< Matendo 2 >

1 Siku ya Pentekoste ilipofika, waumini wote walikuwa wamekusanyika pamoja.
Now when the day of Pentecost had come, they were all together in one place.
2 Ghafla, sauti ikasikika kutoka angani; sauti iliyokuwa kama ya upepo mkali, ikajaza ile nyumba yote walimokuwa wamekaa.
Suddenly there came from the sky a sound like the rushing of a mighty wind, and it filled all the house where they were sitting.
3 Kisha, vikatokea vitu vilivyoonekana kama ndimi za moto, vikagawanyika na kutua juu ya kila mmoja wao.
Tongues like fire appeared and were distributed to them, and one sat on each of them.
4 Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema lugha mbalimbali kadiri Roho alivyowawezesha.
They were all filled with the Holy Spirit, and began to speak in other languages, as the Spirit enabled them to speak out.
5 Na huko Yerusalemu walikuwako Wayahudi, watu wamchao Mungu, waliotoka katika kila nchi duniani.
Now there were dwelling in Jerusalem Jews, devout people from every nation under the sky.
6 Waliposikia sauti hiyo, kundi kubwa la watu lilikusanyika. Wote walishtuka sana kwani kila mmoja wao aliwasikia hao waumini wakisema kwa lugha yake mwenyewe.
When this sound was heard, the crowd came together, and were bewildered, because everyone heard them speaking in his own language.
7 Walistaajabu na kushangaa, wakisema, “Je, hawa wote tunaowasikia wakisema hivi, si wenyeji wa Galilaya?
They were all amazed and marveled, saying, "Look, are not all these who speak Galileans?
8 Imekuwaje, basi, kwamba kila mmoja wetu anawasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe?
How do we hear, everyone in our own native language?
9 Baadhi yetu ni Waparthi, Wamedi na Waelami; wengine ni wenyeji wa Mesopotamia, Yudea, Kapadokia, Ponto na Asia,
Parthians, Medes, Elamites, and people from Mesopotamia, Judea, Cappadocia, Pontus, Asia,
10 Frugia na Pamfulia, Misri na sehemu za Libya karibu na Kurene; wengine wetu ni wageni kutoka Roma,
Phrygia, Pamphylia, Egypt, the parts of Libya around Cyrene, visitors from Rome, both Jews and proselytes,
11 Wayahudi na watu walioongokea dini ya Kiyahudi; wengine wametoka Krete na Arabia. Sisi sote tunasikia wakisema kwa lugha zetu wenyewe mambo makuu ya Mungu.”
Cretans and Arabians: we hear them speaking in our tongues the mighty works of God."
12 Wote walishangaa na kufadhaika huku wakiulizana, “Hii ina maana gani?”
They were all amazed, and were perplexed, saying one to another, "What does this mean?"
13 Lakini wengine wakawadhihaki wakisema, “Watu hawa wamelewa divai mpya!”
Others, mocking, said, "They are filled with new wine."
14 Lakini Petro alisimama pamoja na wale kumi na mmoja akaanza kuwahutubia watu kwa sauti kubwa: “Ndugu Wayahudi nanyi nyote mnaokaa hapa Yerusalemu, sikilizeni kwa makini maneno yangu.
But Peter, standing up with the eleven, lifted up his voice, and spoke out to them, "You men of Judea, and all you who live in Jerusalem, let this be known to you, and listen to my words.
15 Watu hawa hawakulewa kama mnavyodhani; mbona ni saa tatu tu asubuhi?
For these are not drunk, as you suppose, seeing it is only nine in the morning.
16 Ukweli ni kwamba jambo hili ni lile alilosema nabii Yoeli:
But this is what has been spoken through the prophet Joel:
17 Katika siku zile za mwisho, asema Bwana, nitawamiminia binadamu wote Roho wangu. Watoto wenu, wanaume kwa wanawake, watautangaza ujumbe wangu; vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota ndoto.
'And it will be in the last days, says God, that I will pour out my Spirit on all flesh; and your sons and your daughters will prophesy, and your young men will see visions, and your old men will dream dreams.
