< Matendo 16 >
1 Paulo alifika Derbe na Lustra, ambako aliishi mfuasi mmoja aitwaye Timotheo. Mama yake ambaye pia alikuwa mfuasi, alikuwa Myahudi; lakini baba yake alikuwa Mgiriki.
Paul arriva à Derbe et à Lystre. Il y avait là un disciple, nommé Timothée, fils d'une Juive fidèle et d'un père grec.
2 Timotheo alikuwa na sifa kubwa kati ya wale ndugu wa Lustra na Ikonio.
Les frères de Lystre et d'Iconium lui rendaient un bon témoignage.
3 Paulo alitaka Timotheo aandamane naye safarini, kwa hiyo alimtahiri. Alifanya hivyo kwa sababu Wayahudi wote walioishi sehemu hizo walijua kwamba baba yake Timotheo alikuwa Mgiriki.
Paul voulut l'emmener avec lui; et, l'ayant pris, il le circoncit, à cause des Juifs qui vivaient dans ces pays-là; car tous savaient que son père était Grec.
4 Walipokuwa wanapita katika ile miji waliwapa watu yale maagizo yaliyotolewa na mitume na wazee kule Yerusalemu, wakawaambia wayazingatie.
Dans les villes où ils passaient, ils recommandaient d'observer les décisions prises par les apôtres et par les anciens de Jérusalem.
5 Hivyo, yale makanisa yalizidi kuwa imara katika imani, na idadi ya waumini ikaongezeka kila siku.
Ainsi les Églises étaient affermies dans la foi, et elles augmentaient en nombre de jour en jour.
6 Walipitia sehemu za Frugia na Galatia kwani Roho Mtakatifu hakuwaruhusu kuhubiri huo ujumbe mkoani Asia.
Puis, ils traversèrent la Phrygie et le pays des Galates, le Saint-Esprit les ayant empêchés d'annoncer la parole en Asie.
7 Walipofika kwenye mipaka ya Musia, walijaribu kuingia mkoani Bithunia, lakini Roho wa Yesu hakuwaruhusu.
Arrivés près de la Mysie, ils se disposaient à aller en Bithynie; mais l'Esprit de Jésus ne le leur permit pas.
8 Basi, walipitia Musia, wakaenda moja kwa moja mpaka Troa.
Alors ils traversèrent rapidement la Mysie, et ils descendirent à Troas. Paul se rend en Macédoine
9 Usiku huo, Paulo aliona ono ambalo alimwona mtu mmoja wa Makedonia amesimama pale na kumwomba: “Vuka, uje Makedonia ukatusaidie.”
Pendant la nuit, Paul eut une vision; un Macédonien se tenait devant lui et le suppliait, en disant: Passe en Macédoine et viens nous secourir!
10 Mara baada ya Paulo kuona ono hilo, tulijitayarisha kwenda Makedonia bila kukawia, tukiwa na hakika kwamba Mungu ametuita tuwapelekee Habari Njema.
Aussitôt après cette vision de Paul, nous cherchâmes à partir pour la Macédoine, convaincus que Dieu nous appelait à y annoncer l'Évangile.
11 Kutoka Troa, tulisafiri kwa meli moja kwa moja mpaka Samothrake, na kesho yake tukatia nanga Neapoli.
Étant donc partis de Troas, nous naviguâmes droit sur Samothrace, et le lendemain, sur Néapolis;
12 Kutoka huko, tulikwenda mpaka Filipi, mji wa wilaya ya kwanza ya Makedonia, na ambao pia ni koloni la Waroma. Tulikaa katika mji huo siku kadhaa.
de là, nous vînmes à Philippes, la première ville de la province de la Macédoine, et une colonie romaine. Nous y séjournâmes quelques jours.
13 Siku ya Sabato tulitoka nje ya mji, tukaenda kando ya mto ambapo tulidhani ya kuwa ni mahali pa kusali. Tuliketi, tukaongea na wanawake waliokusanyika mahali hapo.
Le jour du sabbat, nous nous rendîmes hors des portes, au bord de la rivière, où nous pensions qu'on se rassemblait pour la prière; et, nous étant assis, nous parlions aux femmes qui s'y trouvaient réunies.
14 Miongoni mwa wale waliotusikiliza alikuwa mwanamke mmoja mcha Mungu aitwaye Ludia mwenyeji wa Thuatira, ambaye alikuwa mfanyabiashara ya nguo za kitani za rangi ya zambarau. Bwana aliufungua moyo wake hata akayapokea yale maneno Paulo aliyokuwa anasema.
