< Matendo 5 >
1 Mtu mmoja aitwaye Anania na mkewe Safira waliuza shamba lao vilevile.
But there was one of [the believers] whose name was Ananias, and whose wife’s name was Sapphira. He [also] sold some land.
2 Lakini, mkewe akiwa anajua, Anania akajiwekea sehemu ya fedha alizopata na ile sehemu nyingine akawakabidhi mitume.
He kept for himself some of the money [he had received for the land], and his wife knew that he had done that. Then he brought the rest of the money and presented it to the apostles [MTY].
3 Basi, Petro akamwuliza, “Anania, mbona Shetani ameuingia moyo wako na kukufanya umdanganye Roho Mtakatifu kwa kujiwekea sehemu ya fedha ulizopata kutokana na lile shamba?
Then Peter said, “Ananias, you [(sg)] let Satan completely control you [MTY] so that you [(sg) tried to] deceive the Holy Spirit [and us(exc)]. (That was [terrible!/Why did you do such a terrible thing]?) [RHQ] [You] have kept for yourself some of the money you [(sg)] received for [selling] the land, [pretending that you(sg) were giving us all of it].
4 Kabla ya kuliuza lilikuwa mali yako, na baada ya kuliuza, bado hizo fedha zilikuwa zako uzitumie utakavyo. Kwa nini basi, uliamua moyoni mwako kufanya jambo la namna hii? Hukumdanganya mtu; umemdanganya Mungu!”
Before you [(sg)] sold that land, you truly owned [RHQ] it. And after you sold it, you could [RHQ] certainly still have used the money any way you wanted [to]. So why did you [(sg) ever] think [RHQ] about doing this [wicked] thing? You were not [merely trying to] deceive us! No, [you tried to deceive] God [himself!]!”
5 Anania aliposikia hayo, akaanguka chini, akafa. Watu wote waliosikia habari ya tukio hilo waliogopa sana.
When Ananias heard that, [immediately] he fell down dead. So all [who were there] who heard [about Ananias’ death] became terrified [PRS].
6 Vijana wakafika wakaufunika mwili wake, wakamtoa nje, wakamzika.
Some young men came in, wrapped his [body in a sheet], and carried it out [and] buried it.
7 Baada ya muda wa saa tatu hivi, mke wake, bila kufahamu mambo yaliyotukia, akaingia mle ndani.
About three hours later, his wife came in, [but] she did not know what had happened.
8 Petro akamwambia, “Niambie! Je, kiasi hiki cha fedha ndicho mlichopata kwa kuuza lile shamba?” Yeye akamjibu, “Naam, ni kiasi hicho.”
[As] Peter [showed her the money] that [Ananias had brought], he asked her, “Tell me, is this the amount [of money you two received for] the land you sold?” She said, “Yes, that’s [what we(exc) received].”
9 Naye Petro akamwambia, “Mbona mmekula njama kumjaribu Roho wa Bwana? Sikiliza! Wale watu waliokwenda kumzika mume wako, sasa wako mlangoni na watakuchukua wewe pia.”
So Peter said to her, “[You both did a terrible thing!] You two agreed [RHQ] to try to determine if you could do that without the Spirit of the Lord [God] revealing [to anyone that you two tried to deceive them!] Listen! [Do you(sg) hear the] footsteps [SYN] of the men who buried your husband? They are right outside this door, and they will carry your [corpse] out [to bury it, too]!”
10 Mara Safira akaanguka mbele ya miguu ya Petro, akafa. Wale vijana walipoingia, walimkuta amekwisha kufa; hivyo wakamtoa nje, wakamzika karibu na mume wake.
Immediately Sapphira fell down dead at Peter’s feet. Then the young men came in. When they saw that she was dead, they carried her [body] out and buried it beside her husband’s [body].
11 Kanisa lote pamoja na wote waliosikia habari ya tukio hilo, waliogopa sana.
So all the believers [in Jerusalem] became greatly frightened [PRS] [because of what God had done to Ananias and Sapphira. And] all [the others] who heard [people tell about] those things also [became greatly frightened].
12 Mitume walifanya miujiza na maajabu mengi kati ya watu. Waumini walikuwa wakikutana pamoja katika ukumbi wa Solomoni.
[God was enabling] the apostles to do many amazing miracles among the people. All the believers were meeting together regularly [in the temple courtyard] at [the place called] Solomon’s Porch.
13 Mtu yeyote mwingine ambaye hakuwa mwamini hakuthubutu kujiunga nao. Hata hivyo, watu wengine wasiokuwa wa imani hiyo waliwasifu.
All of the other people [who had not yet believed in Jesus] were afraid to associate with the believers, [because they knew that if they did anything evil, God would punish them, as well as revealing it to the believers]. However, those people continued to greatly respect the believers.
14 Idadi ya watu waliomwamini Bwana, wanaume kwa wanawake, iliongezeka zaidi na zaidi.
Many more men and women started believing in the Lord [Jesus], and they joined the [group of] believers.
15 Kwa sababu hiyo, watu walikuwa wakipeleka wagonjwa barabarani na kuwalaza juu ya vitanda na mikeka ili Petro akipita, walau kivuli chake kiwaguse baadhi yao.
