< Matendo 16 >

1 Paulo alifika Derbe na Lustra, ambako aliishi mfuasi mmoja aitwaye Timotheo. Mama yake ambaye pia alikuwa mfuasi, alikuwa Myahudi; lakini baba yake alikuwa Mgiriki.
Paul [and Silas] to Derbe [city and visited the believers there]. Next [they went to] Lystra [city]. A believer whose name was Timothy lived there. His mother was a Jewish believer, but his father was a Greek.
2 Timotheo alikuwa na sifa kubwa kati ya wale ndugu wa Lustra na Ikonio.
The believers in Lystra and Iconium said good things about Timothy,
3 Paulo alitaka Timotheo aandamane naye safarini, kwa hiyo alimtahiri. Alifanya hivyo kwa sababu Wayahudi wote walioishi sehemu hizo walijua kwamba baba yake Timotheo alikuwa Mgiriki.
and Paul wanted to take Timothy with him [when he went] to other places, so he circumcised Timothy. [He did that so that] the Jews who lived in those places [would accept Timothy], because they knew that his non-Jewish father [had not allowed him to be circumcised] {[anyone to circumcise his son]}.
4 Walipokuwa wanapita katika ile miji waliwapa watu yale maagizo yaliyotolewa na mitume na wazee kule Yerusalemu, wakawaambia wayazingatie.
[So Timothy went with Paul and Silas] and they traveled to many other towns. [In each town] they told [the] believers the rules that had been decided by the apostles and elders in Jerusalem {that the apostles and elders in Jerusalem had decided} that [non-Jewish] believers should obey.
5 Hivyo, yale makanisa yalizidi kuwa imara katika imani, na idadi ya waumini ikaongezeka kila siku.
[God was helping] the believers in those towns to trust more strongly [in the Lord Jesus], and every day more people became believers.
6 Walipitia sehemu za Frugia na Galatia kwani Roho Mtakatifu hakuwaruhusu kuhubiri huo ujumbe mkoani Asia.
Paul and his companions wanted/planned to enter Asia [province] preach the message [about Jesus] there, but they were prevented by the Holy Spirit {the Holy Spirit prevented them} [from going there. So] they traveled through Phrygia and Galatia [provinces].
7 Walipofika kwenye mipaka ya Musia, walijaribu kuingia mkoani Bithunia, lakini Roho wa Yesu hakuwaruhusu.
They arrived at the border of Mysia [province] and they wanted to go [north] Bithynia [province]. But [again] the Spirit of Jesus showed them that they should not [go there].
8 Basi, walipitia Musia, wakaenda moja kwa moja mpaka Troa.
So they went through Mysia [province] and arrived at Troas, a [port city. I, Luke, joined them there].
9 Usiku huo, Paulo aliona ono ambalo alimwona mtu mmoja wa Makedonia amesimama pale na kumwomba: “Vuka, uje Makedonia ukatusaidie.”
That night [God gave] Paul a vision in which he saw a man [who was a native] of Macedonia [province]. He was standing [some distance away], and he was earnestly calling to Paul, “[Please] come over [here] to Macedonia and help us!”
10 Mara baada ya Paulo kuona ono hilo, tulijitayarisha kwenda Makedonia bila kukawia, tukiwa na hakika kwamba Mungu ametuita tuwapelekee Habari Njema.
[The next morning] we [(exc)] immediately got ready to go to Macedonia, because we believed that God had called us to [go and] preach the good message to the people there.
11 Kutoka Troa, tulisafiri kwa meli moja kwa moja mpaka Samothrake, na kesho yake tukatia nanga Neapoli.
So we [(exc)] got on a ship in Troas and sailed across [the sea] Samothrace [Island. We spent the night there], and the next day [we sailed again across the sea and arrived] at Neapolis [port/town].
12 Kutoka huko, tulikwenda mpaka Filipi, mji wa wilaya ya kwanza ya Makedonia, na ambao pia ni koloni la Waroma. Tulikaa katika mji huo siku kadhaa.
Then we [left Neapolis and] went [by land] to Philippi. It was a very important city in Macedonia [province, where many] Roman citizens lived. We stayed in Philippi several days.
13 Siku ya Sabato tulitoka nje ya mji, tukaenda kando ya mto ambapo tulidhani ya kuwa ni mahali pa kusali. Tuliketi, tukaongea na wanawake waliokusanyika mahali hapo.
On the first (Sabbath/Jewish day of rest) [after we(exc) arrived], we went outside the city gate [down] to the river. We had heard [someone say] that [Jewish] people gathered to pray there. [When we arrived there, we saw] some women who had gathered [to pray]. So we sat down and began to tell them [the message about Jesus].
14 Miongoni mwa wale waliotusikiliza alikuwa mwanamke mmoja mcha Mungu aitwaye Ludia mwenyeji wa Thuatira, ambaye alikuwa mfanyabiashara ya nguo za kitani za rangi ya zambarau. Bwana aliufungua moyo wake hata akayapokea yale maneno Paulo aliyokuwa anasema.
