< Matendo 25 >

1 Siku tatu baada ya kufika mkoani, Festo alitoka Kaisarea, akaenda Yerusalemu.
anantaraM phISTO nijarAjyam Agatya dinatrayAt paraM kaisariyAtO yirUzAlamnagaram Agamat|
2 Makuhani wakuu pamoja na viongozi wa Wayahudi walimpa habari kuhusu mashtaka yaliyokuwa yanamkabili Paulo. Walimsihi Festo
tadA mahAyAjakO yihUdIyAnAM pradhAnalOkAzca tasya samakSaM paulam apAvadanta|
3 awafanyie fadhili kwa kumleta Paulo Yerusalemu; walikuwa wamekula njama wamuue akiwa njiani.
bhavAn taM yirUzAlamam AnEtum AjnjApayatviti vinIya tE tasmAd anugrahaM vAnjchitavantaH|
4 Lakini Festo alijibu, “Paulo atabaki kizuizini kule Kaisarea na mimi nitakwenda huko karibuni.
yataH pathimadhyE gOpanEna paulaM hantuM tai rghAtakA niyuktAH| phISTa uttaraM dattavAn paulaH kaisariyAyAM sthAsyati punaralpadinAt param ahaM tatra yAsyAmi|
5 Waacheni viongozi wenu waende huko pamoja nami wakatoe mashtaka yao juu yake kama amefanya chochote kiovu.”
tatastasya mAnuSasya yadi kazcid aparAdhastiSThati tarhi yuSmAkaM yE zaknuvanti tE mayA saha tatra gatvA tamapavadantu sa EtAM kathAM kathitavAn|
6 Festo alikaa nao kwa muda wa siku nane au kumi hivi, kisha akarudi Kaisarea. Kesho yake alikwenda barazani, akaamuru Paulo aletwe ndani.
dazadivasEbhyO'dhikaM vilambya phISTastasmAt kaisariyAnagaraM gatvA parasmin divasE vicArAsana upadizya paulam AnEtum AjnjApayat|
7 Wakati Paulo alipofika, Wayahudi waliokuwa wametoka Yerusalemu walimzunguka wakaanza kutoa mashtaka mengi mazitomazito ambayo hawakuweza kuthibitisha.
paulE samupasthitE sati yirUzAlamnagarAd AgatA yihUdIyalOkAstaM caturdizi saMvESTya tasya viruddhaM bahUn mahAdOSAn utthApitavantaH kintu tESAM kimapi pramANaM dAtuM na zaknuvantaH|
8 Kwa kujitetea, Paulo alisema, “Mimi sikufanya kosa lolote kuhusu Sheria ya Wayahudi, wala kuhusu Hekalu, wala kumhusu Kaisari.”
tataH paulaH svasmin uttaramidam uditavAn, yihUdIyAnAM vyavasthAyA mandirasya kaisarasya vA pratikUlaM kimapi karmma nAhaM kRtavAn|
9 Festo alitaka kujipendekeza kwa Wayahudi na hivyo akamwuliza Paulo, “Je, ungependa kwenda Yerusalemu na huko ukahukumiwe mbele yangu kuhusu mashtaka haya?”
kintu phISTO yihUdIyAn santuSTAn karttum abhilaSan paulam abhASata tvaM kiM yirUzAlamaM gatvAsmin abhiyOgE mama sAkSAd vicAritO bhaviSyasi?
10 Paulo akajibu, “Nasimama mbele ya mahakama ya Kaisari na papa hapa ndipo ninapopaswa kupewa hukumu. Kama unavyojua vizuri, sikuwatendea Wayahudi ubaya wowote.
tataH paula uttaraM prOktavAn, yatra mama vicArO bhavituM yOgyaH kaisarasya tatra vicArAsana Eva samupasthitOsmi; ahaM yihUdIyAnAM kAmapi hAniM nAkArSam iti bhavAn yathArthatO vijAnAti|
11 Basi, ikiwa nimepatikana na kosa linalostahili adhabu ya kifo, siombi kusamehewa adhabu hiyo. Lakini kama hakuna ukweli katika mashtaka waliyotoa watu hawa, hakuna awezaye kunikabidhi kwao. Nakata rufani kwa Kaisari!”
kanjcidaparAdhaM kinjcana vadhArhaM karmma vA yadyaham akariSyaM tarhi prANahananadaNPamapi bhOktum udyatO'bhaviSyaM, kintu tE mama samapavAdaM kurvvanti sa yadi kalpitamAtrO bhavati tarhi tESAM karESu mAM samarpayituM kasyApyadhikArO nAsti, kaisarasya nikaTE mama vicArO bhavatu|
12 Basi, baada ya Festo kuzungumza na washauri wake, akamwambia Paulo, “Umekata rufani kwa Kaisari, basi, utakwenda kwa Kaisari.”
tadA phISTO mantribhiH sArddhaM saMmantrya paulAya kathitavAn, kaisarasya nikaTE kiM tava vicArO bhaviSyati? kaisarasya samIpaM gamiSyasi|
13 Siku chache baadaye, mfalme Agripa na Bernike walifika Kaisarea ili kutoa heshima zao kwa Festo.
kiyaddinEbhyaH param AgripparAjA barNIkI ca phISTaM sAkSAt karttuM kaisariyAnagaram Agatavantau|
14 Walikuwa huko siku kadhaa naye Festo akamweleza mfalme kesi ya Paulo: “Kuna mtu mmoja hapa ambaye Felisi alimwacha kizuizini.