[The apostles were doing amazing miracles], so [people] were bringing those who were sick into the streets, and laying them on stretchers and mats, in order that [when] Peter came by [he would touch them, or] at least his shadow might fall upon some of them [and heal them].
16 Watu wengi walifika kutoka katika miji ya kando kando ya Yerusalemu, wakiwaleta wagonjwa wao na wale waliokuwa na pepo wachafu, nao wote wakaponywa.
Crowds of people were also coming [to the apostles] from the towns near Jerusalem. They were bringing their sick [relatives/friends] and those who were being tormented/troubled by evil spirits {whom evil spirits were tormenting/troubling}, and [God] healed all of them.
17 Kisha, Kuhani Mkuu na wenzake waliokuwa wa kikundi cha Masadukayo wa mahali hapo, wakawaonea mitume wivu.
Then the high priest and all who were with him, who were members of the [local] Sadducee [sect in Jerusalem], became very jealous [of the apostles, because many people were accepting the apostles’ message].
18 Basi, wakawatia nguvuni, wakawafunga ndani ya gereza kuu.
So they commanded the Temple guards to seize the apostles and put them in the public jail.
19 Lakini usiku malaika wa Bwana aliifungua milango ya gereza, akawatoa nje, akawaambia,
[The guards did that], but during the night an angel from the Lord [God] opened the jail doors and brought the apostles outside! [The guards were not aware of what the angel had done].
20 “Nendeni mkasimame Hekaluni na kuwaambia watu kila kitu kuhusu maisha haya mapya.”
Then the angel said [to the apostles], “Go to the Temple [courtyard], stand there, and tell the people all about [how God can give them eternal] life!”
21 Mitume walitii, wakaingia Hekaluni asubuhi na mapema, wakaanza kufundisha. Kuhani Mkuu na wenzake walipofika, waliita mkutano wa Baraza kuu, yaani halmashauri yote ya wazee wa Wayahudi halafu wakawatuma watu gerezani wawalete wale mitume.
So having heard this, about dawn they entered the Temple [courtyard] and began to teach the people again [about Jesus]. Acts 5:21b-24 Meanwhile, the high priest and those who were with him summoned the other Jewish Council members. Altogether they made up the entire Council of Israel. [After they all gathered together], they sent [guards] to the jail to bring in the apostles.
22 Lakini hao watumishi walipofika huko hawakuwakuta mle gerezani. Hivyo walirudi, wakatoa taarifa mkutanoni,
But when the guards arrived at the jail, they discovered that the apostles were not there. So they returned to the Council, and [one of] them reported,
23 wakisema, “Tulikuta gereza limefungwa kila upande na walinzi wakilinda milango. Lakini tulipofungua hatukumkuta mtu yeyote ndani.”
“We [(exc)] saw that the jail [doors] were very securely locked, and the guards were standing at the doors. But when we opened [the doors and went in to get those men], none [of them was] inside [the jail]!”
24 Mkuu wa walinzi wa Hekalu na makuhani wakuu waliposikia habari hiyo wakawa na wasiwasi, wasijue yaliyowapata.
When the captain of the temple guards and the chief priests heard that, they became greatly perplexed, [wondering] what might result from all this.
25 Akafika mtu mmoja, akawaambia, “Wale watu mliowafunga gerezani, hivi sasa wamo Hekaluni, wanawafundisha watu.”
Then someone came [from the Temple courtyard] and [excitedly] reported to them, “Listen [to this! Right now] the men whom you put in jail are standing in the Temple [courtyard] and they are teaching the people [about Jesus]!”
26 Hapo mkuu wa walinzi wa Hekalu pamoja na watu wake walikwenda Hekaluni, akawaleta. Lakini hawakuwakamata kwa kutumia nguvu, maana waliogopa kwamba watu wangewapiga mawe.
So the captain [of the Temple guards] went [to the Temple courtyard] with the officers, and they brought the apostles [back to the Council room. But they] did not treat them roughly, because they were afraid that the people would [kill them by] throwing stones at them [if they hurt the apostles].
27 Basi, wakawapeleka, wakawasimamisha mbele ya Baraza. Kuhani Mkuu akawaambia,
After [the captain and his officers] had brought [the apostles to the Council room], they commanded them to stand in front of the Council members, and the high priest questioned them.
28 “Tuliwakatazeni waziwazi kufundisha kwa jina la mtu huyu; sasa mmeyaeneza mafundisho yenu pote katika Yerusalemu na mnakusudia kutuwekea lawama ya kifo cha mtu huyo.”
He said to them [accusingly], “We [(exc)] strongly commanded you not to teach people about that man [MTY] [Jesus] But [you have disobeyed us, and] you have taught people all over Jerusalem [about him]! Furthermore, you are trying to make it seem that we [(exc)] are the ones who are guilty [MTY] for that man’s death!”
29 Hapo Petro, akiwa pamoja na wale mitume wengine, akajibu, “Lazima tumtii Mungu, na siyo binadamu.
But Peter, [speaking for himself] and the other apostles, replied, “We [(exc)] have to obey [what] God [commands us to do], not what [you] people [tell us to do]!
