< Matendo 14 >

1 Kule Ikonio, mambo yalikuwa kama yalivyokuwa kule Antiokia; Paulo na Barnaba walikwenda katika sunagogi la Wayahudi wakaongea kwa uhodari hata Wayahudi wengi na Wagiriki wakawa waumini.
Now it happened in Iconium that they entered together into the synagogue of the Jews, and they spoke in such a way that a copious multitude of both Jews and Greeks believed.
2 Lakini Wayahudi wengine waliokataa kuwa waumini walichochea na kutia chuki katika mioyo ya watu wa mataifa mengine ili wawapinge hao ndugu.
Yet truly, the Jews who were unbelieving had incited and enflamed the souls of the Gentiles against the brothers.
3 Paulo na Barnaba waliendelea kukaa huko kwa muda mrefu. Waliongea kwa uhodari juu ya Bwana, naye Bwana akathibitisha ukweli wa ujumbe walioutoa juu ya neema yake, kwa kuwawezesha kutenda miujiza na maajabu.
And so, they remained for a long time, acting faithfully in the Lord, offering testimony to the Word of his grace, providing signs and wonders done by their hands.
4 Watu wa mji huo waligawanyika: wengine waliwaunga mkono Wayahudi, na wengine walikuwa upande wa mitume.
Then the multitude of the city was divided. And certainly, some were with the Jews, yet truly others were with the Apostles.
5 Mwishowe, baadhi ya watu wa mataifa mengine na Wayahudi, wakishirikiana na wakuu wao, waliazimu kuwatendea vibaya hao mitume na kuwapiga mawe.
Now when an assault had been planned by the Gentiles and the Jews with their leaders, so that they might treat them with contempt and stone them,
6 Mitume walipogundua jambo hilo, walikimbilia Lustra na Derbe, miji ya Lukaonia, na katika sehemu za jirani,
they, realizing this, fled together to Lystra and Derbe, cities of Lycaonia, and to the entire surrounding region.
7 wakawa wanahubiri Habari Njema huko.
And they were evangelizing in that place.
8 Kulikuwa na mtu mmoja huko Lustra ambaye alikuwa amelemaa miguu tangu kuzaliwa, na alikuwa hajapata kutembea kamwe.
And a certain man was sitting at Lystra, disabled in his feet, lame from his mother’s womb, who had never walked.
9 Mtu huyo alikuwa anamsikiliza Paulo alipokuwa anahubiri. Paulo alimtazama kwa makini, na alipoona kuwa alikuwa na imani ya kuweza kuponywa,
This man heard Paul speaking. And Paul, gazing at him intently, and perceiving that he had faith, so that he might be healed,
10 akasema kwa sauti kubwa, “Simama wima kwa miguu yako!” Huyo mtu aliyelemaa akainuka ghafla, akaanza kutembea.
said with a loud voice, “Stand upright upon your feet!” And he leaped up and walked around.
11 Umati wa watu walipoona alichofanya Paulo, ulianza kupiga kelele kwa lugha ya Kilukaonia: “Miungu imetujia katika sura za binadamu!”
But when the crowds had seen what Paul had done, they lifted up their voice in the Lycaonian language, saying, “The gods, having taken the likenesses of men, have descended to us!”
12 Barnaba akaitwa Zeu, na Paulo, kwa vile yeye ndiye aliyekuwa anaongea, akaitwa Herme.
And they called Barnabas, ‘Jupiter,’ yet truly they called Paul, ‘Mercury,’ because he was the lead speaker.
13 Naye kuhani wa hekalu la Zeu lililokuwa nje ya mji akaleta fahali na shada za maua mbele ya mlango mkuu wa mji, na pamoja na ule umati wa watu akataka kuwatambikia mitume.
Also, the priest of Jupiter, who was outside the city, in front of the gate, bringing in oxen and garlands, was willing to offer sacrifice with the people.