L'une d'elles, nommée Lydie, de la ville de Thyatire, marchande de pourpre, qui craignait Dieu, nous écouta; et le Seigneur lui ouvrit le coeur pour qu'elle fût attentive à ce que Paul disait.
15 Baada ya huyo mama pamoja na jamaa yake kubatizwa, alitualika akisema, “Kama kweli mmeona kwamba mimi namwamini Bwana, karibuni nyumbani kwangu mkakae.” Akatuhimiza twende.
Quand elle eut été baptisée avec sa famille, elle nous adressa cette demande: Si vous m'avez jugée fidèle au Seigneur, entrez dans ma maison, et demeurez-y; et elle nous y obligea.
16 Siku moja, tulipokuwa tunakwenda mahali pa kusali, msichana mmoja aliyekuwa na pepo mwenye uwezo wa kuagua alikutana nasi. Msichana huyo alikuwa anawapatia matajiri wake fedha nyingi kwa uaguzi wake.
Un jour que nous allions à la prière, une servante, qui avait un esprit de Python, et qui, en devinant, procurait un grand profit à ses maîtres, nous rencontra.
17 Basi, huyo msichana alimfuata Paulo na sisi, akipiga kelele na kusema, “Hawa watu ni watumishi wa Mungu Mkuu. Wanawatangazieni njia ya wokovu.”
Elle se mit à nous suivre, Paul et nous, en criant: Ces hommes-là sont des serviteurs du Dieu Très-Haut; ils vous annoncent la voie du salut.
18 Akawa anafanya hivyo kwa siku nyingi hata siku moja Paulo alikasirika, akamgeukia na kumwambia huyo pepo, “Nakuamuru kwa jina la Yesu Kristo, mtoke huyu!” Mara huyo pepo akamtoka.
Elle fit ainsi pendant plusieurs jours; mais Paul, en étant importuné, se retourna et dit à l'esprit: Je te commande, au nom de Jésus-Christ, de sortir de cette femme. Et l'esprit sortit à l'heure même.
19 Matajiri wa yule msichana walipoona kwamba tumaini lao la kupata mali limekwisha, waliwakamata Paulo na Sila, wakawaburuta mpaka hadharani, mbele ya wakuu.
Cependant les maîtres de cette servante, voyant disparaître l'espoir de leur gain, se saisirent de Paul et de Silas, les traînèrent sur la place publique devant les magistrats,
20 Wakawashtaki kwa mahakimu wakisema, “Watu hawa ni Wayahudi na wanafanya fujo katika mji wetu.
et, les ayant amenés aux préteurs, ils dirent: Ces hommes troublent notre ville!
21 Wanafundisha desturi ambazo sisi raia wa Roma haturuhusiwi kuzikubali wala kuzifuata.”
Ce sont des Juifs; et ils enseignent des coutumes qu'il ne nous est permis ni d'accepter ni de suivre, à nous qui sommes Romains.
22 Kundi la watu likajiunga nao, likawashambulia. Wale mahakimu wakawatatulia Paulo na Sila mavazi yao, wakaamuru wapigwe viboko.
La foule se souleva aussi contre eux, et les préteurs, les ayant fait dépouiller de leurs vêtements, ordonnèrent qu'ils fussent battus de verges.
23 Baada ya kupigwa sana wakatiwa ndani, na askari wa gereza akaamriwa kuwaweka chini ya ulinzi mkali.
Après qu'on leur eut donné plusieurs coups, ils les firent jeter en prison, en recommandant au geôlier de les tenir sous bonne garde.
24 Kutokana na maagizo hayo, huyo askari aliwaweka katika chumba cha ndani kabisa cha gereza na kuifunga miguu yao kwenye nguzo.
Ayant reçu cet ordre, il les mit au fond de la prison, et leur serra les pieds dans des entraves.
25 Karibu na usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakisali na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu, huku wafungwa wengine wakiwa wanasikiliza.
Vers le milieu de la nuit, Paul et Silas, étant en prières, chantaient les louanges de Dieu, et les prisonniers les écoutaient.
26 Ghafla, kulitokea mtetemeko mkuu wa ardhi ambao uliitikisa misingi ya gereza. Mara, milango yote ikafunguka na minyororo iliyowafunga hao wafungwa ikaachana.
Tout à coup, il se fit un grand tremblement de terre, de sorte que les fondements de la prison furent ébranlés. En même temps toutes les portes s'ouvrirent, et les liens de tous les prisonniers tombèrent.
