akaanza safari. Wakati huohuo kulikuwa na Mwethiopia mmoja, towashi, ambaye alikuwa anasafiri kuelekea nyumbani. Huyo mtu alikuwa ofisa maarufu wa hazina ya Kandake, malkia wa Ethiopia. Alikuwa amekwenda huko Yerusalemu kuabudu na wakati huo alikuwa anarudi akiwa amepanda gari la kukokotwa.
Og han stod op og gik. Og se, der var en Æthioper, en Hofmand, en mægtig Mand hos Kandake, Æthiopernes Dronning, som var sat over alle hendes Skatte; han var kommen til Jerusalem for at tilbede.
28 Alipokuwa anasafiri, alikuwa akijisomea kitabu cha nabii Isaya.
Og han var paa Hjemvejen og sad paa sin Vogn og læste Profeten Esajas.
29 Basi, Roho Mtakatifu akamwambia Filipo, “Nenda karibu na gari hilo ukafuatane nalo.”
Men Aanden sagde til Filip: „Gaa hen og hold dig til denne Vogn!”
30 Filipo akakimbilia karibu na gari, akamsikia huyo mtu akisoma katika kitabu cha nabii Isaya. Hapo Filipo akamwuliza, “Je, unaelewa hayo unayosoma?”
Og Filip løb derhen og hørte ham læse Profeten Esajas; og han sagde: „Forstaar du ogsaa det, som du læser?”
31 Huyo mtu akamjibu, “Ninawezaje kuelewa bila mtu kunielewesha?” Hapo akamwalika Filipo apande juu, aketi pamoja naye.
Men han sagde: „Hvorledes skulde jeg kunne det, uden nogen vejleder mig?” Og han bad Filip stige op og sætte sig hos ham.
32 Basi, sehemu ya Maandiko Matakatifu aliyokuwa anasoma ilikuwa hii: “Alikuwa kama kondoo anayepelekwa kuchinjwa; kimya kama vile mwana kondoo anaponyolewa manyoya, yeye naye hakutoa sauti hata kidogo.
Men det Stykke af Skriften, som han læste, var dette: „Som et Faar blev han ført til Slagtning, og som et Lam er stumt imod den, der klipper det, saaledes oplader han ej sin Mund.
33 Alifedheheshwa na kunyimwa haki. Hakuna atakayeweza kuongea juu ya kizazi chake, kwa maana maisha yake yameondolewa duniani.”
I Fornedrelsen blev hans Dom taget bort; hvem kan fortælle om hans Slægt, efterdi hans Liv borttages fra Jorden?”
34 Huyo Mwethiopia akamwambia Filipo, “Niambie, huyu nabii anasema juu ya nani? Anasema mambo haya juu yake yeye mwenyewe au juu ya mtu mwingine?”
Men Hofmanden talte til Filip og sagde: „Jeg beder dig, om hvem siger Profeten dette? om sig selv eller om en anden?”
35 Basi, Filipo akianzia na sehemu hiyo ya Maandiko Matakatifu, akamweleza Habari Njema juu ya Yesu.
Da oplod Filip sin Mund, og idet han begyndte fra dette Skriftsted, forkyndte han ham Evangeliet om Jesus.
36 Walipokuwa bado wanaendelea na safari walifika mahali penye maji na huyo ofisa akasema, “Mahali hapa pana maji; je, kuna chochote cha kunizuia nisibatizwe?”
Men som de droge frem ad Vejen, kom de til noget Vand; og Hofmanden siger: „Se, her er Vand, hvad hindrer mig fra at blive døbt?”
37 Filipo akasema, “Kama unaamini kwa moyo wako wote unaweza kubatizwa.” Naye akajibu, “Naam, ninaamini kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu.”
[Men Filip sagde: „Dersom du tror af hele dit Hjerte, kan det ske.” Men han svarede og sagde: „Jeg tror, at Jesus Kristus er Guds Søn.”]
38 Basi, huyo ofisa akaamuru lile gari lisimame; na wote wawili, Filipo na huyo ofisa wakashuka majini, naye Filipo akambatiza.
Og han bød, at Vognen skulde holde, og de stege begge ned i Vandet, baade Filip og Hofmanden; og han døbte ham.
39 Walipotoka majini Roho wa Bwana akamfanya Filipo atoweke. Na huyo Mwethiopia hakumwona tena; lakini akaendelea na safari yake akiwa amejaa furaha.
Men da de stege op af Vandet, bortrykkede Herrens Aand Filip, og Hofmanden saa ham ikke mere; thi han drog sin Vej med Glæde.
40 Filipo akajikuta yuko Azoto, akapita katika miji yote akihubiri Habari Njema mpaka alipofika Kaisarea.
Men Filip blev funden i Asdod, og han drog omkring og forkyndte Evangeliet i alle Byerne, indtil han kom til Kæsarea.

< Matendo 8 >