18 Naam, hata watumishi wangu, wanaume kwa wanawake, nitawamiminia Roho wangu, siku zile, nao watautangaza ujumbe wangu.
And even on my servants, both men and women, I will pour out my Spirit in those days, and they will prophesy.
19 Nitatenda miujiza juu angani, na ishara chini duniani; kutakuwa na damu, moto na moshi mzito;
And I will show wonders in the sky above, and signs on the earth beneath; blood, and fire, and billows of smoke.
20 jua litatiwa giza, na mwezi utakuwa mwekundu kama damu, kabla ya kutokea ile siku kuu na tukufu ya Bwana.
The sun will be turned into darkness, and the moon into blood, before the great and glorious day of the Lord comes.
21 Hapo, yeyote atakayeomba kwa jina la Bwana, ataokolewa.
And it will be that whoever will call on the name of the Lord will be saved.'
22 “Wananchi wa Israeli, sikilizeni maneno haya! Yesu wa Nazareti alikuwa mtu ambaye mamlaka yake ya kimungu yalithibitishwa kwenu kwa miujiza, maajabu na ishara Mungu alizofanya kati yenu kwa njia yake, kama mnavyojua.
"Men of Israel, hear these words. Jesus the Nazorean, a man approved by God to you by mighty works and wonders and signs which God did by him in the midst of you, even as you yourselves know,
23 Kufuatana na mpango wake mwenyewe Mungu alikwisha amua kwamba Yesu angetiwa mikononi mwenu; nanyi mkamuua kwa kuwaachia watu wabaya wamsulubishe.
him, being delivered up by the determined counsel and foreknowledge of God, by the hand of lawless men, crucified and killed;
24 Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu akamwokoa katika maumivu ya kifo kwa maana haingewezekana kabisa kifo kimfunge.
whom God raised up, having freed him from the pains of death, because it was not possible that he should be held by it.
25 Maana Daudi alisema juu yake hivi: Nilimwona Bwana mbele yangu daima; yuko nami upande wangu wa kulia, na hivyo sitatikisika.
For David says concerning him, 'I saw the Lord always before me, for he is at my right hand, that I should not be shaken.
26 Kwa hiyo, moyo wangu ulifurahi; tena nilipiga vigelegele vya furaha. Mwili wangu utakaa katika tumaini;
Therefore my heart was glad, and my tongue rejoiced, and moreover my flesh also will dwell in hope;
27 kwa kuwa hutaiacha roho yangu katika kuzimu, wala kumruhusu mtakatifu wako aoze. (Hadēs g86)
because you will not abandon my soul in Sheol, neither will you allow your Holy One to see decay. (Hadēs g86)
28 Umenionyesha njia za kuufikia uzima, kuwako kwako kwanijaza furaha!
You made known to me the paths of life. You will make me full of joy in your presence.'
29 “Ndugu zangu, napenda kuwaambieni waziwazi juu ya mambo yaliyompata Daudi, babu yetu. Yeye alikufa, akazikwa, tena kaburi lake liko papa hapa petu mpaka leo.
"Brothers, I may tell you freely of the patriarch David, that he both died and was buried, and his tomb is with us to this day.
30 Lakini kwa vile Daudi alikuwa nabii, alijua kuwa Mungu alimwapia kiapo kwamba atamtawaza mmoja wa uzawa wake kuwa mfalme mahali pake.
Therefore, being a prophet, and knowing that God had sworn with an oath to him that one of his descendants would sit on his throne,
31 Daudi aliona kabla mambo yatakayofanywa na Mungu na hivyo akasema juu ya ufufuo wa Kristo wakati aliposema: Hakuachwa kuzimu, mwili wake haukuoza. (Hadēs g86)
he foreseeing this spoke about the resurrection of the Christ, that neither was he left in Sheol, nor did his flesh see decay. (Hadēs g86)
32 Basi, Mungu alimfufua huyo Yesu na sisi sote ni mashahidi wa tukio hilo.
This Jesus God raised up, to which we all are witnesses.
