< Matendo 2 >

1 Siku ya Pentekoste ilipofika, waumini wote walikuwa wamekusanyika pamoja.
When the day of Pentecost had come, they were all together with one purpose.
2 Ghafla, sauti ikasikika kutoka angani; sauti iliyokuwa kama ya upepo mkali, ikajaza ile nyumba yote walimokuwa wamekaa.
And suddenly a roar came out of the sky, like the rushing of a violent wind, and it filled the whole house where they were sitting.
3 Kisha, vikatokea vitu vilivyoonekana kama ndimi za moto, vikagawanyika na kutua juu ya kila mmoja wao.
Fiery tongues appeared and were distributed to them, and it [a tongue] landed on each one of them.
4 Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema lugha mbalimbali kadiri Roho alivyowawezesha.
And they were all filled with Holy Spirit and began to speak different languages, as the Spirit was granting to them to speak out.
5 Na huko Yerusalemu walikuwako Wayahudi, watu wamchao Mungu, waliotoka katika kila nchi duniani.
Now there were devout men, Jews, from every nation under heaven, dwelling in Jerusalem.
6 Waliposikia sauti hiyo, kundi kubwa la watu lilikusanyika. Wote walishtuka sana kwani kila mmoja wao aliwasikia hao waumini wakisema kwa lugha yake mwenyewe.
So when that roar occurred, the crowd came together, and was bewildered, because each one was hearing them speaking to him in his own dialect.
7 Walistaajabu na kushangaa, wakisema, “Je, hawa wote tunaowasikia wakisema hivi, si wenyeji wa Galilaya?
So they were amazed and marveled, saying to one another: “Hey, aren't all these who are speaking Galileans?
8 Imekuwaje, basi, kwamba kila mmoja wetu anawasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe?
So how can each of us be hearing our own dialect in which we were born?
9 Baadhi yetu ni Waparthi, Wamedi na Waelami; wengine ni wenyeji wa Mesopotamia, Yudea, Kapadokia, Ponto na Asia,
Parthians and Medes and Elamites; those dwelling in Mesopotamia, in Judea and Cappadocia, in Pontus and Asia,
10 Frugia na Pamfulia, Misri na sehemu za Libya karibu na Kurene; wengine wetu ni wageni kutoka Roma,
in Phrygia and Pamphylia, in Egypt and the parts of Libya adjoining Cyrene; and visitors from Rome—both Jews and proselytes—
11 Wayahudi na watu walioongokea dini ya Kiyahudi; wengine wametoka Krete na Arabia. Sisi sote tunasikia wakisema kwa lugha zetu wenyewe mambo makuu ya Mungu.”
Cretans and Arabians; we hear them declaring the great works of God in our own languages.”
12 Wote walishangaa na kufadhaika huku wakiulizana, “Hii ina maana gani?”
Yes they were all amazed and perplexed, saying one to another, “Whatever is going on?”
13 Lakini wengine wakawadhihaki wakisema, “Watu hawa wamelewa divai mpya!”
But different ones were jeering, saying, “They are full of sweet wine!”
14 Lakini Petro alisimama pamoja na wale kumi na mmoja akaanza kuwahutubia watu kwa sauti kubwa: “Ndugu Wayahudi nanyi nyote mnaokaa hapa Yerusalemu, sikilizeni kwa makini maneno yangu.
So Peter, standing with the eleven, raised his voice and proclaimed to them: “Men—Jews and all who are dwelling in Jerusalem—let this be known to you; indeed, listen to my speech!
15 Watu hawa hawakulewa kama mnavyodhani; mbona ni saa tatu tu asubuhi?
Because these are not drunk, as you suppose (since it is only the third hour of the day),
16 Ukweli ni kwamba jambo hili ni lile alilosema nabii Yoeli:
but this is what was spoken through the prophet Joel:
17 Katika siku zile za mwisho, asema Bwana, nitawamiminia binadamu wote Roho wangu. Watoto wenu, wanaume kwa wanawake, watautangaza ujumbe wangu; vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota ndoto.