A woman whose name was Lydia was one of those who were listening [to Paul. She was a non-Jewish woman], from Thyatira [city, who bought and] sold [expensive] purple cloth. She had accepted what the Jews believe about God. The Lord [God] caused her to pay attention to the message that Paul preached, and she believed it. [The members of her household also heard the good message and believed in Jesus] [MTY].
15 Baada ya huyo mama pamoja na jamaa yake kubatizwa, alitualika akisema, “Kama kweli mmeona kwamba mimi namwamini Bwana, karibuni nyumbani kwangu mkakae.” Akatuhimiza twende.
After [Paul and Silas] baptized Lydia and the others who lived in her house [MTY] {After Lydia and the others who lived in her house were baptized}, she invited us to [go and stay in] her home. She said, “You [(pl)] know that I [now] believe in the Lord [Jesus], so [please] come and stay in my house.” She persuaded us [to do that, so we(exc) stayed there].
16 Siku moja, tulipokuwa tunakwenda mahali pa kusali, msichana mmoja aliyekuwa na pepo mwenye uwezo wa kuagua alikutana nasi. Msichana huyo alikuwa anawapatia matajiri wake fedha nyingi kwa uaguzi wake.
Another day, while we [(exc)] were going to the place where people regularly gathered to pray, we met a young woman who was a slave. An evil spirit was enabling her to be a ventriloquist and to tell people what would happen [to them]. People paid a lot of money to [the men who were] her owners, in return for her telling them things that [she said] would happen [to them].
17 Basi, huyo msichana alimfuata Paulo na sisi, akipiga kelele na kusema, “Hawa watu ni watumishi wa Mungu Mkuu. Wanawatangazieni njia ya wokovu.”
This young woman followed Paul and the rest of us. She continually shouted, “These men serve the God who is the greatest [of all gods]! They are telling you how ([God] can save you [so that he will not punish you/to be] saved)”
18 Akawa anafanya hivyo kwa siku nyingi hata siku moja Paulo alikasirika, akamgeukia na kumwambia huyo pepo, “Nakuamuru kwa jina la Yesu Kristo, mtoke huyu!” Mara huyo pepo akamtoka.
She continued to do that for many days. Finally Paul became irritated. So he turned [toward the young woman] and rebuked the evil spirit [that was in her. He said], “By the authority [MTY] of Jesus Christ, I command you [(sg)] to come out of this young woman!” Right away the evil spirit left her.
19 Matajiri wa yule msichana walipoona kwamba tumaini lao la kupata mali limekwisha, waliwakamata Paulo na Sila, wakawaburuta mpaka hadharani, mbele ya wakuu.
And then her owners realized that she could no longer earn money for them [because she could no longer predict what would happen to people, so they were angry]. They grabbed Paul and Silas and forcefully took them to the public square, to [the place where] the government authorities and [a lot of other people were gathered].
20 Wakawashtaki kwa mahakimu wakisema, “Watu hawa ni Wayahudi na wanafanya fujo katika mji wetu.
The owners [of the young woman] brought Paul and Silas to the city officials and told them, “These men are Jews, and they are greatly troubling [the people in] [MTY] our city.
21 Wanafundisha desturi ambazo sisi raia wa Roma haturuhusiwi kuzikubali wala kuzifuata.”
They are teaching that we [(inc)] should follow customs that our laws do not allow us Romans to consider [to be correct] or to obey!”
22 Kundi la watu likajiunga nao, likawashambulia. Wale mahakimu wakawatatulia Paulo na Sila mavazi yao, wakaamuru wapigwe viboko.
Many of the crowd joined [those who were accusing] Paul and Silas, and started beating them. Then the [Roman] authorities commanded [soldiers] to tear the shirts off Paul and Silas and to beat them [with rods/sticks].
23 Baada ya kupigwa sana wakatiwa ndani, na askari wa gereza akaamriwa kuwaweka chini ya ulinzi mkali.
[So the soldiers] beat Paul and Silas vigorously [with rods]. After that, they [took them and] shoved them into the prison. They told the jailer that he should lock them up securely.
24 Kutokana na maagizo hayo, huyo askari aliwaweka katika chumba cha ndani kabisa cha gereza na kuifunga miguu yao kwenye nguzo.
[Because the officials] had [commanded] him [to do that], the jailer shoved Paul and Silas into the cell that was farthest inside. [There, he made them sit down on the floor/ground and stretch out their legs]. Then he fastened their ankles in [grooves] between two large wooden beams, [so that Paul and Silas could not move their legs].
25 Karibu na usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakisali na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu, huku wafungwa wengine wakiwa wanasikiliza.
About midnight, Paul and Silas were praying [aloud] and praising God by singing hymns. The [other] prisoners were listening attentively to them.
26 Ghafla, kulitokea mtetemeko mkuu wa ardhi ambao uliitikisa misingi ya gereza. Mara, milango yote ikafunguka na minyororo iliyowafunga hao wafungwa ikaachana.
Suddenly there was a very strong earthquake. It shook the entire jail [SYN] and its foundation [SYN]. [The earthquake caused] all the doors [of the jail] to open suddenly, and [caused] all the chains that fastened the prisoners to fall off.
