< Matendo 16 >
1 Paulo alifika Derbe na Lustra, ambako aliishi mfuasi mmoja aitwaye Timotheo. Mama yake ambaye pia alikuwa mfuasi, alikuwa Myahudi; lakini baba yake alikuwa Mgiriki.
And he came to Derbe and Lystra; and behold, a certain disciple was there, named Timothy, the son of a Jewess, who was a believer; but his father was a Greek.
2 Timotheo alikuwa na sifa kubwa kati ya wale ndugu wa Lustra na Ikonio.
A good report was given of him by the brethren in Lystra and Iconium.
3 Paulo alitaka Timotheo aandamane naye safarini, kwa hiyo alimtahiri. Alifanya hivyo kwa sababu Wayahudi wote walioishi sehemu hizo walijua kwamba baba yake Timotheo alikuwa Mgiriki.
This man Paul wished to go with him: and he took him and circumcised him, on account of the Jews that were in those places: for they all knew that his father was a Greek.
4 Walipokuwa wanapita katika ile miji waliwapa watu yale maagizo yaliyotolewa na mitume na wazee kule Yerusalemu, wakawaambia wayazingatie.
And as they went through the cities, they delivered to them the decrees that had been resolved on by the apostles and elders at Jerusalem, that they might keep them.
5 Hivyo, yale makanisa yalizidi kuwa imara katika imani, na idadi ya waumini ikaongezeka kila siku.
Therefore, the churches were established in the faith, and they increased in number daily.
6 Walipitia sehemu za Frugia na Galatia kwani Roho Mtakatifu hakuwaruhusu kuhubiri huo ujumbe mkoani Asia.
When they had gone throughout Phrygia and the region of Galatia, being forbidden by the Holy Spirit to preach the word in Asia,
7 Walipofika kwenye mipaka ya Musia, walijaribu kuingia mkoani Bithunia, lakini Roho wa Yesu hakuwaruhusu.
and had come to Mysia, they attempted to go into Bithynia; and the Spirit did not permit them.
8 Basi, walipitia Musia, wakaenda moja kwa moja mpaka Troa.
But having passed by Mysia, they came down to Troas.
9 Usiku huo, Paulo aliona ono ambalo alimwona mtu mmoja wa Makedonia amesimama pale na kumwomba: “Vuka, uje Makedonia ukatusaidie.”
And, during the night, a vision appeared to Paul. A certain man of Macedonia stood and besought him, saying: Come over to Macedonia and help us.
10 Mara baada ya Paulo kuona ono hilo, tulijitayarisha kwenda Makedonia bila kukawia, tukiwa na hakika kwamba Mungu ametuita tuwapelekee Habari Njema.
After he had seen the vision, we immediately endeavored to go into Macedonia, concluding that the Lord had called us to preach the gospel to them.
11 Kutoka Troa, tulisafiri kwa meli moja kwa moja mpaka Samothrake, na kesho yake tukatia nanga Neapoli.
Therefore, setting sail from Troas, we came by a straight course to Samothracia, and, on the following day, to Neapolis,
12 Kutoka huko, tulikwenda mpaka Filipi, mji wa wilaya ya kwanza ya Makedonia, na ambao pia ni koloni la Waroma. Tulikaa katika mji huo siku kadhaa.
and thence to Philippi, which is the first city of that part of Macedonia, and a colony. We remained in that city some days:
13 Siku ya Sabato tulitoka nje ya mji, tukaenda kando ya mto ambapo tulidhani ya kuwa ni mahali pa kusali. Tuliketi, tukaongea na wanawake waliokusanyika mahali hapo.
and on the sabbath-day we went out of the city to the side of a river, where, as usual, was the house of prayer; and we sat down and spoke to the women who had come together.
14 Miongoni mwa wale waliotusikiliza alikuwa mwanamke mmoja mcha Mungu aitwaye Ludia mwenyeji wa Thuatira, ambaye alikuwa mfanyabiashara ya nguo za kitani za rangi ya zambarau. Bwana aliufungua moyo wake hata akayapokea yale maneno Paulo aliyokuwa anasema.
And a certain woman, named Lydia, a seller of purple, of the city of Thyatira, who worshiped God, heard; whose heart the Lord opened to attend to the things that were spoken by Paul.
15 Baada ya huyo mama pamoja na jamaa yake kubatizwa, alitualika akisema, “Kama kweli mmeona kwamba mimi namwamini Bwana, karibuni nyumbani kwangu mkakae.” Akatuhimiza twende.
And when she and her household had been immersed, she besought us, saying: If you judge me to be faithful to the Lord, come into my house, and make it your home. And she con strained us.
16 Siku moja, tulipokuwa tunakwenda mahali pa kusali, msichana mmoja aliyekuwa na pepo mwenye uwezo wa kuagua alikutana nasi. Msichana huyo alikuwa anawapatia matajiri wake fedha nyingi kwa uaguzi wake.
And it came to pass, that as we were going to the house of prayer, there met us a certain maid-servant that had a spirit of Python, who brought much gain to her masters, by giving responses.
17 Basi, huyo msichana alimfuata Paulo na sisi, akipiga kelele na kusema, “Hawa watu ni watumishi wa Mungu Mkuu. Wanawatangazieni njia ya wokovu.”
She followed Paul and us, and cried out, saying: These men are the servants of the most High God, who show us the way of salvation.
18 Akawa anafanya hivyo kwa siku nyingi hata siku moja Paulo alikasirika, akamgeukia na kumwambia huyo pepo, “Nakuamuru kwa jina la Yesu Kristo, mtoke huyu!” Mara huyo pepo akamtoka.
And this she continued to do for many days. But Paul, being grieved, turned and said to the spirit: I command you, in the name of Jesus Christ, to come out of her. And it came out that very hour.