33 Yesu aliinuliwa juu mpaka upande wa kulia wa Mungu, akapokea kutoka kwa Baba ile zawadi aliyoahidi yaani Roho Mtakatifu; na mnachoona sasa na kusikia ni mmiminiko wa huyo Roho.
Being therefore exalted by the right hand of God, and having received from the Father the promise of the Holy Spirit, he has poured out this, which you see and hear.
34 Maana Daudi mwenyewe, hakupanda mpaka mbinguni; ila yeye alisema: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia,
For David did not ascend into the heavens, but he says himself, 'The Lord said to my Lord, "Sit by my right hand,
35 hadi nitakapowafanya adui zako kibao cha kukanyagia miguu yako.
until I make your enemies a footstool for your feet."'
36 “Watu wote wa Israeli wanapaswa kufahamu kwa hakika kwamba huyo Yesu mliyemsulubisha ninyi, ndiye huyo ambaye Mungu amemfanya kuwa Bwana na Kristo.”
"Let all the house of Israel therefore know certainly that God has made him both Lord and Christ, this Jesus whom you crucified."
37 Basi, watu waliposikia hayo, walichomwa moyo, wakawauliza Petro na wale mitume wenzake: “Ndugu zetu, tufanye nini?”
Now when they heard this, they were acutely distressed, and said to Peter and the rest of the apostles, "Brothers, what should we do?"
38 Petro akajibu, “Tubuni na kila mmoja wenu abatizwe kwa jina la Yesu Kristo ili mpate kuondolewa dhambi zenu na kupokea ile zawadi ya Roho Mtakatifu.
Peter said to them, "Repent, and be baptized, every one of you, in the name of Jesus Christ for the forgiveness of your sins, and you will receive the gift of the Holy Spirit.
39 Maana, ahadi ile ilikuwa kwa ajili yenu, kwa ajili ya watoto wenu, kwa ajili ya wote wanaokaa mbali; na kwa ajili ya kila mtu ambaye Bwana Mungu wetu atamwita kwake.”
For to you is the promise, and to your children, and to all who are far off, even as many as the Lord our God will call to himself."
40 Kwa maneno mengine mengi, Petro alisisitiza na kuwahimiza watu akisema, “Jiokoeni katika kizazi hiki kiovu.”
With many other words he testified, and exhorted them, saying, "Save yourselves from this crooked generation."
41 Wengi waliyakubali maneno yake, wakabatizwa. Watu wapatao elfu tatu wakaongezeka katika kile kikundi siku hiyo.
Then those who received his word were baptized. There were added that day about three thousand souls.
42 Hawa wote waliendelea kujifunza kutoka kwa mitume, kuishi pamoja kidugu, kumega mkate na kusali.
They continued steadfastly in the apostles' teaching and fellowship, in the breaking of bread, and prayer.
43 Miujiza na maajabu mengi yalifanyika kwa njia ya mitume hata kila mtu akajawa na hofu.
Fear came on every soul, and many wonders and signs were done through the apostles.
44 Waumini wote waliendelea kuwa kitu kimoja na mali zao waligawana pamoja.
All who believed were together, and had all things in common.
45 Walikuwa wakiuza mali na vitu vyao kisha wakagawana fedha kadiri ya mahitaji ya kila mmoja.
They sold their possessions and goods, and distributed them to all, according as anyone had need.
46 Waliendelea kukutana pamoja kila siku Hekaluni. Lakini wakati wa kumega mkate, walikutana katika nyumba zao na wakakishiriki chakula hicho kwa furaha na moyo mkunjufu.
Day by day, continuing steadfastly with one accord in the temple, and breaking bread at home, they took their food with gladness and singleness of heart,
47 Walimtukuza Mungu, wakapendwa na watu wote. Kila siku Bwana aliwaongezea idadi ya watu waliokuwa wakiokolewa.
praising God, and having favor with all the people. The Lord added to their number day by day those who were being saved.

< Matendo 2 >