< Matendo 21 >

1 Tulipokwisha agana nao, tulipanda meli tukaenda moja kwa moja mpaka Kosi. Kesho yake tulifika Rodo, na kutoka huko tulikwenda Patara.
Skončilo loučení a loď zvedla kotvy. Pluli jsme k ostrovu Kós, druhý den na ostrov Rodos a jižního pobřeží Malé Asie jsme dosáhli v přístavu Patara.
2 Huko, tulikuta meli iliyokuwa inakwenda Foinike, hivyo tulipanda, tukasafiri.
Tam jsme přestoupili na loď, která směřovala do fénických měst v Palestině.
3 Baada ya kufika mahali ambapo tuliweza kuona Kupro, tulipitia upande wake wa kusini tukaelekea Siria. Tulitia nanga katika mji wa Tiro ambapo ile meli ilikuwa ipakuliwe shehena yake.
Kypr jsme obepluli vpravo a dorazili jsme do Týru, kam loď vezla nějaký náklad.
4 Tulikuta waumini huko, tukakaa pamoja nao kwa muda wa juma moja. Waumini hao wakawa waongea kwa nguvu ya Roho, wakamwambia Paulo asiende Yerusalemu.
Využili jsme času a strávili jsme celý týden s tamními křesťany. Také těm Bůh vnukl obavu, že Pavla nečeká v Jeruzalémě nic dobrého, a tak mu další cestu rozmlouvali.
5 Lakini muda wetu ulipokwisha tuliondoka. Wote pamoja na wanawake na watoto wao walitusindikiza mpaka nje ya mji. Tulipofika pwani, sote tulipiga magoti tukasali.
Přesto jsme pokračovali dál. Vyprovodili nás s celými svými rodinami až za město. Na pobřeží jsme společně klečeli a modlili se.
6 Kisha tuliagana; sisi tukapanda meli nao wakarudi makwao.
Pak jsme se rozloučili a vypluli do Ptolemaidy. Také tam jsme mohli zůstat jeden den s věřícími. Naše loď končila svou plavbu v Césareji, kde jsme navštívili známého kazatele Filipa, jednoho z těch prvních sedmi apoštolských pomocníků. Ubytoval nás jako hosty své rodiny.
7 Sisi tuliendelea na safari yetu kutoka Tiro tukafika Tolemai ambapo tuliwasalimu ndugu zetu, tukakaa nao siku moja.
8 Kesho yake tuliondoka tukaenda Kaisarea. Huko Kaisarea tulikwenda nyumbani kwa mhubiri Filipo. Yeye alikuwa mmoja wa wale saba waliochaguliwa kule Yerusalemu.
9 Alikuwa na binti watatu ambao walikuwa na kipaji cha unabii.
Filipovy čtyři svobodné dcery byly také nadšené tlumočnice Kristova poselství.
10 Baada ya kukaa huko siku kadhaa, nabii mmoja aitwaye Agabo alifika kutoka Yudea.
Po několika dnech tam přišel jeden křesťan z Judska, Agabos, který měl prorocký dar.
11 Alitujia, akachukua mkanda wa Paulo, akajifunga mikono na miguu, akasema “Roho Mtakatifu asema hivi: Wayahudi kule Yerusalemu watamfunga namna hii mtu mwenye ukanda na kumtia mikononi mwa watu wa mataifa.”
Půjčil si od Pavla jeho opasek, spoutal si jím ruce i nohy a řekl: „Duch svatý mi ukázal, že majitele tohoto pásu židé v Jeruzalémě takhle svážou a vydají ho pohanům.“
12 Tuliposikia hayo, sisi na wale watu wengine waliokuwa hapo tulimsihi Paulo asiende Yerusalemu.
To už bylo příliš, a tak jsme všichni, průvodci i místní křesťané, začali Pavla přemlouvat, aby do Jeruzaléma nechodil.
13 Lakini yeye alijibu, “Mnataka kufanya nini? Mnataka kuvunja moyo wangu kwa machozi? Niko tayari siyo tu kutiwa ndani kule Yerusalemu, ila hata kufa kwa ajili ya Bwana Yesu.”
On nás však napomenul: „Proč tolik pláčete a děláte mi to těžší? Pán Ježíš přece stojí za to, abych byl pro něho uvězněn a třeba i zabit.“
14 Tuliposhindwa kumshawishi tulinyamaza, tukasema tu: “Mapenzi ya Bwana yafanyike”
Viděli jsme, že je marné na Pavla naléhat, a tak jsme řekli: „Ať se tedy stane, co chce Bůh.“
15 Baada ya kukaa pale kwa muda, tulifunga mizigo yetu, tukaendelea na safari kwenda Yerusalemu.
Skončil odpočinek u Filipovy rodiny a my nachystali svá zavazadla na poslední pěší úsek cesty do Jeruzaléma.