‘It will be in the last days, says God: I will pour out from my Spirit upon all flesh; your sons and your daughters will prophesy; your young men will see visions; your old men will dream a dream.
18 Naam, hata watumishi wangu, wanaume kwa wanawake, nitawamiminia Roho wangu, siku zile, nao watautangaza ujumbe wangu.
In those days I will indeed pour out from my Spirit upon my male slaves and upon my female slaves, and they will prophesy.
19 Nitatenda miujiza juu angani, na ishara chini duniani; kutakuwa na damu, moto na moshi mzito;
I will show wonders in the heaven above and signs on the earth below: blood and fire and smoke vapor.
20 jua litatiwa giza, na mwezi utakuwa mwekundu kama damu, kabla ya kutokea ile siku kuu na tukufu ya Bwana.
The sun will be turned into darkness and the moon into ‘blood’ before the great and glorious day of the Lord will come.
21 Hapo, yeyote atakayeomba kwa jina la Bwana, ataokolewa.
And it will be: whoever calls on the name of the Lord will be saved!’
22 “Wananchi wa Israeli, sikilizeni maneno haya! Yesu wa Nazareti alikuwa mtu ambaye mamlaka yake ya kimungu yalithibitishwa kwenu kwa miujiza, maajabu na ishara Mungu alizofanya kati yenu kwa njia yake, kama mnavyojua.
“Men of Israel, listen to these words: Jesus the Natsorean, a man from God attested to you by miracles and wonders and signs, which God did by Him in your midst, as you yourselves well know,
23 Kufuatana na mpango wake mwenyewe Mungu alikwisha amua kwamba Yesu angetiwa mikononi mwenu; nanyi mkamuua kwa kuwaachia watu wabaya wamsulubishe.
Him—being delivered up by the established purpose and foreknowledge of God—you murdered, having taken Him with lawless hands and crucified Him;
24 Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu akamwokoa katika maumivu ya kifo kwa maana haingewezekana kabisa kifo kimfunge.
whom God raised up, ending the labor pains of death, because it was not possible that He should be held by it.
25 Maana Daudi alisema juu yake hivi: Nilimwona Bwana mbele yangu daima; yuko nami upande wangu wa kulia, na hivyo sitatikisika.
For David says concerning Him: ‘I always saw the Lord before my face, because He is at my right side so that I not be shaken.
26 Kwa hiyo, moyo wangu ulifurahi; tena nilipiga vigelegele vya furaha. Mwili wangu utakaa katika tumaini;
Therefore my heart was glad and my tongue rejoiced. Furthermore, even my flesh will repose upon hope,
27 kwa kuwa hutaiacha roho yangu katika kuzimu, wala kumruhusu mtakatifu wako aoze. (Hadēs g86)
because You will not abandon my soul in Hades, nor will You allow Your Holy One to see decay. (Hadēs g86)
28 Umenionyesha njia za kuufikia uzima, kuwako kwako kwanijaza furaha!
You have made known to me roads of life; with Your presence You make me full of gladness.’
29 “Ndugu zangu, napenda kuwaambieni waziwazi juu ya mambo yaliyompata Daudi, babu yetu. Yeye alikufa, akazikwa, tena kaburi lake liko papa hapa petu mpaka leo.
“Men, brothers, be it permitted to speak to you plainly about the patriarch David, that he both died and was buried, and his tomb is with us to this day.
30 Lakini kwa vile Daudi alikuwa nabii, alijua kuwa Mungu alimwapia kiapo kwamba atamtawaza mmoja wa uzawa wake kuwa mfalme mahali pake.
So then, he being a prophet and knowing that God had sworn to him with an oath that of the fruit, according to flesh, of his loins He would raise up the Messiah to sit on his throne,
31 Daudi aliona kabla mambo yatakayofanywa na Mungu na hivyo akasema juu ya ufufuo wa Kristo wakati aliposema: Hakuachwa kuzimu, mwili wake haukuoza. (Hadēs g86)
he foreseeing this spoke about the resurrection of the Messiah, that His soul was not abandoned in Hades, nor did His flesh see decay. (Hadēs g86)
32 Basi, Mungu alimfufua huyo Yesu na sisi sote ni mashahidi wa tukio hilo.
“This Jesus God raised, to which we all are witnesses.
