< Matendo 22 >
1 “Ndugu zangu na akina baba, nisikilizeni sasa nikijitetea mbele yenu!”
Men, brethren, and fathers, hear now my apology unto you.
2 Waliposikia akiongea nao kwa Kiebrania wakazidi kukaa kimya zaidi kuliko hapo awali. Naye Paulo akaendelea kusema,
And hearing that he was speaking to them in the Hebrew tongue, they kept silent the more.
3 “Mimi ni Myahudi, mzaliwa wa Tarso katika Kilikia. Lakini nililelewa papa hapa mjini Yerusalemu chini ya mkufunzi Gamalieli. Nilifundishwa kufuata kwa uthabiti Sheria ya wazee wetu. Nilijitolea kwa moyo wote kwa Mungu kama ninyi wenyewe mlivyo hivi leo.
And he says, I am Jewish man, having been born in Tarsus of Cilicia, having been brought up in this city, educated at the feet of Gamaliel according to the accuracy of patristic law, being a zealot of God, as you all are this day;
4 Niliwatesa hata kuwaua wale watu waliofuata Njia hii. Niliwatia nguvuni wanaume kwa wanawake na kuwafunga gerezani.
who after this way persecuted unto death, binding and committing to prison both men and women;
5 Kuhani Mkuu na baraza lote la wazee wanaweza kushuhudia jambo hilo. Kutoka kwao nilipokea barua walioandikiwa wale ndugu Wayahudi waliokuwa huko Damasko. Nilikwenda Damasko ili niwatie nguvuni watu hao na kuwaleta wamefungwa mpaka Yerusalemu ili waadhibiwe.
as the high priest also, and all the eldership, witnessed me: from whom having also received letters from the brethren in Damascus, I was on my way, being about to lead them also hither into Jerusalem bound, that they might be punished.
6 “Basi, nilipokuwa njiani karibu kufika Damasko, yapata saa sita mchana, mwangu mkubwa kutoka mbinguni ulitokea ghafla ukaniangazia pande zote.
And it came to pass, while I was journeying, and nigh unto Damascus, a great light, about midday, suddenly shone from heaven around me;
7 Hapo nilianguka chini, nikasikia sauti ikiniambia: Saulo, Saulo! Kwa nini unanitesa?
and I felt upon the ground, and heard a voice, saying to me, Saul, Saul, why persecutest thou me?
8 Nami nikauliza: Nani wewe, Bwana? Naye akaniambia: Mimi ni Yesu wa Nazareti ambaye wewe unamtesa.
And I responded, Who art thou, Lord? And He said to me, I am Jesus the Nazarene, whom thou art persecuting.
9 Wale wenzangu waliuona ule mwanga lakini hawakusikia sauti ya yule aliyeongea nami.
And those being along with me saw the light indeed, but heard not the voice of the one speaking to me.
10 Basi, mimi nikauliza: Nifanye nini Bwana? Naye Bwana akaniambia: Simama, nenda Damasko na huko utaambiwa yote ambayo umepangiwa kufanya.
And I said, What shall I do, Lord? And the Lord said to me, Rising up, go into Damascus; and there it shall be told thee concerning all things which have been ordained for thee to do.
11 Kutokana na ule mwanga mkali sikuweza kuona na hivyo iliwabidi wale wenzangu kuniongoza kwa kunishika mkono mpaka nikafika Damasko.
And when I did not see on account of the glory of that light, and being led by the hand by those journeying with me, I came into Damascus.
12 “Huko kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Anania, mtu mcha Mungu, mwenye kuitii Sheria yetu na aliyeheshimika sana mbele ya Wayahudi waliokuwa wanaishi Damasko.
And a certain Ananias, a man godly according to the law, and of good report by all the Jews dwelling there,
13 Yeye alikuja kuniona, akasimama karibu nami, akasema: Ndugu Saulo! Ona tena. Papo hapo nikaona tena, nikamwangalia.
having come to me, and standing over me, said, Brother Saul, look up. And I at that hour looked up unto him.
14 Halafu Anania akasema: Mungu wa babu zetu amekuchagua upate kujua matakwa yake na kumwona yule mtumishi wake mwadilifu na kumsikia yeye mwenyewe akiongea.
And he said, The God of our fathers hath chosen thee to know His will, and see the Just One, and hear the voice from His mouth;
15 Kwa maana utamshuhudia kwa watu wote ukiwaambia yale uliyoyaona na kuyasikia.
because thou shalt be a witness for Him to all men of those things which thou hast seen and heard.