tadA tau bahudinAni tatra sthitau tataH phISTastaM rAjAnaM paulasya kathAM vijnjApya kathayitum Arabhata paulanAmAnam EkaM bandi phIlikSO baddhaM saMsthApya gatavAn|
15 Nilipokwenda Yerusalemu makuhani wakuu na wazee wa Wayahudi walimshtaki na kuniomba nimhukumu.
yirUzAlami mama sthitikAlE mahAyAjakO yihUdIyAnAM prAcInalOkAzca tam apOdya tamprati daNPAjnjAM prArthayanta|
16 Lakini mimi niliwajibu kwamba si desturi ya Waroma kumtoa mtu aadhibiwe kabla mshtakiwa hajakutana na washtaki wake ana kwa ana na kupewa fursa ya kujitetea kuhusu hayo mashtaka.
tatOham ityuttaram avadaM yAvad apOditO janaH svApavAdakAn sAkSAt kRtvA svasmin yO'parAdha ArOpitastasya pratyuttaraM dAtuM suyOgaM na prApnOti, tAvatkAlaM kasyApi mAnuSasya prANanAzAjnjApanaM rOmilOkAnAM rIti rnahi|
17 Basi, walipofika hapa sikukawia, ila nilifanya kikao mahakamani kesho yake, nikaamuru mtu huyo aletwe.
tatastESvatrAgatESu parasmin divasE'ham avilambaM vicArAsana upavizya taM mAnuSam AnEtum AjnjApayam|
18 Washtaki wake walisimama lakini hawakutoa mashtaka maovu kama nilivyokuwa ninatazamia.
tadanantaraM tasyApavAdakA upasthAya yAdRzam ahaM cintitavAn tAdRzaM kanjcana mahApavAdaM nOtthApya
19 Ila tu walikuwa na mabishano kadhaa pamoja naye kuhusu dini yao na kuhusu mtu mmoja aitwaye Yesu ambaye alikufa, lakini Paulo anashikilia kwamba yu hai.
svESAM matE tathA paulO yaM sajIvaM vadati tasmin yIzunAmani mRtajanE ca tasya viruddhaM kathitavantaH|
20 Sikujua la kufanya kuhusu shauri hilo. Basi, nilimwuliza Paulo kama angependa kwenda mahakamani kule Yerusalemu kwa ajili ya mashtaka hayo.
tatOhaM tAdRgvicArE saMzayAnaH san kathitavAn tvaM yirUzAlamaM gatvA kiM tatra vicAritO bhavitum icchasi?
21 Lakini Paulo alikata rufani, akaomba aachwe kizuizini mpaka uamuzi wa shauri hilo ufanywe na Kaisari. Kwa hiyo niliamua akae kizuizini mpaka nitakapoweza kumpeleka kwa Kaisari.”
tadA paulO mahArAjasya nikaTE vicAritO bhavituM prArthayata, tasmAd yAvatkAlaM taM kaisarasya samIpaM prESayituM na zaknOmi tAvatkAlaM tamatra sthApayitum AdiSTavAn|
22 Basi Agripa akamwambia Festo, “Ningependa kumsikia mtu huyu mimi mwenyewe.” Festo akamwambia, “Utamsikia kesho.”
tata AgrippaH phISTam uktavAn, ahamapi tasya mAnuSasya kathAM zrOtum abhilaSAmi| tadA phISTO vyAharat zvastadIyAM kathAM tvaM zrOSyasi|
23 Hivyo, kesho yake, Agripa na Bernike walifika kwa shangwe katika ukumbi wa mkutano wakiwa wameandamana na wakuu wa majeshi na viongozi wa mji. Festo aliamuru Paulo aletwe ndani,
parasmin divasE AgrippO barNIkI ca mahAsamAgamaM kRtvA pradhAnavAhinIpatibhi rnagarasthapradhAnalOkaizca saha militvA rAjagRhamAgatya samupasthitau tadA phISTasyAjnjayA paula AnItO'bhavat|
24 Kisha akasema, “Mfalme Agripa na wote mlioko hapa pamoja nasi! Hapa mbele yenu yuko mtu ambaye jumuiya yote ya Wayahudi hapa na kule Yerusalemu walinilalamikia wakipiga kelele kwamba hastahili kuishi tena.
tadA phISTaH kathitavAn hE rAjan Agrippa hE upasthitAH sarvvE lOkA yirUzAlamnagarE yihUdIyalOkasamUhO yasmin mAnuSE mama samIpE nivEdanaM kRtvA prOccaiH kathAmimAM kathitavAn punaralpakAlamapi tasya jIvanaM nOcitaM tamEtaM mAnuSaM pazyata|
25 Lakini mimi sikuona kuwa alikuwa ametenda chochote kibaya hata astahili kupewa adhabu ya kifo. Lakini, kwa vile Paulo mwenyewe alikata rufani kwa Kaisari, niliamua kumpeleka.
kintvESa janaH prANanAzarhaM kimapi karmma na kRtavAn ityajAnAM tathApi sa mahArAjasya sannidhau vicAritO bhavituM prArthayata tasmAt tasya samIpaM taM prESayituM matimakaravam|
26 Kwa upande wangu sina habari kamili ambayo naweza kumwandikia Kaisari juu yake. Ndiyo maana nimemleta hapa mbele yenu na mbele yako mfalme Agripa, ili baada ya kumchunguza, niweze kuwa na la kuandika.
kintu zrIyuktasya samIpam Etasmin kiM lEkhanIyam ityasya kasyacin nirNayasya na jAtatvAd Etasya vicArE sati yathAhaM lEkhituM kinjcana nizcitaM prApnOmi tadarthaM yuSmAkaM samakSaM vizESatO hE AgripparAja bhavataH samakSam Etam AnayE|
27 Kwa maana nadhani itakuwa kichekesho kumpeleka mfungwa bila kutaja wazi mashtaka yanayomkabili.”
yatO bandiprESaNasamayE tasyAbhiyOgasya kinjcidalEkhanam aham ayuktaM jAnAmi|

< Matendo 25 >