14 Barnaba na Paulo walipopata habari hiyo waliyararua mavazi yao na kukimbilia katika lile kundi la watu wakisema kwa sauti kubwa:
And as soon as the Apostles, Barnabas and Paul, had heard this, tearing their tunics, they leapt into the crowd, crying out
15 “Ndugu, kwa nini mnafanya mambo hayo? Sisi pia ni binadamu kama ninyi. Na, tuko hapa kuwahubirieni Habari Njema, mpate kuziacha hizi sanamu tupu, mkamgeukie Mungu aliye hai, Mungu aliyeumba mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo.
and saying: “Men, why would you do this? We also are mortals, men like yourselves, preaching to you to be converted, from these vain things, to the living God, who made heaven and earth and the sea and all that is in them.
16 Zamani Mungu aliruhusu kila taifa lifanye lilivyopenda.
In previous generations, he permitted all nations to walk in their own ways.
17 Hata hivyo, Mungu hakuacha kujidhihirisha kwa mambo mema anayowatendea: huwanyeshea mvua toka angani, huwapa mavuno kwa wakati wake, huwapa chakula na kuijaza mioyo yenu furaha.”
But certainly, he did not leave himself without testimony, doing good from heaven, giving rains and fruitful seasons, filling their hearts with food and gladness.”
18 Ingawa walisema hivyo haikuwa rahisi kuwazuia wale watu wasiwatambikie.
And by saying these things, they were barely able to restrain the crowds from immolating to them.
19 Lakini Wayahudi kadhaa walikuja kutoka Antiokia na Ikonio, wakawafanya watu wajiunge nao, wakampiga mawe Paulo na kumburuta hadi nje ya mji wakidhani amekwisha kufa.
Now certain Jews from Antioch and Iconium arrived there. And having persuaded the crowd, they stoned Paul and dragged him outside of the city, thinking him to be dead.
20 Lakini waumini walipokusanyika na kumzunguka, aliamka akarudi mjini. Kesho yake, yeye pamoja na Barnaba walikwenda Derbe.
But as the disciples were standing around him, he got up and entered the city. And the next day, he set out with Barnabas for Derbe.
21 Baada ya Paulo na Barnabas kuhubiri Habari Njema huko Derbe na kupata wafuasi wengi, walifunga safari kwenda Antiokia kwa kupitia Lustra na Ikonio.
And when they had evangelized that city, and had taught many, they returned again to Lystra and to Iconium and to Antioch,
22 Waliwaimarisha waumini wa miji hiyo na kuwatia moyo wabaki imara katika imani. Wakawaambia, “Ni lazima sisi sote tupitie katika taabu nyingi ili tuingie katika ufalme wa Mungu.”
strengthening the souls of the disciples, and exhorting them that they should remain always in the faith, and that it is necessary for us to enter into the kingdom of God through many tribulations.
23 Waliteua wazee katika kila kanisa kwa ajili ya waumini, na baada ya kusali na kufunga, wakawaweka chini ya ulinzi wa Bwana ambaye walikuwa wanamwamini.
And when they had established priests for them in each church, and had prayed with fasting, they commended them to the Lord, in whom they believed.
24 Baada ya kupitia katika nchi ya Pisidia, walifika Pamfulia.
And traveling by way of Pisidia, they arrived in Pamphylia.
25 Baada ya kuhubiri ule ujumbe huko Perga, walikwenda Atalia.
And having spoken the word of the Lord in Perga, they went down into Attalia.
26 Kutoka huko walisafiri kwa meli wakarudi Antiokia ambako hapo awali walikuwa wamewekwa chini ya ulinzi wa neema ya Mungu kwa ajili ya kazi ambayo sasa walikuwa wameitimiza.
And from there, they sailed to Antioch, where they had been commended to the grace of God for the work which they had now accomplished.
27 Walipofika huko Antiokia walifanya mkutano wa kanisa la mahali hapo, wakawapa taarifa juu ya mambo Mungu aliyofanya pamoja nao, na jinsi alivyowafungulia mlango watu wa mataifa mengine mlango wa kuingia katika imani.
And when they had arrived and had gathered together the church, they related what great things God had done with them, and how he had opened the door of faith to the Gentiles.
28 Wakakaa pamoja na wale waumini kwa muda mrefu.
And they remained for no small amount of time with the disciples.

< Matendo 14 >