27 Askari wa gereza alipoamka na kuiona milango ya gereza imefunguliwa, alidhani kwamba wafungwa wote walikuwa wametoroka na hivyo akauchomoa upanga wake, akataka kujiua.
The jailer woke up and saw that the doors of the jail were open. He thought that the prisoners had escaped. So he pulled out his sword in order to kill himself, [because he knew that the officials would kill him if the prisoners escaped].
28 Lakini Paulo akaita kwa sauti kubwa: “Usijidhuru mwenyewe kwa maana sisi sote tuko hapa.”
Paul [saw the jailer and] shouted to him, “Do not harm yourself! We [(exc) prisoners] are all here!”
29 Baada ya kumwita mtu alete taa, huyo askari wa gereza alikimbilia ndani, akajitupa mbele ya miguu ya Paulo na Sila huku akitetemeka kwa hofu.
The jailer shouted [to someone] to bring torches/lanterns, [and after they brought them], he rushed into the jail and knelt down in front of Paul and Silas. [He was very afraid, so] much so that he was trembling/shaking.
30 Halafu aliwaongoza nje, akawauliza, “Waheshimiwa, nifanye nini nipate kuokoka?”
Then he brought Paul and Silas out [of the jail] and asked: “Sirs, what do I need to do to be saved [from being punished for my sins]?”
31 Wao wakamjibu, “Mwamini Bwana Yesu nawe utaokolewa pamoja na jamaa yako yote.”
[They answered], “Trust in [what] the Lord Jesus [has done for you], and you will be saved {[God] will save you}, and the others who live in [MTY] your house will [also] be saved [if they believe in Jesus].”
32 Basi, wakamhubiria neno la Bwana yeye pamoja na jamaa yake.
Then the jailer took Paul and Silas into his house, washed their wounds, and gave them a meal. [He woke up all the people in his house, and] Paul and Silas told all of them the message about the Lord [Jesus. They all believed in him]. Immediately [after that, the jailer and all his family were baptized] {[Paul and Silas] baptized the jailer and all his family}. They were very happy, because now they all believed in God.
33 Yule askari aliwachukua saa ileile ya usiku akawasafisha majeraha yao, kisha yeye na jamaa yake wakabatizwa papo hapo.
34 Halafu akawachukua Paulo na Sila nyumbani kwake, akawapa chakula. Yeye na jamaa yake yote wakafanya sherehe kwa vile sasa walikuwa wanamwamini Mungu.
35 Kesho yake asubuhi, mahakimu waliwatuma maofisa wao wakisema, “Wafungueni wale watu.”
The next morning, the [Roman] officials commanded [some] police officers [to go to the jail to say to the jailer], “[Our bosses] say, ‘Let those [two] prisoners go [now]!’”
36 Yule askari wa gereza alimpasha habari Paulo: “Mahakimu wametuma ujumbe ili mfunguliwe. Sasa mnaweza kutoka na kwenda zenu kwa amani.”
[After the officers went and told that to] the jailer, he [went and] told Paul, “The [Roman] authorities have sent a message [(sg)] saying that I should release you [(sg)] and Silas [from prison]. So you [two] can leave [the jail] now. Now you can go peacefully!”
37 Lakini Paulo alimjibu, “Ati nini? Ingawa hatukuwa na kosa, walitupiga viboko hadharani hali sisi ni raia wa Roma. Tena, walitutia ndani na sasa wanataka kutufungulia kwa siri! Hata kidogo! Ni lazima wao wenyewe waje hapa watufungulie.”
But Paul said to the police officers, “The authorities [commanded men to] beat us in front of a crowd before [those authorities] had learned if we [(exc)] had done anything wrong! Then they [ordered men to] shove us into jail! [But that was not legal, because] we [(exc)] are Roman citizens! And now they want [RHQ] to send us away secretly! We will not accept that! Those [Roman] officials must come themselves and [tell us that they are sorry], and take us out [of jail].”
38 Hao maofisa waliwapasha habari mahakimu juu ya jambo hilo, nao waliposikia kwamba Paulo na Sila walikuwa raia wa Roma, waliogopa.
So the police officers [went and] told the city authorities [what Paul had said]. When those authorities heard that Paul and Silas were Roman citizens, they were afraid [that someone would report to more important officials what they had done, and as a result they would be punished] {[those officials would punish them]}.
39 Hivyo, walikwenda kuwataka radhi na baada ya kuwatoa ndani waliwaomba watoke katika mji ule.
So the city authorities came to Paul and Silas and told them that they were sorry for what they had done to them. The authorities brought them out of the jail, and repeatedly asked them to leave the city [soon].
40 Paulo na Sila walitoka gerezani, wakaenda nyumbani kwa Ludia. Huko walionana na ndugu waumini na baada ya kuwatia moyo wakaondoka.
After Paul and Silas left the jail, they went to Lydia’s house. There they met with her and the [other] believers. They encouraged the believers [to continue trusting in the Lord Jesus], and then the two apostles left [Philippi].

< Matendo 16 >