16 Sasa basi, ya nini kukawia zaidi? Simama ubatizwe na uondolewe dhambi zako kwa kuliungama jina lake.
And now why tarriest thou? arising, be baptized, and wash away thy sins, calling on His name.
17 “Basi, nilirudi Yerusalemu, na nilipokuwa nikisali Hekaluni, niliona maono.
And it happened unto me, having returned into Jerusalem, and while I was praying in the temple, I was in an ecstasy;
18 Nilimwona Bwana akiniambia: Haraka! Ondoka Yerusalemu upesi kwa maana watu wa hapa binadamu hawataukubali ushuhuda wako juu yangu.
and I saw Him speaking to me, Hasten, and depart quickly out of Jerusalem, because they will not receive thy testimony concerning me.
19 Nami nikamjibu: Bwana, wao wanajua wazi kwamba mimi ni yule aliyekuwa anapitapita katika masunagogi na kuwatia nguvuni na kuwapiga wale waliokuwa wanakuamini.
And I said, Lord, they know that I was imprisoning and binding those believing on thee throughout the synagogue;
20 Na kwamba wakati shahidi wako Stefano alipouawa, mimi binafsi nilikuwako pale nikakubaliana na kitendo hicho na kuyalinda makoti ya wale waliokuwa wanamuua.
and when the blood of thy martyr Stephen was shed, I was standing by, and consenting, and keeping the garments of those killing him.
21 Naye Bwana akaniambia: Nenda; ninakutuma mbali kwa mataifa mengine.”
And He said to me, Go: because I will send thee far away to the Gentiles.
22 Mpaka hapa, wale watu walikuwa wanamsikiza, lakini aliposema maneno haya, walianza kusema kwa sauti kubwa, “Mwondoe duniani! Mtu wa namna hiyo hastahili kuishi.”
And they continued to hear him until this word, and lifted up their voice, saying, Take away such a one from the earth: for it is not appropriate for him to live.
23 Waliendelea kupayukapayuka huku wakitikisa makoti yao na kurusha vumbi angani.
And they crying out, and rending their garments, and throwing dust into the air,
24 Mkuu wa jeshi aliwaamuru watu wake wampeleke Paulo ndani ya ngome, akawaambia wamchape viboko ili wapate kujua kisa cha Wayahudi kumpigia kelele.
the chiliarch commanded that he should be led into the castle, saying that he should be tested by scourges, in order that he might know on account of what cause they continued so to cry out against him.
25 Lakini walipokwisha mfunga ili wamchape viboko, Paulo alimwuliza jemadari mmoja aliyesimama hapo, “Je, ni halali kwenu kumpiga viboko raia wa Roma kabla hajahukumiwa?”
And when they were extending him to the scourges, Paul said to the centurion standing by, Is it lawful for you to scourge a man who is a Roman, and uncondemned?
26 Yule jemadari aliposikia hayo, alimpasha habari mkuu wa jeshi akisema, “Unataka kufanya nini? Mtu huyu ni raia wa Roma!”
And the centurion hearing, having come to the chiliarch, announced to him, saying, What are you about to do? for this man is a Roman.
27 Basi, mkuu wa jeshi alimwendea Paulo, akamwambia, “Niambie; je, wewe ni raia wa Roma?” Paulo akamjibu, “Naam.”
And the chiliarch, having come to him, said; Tell me, are you a Roman? And he said, Yes.
28 Mkuu wa jeshi akasema, “Mimi nami nimekuwa raia wa Roma kwa kulipa gharama kubwa.” Paulo akasema, “Lakini mimi ni raia wa Roma kwa kuzaliwa.”
And the chiliarch responded, With a great sum obtained I this citizenship. And Paul said, But I was indeed born (a Roman citizen).
29 Wale watu ambao walikuwa tayari kumchunguza Paulo walitoweka mara. Hata yule mkuu wa jeshi aliogopa alipojua kwamba Paulo ni raia wa Roma na kwamba alikuwa amekwisha mfunga minyororo.
Then immediately those about to scourge him departed from him: and the chiliarch also feared, knowing that he was a Roman, and that he had bound him.
30 Kesho yake, mkuu wa jeshi alitaka kujua mashtaka kamili ambayo Wayahudi walikuwa wamemwekea Paulo. Hivyo, alimfungua Paulo minyororo, akaamuru makuhani wakuu na Baraza lote wafanye kikao. Kisha alimleta Paulo, akamsimamisha mbele ya Baraza.
And on the following day, wishing to know the certainty as to what he is accused of by the Jews, he loosed him, and commanded the chief priests and all the sanhedrin to come together, and leading down Paul, he placed him in their midst.