33 Yesu aliinuliwa juu mpaka upande wa kulia wa Mungu, akapokea kutoka kwa Baba ile zawadi aliyoahidi yaani Roho Mtakatifu; na mnachoona sasa na kusikia ni mmiminiko wa huyo Roho.
Therefore, having been exalted to God's right hand, and having received from the Father the promise of the Holy Spirit, He poured out this that you now see and hear.
34 Maana Daudi mwenyewe, hakupanda mpaka mbinguni; ila yeye alisema: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia,
Further, David did not ascend into the heavens, but he himself says: ‘The Lord said to my Lord: Sit at my right hand
35 hadi nitakapowafanya adui zako kibao cha kukanyagia miguu yako.
until I make your enemies a footstool for your feet.’
36 “Watu wote wa Israeli wanapaswa kufahamu kwa hakika kwamba huyo Yesu mliyemsulubisha ninyi, ndiye huyo ambaye Mungu amemfanya kuwa Bwana na Kristo.”
Therefore, let all the house of Israel know assuredly that God has made Him both Lord and Christ, this Jesus whom you crucified!”
37 Basi, watu waliposikia hayo, walichomwa moyo, wakawauliza Petro na wale mitume wenzake: “Ndugu zetu, tufanye nini?”
Now upon hearing this they were cut to the heart and said to Peter, and the rest of the Apostles, “Men, brothers, what shall we do?!”
38 Petro akajibu, “Tubuni na kila mmoja wenu abatizwe kwa jina la Yesu Kristo ili mpate kuondolewa dhambi zenu na kupokea ile zawadi ya Roho Mtakatifu.
So Peter said to them: “Repent and be baptized, each one of you, upon the name of Jesus Christ, for forgiveness of sins, and you will receive the gift of the Holy Spirit.
39 Maana, ahadi ile ilikuwa kwa ajili yenu, kwa ajili ya watoto wenu, kwa ajili ya wote wanaokaa mbali; na kwa ajili ya kila mtu ambaye Bwana Mungu wetu atamwita kwake.”
For the promise is to you, and to your children, and to all who are far away—as many, that is, as the Lord our God may call.”
40 Kwa maneno mengine mengi, Petro alisisitiza na kuwahimiza watu akisema, “Jiokoeni katika kizazi hiki kiovu.”
With many different words he both testified and kept exhorting, saying, “Escape from this perverse generation!”
41 Wengi waliyakubali maneno yake, wakabatizwa. Watu wapatao elfu tatu wakaongezeka katika kile kikundi siku hiyo.
Then those who gladly received his word were baptized, and that day about three thousand souls were added.
42 Hawa wote waliendelea kujifunza kutoka kwa mitume, kuishi pamoja kidugu, kumega mkate na kusali.
And they continued steadfastly in the Apostles' teaching and in the fellowship, both in the breaking of the bread and in the prayers.
43 Miujiza na maajabu mengi yalifanyika kwa njia ya mitume hata kila mtu akajawa na hofu.
Fear came upon every soul—many wonders and signs were taking place through the Apostles.
44 Waumini wote waliendelea kuwa kitu kimoja na mali zao waligawana pamoja.
Now all who believed were together and had all things in common;
45 Walikuwa wakiuza mali na vitu vyao kisha wakagawana fedha kadiri ya mahitaji ya kila mmoja.
they started selling both possessions and goods and were distributing to all according as anyone had need.
46 Waliendelea kukutana pamoja kila siku Hekaluni. Lakini wakati wa kumega mkate, walikutana katika nyumba zao na wakakishiriki chakula hicho kwa furaha na moyo mkunjufu.
So day by day they continued steadfastly with one purpose in the temple and broke bread from house to house; they received their share of food with gladness and singleness of heart,
47 Walimtukuza Mungu, wakapendwa na watu wote. Kila siku Bwana aliwaongezea idadi ya watu waliokuwa wakiokolewa.
praising God and having favor with all the people. And day by day the Lord added to the Church those who were being saved.

< Matendo 2 >