< Matendo 3 >

1 Siku moja, saa tisa alasiri, Petro na Yohane walikuwa wanakwenda Hekaluni, wakati wa sala.
And Peter and John were going up at the same time into the temple, at the hour of the prayer, the ninth [hour],
2 Na pale karibu na mlango wa Hekalu uitwao “Mlango Mzuri”, palikuwa na mtu mmoja, kiwete tangu kuzaliwa. Watu walimbeba huyo mtu kila siku na kumweka hapo ili aombe chochote kwa wale waliokuwa wakiingia Hekaluni.
and a certain man, being lame from the womb of his mother, was being carried, whom they were laying every day at the gate of the temple, called Beautiful, to ask a kindness from those entering into the temple,
3 Alipowaona Petro na Yohane wakiingia Hekaluni, aliwaomba wampe chochote.
who, having seen Peter and John about to go into the temple, was begging to receive a kindness.
4 Petro na Yohane walimkodolea macho, naye Petro akamwambia, “Tutazame!”
And Peter, having looked steadfastly toward him with John, said, “Look toward us”;
5 Naye akawageukia, akitazamia kupata kitu kutoka kwao.
and he was giving heed to them, looking to receive something from them;
6 Kisha Petro akamwambia, “Sina fedha wala dhahabu lakini kile nilicho nacho nitakupa. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, tembea!”
and Peter said, “I have no silver and gold, but what I have, that I give to you; in the Name of Jesus Christ of Nazareth, rise up and be walking.”
7 Halafu, akamshika mkono wa kulia, akamwinua. Papo hapo miguu na magoti yake yakapata nguvu.
And having seized him by the right hand, he raised [him] up, and instantly his feet and ankles were strengthened,
8 Akaruka, akasimama na kuanza kutembea. Halafu akaingia pamoja nao Hekaluni, akitembea na kurukaruka huku akimtukuza Mungu.
and springing up, he stood, and was walking, and entered with them into the temple, walking and springing, and praising God;
9 Watu wote waliokuwa hapo walimwona akitembea na kumsifu Mungu.
and all the people saw him walking and praising God,
10 Walipomtambua kuwa ndiye yule aliyekuwa anaombaomba karibu na ule “Mlango Mzuri” wa Hekalu, wakashangaa mno hata wasiweze kuelewa yaliyompata.
and they knew him, that this it was who for a kindness was sitting at the Beautiful Gate of the temple, and they were filled with wonder and amazement at what has happened to him.
11 Watu wote, wakiwa na mshangao mkubwa wakaanza kukimbilia mahali palipoitwa “Ukumbi wa Solomoni,” ambapo yule mtu alikuwa bado anaandamana na Petro na Yohane.
And at the lame man who was healed holding Peter and John, all the people ran together to them in the porch called Solomon’s—greatly amazed,
12 Basi, Petro alipowaona watu hao akawaambia, “Wananchi wa Israeli, kwa nini mnashangazwa na jambo hili? Mbona mnatukodolea macho kana kwamba ni kwa nguvu zetu au utakatifu wetu sisi wenyewe tumemfanya mtu huyu aweze kutembea?
and Peter having seen, answered to the people, “Men, Israelites! Why do you wonder at this? Or why do you look on us so earnestly, as if by our own power or piety we have made him to walk?
13 Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Mungu wa baba zetu amemtukuza Yesu mtumishi wake. Yeye ndiye yuleyule mliyemtia mikononi mwa wakuu na kumkataa mbele ya Pilato hata baada ya Pilato kuamua kumwacha huru.
The God of Abraham, and of Isaac, and of Jacob, the God of our fathers, glorified His child Jesus, whom you delivered up, and denied Him in the presence of Pilate, he having given judgment to release [Him],
14 Alikuwa mtakatifu na mwema; lakini ninyi mlimkataa, mkataka mtu mwingine aliyekuwa muuaji afunguliwe.
and you denied the Holy and Righteous One, and desired a man—a murderer—to be granted to you,
15 Basi, mlimuua yule ambaye ni chanzo cha uzima. Lakini Mungu alimfufua, na sisi ni mashahidi wa tukio hilo.
and the Prince of life you killed, whom God raised out of the dead, of which we are witnesses;
16 Jina la Yesu na imani katika jina hilo ndivyo vilivyompa nguvu mtu huyu mnayemwona na kumfahamu. Imani kwa Yesu ndiyo iliyomponya kabisa mtu huyu kama mnavyoona nyote.
and on the faith of His Name, this one whom you see and have known, His Name made strong, even the faith that [is] through Him gave to him this perfect soundness before you all.
17 “Sasa ndugu zangu, nafahamu kwamba ninyi na wakuu wenu mlitenda hayo kwa sababu ya kutojua kwenu.
And now, brothers, I have known that through ignorance you did [it], as also your rulers;
18 Lakini ndivyo Mungu alivyotimiza yale aliyotangaza zamani kwa njia ya manabii wote, kwamba ilikuwa lazima Kristo wake ateseke.
and God, what things He had declared before through the mouth of all His prophets, that the Christ should suffer, He thus fulfilled;
19 Basi, tubuni mkamrudie Mungu ili afute dhambi zenu.
convert, therefore, and turn back, for your sins being blotted out, that times of refreshing may come from the presence of the LORD,
20 Fanyeni hivyo ili Bwana awape nyakati za kuburudika rohoni na kuwaletea yule Kristo aliyemteua ambaye ndiye Yesu.
and He may send Jesus Christ who before has been preached to you,
21 Ni lazima yeye abaki huko mbinguni mpaka utakapofika wakati wa kurekebishwa vitu vyote, kama Mungu alivyosema kwa njia ya manabii wake watakatifu wa tangu zamani. (aiōn g165)
whom Heaven required, indeed, to receive until times of a restitution of all things, of which God spoke through the mouth of all His holy prophets from the age. (aiōn g165)
22 Kwa maana Mose alisema, Bwana Mungu wenu atawapelekeeni nabii kama mimi kutoka kati yenu ninyi wenyewe.
For Moses, indeed, said to the fathers—The LORD your God will raise up a Prophet to you out of your brothers, like to me; you will hear Him in all things, as many as He may speak to you;
23 Yeyote yule ambaye hatamsikiliza nabii huyo atatengwa mbali na watu wa Mungu na kuangamizwa.
and it will be, every soul that may not hear that Prophet will be utterly destroyed out of the people;
24 Manabii wote, kuanzia Samweli na wale waliomfuata, walitangaza habari za mambo haya ambayo yamekuwa yakitendeka siku hizi.
and also all the prophets from Samuel and those following in order, as many as spoke, also foretold of these days.
25 Ahadi zile Mungu alizotoa kwa njia ya manabii ni kwa ajili yenu; na mnashiriki lile agano Mungu alilofanya na babu zenu, kama alivyomwambia Abrahamu: Kwa njia ya wazawa wako, jamaa zote za dunia zitabarikiwa.
You are sons of the prophets, and of the covenant that God made to our fathers, saying to Abraham: And in your Seed will all the families of the earth be blessed;
26 Basi, ilikuwa kwa ajili yenu kwanza kwamba Mungu alimfufua mtumishi wake, alimtuma awabariki kwa kumfanya kila mmoja wenu aachane kabisa na maovu yake.”
to you first, God, having raised up His child Jesus, sent Him, blessing you, in the turning away of each one from your evil ways.”

< Matendo 3 >