30 Mungu wa babu zetu alimfufua Yesu baada ya ninyi kumwua kwa kumtundika msalabani.
God considers that you are the ones who killed Jesus by nailing him to a cross! But God, whom our ancestors [worshipped], (caused Jesus to become alive again after he died/raised Jesus from the dead).
31 Huyu ndiye yule aliyekwezwa na Mungu mpaka upande wake wa kulia, akawa kiongozi na Mwokozi, ili awawezeshe watu wa Israeli watubu, wapate kusamehewa dhambi zao.
God has greatly honored Jesus. [He has taken him up to heaven! He has authorized him] to be the one who will save us and to rule [over our lives! God did this] so that he might enable [us] Israelites [MTY] to turn away from [our] sinful behavior and [that he might] forgive [us for our sins].
32 Sisi ni mashahidi wa tukio hilo, naye Roho Mtakatifu ambaye Mungu amewapa wale wanaomtii, anashuhudia pia tukio hilo.”
We [(exc)] tell people about these things [that we know happened to Jesus], and the Holy Spirit, whom God has sent to [us] who obey him, is also confirming [that these things are true].”
33 Wajumbe wote wa lile Baraza waliposikia hayo, wakawaka hasira, hata wakaamua kuwaua.
When the Council members heard those words, they became very angry [with the apostles], and they wanted to kill them.
34 Lakini Mfarisayo mmoja aitwaye Gamalieli ambaye alikuwa mwalimu wa Sheria na aliyeheshimika sana mbele ya watu wote, alisimama mbele ya lile Baraza, akataka wale mitume watolewe nje kwa muda mfupi.
But [there was a Council member] named Gamaliel. He was a Pharisee, and one who taught people the [Jewish] laws, and all the [Jewish] people respected him. He stood up in the Council and told [guards] to take the apostles out [of the room] for a short time.
35 Kisha akawaambia wale wajumbe wa Baraza, “Wananchi wa Israeli, tahadhari kabla ya kutekeleza hicho mnachotaka kuwatenda watu hawa!
[After the guards had taken the apostles out], he said to the other Council members, “Fellow Israelites, you need to think carefully about what you are about to do to these men, [and I will tell you why].
36 Zamani kidogo, kulitokea mtu mmoja jina lake Theuda, akajisema kuwa mtu wa maana na watu karibu mia nne wakajiunga naye. Lakini aliuawa, kisha wafuasi wake wote wakatawanyika na kikundi chake kikafa.
Some years ago [a man named] Theudas rebelled [against the Roman government]. He told people that he was an important person, and about 400 men joined [him. But he was killed] {[soldiers] killed him} and all those who had been accompanying him were scattered. [So they] were not able to do anything [that they had planned].
37 Tena, baadaye, wakati ule wa kuhesabiwa watu, alitokea Yuda wa Galilaya. Huyu naye, aliwavuta watu wakamfuata; lakini naye pia aliuawa, na wafuasi wake wakatawanyika.
After that, during the time when they were (writing down names of the people/taking the census) [in order to tax people, a man named] Judas from Galilee [province] rebelled [against the Roman government]. He persuaded some people to accompany him. But [soldiers] killed him, too, and all those who had accompanied him went off in different directions.
38 Na sasa pia mimi nawaambieni, msiwachukulie watu hawa hatua yoyote; waacheni! Kwa maana, ikiwa mpango huu au shughuli hii yao imeanzishwa na binadamu, itatoweka yenyewe.
So now I say [this] to you: Do not harm these men! Release them! I say this because if [this is just something] that humans have planned, they will not be able to do it. They will fail, [like Theudas and Judas did]
39 Lakini kama imeanzishwa na Mungu, siyo tu kwamba hamtaweza kuwashinda, bali mtajikuta mnapigana na Mungu.” Basi, wakakubaliana naye.
But, if God [has commanded them to do it], you will not be able to prevent them [from doing it, because] you will find out that you are opposing God!” The other members of the Council accepted what Gamaliel said.
40 Hivyo wakawaita wale mitume, wakaamuru wachapwe viboko na kuwaonya wasifundishe tena kwa jina la Yesu; kisha wakawaacha waende zao.
They told the [temple guards to bring the apostles and flog them. So the guards] brought them [into the Council room] and flogged them. Then the Council members commanded them not to speak to people about [MTY] Jesus, and they released the apostles.
41 Basi, mitume wakatoka nje ya ule mkutano wa halmashauri wakiwa wamejaa furaha, kwani walistahili kuaibishwa kwa ajili ya jina la Yesu.
So the apostles left the Council. They were rejoicing, because [they knew God] had honored them [by letting people] disgrace them because they were followers [MTY] of Jesus.
42 Wakaendelea kila siku kufundisha na kuhubiri Habari Njema ya Kristo, Hekaluni na nyumbani mwa watu.
And every day [the apostles went to] the temple [area] and to various [people’s] houses, [and] they continued [LIT] teaching [people] and telling [them] that Jesus is the Messiah.