16 Wengine kati ya wale wafuasi wa Kaisarea walienda pamoja nasi, wakatupeleka nyumbani kwa Mnasoni ambaye tulikuwa tunakwenda kukaa naye kwa muda. Mnasoni alikuwa mwenyeji wa Kupro na alikuwa amekuwa muumini kwa siku nyingi.
Několik křesťanů z Césareje nás doprovodilo až do cíle. Zavedli nás tam k našemu dalšímu hostiteli, Mnasonovi z Kypru, jednomu z prvních křesťanů. Jeruzalémská církev nás přijala radostně.
17 Tulipofika Yerusalemu, ndugu waumini walitupokea vizuri sana.
18 Kesho yake Paulo alikwenda pamoja nasi kumwamkia Yakobo, na wazee wote wa kanisa walikuwako pia.
Hned druhý den jsme byli všichni pozváni k Jakubovi, představenému sboru, kde se shromáždili všichni starší.
19 Baada ya kuwasalimu, Paulo aliwapa taarifa kamili kuhusu yote Mungu aliyokuwa ametenda kati ya mataifa kwa njia ya utumishi wake.
Pavel se s nimi pozdravil a podal jim zevrubnou zprávu o výsledcích práce mezi pohany, k níž ho Bůh zmocnil.
20 Waliposikia hayo, walimtukuza Mungu. Kisha wakamwambia Paulo, “Ndugu, unaweza kuona kwamba kuna maelfu ya Wayahudi ambao sasa wamekuwa waumini na wote hao wanashika kwa makini Sheria ya Mose.
Rádi to slyšeli a chválili Boha. Potom však řekli Pavlovi: „Jistě už víš, že u nás již několik tisíc židů uvěřilo v Pána Ježíše a ti i nadále horlivě zachovávají Mojžíšův zákon.
21 Wamepata habari zako kwamba umekuwa ukiwafundisha Wayahudi wanaoishi kati ya mataifa mengine kuwa wasiijali Sheria ya Mose, wasiwatahiri watoto wao na kwamba wasizifuate mila za Wayahudi.
Zde se však šíří zprávy, že ty přesvědčuješ židy v pohanském světě, aby od zákona odstoupili, syny už nedávali obřezat a vůbec zavrhli starobylé židovské zvyky.
22 Sasa, mambo yatakuwaje? Ni dhahiri kuwa watapata habari kwamba umekwisha wasili hapa.
Měl bys něco podniknout dříve, než se všichni dozvědí, že jsi tady.
23 Basi, fanya kama tunavyokushauri. Tunao hapa watu wanne ambao wameweka nadhiri.
Máme pro tebe tento návrh: Mezi námi jsou teď čtyři muži, kteří se zavázali plnit nazírský slib. Jejich lhůta vypršela, ale jsou chudí a nemají prostředky na závěrečný obřad v chrámu. Jistě by na židy dobře zapůsobilo, kdybys za ty muže zaplatil a při té příležitosti podstoupil očišťování navrátilců z pohanské ciziny. Všichni by viděli, že máš zákon v úctě a pomlouvačům by to vzalo vítr z plachet.
24 Jiunge nao katika ibada ya kujitakasa, ukalipe na gharama zinazohusika, kisha wanyolewe nywele zao. Hivyo watu wote watatambua kwamba habari zile walizoambiwa juu yako hazina msingi wowote, na kwamba wewe binafsi bado unaishi kufuatana na maagizo ya Sheria za Mose.
25 Kuhusu wale watu wa mataifa mengine ambao wamekuwa waumini, tumekwisha wapelekea barua tukiwaambia mambo tuliyoamua: wasile chochote kilichotambikiwa miungu ya uongo, wasinywe damu, wasile nyama ya mnyama aliyenyongwa, na wajiepushe na uasherati.”
Pro obrácené pohany ovšem platí naše původní rozhodnutí, které jsme vám kdysi dali písemně. Žádáme od nich jen základní ohled na zákon, aby totiž nejedli maso obětované předem modlám, krev a maso s krví a především aby odložili pohanskou pohlavní nevázanost.“
26 Basi, kesho yake Paulo aliwachukua wale watu akafanya ibada ya kujitakasa pamoja nao. Kisha akaingia Hekaluni kutoa taarifa kuhusu mwisho wa siku za kujitakasa na kuhusu dhabihu itakayotolewa kwa ajili ya kila mmoja wao.
Druhého dne tedy Pavel podstoupil spolu s těmi čtyřmi muži obřad očištění. Pak šel do chrámu, aby oznámil, kdy skončí jejich nazírský závazek a jeho očišťování, a aby za každého z nich objednal oběti.