19 Matajiri wa yule msichana walipoona kwamba tumaini lao la kupata mali limekwisha, waliwakamata Paulo na Sila, wakawaburuta mpaka hadharani, mbele ya wakuu.
And when her masters saw that the hope of their gain was gone, they seized Paul and Silas, and dragged them into the market to the rulers.
20 Wakawashtaki kwa mahakimu wakisema, “Watu hawa ni Wayahudi na wanafanya fujo katika mji wetu.
And having brought them to the magistrates, they said: These men, who are Jews, do greatly trouble our city;
21 Wanafundisha desturi ambazo sisi raia wa Roma haturuhusiwi kuzikubali wala kuzifuata.”
and they teach customs which it is not lawful for us, who are Romans, to receive or to observe.
22 Kundi la watu likajiunga nao, likawashambulia. Wale mahakimu wakawatatulia Paulo na Sila mavazi yao, wakaamuru wapigwe viboko.
And the multitude rose up together against them; and the magistrates stripped off their clothes, and gave command to beat them with rods.
23 Baada ya kupigwa sana wakatiwa ndani, na askari wa gereza akaamriwa kuwaweka chini ya ulinzi mkali.
And when they had laid many stripes on them, they threw them into prison, and charged the jailer to keep them securely.
24 Kutokana na maagizo hayo, huyo askari aliwaweka katika chumba cha ndani kabisa cha gereza na kuifunga miguu yao kwenye nguzo.
And having received such a charge, he put them into the inner prison, and made their feet fast in the stocks.
25 Karibu na usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakisali na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu, huku wafungwa wengine wakiwa wanasikiliza.
And at midnight Paul and Silas prayed, and sung a hymn to God; and the prisoners were listening to them.
26 Ghafla, kulitokea mtetemeko mkuu wa ardhi ambao uliitikisa misingi ya gereza. Mara, milango yote ikafunguka na minyororo iliyowafunga hao wafungwa ikaachana.
And suddenly there was a great earthquake, so that the foundations of the prison were shaken; and immediately all the doors were opened, and every one’s bonds were loosed.
27 Askari wa gereza alipoamka na kuiona milango ya gereza imefunguliwa, alidhani kwamba wafungwa wote walikuwa wametoroka na hivyo akauchomoa upanga wake, akataka kujiua.
And the jailer, being aroused from sleep, and seeing the doors of the prison open, drew his sword, and was about to kill himself, supposing that the prisoners had fled.
28 Lakini Paulo akaita kwa sauti kubwa: “Usijidhuru mwenyewe kwa maana sisi sote tuko hapa.”
But Paul called out with a loud voice, saying: Do yourself no harm, for we are all here.
29 Baada ya kumwita mtu alete taa, huyo askari wa gereza alikimbilia ndani, akajitupa mbele ya miguu ya Paulo na Sila huku akitetemeka kwa hofu.
Then he called for a light, and sprang in, and trembling, he fell down before Paul and Silas;
30 Halafu aliwaongoza nje, akawauliza, “Waheshimiwa, nifanye nini nipate kuokoka?”
and, having brought them out, he said: Sirs, what must I do to be saved?
31 Wao wakamjibu, “Mwamini Bwana Yesu nawe utaokolewa pamoja na jamaa yako yote.”
They replied: Believe on the Lord Jesus Christ, and you and your house shall be saved.
32 Basi, wakamhubiria neno la Bwana yeye pamoja na jamaa yake.
And they spoke the word of the Lord to him, and to all that were in his house.
33 Yule askari aliwachukua saa ileile ya usiku akawasafisha majeraha yao, kisha yeye na jamaa yake wakabatizwa papo hapo.
And he took them at that hour of the night, and washed the blood from their stripes; and he was immersed, himself and all his, immediately.
34 Halafu akawachukua Paulo na Sila nyumbani kwake, akawapa chakula. Yeye na jamaa yake yote wakafanya sherehe kwa vile sasa walikuwa wanamwamini Mungu.
And he brought them into his house, and set food before them, and rejoiced, believing in God, with all his house.
35 Kesho yake asubuhi, mahakimu waliwatuma maofisa wao wakisema, “Wafungueni wale watu.”
But when it was day, the magistrates sent the lictors, saying: Release those men.
36 Yule askari wa gereza alimpasha habari Paulo: “Mahakimu wametuma ujumbe ili mfunguliwe. Sasa mnaweza kutoka na kwenda zenu kwa amani.”
And the jailer told these words to Paul: The magistrates have sent to release you. Now, therefore, come out, and go in peace.
37 Lakini Paulo alimjibu, “Ati nini? Ingawa hatukuwa na kosa, walitupiga viboko hadharani hali sisi ni raia wa Roma. Tena, walitutia ndani na sasa wanataka kutufungulia kwa siri! Hata kidogo! Ni lazima wao wenyewe waje hapa watufungulie.”
But Paul said to them: Having publicly scourged us uncondemned, us who are Romans, they threw us into prison: and do they now put us out secretly? No, verily: but let them come and lead us out.
38 Hao maofisa waliwapasha habari mahakimu juu ya jambo hilo, nao waliposikia kwamba Paulo na Sila walikuwa raia wa Roma, waliogopa.
And the lictors told these words to the magistrates: and they were alarmed when they heard that they were Romans;
39 Hivyo, walikwenda kuwataka radhi na baada ya kuwatoa ndani waliwaomba watoke katika mji ule.
and they came, and entreated them, and led them out, and requested them to depart from the city.
40 Paulo na Sila walitoka gerezani, wakaenda nyumbani kwa Ludia. Huko walionana na ndugu waumini na baada ya kuwatia moyo wakaondoka.
And having come out of the prison, they went into the house of Lydia; and when they had seen the brethren, they comforted them, and departed.