27 Askari wa gereza alipoamka na kuiona milango ya gereza imefunguliwa, alidhani kwamba wafungwa wote walikuwa wametoroka na hivyo akauchomoa upanga wake, akataka kujiua.
Le geôlier, réveillé en sursaut et voyant les portes de la prison ouvertes, tira son épée; et il allait se tuer, croyant que les prisonniers s'étaient enfuis.
28 Lakini Paulo akaita kwa sauti kubwa: “Usijidhuru mwenyewe kwa maana sisi sote tuko hapa.”
Mais Paul lui cria à haute voix: Ne te fais point de mal; nous sommes tous ici!
29 Baada ya kumwita mtu alete taa, huyo askari wa gereza alikimbilia ndani, akajitupa mbele ya miguu ya Paulo na Sila huku akitetemeka kwa hofu.
Alors le geôlier, ayant demandé de la lumière, accourut; et, tout tremblant, il se jeta aux pieds de Paul et de Silas.
30 Halafu aliwaongoza nje, akawauliza, “Waheshimiwa, nifanye nini nipate kuokoka?”
Puis, les ayant menés dehors, il leur dit: Seigneurs, que faut-il que je fasse pour être sauvé?
31 Wao wakamjibu, “Mwamini Bwana Yesu nawe utaokolewa pamoja na jamaa yako yote.”
Ils lui dirent: Crois au Seigneur Jésus, et tu seras sauvé, toi et ta famille.
32 Basi, wakamhubiria neno la Bwana yeye pamoja na jamaa yake.
Alors ils lui annoncèrent la parole de Dieu, ainsi qu'à tous ceux qui étaient dans sa maison.
33 Yule askari aliwachukua saa ileile ya usiku akawasafisha majeraha yao, kisha yeye na jamaa yake wakabatizwa papo hapo.
Le geôlier, les prenant avec lui à cette même heure de la nuit, lava leurs plaies; et aussitôt il fut baptisé, lui et tous les siens.
34 Halafu akawachukua Paulo na Sila nyumbani kwake, akawapa chakula. Yeye na jamaa yake yote wakafanya sherehe kwa vile sasa walikuwa wanamwamini Mungu.
Puis, les ayant fait monter dans son logement, il fit dresser la table, et il se réjouit avec toute sa famille de ce qu'il avait cru en Dieu.
35 Kesho yake asubuhi, mahakimu waliwatuma maofisa wao wakisema, “Wafungueni wale watu.”
Quand le jour fut venu, les préteurs envoyèrent les licteurs dire au geôlier: Laisse aller ces hommes.
36 Yule askari wa gereza alimpasha habari Paulo: “Mahakimu wametuma ujumbe ili mfunguliwe. Sasa mnaweza kutoka na kwenda zenu kwa amani.”
Le geôlier rapporta ces paroles à Paul: Les préteurs me font dire de vous laisser partir. Sortez donc, et allez en paix.
37 Lakini Paulo alimjibu, “Ati nini? Ingawa hatukuwa na kosa, walitupiga viboko hadharani hali sisi ni raia wa Roma. Tena, walitutia ndani na sasa wanataka kutufungulia kwa siri! Hata kidogo! Ni lazima wao wenyewe waje hapa watufungulie.”
Mais Paul dit aux licteurs: Après nous avoir battus de verges en public et sans jugement, nous qui sommes citoyens romains, ils nous ont mis en prison; et maintenant, ils nous font sortir en cachette! Cela ne sera pas! Qu'ils viennent eux-mêmes nous mettre en liberté!
38 Hao maofisa waliwapasha habari mahakimu juu ya jambo hilo, nao waliposikia kwamba Paulo na Sila walikuwa raia wa Roma, waliogopa.
Les licteurs rapportèrent ces paroles aux préteurs, qui furent effrayés en apprenant qu'ils étaient Romains.
39 Hivyo, walikwenda kuwataka radhi na baada ya kuwatoa ndani waliwaomba watoke katika mji ule.
Ils vinrent leur parler; ils les mirent en liberté et les prièrent de quitter la ville.
40 Paulo na Sila walitoka gerezani, wakaenda nyumbani kwa Ludia. Huko walionana na ndugu waumini na baada ya kuwatia moyo wakaondoka.
Quand ils furent sortis de la prison, les apôtres entrèrent chez Lydie, et, après avoir vu les frères et les avoir exhortés, ils partirent.