< Matendo 6 >

1 Baadaye, idadi ya wanafunzi ilipokuwa inazidi kuongezeka, kulitokea manung'uniko kati ya wanafunzi waliosema Kigiriki na wale waliosema Kiebrania. Wale waliosema Kigiriki walinung'unika kwamba wajane wao walikuwa wanasahauliwa katika ugawaji wa mahitaji ya kila siku.
tasmin samayE ziSyANAM bAhulyAt prAtyahikadAnasya vizrANanai rbhinnadEzIyAnAM vidhavAstrIgaNa upEkSitE sati ibrIyalOkaiH sahAnyadEzIyAnAM vivAda upAtiSThat|
2 Kwa hiyo, mitume kumi na wawili waliita jumuiya yote ya wanafunzi, wakasema, “Si vizuri sisi tuache kulihubiri neno la Mungu ili tushughulikie ugawaji wa mahitaji.
tadA dvAdazaprEritAH sarvvAn ziSyAn saMgRhyAkathayan Izvarasya kathApracAraM parityajya bhOjanagavESaNam asmAkam ucitaM nahi|
3 Hivyo, ndugu zetu, chagueni miongoni mwenu watu saba wenye sifa njema, waliojawa na Roho na wenye hekima; nasi tutawakabidhi jukumu hilo.
atO hE bhrAtRgaNa vayam EtatkarmmaNO bhAraM yEbhyO dAtuM zaknuma EtAdRzAn sukhyAtyApannAn pavitrENAtmanA jnjAnEna ca pUrNAn sapprajanAn yUyaM svESAM madhyE manOnItAn kuruta,
4 Sisi, lakini, tutashughulika na sala na kazi ya kuhubiri neno la Mungu.”
kintu vayaM prArthanAyAM kathApracArakarmmaNi ca nityapravRttAH sthAsyAmaH|
5 Jambo hilo likaipendeza jumuiya yote ya waumini. Wakawachagua Stefano, mtu mwenye imani kubwa na mwenye kujawa na Roho Mtakatifu, Filipo, Prokoro, Nikanora, Timona, Parmena na Nikolao wa Antiokia ambaye hapo awali alikuwa ameongokea dini ya Kiyahudi.
EtasyAM kathAyAM sarvvE lOkAH santuSTAH santaH svESAM madhyAt stiphAnaH philipaH prakharO nikAnOr tIman parmmiNA yihUdimatagrAhI-AntiyakhiyAnagarIyO nikalA EtAn paramabhaktAn pavitrENAtmanA paripUrNAn sapta janAn
6 Wakawaweka mbele ya mitume, nao wakawaombea na kuwawekea mikono.
prEritAnAM samakSam Anayan, tatastE prArthanAM kRtvA tESAM ziraHsu hastAn Arpayan|
7 Neno la Mungu likazidi kuenea na idadi ya waumini huko Yerusalemu ikaongezeka zaidi, na kundi kubwa la makuhani wakaipokea imani.
aparanjca Izvarasya kathA dEzaM vyApnOt vizESatO yirUzAlami nagarE ziSyANAM saMkhyA prabhUtarUpENAvarddhata yAjakAnAM madhyEpi bahavaH khrISTamatagrAhiNO'bhavan|
8 Mungu alimjalia Stefano neema tele, akampa nguvu nyingi hata akawa anatenda miujiza na maajabu kati ya watu.
stiphAnO vizvAsEna parAkramENa ca paripUrNaH san lOkAnAM madhyE bahuvidham adbhutam AzcaryyaM karmmAkarOt|
9 Lakini watu fulani wakatokea ili wabishane na Stefano. Baadhi ya watu hao walikuwa wa sunagogi moja lililoitwa “Sunagogi la Watu Huru”, nao walitoka Kurene na Aleksandria; wengine walitoka Kilikia na Asia.
tEna libarttinIyanAmnA vikhyAtasagghasya katipayajanAH kurINIyasikandarIya-kilikIyAzIyAdEzIyAH kiyantO janAzcOtthAya stiphAnEna sArddhaM vyavadanta|
10 Lakini hawakuweza kumshinda kwa sababu ya hekima yake na kwa sababu ya yule Roho aliyeongoza maneno yake.
kintu stiphAnO jnjAnEna pavitrENAtmanA ca IdRzIM kathAM kathitavAn yasyAstE ApattiM karttuM nAzaknuvan|
11 Kwa hiyo waliwahonga watu kadhaa waseme: “Tumemsikia Stefano akisema maneno ya kumkashifu Mose na kumkashifu Mungu.”
pazcAt tai rlObhitAH katipayajanAH kathAmEnAm akathayan, vayaM tasya mukhatO mUsA Izvarasya ca nindAvAkyam azrauSma|
12 Kwa namna hiyo, waliwachochea watu, wazee na walimu wa Sheria. Basi, wakamjia Stefano, wakamkamata na kumleta mbele ya Baraza kuu.
tE lOkAnAM lOkaprAcInAnAm adhyApakAnAnjca pravRttiM janayitvA stiphAnasya sannidhim Agatya taM dhRtvA mahAsabhAmadhyam Anayan|
13 Walileta Barazani mashahidi wa uongo ambao walisema, “Mtu huyu haachi kamwe kusema maneno ya kupakashifu mahali hapa patakatifu na Sheria ya Mose.
tadanantaraM katipayajanESu mithyAsAkSiSu samAnItESu tE'kathayan ESa jana EtatpuNyasthAnavyavasthayO rnindAtaH kadApi na nivarttatE|
14 Kwa maana tulikwisha msikia akisema eti huyo Yesu wa Nazareti atapaharibu kabisa mahali hapa na kufutilia mbali desturi zile tulizopokea kutoka kwa Mose.”
phalatO nAsaratIyayIzuH sthAnamEtad ucchinnaM kariSyati mUsAsamarpitam asmAkaM vyavaharaNam anyarUpaM kariSyati tasyaitAdRzIM kathAM vayam azRNuma|
15 Wote waliokuwa katika kile kikao cha Baraza walimkodolea macho Stefano, wakauona uso wake umekuwa kama wa malaika.
tadA mahAsabhAsthAH sarvvE taM prati sthirAM dRSTiM kRtvA svargadUtamukhasadRzaM tasya mukham apazyan|

< Matendo 6 >