27 Wakati siku hizo saba zilipokaribia kuisha, Wayahudi waliokuwa wametoka katika mkoa wa Asia walimwona Paulo Hekaluni. Wakachochea hasira kati ya kundi lote la watu, wakamtia nguvuni
Když končilo sedm dní a Pavel s nimi přišel zase do chrámu, aby byli obřadně prohlášeni za čisté, poznali ho židovští poutníci z Malé Asie. Poštvali na něho okolostojící, popadli ho
28 wakipiga kelele: “Wananchi wa Israeli, msaada, msaada! Huyu ndiye yule mtu anayewafundisha watu kila mahali mambo yanayopinga watu wa Israeli, yanayopinga Sheria ya Mose na mahali hapa patakatifu. Hata sasa amewaingiza watu wa mataifa mengine Hekaluni na kupatia najisi mahali hapa patakatifu.”
a křičeli: „Věrní Izraelci, pojďte sem! Tady máme toho odpadlíka! Všude hlásá bludy a nic mu není svaté: ani naše vyvolení, ani zákon, ani chrám. Teď sem dokonce přivedl pohany, aby poskvrnil svaté místo.“
29 Sababu ya kusema hivyo ni kwamba walikuwa wamemwona Trofimo mwenyeji, wa Efeso, akiwa pamoja na Paulo mjini, wakadhani kwamba Paulo alikuwa amemwingiza Hekaluni.
Předtím totiž Pavla zahlédli ve městě s Trofimem z Efezu a mysleli, že ho vzal i do chrámu, kam pohané nesměli.
30 Mji wote ulienea ghasia; watu wakaja kutoka pande zote, wakamkamata Paulo, wakamburuta, wakamtoa nje ya Hekalu na papo hapo milango ya Hekalu ikafungwa.
To ovšem vyvolalo obrovský rozruch a lidé se sbíhali ze všech stran. Mezitím vyvedli Pavla z vnitřního chrámového nádvoří a brány rychle zavřeli.
31 Walikuwa tayari kumuua, lakini habari zilimfikia mkuu wa jeshi la Kiroma kuwa Yerusalemu yote ilikuwa imejaa ghasia.
Vypadalo to, že rozlícený dav Pavla utluče, když vtom zasáhli Římané. Velitel posádky hradu Antonia, který přiléhal přímo ke chrámu, dostal hlášení o nepokoji
32 Mara, mkuu wa jeshi akawachukua askari na jemadari, akalikabili lile kundi la watu. Nao walipomwona mkuu wa jeshi na askari, wakaacha kumpiga Paulo.
a seběhl s pohotovostní četou do nádvoří. Lidé se vojáků lekli, přestali Pavla tlouci a stáhli se od něho.
33 Mkuu wa jeshi alimwendea Paulo, akamtia nguvuni na kuamuru afungwe minyororo miwili. Kisha akauliza, “Ni mtu gani huyu, na amefanya nini?”
Velitel ho považoval za původce výtržnosti, dal ho zatknout a nasadit mu pouta. Pak začal vyšetřovat, kdo to je a co udělal.
34 Wengine katika lile kundi la watu walikuwa wanapayuka kitu hiki na wengine kitu kingine. Kwa sababu ya ghasia hiyo, mkuu wa jeshi hakufaulu kujua kisa kamili. Hivyo, aliamuru watu wake wampeleke Paulo ndani ya ngome.
Lidé křičeli jeden přes druhého. Velitel viděl, že se takhle nic nedozví, a tak dal rozkaz odvést Pavla do pevnosti.
35 Paulo alipofika kwenye ngazi, askari walilazimika kumbeba kwa sababu ya fujo za watu.
Dav však táhl za nimi, dorážel a křičel: „Zabijte ho!“Po schodišti do hradu museli vojáci vězně dokonce nést, aby na něho rozzuření lidé nemohli.
36 Kwa maana kundi kubwa la watu walimfuata wakipiga kelele, “Muulie mbali!”
37 Walipokuwa wanamwingiza ndani ya ngome, Paulo alimwomba mkuu wa jeshi akisema, “Naweza kukwambia kitu?” Yule mkuu wa jeshi akamjibu, “Je unajua Kigiriki?
Pavel se zeptal velitele, zda s ním může mluvit. Ten se podivil: „Ty mluvíš řecky?
38 Kwani wewe si yule Mmisri ambaye hivi majuzi alianzisha uasi na kuwaongoza majahili elfu nne hadi jangwani?”
Já jsem myslel, že jsi ten Egypťan, co se před nedávnem pokusil o povstání a schovává se někde v poušti se čtyřmi tisíci banditů.“
39 Paulo akajibu, “Mimi ni Myahudi, mzaliwa wa Tarso katika Kilikia; mimi ni raia wa mji maarufu. Tafadhali, niruhusu niongee na watu.
„Ne, “řekl Pavel, „jsem žid z Tarsu v Kilikii, římský občan. Dovol mi, prosím, promluvit k těm lidem.“
40 Yule mkuu wa jeshi akamruhusu. Hivyo Paulo alisimama juu ya ngazi, akawapungia mkono wale watu na walipokaa kimya, akaanza kuongea nao kwa Kiebrania.
Velitel souhlasil, Pavla postavili na vrchol schodiště a on dal znamení, že chce mluvit. Dav se utišil a Pavel začal hebrejsky:

< Matendo 21 >