< Matendo 3 >

1 Siku moja, saa tisa alasiri, Petro na Yohane walikuwa wanakwenda Hekaluni, wakati wa sala.
Wori Petro na Yohana bhaliga mbagenda mwi hekalu omwanya gwo kusabhwa, saa mwenda.
2 Na pale karibu na mlango wa Hekalu uitwao “Mlango Mzuri”, palikuwa na mtu mmoja, kiwete tangu kuzaliwa. Watu walimbeba huyo mtu kila siku na kumweka hapo ili aombe chochote kwa wale waliokuwa wakiingia Hekaluni.
Omunu kutya, omurema okusoka okwibhurwa, aliga nayekwa bhuli siku na aliga namamibhwa ku muryango gwa lihekalu ogwo ogubhilikirwa omukonde, korereki ature okusabha e bhiyanwa okusoka ku bhanu bhaliga mbagenda mwi hekalu.
3 Alipowaona Petro na Yohane wakiingia Hekaluni, aliwaomba wampe chochote.
Ejire abharora Petro na Yohana mbarebherera okwingira mwi hekalu, nasabhwa ebhiyanwa.
4 Petro na Yohane walimkodolea macho, naye Petro akamwambia, “Tutazame!”
Petro, amukajisishe ameso, amwi na Yohana, aikile, “nuchirore eswe.”
5 Naye akawageukia, akitazamia kupata kitu kutoka kwao.
Omurema nabharora, netogera okubhona echinu kutya okusoka kubhene.
6 Kisha Petro akamwambia, “Sina fedha wala dhahabu lakini kile nilicho nacho nitakupa. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, tembea!”
Nawe Petro naika, “jiyera na jidhaabu anye ntanajo, nawe echo ninacho enisosha kwawe. Kwa lisina lya Yesu Kristo wa Nazareth, libhata.”
7 Halafu, akamshika mkono wa kulia, akamwinua. Papo hapo miguu na magoti yake yakapata nguvu.
Petro namugega kwo kubhoko kwaye kwe bhuryo, namwimusha inguru: amaguru gaye ne bhikongochwa bhya mawa gaye mbijira amanaga.
8 Akaruka, akasimama na kuanza kutembea. Halafu akaingia pamoja nao Hekaluni, akitembea na kurukaruka huku akimtukuza Mungu.
Nachuma inguru, omunu omurema nemereguru namba okulibhata; nengira mwi hekalu amwi na Petro na Yohana, nalibhata, nachuma, namukuya Nyamuanga.
9 Watu wote waliokuwa hapo walimwona akitembea na kumsifu Mungu.
Abhanu bhone bhamurorere nalibhata no kumukuya Nyamuanga.
10 Walipomtambua kuwa ndiye yule aliyekuwa anaombaomba karibu na ule “Mlango Mzuri” wa Hekalu, wakashangaa mno hata wasiweze kuelewa yaliyompata.
Nibhamenya ati liga ali munu uliya oyo aliga neyanja nasabhwa ebhiyanwa ku muryango omukonde gwa lihekalu; nibhejurwa ne chiruguro no kutang'ang'ara kunjuno yecho chasokereye ku mwene.
11 Watu wote, wakiwa na mshangao mkubwa wakaanza kukimbilia mahali palipoitwa “Ukumbi wa Solomoni,” ambapo yule mtu alikuwa bado anaandamana na Petro na Yohane.
Kutyo aliga abhagwatirie Petro na Yohana, abhanu bhona amwi nibhabhilimira mu chisunya echo ehibhirikirwa cha Sulemani, nibharugura muno.
12 Basi, Petro alipowaona watu hao akawaambia, “Wananchi wa Israeli, kwa nini mnashangazwa na jambo hili? Mbona mnatukodolea macho kana kwamba ni kwa nguvu zetu au utakatifu wetu sisi wenyewe tumemfanya mtu huyu aweze kutembea?
Petro ejile alirora linu, omwene nabhasubhya abhanu, “Emwe abhanu bha Israeli, okubhaki omurugura? Okubhaki omurosha ameso gemwe kweswe, korere ati chamkora unu alibhate kwa managa geswe abhene?”
13 Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Mungu wa baba zetu amemtukuza Yesu mtumishi wake. Yeye ndiye yuleyule mliyemtia mikononi mwa wakuu na kumkataa mbele ya Pilato hata baada ya Pilato kuamua kumwacha huru.
Nyamuanga wa Ibrahimu, no wa Isaka, no wa Yakobo, Nyamuanga wa bhalata bheswe, amukusishe omukosi waye Yesu. Unu niwe oyo emwe mwananire no kumurema imbele yo bhusu bhwa Pilato, nawe omwene aliga aramuye okumutatira obhweru.
14 Alikuwa mtakatifu na mwema; lakini ninyi mlimkataa, mkataka mtu mwingine aliyekuwa muuaji afunguliwe.
Mwamuremere Mmweru no mulegeresi, na badala yo mwene nimwenda omwiti atatirwe.
15 Basi, mlimuua yule ambaye ni chanzo cha uzima. Lakini Mungu alimfufua, na sisi ni mashahidi wa tukio hilo.
Emwe mwamwitile Omukama wo bhujima, oyo Nyamuanga amwiruye okusoka mubhafuye eswe ni bhabhambasi bha linu.
16 Jina la Yesu na imani katika jina hilo ndivyo vilivyompa nguvu mtu huyu mnayemwona na kumfahamu. Imani kwa Yesu ndiyo iliyomponya kabisa mtu huyu kama mnavyoona nyote.
Mbe oli, kwo kwikirisha mwi sina lyaye, omunu unu oyo omumurora no kumenya, akorerwe kubha na managa. Elikirisha eryo elirabha ku Yesu limuyanire omwene obhuanga bhunu bhugumile, imbele yemwe emwe bhona.
17 “Sasa ndugu zangu, nafahamu kwamba ninyi na wakuu wenu mlitenda hayo kwa sababu ya kutojua kwenu.
Mbe oli, Bhaili, enimenya ati mwakorere kutyo kwo bhumumu, nikwo kutyo bhakorere abhabhemberesi bhemwe.
18 Lakini ndivyo Mungu alivyotimiza yale aliyotangaza zamani kwa njia ya manabii wote, kwamba ilikuwa lazima Kristo wake ateseke.
Nawe amagambo ago Nyamuanga abhabhwiliye bhwangu kwe minwa ja bharagi bhona, ati unu Kristo kajonyaka, oli agamalire.
19 Basi, tubuni mkamrudie Mungu ili afute dhambi zenu.
Mbe oli, mwigambe muinduke, korereki ati ebhiyeno bhyemwe bhisosibhweko chimwi, kunsonga gwije omwanya gwo kukondererwa okusokana no kubhao kwo Mukama;
20 Fanyeni hivyo ili Bwana awape nyakati za kuburudika rohoni na kuwaletea yule Kristo aliyemteua ambaye ndiye Yesu.
na ati ature okumuragirira Kristo oyo asorerwe kwemwe, Yesu.
21 Ni lazima yeye abaki huko mbinguni mpaka utakapofika wakati wa kurekebishwa vitu vyote, kama Mungu alivyosema kwa njia ya manabii wake watakatifu wa tangu zamani. (aiōn g165)
Omwene niwe oyo orwire lumuramire mpaka omwanya gwo kusubhya ebhinu bhyona, ebhyo Nyamuanga alomere kara kwe minwa ja bharagi bheru. (aiōn g165)
22 Kwa maana Mose alisema, Bwana Mungu wenu atawapelekeeni nabii kama mimi kutoka kati yenu ninyi wenyewe.
Ka chimwi Musa aikile, 'Omukama Nyamuanga kemusha omuragi lwanye okusoka mu bhaili bhemwe. Mumutegereshe bhuli chinu echo kabhabhwira emwe.
23 Yeyote yule ambaye hatamsikiliza nabii huyo atatengwa mbali na watu wa Mungu na kuangamizwa.
Eisokerera ati bhuli munu oyo atakutegeresha ku muragi oyo ketibhwa chimwi asoke ku bhanu.'
24 Manabii wote, kuanzia Samweli na wale waliomfuata, walitangaza habari za mambo haya ambayo yamekuwa yakitendeka siku hizi.
Yee, na bharagi bhona okusokerera Samweli na bhaliya bharubhile ku mwene, bharomere no kusimura jinsiku jinu.
25 Ahadi zile Mungu alizotoa kwa njia ya manabii ni kwa ajili yenu; na mnashiriki lile agano Mungu alilofanya na babu zenu, kama alivyomwambia Abrahamu: Kwa njia ya wazawa wako, jamaa zote za dunia zitabarikiwa.
Emwe muri bhana bha bharagi na bha liagano eryo Nyamuanga akorere amwi na bhakaruka, lwa kutyo aikire kwa Abrahamu, 'Mu mbegu yao jinganda jona eja kuchalo ejibharikiwa.'
26 Basi, ilikuwa kwa ajili yenu kwanza kwamba Mungu alimfufua mtumishi wake, alimtuma awabariki kwa kumfanya kila mmoja wenu aachane kabisa na maovu yake.”
Baada ya Nyamuanga okumukusha omukosi waye, amutumile kwemwe kwamba, korereki abhabariki emwe kwo kuinduka okusoka ku bhiyeno bhyemwe.

< Matendo 3 >